Hili ni jambo linalonishangaza sana ! na kwa kweli naomba mwenye kujua siri ya hili anifahamishe.
Wanachama na viongozi wa upinzani kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita wamenyanyaswa kuliko miaka yote ya ukoloni nchini Tanganyika enzi zile, wameteswa , wamepotezwa, wamepigwa risasi, wamefungwa, wamebaguliwa, wamebezwa, wametukanwa kila aina ya matusi na kufanyiwa kila unyama, lakini mbona bado wana furaha? Kwanini?