Pamoja na mgomo wa wafanyabiashara, mimi nasimama upande wa TRA

Pamoja na mgomo wa wafanyabiashara, mimi nasimama upande wa TRA

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Wengi wa wafanyabiashara wamegoma nchi nzima na moja ya ajenda yao ni ukaguzi wa risiti za EFD zisitishwe mara moja. Mimi ni mwananchi wa kawaida kabisa na asilimia 95 ya wafanyabiashara wa nchi hii hawatoi risiti halali.

Pale unaponunua bidhaa ukiomba risiti toka kwa mfanyabiashara ni mgogoro na utaambiwa mashine ni mbovu ooh nikupe risiti iliyo na upungufu wa fedha uliyotoa n.k. Ukikomaa watakuona wewe siyo mtu wa kawaida. Kwa nini ninyi wafanyabiashara hamtaki kutoa risiti halali kwa bidhaa aliyonunua mteja?

Maduka machache yanayotoa risiti halali ni kama ALAF na maduka yanayosimamiwa na wazungu. Wahindi ndo wamekuwa wajanja kupitiliza na mara anakudanganya nikikuuzia bei hii sitakupa risiti kwa sababu tayari nimekupunguzia kumbe ni upuuzi mtupu.

Ndugu zangu nchi inajengwa na wananchi wenyewe, TOENI RISITI YA EFD na wananchi DAINI RISITI HALALI YA EFD.
 
Acha kusimama upande wa TRA tu, hata ungekuwa unasiamamishia TRA, hakuna shida.
 
Wengi wa wafanyabiashara wamegoma nchi nzima na moja ya ajenda yao ni ukaguzi wa risiti za EFD zisitishwe mara moja. Mimi ni mwananchi wa kawaida kabisa na asilimia 95 ya wafanyabiashara wa nchi hii hawatoi risiti halali.

Pale unaponunua bidhaa ukiomba risiti toka kwa mfanyabiashara ni mgogoro na utaambiwa mashine ni mbovu ooh nikupe risiti iliyo na upungufu wa fedha uliyotoa n.k. Ukikomaa watakuona wewe siyo mtu wa kawaida. Kwa nini ninyi wafanyabiashara hamtaki kutoa risiti halali kwa bidhaa aliyonunua mteja?

Maduka machache yanayotoa risiti halali ni kama ALAF na maduka yanayosimamiwa na wazungu. Wahindi ndo wamekuwa wajanja kupitiliza na mara anakudanganya nikikuuzia bei hii sitakupa risiti kwa sababu tayari nimekupunguzia kumbe ni upuuzi mtupu.

Ndugu zangu nchi inajengwa na wananchi wenyewe, TOENI RISITI YA EFD na wananchi DAINI RISITI HALALI YA EFD.
hii mada yako ingekuwa umetoa usiku tungekwambia kojoa ukalale
 
Mimi niliwahi kufungua Kimgahawa nikaambiwa nilipe Income Tax halafu Hotel Levy Catering Levy ushuru wa Halmashauri nk. Mpaka nikakafunga kale Kamgahawa.

Halafu kila ukifungua Redio unasikia Mabilioni yamepigwa yaani Loho inauma sana Wagabho.
 
Wengi wa wafanyabiashara wamegoma nchi nzima na moja ya ajenda yao ni ukaguzi wa risiti za EFD zisitishwe mara moja. Mimi ni mwananchi wa kawaida kabisa na asilimia 95 ya wafanyabiashara wa nchi hii hawatoi risiti halali.

Pale unaponunua bidhaa ukiomba risiti toka kwa mfanyabiashara ni mgogoro na utaambiwa mashine ni mbovu ooh nikupe risiti iliyo na upungufu wa fedha uliyotoa n.k. Ukikomaa watakuona wewe siyo mtu wa kawaida. Kwa nini ninyi wafanyabiashara hamtaki kutoa risiti halali kwa bidhaa aliyonunua mteja?

Maduka machache yanayotoa risiti halali ni kama ALAF na maduka yanayosimamiwa na wazungu. Wahindi ndo wamekuwa wajanja kupitiliza na mara anakudanganya nikikuuzia bei hii sitakupa risiti kwa sababu tayari nimekupunguzia kumbe ni upuuzi mtupu.

Ndugu zangu nchi inajengwa na wananchi wenyewe, TOENI RISITI YA EFD na wananchi DAINI RISITI HALALI YA EFD.
Utitiri wa kodi, tozo ndio unakwaza wafanyabiashara. Jaribu kuanzisha biashara uyaone. Umesema vyema kabisa kuwa "nchi inajengwa na wananchi wenyewe" lakini jee viongozi wa nchi hii nao ni sehemu ya wananchi? Mbona wanaishi maisha ya kifahari sana? Kama ni kubanana hata posho za wabunge zikatwe kodi na kikokotoo kiwapitie pia.
 
Hao wafanyabiashara wakwepaji wakubwa wa kodi tu hamna lolote.
Mlipa kodi number moja nchini ni mfanyakazi.

Kitu kinakatwa 18% to 30% kwa mshahara wake.

Akienda kununua bidhaa yoyote kwa mshahara wake huo huo anakutana na kitu kingine 18% VAT.

Nipo upande wa TRA; though kuna muda mwingine na wao serikari walizipata hizi hela hebu wapunguze anasa basi maana na sisi walipa kodi roho zinatuuma.
 
Wengi wa wafanyabiashara wamegoma nchi nzima na moja ya ajenda yao ni ukaguzi wa risiti za EFD zisitishwe mara moja. Mimi ni mwananchi wa kawaida kabisa na asilimia 95 ya wafanyabiashara wa nchi hii hawatoi risiti halali.

Pale unaponunua bidhaa ukiomba risiti toka kwa mfanyabiashara ni mgogoro na utaambiwa mashine ni mbovu ooh nikupe risiti iliyo na upungufu wa fedha uliyotoa n.k. Ukikomaa watakuona wewe siyo mtu wa kawaida. Kwa nini ninyi wafanyabiashara hamtaki kutoa risiti halali kwa bidhaa aliyonunua mteja?

Maduka machache yanayotoa risiti halali ni kama ALAF na maduka yanayosimamiwa na wazungu. Wahindi ndo wamekuwa wajanja kupitiliza na mara anakudanganya nikikuuzia bei hii sitakupa risiti kwa sababu tayari nimekupunguzia kumbe ni upuuzi mtupu.

Ndugu zangu nchi inajengwa na wananchi wenyewe, TOENI RISITI YA EFD na wananchi DAINI RISITI HALALI YA EFD.

..serikali nayo ipunguze anasa, ufisadi, matumizi mabaya ya kodi.
 
Kodi mnakusanya sawa ila mnazipeleka wapi??

Huduma mbovu 80% kwenye ofisi za umma na mambo ya kijamii.

Niliwahi kutembelea nchi za Scandivania , wana kodi kubwa ila matokeo ya kodi yanaonekana.

Mara ngapi majizi yanatajwa na CAG ila hakuna hatua, nani kafungwa kutokana na report ya CAG?

Serikali ionyeshe mfano kodi zikusanywe ila zirudishe huduma kwa wananchi sio kununua magari ya thamani na kugharamia msafara safari za nje kwenda kukopa.
 
Kodi zingekuwa zinatumika ipasavyo watu wote tungekuwa tunahamasika kulipa Kodi na kuwashughulikia wale wanaosingizia mashine ni mbovu au kukuandikia risti isiyoe ndana na gharama uliyonunulia. Tatizo linakuja anayelipa Kodi mwingine(mwananchi mlala hoi na anayetumbua Kodi zetu ni chura na genge lake la msoga).safi sana wafanyabiashara kuwa kukataahuu uhuni wa hii serikali ovu
 
Back
Top Bottom