Tz mbongo
JF-Expert Member
- Mar 12, 2015
- 13,332
- 7,351
Kwa mkristo atakuwa yupo sawa ila kwa muislamu ataona umekosea,ndio maana nasema inategemea na imani ya mtu.... mkristo akisema Allah ni mungu na Mohamed ni mtume wa uongo atakuwa anakosea?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa mkristo atakuwa yupo sawa ila kwa muislamu ataona umekosea,ndio maana nasema inategemea na imani ya mtu.... mkristo akisema Allah ni mungu na Mohamed ni mtume wa uongo atakuwa anakosea?
Na hapo ndipo inapokuja dhana ya kuheshimu imani ya mwingine hata kama hukubaliani nayo. Ni imani ya wakristo kwamba ardhi ile Israel walipewa na Mungu na mimi niliongea kwa mtazamo huo. Kama kuna mwenye mtazamo tofauti siwezi kumzuia kufikiria anavyotaka.Kwa mkristo atakuwa yupo sawa ila kwa muislamu ataona umekosea,ndio maana nasema inategemea na imani ya mtu.
Piga picha kwanini mungu asingempatia ibrahim maeneo kama uswiss au congo au tanzania maeneo matamu matamu kama hayo kaenda kumueka semi arid area huko ambapo kuna hadi ziwa lenye chumvi nyingi kana kwamba hadi ukitembea hauzami.... kutangaza kuifuta Israel kwenye uso wa duniani was one of the biggest mistakes ever!
Kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila hilo kutekelezeka;
na kwa kuwa ardhi ile alipewa Ibrahim kuwa miliki yake na kizazi chake milele;
na kwa kuwa mbingu na ardhi zitapita bila yodi wala nukta moja ya Torati kutanguka;
hivyo basi, wenye akili wamegundua kuendelea kushupaza shingo ni kujilisha upepo.
Ni busara Palestina ikaungana na waarabu wenzie wenye nia njema kutafuta amani na Israel kwa faida yao wenyewe na vizazi vyao kwani hayo wanayoyatamani na kuyataka hayatokaa yatimie hadi kiama!
Tatizo hili suala haliishii kwenye mitazamo tu.... na hapo ndipo inapokuja dhana ya kuheshimu imani ya mwingine hata kama hukubaliani nayo. Ni imani ya wakristo kwamba ardhi ile Israel walipewa na Mungu na mimi niliongea kwa mtazamo huo. Kama kuna mwenye mtazamo tofauti siwezi kumzuia kufikiria anavyotaka.
... siwezi kujua makusudi ya Mungu mkuu; ila jambo najua, kwamba ndivyo ilivyompendeza. By the waya aliyekudanganya kwamba Congo au Uswiss ni maeneo matamu kuliko nchi ya ahadi; nchi ya maziwa na asali ni nani? Yako mengi yaonekanayo bora pachoni pa wanadamu lakini mbele za Mungu ni machukizo.Piga picha kwanini mungu asingempatia ibrahim maeneo kama uswiss au congo au tanzania maeneo matamu matamu kama hayo kaenda kumueka semi arid area huko ambapo kuna hadi ziwa lenye chumvi nyingi kana kwamba hadi ukitembea hauzami.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ufadhili wote wa magaidi ya Hamas unatoka Iran.Waarabu wengi wameshtuka kwamba wanaihitaji Israel kwa ustawi wa nchi zao.Na km huwezi kushindana nae basi ungana nae.maisha yasonge.Aliyetamka kutaka kuifuta Israel ni Iran wapalestina mnawaonea.
Kuna kipi cha ajabu israel ambacho uswiss hakipo?... siwezi kujua makusudi ya Mungu mkuu; ila jambo najua, kwamba ndivyo ilivyompendeza. By the waya aliyekudanganya kwamba Congo au Uswiss ni maeneo matamu kuliko nchi ya ahadi; nchi ya maziwa na asali ni nani? Yako mengi yaonekanayo bora pachoni pa wanadamu lakini mbele za Mungu ni machukizo.
... tatizo lako unadhani "kuvutia" machoni pako ni kuvutia "pachoni pa Mungu". Hushangai Makkah mji mtukufu ni jangwa la ajabu kuliko maeneo mengi ya dunia. Makusudi ya Mungu sio makusudi ya mwanadamu elewa hilo.Kuna kipi cha ajabu israel ambacho uswiss hakipo?
Na nilipotaja hayo maeneo jua nimeongea kwa fact mfano congo ni misitu minene pamoja na madini mengi tu , tanzania kuna kila kivutio na vingine ambavyo havipo nchi nyenginezo duniani mfano tanzanite ukija uswiss ni nchi yenye milima na maenoe ya kuvutia mno kingine ndo nchi yenye amani duniani kwa kuwa haijawahi kupigana vita vyovyote vya kidunia .
Njoo sasa hapo israel kwanza ni kanchi kadogo sana kana kwamba unaweza kutumia masaa mawili tu kumaliza mpaka mmoja hadi mwengine kiupana njoo kwenye hali ya unusu jangwa ,joto,hakuna mapori na misitu minene, vita kila siku .
Duh! Huyo mungu aliyempa abraham israel atakuwa ana ka upendeleo .
na sisi waafrika Mungu wetu ni yupi?Mungu wa Yakobo aibariki sana Israel. Neno lake litasimama milele na milele. Amen.
Sijaongelea kuvutia machoni pekee nimetaja na utajiri unaopatikana eneo husika ambapo wananchi wake watakuwa wanakula bata kwa hizo rasilimali ,unajua saudia kuna mafuta lakini? Israel mafuta yapo? Sio unakuwa unajibu bila kusoma post vizuri , huyo mungu aliyewaeka kwenye semi desert hao waisrael mbaya zaidi kawanyima rasilimali muhimu muhimu ndo upendo wake huo?... tatizo lako unadhani "kuvutia" machoni pako ni kuvutia "pachoni pa Mungu". Hushangai Makkah mji mtukufu ni jangwa la ajabu kuliko maeneo mengi ya dunia. Makusudi ya Mungu sio makusudi ya mwanadamu elewa hilo.