Ukisikia kuna kupungukiwa akili, ndiyo huku.
Ukikaa mbele ya luninga yako, halafu ukasikia kuwa mazalio ya samaki yanaharibiwa na wavuvi maharamia wa majini. Halafu baadaye ukamsikia mvuvi haramia akitamka kuwa wameanzisha mapambano dhidi ya samaki kwa sababu amezamisha meli ya kisasa ya uvuvi, utasema nini?
Hakika utasema, huyu haramia mvuvi, licha ya siku zote kufahamika ni haramia, ina maana sasa amekuwa mwendawazimu na kichaa?
Eti Mbowe ni gaidi, ama kweli Duniani vioja haviishi.
Miaka ya nyuma nikiwa Sekondari, Mkuu wa Shule alienda Arusha kwaajili ya selection ya wanafunzi wa kwenda kidato cha tano, aliporudi akasema, majitu yasiyo na nidhamu, yenye akili ndogo yanawezaje kulinda usalama? Mkuu huyo wa shule, anasema kuwa kwenye karatasi ihusuyo mwanafunzi mmoja toka shule moja, mkuu wa shule alindika:
"Mwanafunzi huyu uwezo wake darasani ni wa chini sana, ni mkorofi, mara mbili amewahi kukamatwa kwa wizi wa vifaa vya wanafunzi wenzake, pia mara nyingi amewahi kutoroka shule usiku na kwenda kunywa pombe za kienyeji kijiji cha jirani, aliwahi kutuhumiwa kushiriki tendo la ubakaji lakini ushahidi ulikosekana, aliwahi pia kukamatwa na chumvi aliyoiba kwenye jiko la shule ambayo alikuwa akibadilisha na pombe za kienyeji, nadhani kazi pekee ambayo inaweza kumfaa ni kuwa POLISI!"
Yule mkuu wa shule akashangaa ni kwanini mtu mwovu, kazi itakayomfaa iwe ni ya ulinzi wa usalama!
Ukikaa mbele ya luninga yako, halafu ukasikia kuwa mazalio ya samaki yanaharibiwa na wavuvi maharamia wa majini. Halafu baadaye ukamsikia mvuvi haramia akitamka kuwa wameanzisha mapambano dhidi ya samaki kwa sababu amezamisha meli ya kisasa ya uvuvi, utasema nini?
Hakika utasema, huyu haramia mvuvi, licha ya siku zote kufahamika ni haramia, ina maana sasa amekuwa mwendawazimu na kichaa?
Eti Mbowe ni gaidi, ama kweli Duniani vioja haviishi.
Miaka ya nyuma nikiwa Sekondari, Mkuu wa Shule alienda Arusha kwaajili ya selection ya wanafunzi wa kwenda kidato cha tano, aliporudi akasema, majitu yasiyo na nidhamu, yenye akili ndogo yanawezaje kulinda usalama? Mkuu huyo wa shule, anasema kuwa kwenye karatasi ihusuyo mwanafunzi mmoja toka shule moja, mkuu wa shule alindika:
"Mwanafunzi huyu uwezo wake darasani ni wa chini sana, ni mkorofi, mara mbili amewahi kukamatwa kwa wizi wa vifaa vya wanafunzi wenzake, pia mara nyingi amewahi kutoroka shule usiku na kwenda kunywa pombe za kienyeji kijiji cha jirani, aliwahi kutuhumiwa kushiriki tendo la ubakaji lakini ushahidi ulikosekana, aliwahi pia kukamatwa na chumvi aliyoiba kwenye jiko la shule ambayo alikuwa akibadilisha na pombe za kienyeji, nadhani kazi pekee ambayo inaweza kumfaa ni kuwa POLISI!"
Yule mkuu wa shule akashangaa ni kwanini mtu mwovu, kazi itakayomfaa iwe ni ya ulinzi wa usalama!