Pamoja na usomi wangu siachi matambiko na mila ng'oo

Pamoja na usomi wangu siachi matambiko na mila ng'oo

Mkuu wangu nimekupata vema sana aisee umenikumbusha
singer John Lenon alikua anasisitiza hiki kitu kua yeye ndie Mungu na anaamini katika yeye wengi miaka Ile walimwona Atheist mkubwa na mtu aliyekufuru ila alikua sahihi sana na ndio maana ukisikiliza nyimbo zake nyingi Kama Imagine na God zinafungua sana akili ndio maana FBI walimfwekelea mbali maana alikua moto!
Itabidi nitafute nyimbo za huyu jamaa john lenon, sijawahi kumsikia. Thanks
 
Itabidi nitafute nyimbo za huyu jamaa john lenon, sijawahi kumsikia. Thanks
mtafute na msikilize huyu nguli aliyekua Member wa kundi la muziki la The Beatles
Utaona mambo mengi ya kuifungua ubongo halafu utanipa mrejesho hasa sikiliza wimbo unaitwa God na imagine!
 
Mungu ni mmoja tu anayeishi...usipotoshe umma ndugu.

Mungubwa Ibrahim Yakobo na Isaka ndiye MUNGU pekee wa kuabudiwa hapa ulimwenguni...kila ulitajapo jina lake mambo hutokea ni msikivu na mwenye rehema kuu ya milele na milele.
 
Kila mtu abaki vile anavyoamini
Mbona nyie mkihubiri hamtaki kuambiwa kila ktu abaki na anavyoamini?? Tulieni muambiwe ukweli dini zenu zivuliwe nguo. Mbona nyie mnaitukana hadharani mzimu ya baba na babu zetu hadharani na kuiita mapepo mashetani??

Ila nyie mkipewa za uso mnakimbilia kuomba yaishe[emoji3]
 
Mimi na uislam wangu, na uchaga wangu, na usomi wangu siachi matambiko

Huu ndio ukweli unaotusumbua watu weusi, Wazungu wana dini yao, Waarabu wana dini yao, Wahindi wana dini yao, Wachina wana dini yao, na wanaziishi dini zao, ila cc waafrika tulizikataa dini zetu.

UPOTOSHAJI KUHUSU MIZIMU YA KIAFRIKA NA WAAFRIKA JUU YA UTUMWA WA FIKRA

UPOTOSHAJI KUHUSU MIZIMU


Sina haja ya kutoa salam. Kwani najua wengi hampo salama.

Nimeamua kuleta mada hii tata ili kuwafumbua macho walio wengi. Kwanza nakiri kwamba ukweli unashangaza sana. Truth is stranger tha finction. Asilimia 75% ya watu weusi ni watumwa.

Mizimu ni roho za watu ambao ni ndugu zetu waliokufa ambao wamekuwa trapped in 4th dimension na binadamu wa kawaida tupo third dimension. Wao ndio viumbe wa karibu na sisi sana ukizingatia kuna nine dimensions ulimwenguni. Wote sisi ni wasafiri. Na mwisho wa safari yetu ni tisa.

Wengi wa watu weusi wana laana ya asili kwa sababu ya utumwa wa fikra. Lakini silazimishi mtu akiamini kile nachotoa hapa. Kwani wengi wamekuwa trapped by by the matrix system.

Kila jamii zilizo tuzunguka zina miungu yao. Mfano wayahudi (waisraeli) wana mungu wao wa musa aliyetajwa kitabu cha mwazo. Wanasema ni mungu wa haki. Amesemwa ni mngu wa haki kwani ameweka sheria na adhabu kali kwa mwanadamu. Na mungu wa waisraeli ni mungu wa Time (muda) ambaye ameumba vitu. Sikatai.

Pili kuna mungu wa agano jipya chini ya yesu ambaye ni mungu wa upendo. Mungu huyu yupo na anaabudiwa na warumi( warumi ndio wazungu wa sasa hivi au roman empire)

Mungu wa waisraeli, warumi na waarabu ni mungu wa muda hata ukisoma vitabu vyao kila saa wanajisifu wao ndio wana control time.

Kila jamii za kidunia zina miungu yao mfano wahindi wana mungu brahma, kali, vishu na krishna nk., wachina wana budha pamoja na wajapani na watu wote wenye asili ya macho madogo mungu wao ni sanamu lenye tumbo kubwa linaitwa budha.

Waarabu mungu wao ni allah ambaye anawakiliswa na jiwe lipo maka linaitwa black stone jiwe jeusi ambalo lipo al kaba jiwe hilo lilishuka duniani toka kipindi cha adamu na hawa na watu wakienda kuhiji wanalibusu na kusujudia jiwe hilo kwa kulizunguka mara saba. Jiwe hilo linaitwa hajr al aswad.

Ni ibada ya kuabudu sanamu lakini waislamu wengi hawajui ukweli huu. Ndo mana wanipagana vita na kuwauwa watu weusi wenzao kwa makundi kama boko haramu na al shabab. Ni sawa na mawe yanayotumiwa kuchonga sanamu la yesu wa wakrito wakaliabudu. Haina tofauti wote waislamu na wakristo wote wanamuabudu Saturn au Kronos ndo mana waslamu wanaamini biblia ni kitabu cha mungu ambaye ni saturn katika nguzo zao za imani. Nasisitiza mungu wa wakristo ni Saturn pamoja na waislamu ili ujuwe huu ukweli lazima uwe INITIATE. Kawa wewe sio INITIATE utaishi kutoa sadaka na sijda.

Kronos Ndio mungu wa waislamu na wakristo. Na nguvu zake sio kamili kwani mungu halisi hatoi adhabu wala hataki kunyenyekewa ni mungu wa upendo haijalishi unafanya mabaya au hapana yeye yupo tuu wala hawezi kuhukumu kitu. Duniani tupo kwaajili ya kujifunza hivyo hakuna zuri wala baya. Inategemeana na tafsiri ya kile unachokiona nikzuri kwako kinaweza kuwa kibaya kwa mwenzako.

Kwa sasa kuna mawakala wengi sana makanisani na kisikitini wakiwaaminisha kuwa mizimu ni roho chafu za kuzimu ilihali wakijuwa wao wamepokea shahada za ki freemason ambazo ni ibqda za wazungu na hii ipo katika historia ya mqmbabu zao kwamba ndio asili yao wazungu. Wanawatoa watu weusi wenzao katika ukweli ili kulinda maslahi yao ya kidunia.

Wanachofanya hawa watu wazungu ni kututoa katika asili yetu na sisi kufata mambo yao.

Mzimu ni baba au mama yako aliyekufa je baada mzazi wako akifa utamchukia au utamkumbuka kwa wema aliokufanyia kwa malezi mpaka hapo ulipo fika.? Baba na mama yako nao wana wazazi wao ambao nao walisha tangulia mbele za haki mlolongo unaendela hivo. Lengo la ibada ya mizimu ni kutoa shukrani kwa walio tutangukia kwani wao wanatuona ila sisi hawatuoni ila sio kuwa abudu. Kuna tofauti ya kutoa shukranu na kuabudu mfano kujenga kaburi la ndugu au jamaa ni kuonyeaha shukrani fulani.

Wanachofanya watu wa dini mfano wakristo na waslamu kupiga vita mizimu hasara yake hutaiona hapa duniani na pindi utakapo kufa utawakuta ndugu zako na ma bibi na mababu zako ila hawata kupokea kama sehemu yao kwani wakati upo duniani uliwadhihaki na kuwa adui kwao.

Mizimu wanachotaka ni kuwa na hisia za kibinadamu kutowa sadaka mbali mbali kwao ikiwamo za wanyama kwani huwa wametuzunguka na mkikutana kama ukoo huwa wapo na hupenda.

Mizimu inapenda pombe maji au wanyama wanaochunjwa kwa hesma yao kwani ndio life style ya mwanadamu toka enzi watu wanakunywa pombe. Kwa vitu hivo unatengeza conection ya mafanikio yako hapa duniani na ukifa utakuwa na watu watakao kupokea. Ukifa unaenda sehemu ya ugenini lazima uwe na wenyeji walio kutangulia.

Kama ulivyo zaliwa hapa duniani ukapokewa na wazazi wako na ndugu zako na pia utakapo kufa jua kuna wenyeji ambao walisha kutangulia ambao watakupokea. Je hao wenyeji uliwafanyia jambo gani la maana kuonyesha heshima kwao. Wakati bila wao wewe usinge weza kuzaliwa. Kumbuka marehemu babu yako na bibi yako ndio walizaa wazazi wako ambao unawapenda. Na wazazi wako wana wazazi wao ambao wana wapenda na kuwakumbuka cheni ni ndefu sana kurudi nyuma mpaka wewe ukawepo hapo ulipo daganywa na stori za biblia ya warumi na kurani ya waarabu.

Dini zote ambazo mnaziabudu zote zililetwa na watesi wetu na kuwachukua babu na bibi zetu kama watumwa na wameua watu weusi wengi sana. Alafu leo unajifanya mlokole au mkristi safi au muslam safi jua unajidanganya na unaungana na maadui za wazee wetu na kusahau mila.

Ukoo hauishi, kama ulivyo pokelewa hapa duniani na wazazi wako utapokelewa na ahera na mizimu ya waliokutangulia kama ulikuwa unawatoa katika jina la yesu ndonutajua sasa utakapo ishia na mtu akifa kinachobakiwa nae ni kumbukumbu za maisha yake.

Watu weusi ni watumwa wa fikra za historia ipo wazi kuwa tulijishusha chini na kupokea tamaduni za watu wengine hasa waarabu na wazungu. Ili tufanikiwe gundueni tatizo lipo wapi kwanini tuna mali zote lqkini hatuna baraka tupo katika lindi la umaskini na kusalitiana?

Mfano wa wazi ni filamu ya vikings ambapo ragnar alisahau mizumi ya asili kwao kwa kupokea ukristo na mizimu ikamsahau. Ile filamu ni kwaajili ya kutoa fundisho usisahau ulipo toka.

Mimi siabudu mizimu ila natoa shukrani kwa wazee wangu wote waliotangulia mbele za haki ambao bila wao nisinge weza kuzaliwa na baba na mama yangu kwa kutia sadaka ya denge au maji au chochote nachotaka. Kuna mahali nimwekea alter maalumu ila hakuna anaye ishi hapo porini. Ila kwakuwa najua mizimu ipo na mimi inajua nachofanya.

Ombi langu kwako usigombane na mizimu ya watangulizi wako kwani huwezi jua kama wao ni mizimu huenda na wewe ukawa mzimu pia ila ukiwa mzimu wenye maaadui upande wa pili itakuwa ngumu kwako.

Heshimuni tamaduni zenu tukutane mwezi 12 nyumbani. Kuwa kwako mkristo autimatiki unaona waslamu wanaenda motoni wahindi wanaenda matoni na wayahudi pamoja na watoa shukrani kwa mizimu hii ndo mentality wa matrix wana kuwa na Ego kwamba wao dini yao ndo ya haki na wengine wapo dini ya uongo kumbe wote wamepotea.

Wewe unapokesha kumsifia mungu wa waisraeli usije kudhani eti baraka zinakujua kwako hapana zinaenda kwa waisrael na vilevile unavyo msalia mtume na allah baraka zote zinaenda kwa waarabu ndo mana mtu mweusi ni maskini wa mali akili na fikra.

Elimu hii sio ya ku google ni urithi wangu niliopewa. hivo usije kuniambia uislamu au ukristo ni dini ya haki nikikuomba ushahidi ukaniletea maneno kwa biblia imesema au qurani imesema wewe ulikuwepo au wewe ni mwarabu au mrumi.?
Nimesoma, bandiko hili kuna ambayo nina kubaliana nayo moja kwa moja, kuna mengine nataka kuuliza kidgo.

Kuabudu ni nini??, Hawa miungu ya mataifa mengine yanaabudiwaje?
Umesema mizimu tuipatie shukran, Kwanini tusiishi nao kwa upendo, na kuwashukuru wakiwa hai badala ya wakiwa wafu?

Umesema mizimu ni roho za watu walio trapped ktk dimensions ya nne, Kwanini wameshindwa jinasua hapo? Kuwa trapped means uwezo wao una kikomo na ukomo, je, kipi chema ku deal mwenye uwezo mwenye ukomo au asiye na ukomo? Mizimu wanapenda penda pombe , tunawachinjia mbuzi ,tunatoa zawadi ambazo wangekuwa ktk dimensions ya tatu zingewafaa sana, why tuwape zawadi za pombe wakat wao ni wafu ,wafu wanalewa? na kusikia njaaa?? Kwanini hizi zawadi tusiwape ambao bado wapo ktk dimension hii kama njiaa ya kuwapa shukran na furaha uson,ili akifa aende na picha ya upendo kutoka kwetu??

Naungana nawe ktk bandiko lako naomba kujibiwa
 
IMANI ni kuw na uhakika na mambo yatabiriwayo ni bayana na mamb yasiyoonekana,🎯
 
Kiongozi nimekuelewa vizuri sana na hongera kwa kupata ufahamu huo,mila inaua ila dini aiuwi
Mungu wako kaua mamilioni ya watu kwenye biblia.

Huyo mwingine kaua wengi kwenye quran.

Hadi leo ukifa anakuchoma kwa sababu tu ya ugomvi wake na shetani. Kwa nini asikuadhibu shetani anayempotosha mwanadamu wakamalizana wao, badala yake aje kukuchoma wewe?

Naona wewe huelewi unachokiabudu.
 
Ila usiende na watoto wako waache wafike umri wa kujitambua ndio uwaambie matambiko waaingie wenyewe.

Kifupi weww ni mpumbafu unaejidai kujua kafie mbele wewe kama wewe watoto waache hujui kuhusu hayo mambo uko mjinga na gizani sana.
Wewe watoto wako umewaacha wafikishe miaka 18 ndo ukawapeleka kanisani au msikitini??
 
Ungejua kisa cha yeye hadi kuacha kuwatumia majini usingesema hivyo.
Kuna Kazi yenye hela duniani kuliko uganga,maana mganga kuwa na bilioni moja ni kitu cha kawaida tena mganga wa level ya chini tu.
Kama mtu anaamua kuacha utajiri wote na kumfuata Mungu utasema vipi anataka sadaka
 
Huyu ni Learner mwambie akasome 1Samuel 28 ili ajue mzimu ni.nini
Huyo alikuwa na degree za uchawi anamjua shetani nje ndani na anamjua Mungu nje ndani utasemaje ni student,ameuishi uchawi.
Hio Samwel nenda hadi 31.
 
Mungu ni mmoja tu anayeishi...usipotoshe umma ndugu.

Mungubwa Ibrahim Yakobo na Isaka ndiye MUNGU pekee wa kuabudiwa hapa ulimwenguni...kila ulitajapo jina lake mambo hutokea ni msikivu na mwenye rehema kuu ya milele na milele.
Kwendra
 
Nimesoma, bandiko hili kuna ambayo nina kubaliana nayo moja kwa moja, kuna mengine nataka kuuliza kidgo.

Kuabudu ni nini??, Hawa miungu ya mataifa mengine yanaabudiwaje?
Umesema mizimu tuipatie shukran, Kwanini tusiishi nao kwa upendo, na kuwashukuru wakiwa hai badala ya wakiwa wafu?

Umesema mizimu ni roho za watu walio trapped ktk dimensions ya nne, Kwanini wameshindwa jinasua hapo? Kuwa trapped means uwezo wao una kikomo na ukomo, je, kipi chema ku deal mwenye uwezo mwenye ukomo au asiye na ukomo? Mizimu wanapenda penda pombe , tunawachinjia mbuzi ,tunatoa zawadi ambazo wangekuwa ktk dimensions ya tatu zingewafaa sana, why tuwape zawadi za pombe wakat wao ni wafu ,wafu wanalewa? na kusikia njaaa?? Kwanini hizi zawadi tusiwape ambao bado wapo ktk dimension hii kama njiaa ya kuwapa shukran na furaha uson,ili akifa aende na picha ya upendo kutoka kwetu??

Naungana nawe ktk bandiko lako naomba kujibiwa
Jiulize hivi mkuu......Wachina wanaabudu kivyao, wazungu wana wao, wahindi wana wao, waarab wana wao, Africa jee?........ hujiulizi tu?......
 
Back
Top Bottom