Pamoja na ukuta mrefu na JWTZ kulinda Mererani, nani bado wanaiba madini yetu?

Pamoja na ukuta mrefu na JWTZ kulinda Mererani, nani bado wanaiba madini yetu?

Nimemsikia jana Mhe Rais Samia Suluhu Hassan akisema kua madini yanatoroshewa chini na wakikamatwa wanakimbilia kuonyesha jiwe kubwa la madini, najiuliza pamoja na security yote hii ni kina nani waliendelea kutuibia madini yetu?

Maana yake ule ukuta hauna maana zaidi ya kupoteza fedha la walipa kodi kugharamia kuujenga ukuta huo. Imetumika nguvu badala ya akili kulinda yale madini na kututia hasara kubwa nb ila sababu. Hili jambo limeshangaza na kama kuna watu wanapinga hili yawezekana nao ni wapigaji.

Suala liingine la kuuliza, ni kwanini wakati wa utawala wa JPM hawakusema kabisa madini yanaendelea kutoroshwa na badala yake walibaki kusifia kua pato la madini limeongeza na maripoti yao.

Nani anaiba Madini yetu Mererani?
Kwani JWTZ sio watu,hao ndio wezi wenyewe
 
KAMA JIWE ANGEAMBIWA KUWA INGAWA ALITUMIA GHARAMA NYINGI KUJENGA UKUTA NA KUTOA SIFA NYINGI KWA JESHI KWA KULINDA MIGODI YA TANZANITE LAKINI MADINI BADO YALIKUWA YANAIBIWA ANGEONEKANA MJINGA NA HILO LISINGEMPENDEZA MPENDA SIFA YULE!!! ANGEWAKA MOTO!!
Watanzania wengine hamjui hata mnataka nini.Yakiibiwa mbapiga yowe yakipunguzwa kuibiwa mnapuga yowe hopeless kabisa

hatua za Magufuli zimesaidia kuokoa maisha ya wachimbaji wengi na wauzaji madini na kuwasaidia wengi kupata bei nzuri
Wengi walidhulumia na kuuawa wakiuza madini vichochoroni .Visa vya kuuana sababu ya kudhulumiana nk vilikuwa vingi.

wewe fikiria unapata madini ya bilioni 3 halafu unadanganywa kuwa kuna mhindi yuko uchochoro fulani ananunua kwa bilioni 10 unaenda na madini yako wanakukaba wanakupora na hata kukuua pesa hupati na madini yameondoka

Sasa hivi kama mtu anacheza huo mchezo ni at their risk.Serikali imewawekea miundombinu kuanzia ya ulinzi hadi soko hayo mengine ya kwao wakiporwa na kuuawa shauri yao
Ila kwa wengi utaratibu wa serikali unasaidia .Hata wewe ukipata madini peleka tu soki la madini ni Risk kubwa kuuziana vichochoroni .Roho uwe tayari kuiweka rehani
 
Alexander Mnyeti amenunua TCC Club ikiwa ni biashara nyingine baada ya ile ya Gwambina FC
 
Kwanini ule ukuta usiende chini zaidi kupita hayo matundu ya mahandaki
Waulize wa Israel [emoji1134] kwamba ule ukuta wao waliojenga kule Gaza umeweza kuzuia zile tunnels za wapalestina? Yaani hata kama msingi wa ukuta zege lingeenda mita 2 chini bado wakulungwa wangechimba beyond that...
 
Hamna watu Wapigaji kama Wajeda, kuna kamradi kamoja hivi niliwahi kusimamia na bahati nzuri au Mbaya hako kamradi karikuwa kanapita ndani ya eneo la Jeshi , sasa bwana ilikuwa kasheshe, mara uitwe Officini na mkuu wa Kambi mara hichi mara kile, lkn kiufupi tu asee tuwe wakweli, hata hao mnaosema sijui walinzi nao ni binadamu, hela ni hitaji la kila mmoja wetu.
 
Ninyi mna amini kabisa ukuta ndio unaweza kuzuia madini kupitishwa? kwani madini ni gari kusema ukifunga geti haliwezi kupita?

Tujifunze hata kwa private entities kama GGM kule kuna ulinzi mkali sio wa kawaida, na security checks za kutosha, bado wakuu wakijipanga vizuri wanapiga mzigo hapa na pale (japo kwa uchache)

Labda atusaidie 24/7 kinachofanyika huko mererani ni kipi, eti tweenty4seven hebu tupe habari za huko basi, kina nani wanafanya haya?
Hahaa hakuna uwizi wowote kuna mtu kamlisha maza maneno hayo,shida maza nae kuchwani ni mweupe yupoyupo tu..huyo jamaa anataka kurudi kitalu C kwa mgongo wa maza...ni yule mrangi aliekua anaendesha huo mgodi kwa kuiba mawe n kukwepa kodi,hakuna shimo lolote linalotoka nje ya ukuta.
Waziri dotto ameshampa majibu maza kua huo hussein ni kibaka hafai kuitwa mwekezaji
 
Baadhi ya wachimbaji ndio wanatorosha madini kutumia mahandaki waliochimba chini kwa chini kutoka ndani ya migodi yao na kutokomea kusikojulikana.

Kwa kifupi, watanzania wanawaibia watanzania.
Wewe unayeongea hivi hata mirerani hujawahi fika. Hicho kitu unasema hakiwezekani.. acheni kuleta fantasy zenu hapa
 
Wewe unayeongea hivi hata mirerani hujawahi fika. Hicho kitu unasema hakiwezekani.. acheni kuleta fantasy zenu hapa
Mama mwenye aliyasema mchana kweupe mbona hamkumpinga? Kwani kuchoma njia za chini ya ardhi ni kama kwenda sayari nyingine? Jeshi tumefanya sana haya, kule gaza watu wanachimba kila siku.
 
Wewe unayeongea hivi hata mirerani hujawahi fika. Hicho kitu unasema hakiwezekani.. acheni kuleta fantasy zenu hapa
Tukiwa Sekondari wakati wa vita vya nduli Iddi Amin mwaka 1978, tulichimba mahandaki kwa zana duni. Sembuse ya leo na teknolojia hii?
 
Hamna watu Wapigaji kama Wajeda, kuna kamradi kamoja hivi niliwahi kusimamia na bahati nzuri au Mbaya hako kamradi karikuwa kanapita ndani ya eneo la Jeshi , sasa bwana ilikuwa kasheshe, mara uitwe Officini na mkuu wa Kambi mara hichi mara kile, lkn kiufupi tu asee tuwe wakweli, hata hao mnaosema sijui walinzi nao ni binadamu, hela ni hitaji la kila mmoja wetu.
Mradi Gani toa story Mr
 
Nimemsikia jana Mhe Rais Samia Suluhu Hassan akisema kua madini yanatoroshewa chini na wakikamatwa wanakimbilia kuonyesha jiwe kubwa la madini, najiuliza pamoja na security yote hii ni kina nani waliendelea kutuibia madini yetu?

Maana yake ule ukuta hauna maana zaidi ya kupoteza fedha la walipa kodi kugharamia kuujenga ukuta huo. Imetumika nguvu badala ya akili kulinda yale madini na kututia hasara kubwa nb ila sababu. Hili jambo limeshangaza na kama kuna watu wanapinga hili yawezekana nao ni wapigaji.

Suala liingine la kuuliza, ni kwanini wakati wa utawala wa JPM hawakusema kabisa madini yanaendelea kutoroshwa na badala yake walibaki kusifia kua pato la madini limeongeza na maripoti yao.

Nani anaiba Madini yetu Mererani?
Usishangae mtu aliye kwisha kumwaga damu lazima awe na wenge
Hayo uliyo yasikia ni wenge limewapata baada ya kuchukua nchi mikononi mwa jembe letu
 
Back
Top Bottom