Palestina yasitisha mahusino yote baina yake na Israel na Marekani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532

Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas amesitisha mahusiano yote na Marekani na Israel, yakiwemo yanayohusiana na usalama, baada ya kuupinga mpango wa amani ya Mashariki ya Kati uliopendekezwa na Rais wa Marekani Donald Trump.
Abbas alikuwa mjini Cairo kuuhutubia mkutano wa dharura wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, ambayo iliwaunga mkono Wapalestina katika upinzani wao kwa mpango huo wa Trump.

Abbas alisema tayari wameifahamisha Israel kuhusu hatua hiyo ya kusitisha mahusiano. Maafisa wa Israel hawajazungumzia kauli hiyo ya Abbas.

Vikosi vya Israel na Mamlaka ya Palestina kwa muda mrefu vimekuwa vikishirikiana katika maeneo ya ulinzi ya Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel ambayo yako chini ya udhibiti wa Palestina.

Palestina pia ina makubaliano ya ushirikiano wa kijasusi na Shirika la Ujasusi la Marekani - CIA ambayo yaliendelea hata baada ya Wapalestina kuanza kususia juhudi za amani za utawala wa Trump katika mwaka wa 2017.
 
In short hiyo Vita ya Palestine na Israel ni Vita iliyopanngwa na na mungu kabisa. Kwa sababu tukisoma maandiko matakatifu yanasema sauli aliambiwa aue wamareki woote asiache
 
 
Sikujua kuwa tatizo la Mashariki ya Kati ni kati ya Israel na Marekani. Hawa wakitatua tofauti zao Mashariki ya Kati wanapata amani! Angalau Trump kaisaidia dunia kutambua hilo.
 
In short hiyo Vita ya Palestine na Israel ni Vita iliyopanngwa na na mungu kabisa. Kwa sababu tukisoma maandiko matakatifu yanasema sauli aliambiwa aue wamareki woote asiache
Kwa hiyo Wapalestina hawana thamani mbele za Mungu?

Ila Kumbuka watu wa kwanza kumtambua Yesu walikuwa sio Waisrael (Wale wataalamu wa Nyota),wote walitoka nje ya Israel mmoja wapo akitokea Ethiopia,Yesu alishaivunja hii siku nyingi.

Kwa hii Israel ya sasa inayosapoti maswala ya homosexualism Mungu angekuwa tayari angeshaitia kibiriti.
 
Cyo wote ni homosexuals, mbona hata bongo wapo homos
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado Tanganyika tu. Sijui tunasubiri nini kuchukua hiyo hatua ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…