Pamoja na usomi wangu siachi matambiko na mila ng'oo

Pamoja na usomi wangu siachi matambiko na mila ng'oo

Ila usiende na watoto wako waache wafike umri wa kujitambua ndio uwaambie matambiko waaingie wenyewe.

Kifupi weww ni mpumbafu unaejidai kujua kafie mbele wewe kama wewe watoto waache hujui kuhusu hayo mambo uko mjinga na gizani sana.
Mbona povu..jibu hoja acha kutukana esta.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mizimu ni shetani kuvaa sura au uhusika wa wazee wa ukoo.
Roho ikifa haibaki duniani either kuzimu au peponi ikisubiria siku za hukumu.
Ibada ni sehemu mbili either kwa Mungu au Shetani.
Uliiona roho iko mbinguni??

#MaendeleoHayanaChama
 
Akili ya mtu inawezwa ikashindana na elimu na dini na ikashinda hivyo hatukushangai. Kuna watu wamesema kweri kweri lakini nature yao imeishinda hiyo ilimu yap
 
Dini ni mfumo.
Mfumo wa kumtafuta Mwenyezi Mungu.
Mungu ni mmoja hakuna Mungu tofauti na yule alieumba ulimwengu tunaoishi.
Na pia shetani yupo, anaishi ndani ya kila mmoja kama ilivyo Mungu anaishi ndani yetu (Twin souls), a very complicated phenomenon na inahitaji kujifunza ili kuweza kulithibitisha hilo.
Na pia katika kujifunza nimefahamu ya kuwa kifo sio mwisho wa safari, kwamba.. sasa ndio unaenda kukutana na Mungu kama wengi wanavyo amninishwa. Ukifa unaingia kwenye dimension ya juu na unakuwa na nguvu kubwa za kiroho, na utaweza ku interact na dimension ya chini uliyotoka kama ulikuwa na uwezo mkubwa wa kiroho wakati unakufa. So hii inatoa maleezo juu ya lile swala la kuwaomba ma babu/wazee wa jadi waliotangulia ili waweze kutoa hint/muongozo juu ya jambo fulani, lakini haimaanishi kuwa ndio tunatakiwa tuwaabudu wao.
Kila jamii ilikuwa na mfumo waliouamini katika kumuomba Mungu. Waafrika tulikuwa na dini zetu, wazungu dini zao, wachina, wahindi etc. Kilichotokea ni kwamba tuliaminishwa na walio tutawala kuwa dini zetu sio sahihi, tuliaminishwa kuwa mababu zetu na wazee wetu wa jadi walikuwa wakiabudu miungu/mashetani. Isingekuwa rahisi kututawala kama wasingefuta kile tunachokiamini.


Kuhusu Jesus Christ:
Kuna kitu watu wanachanganya sana. Na kuna ambao mpaka leo hudhani ya kwamba 'Jesus Christ' ni jina la myuda aliyeishi nyakati hizo kama ilivyo kawaida ya mtu kutambulika kwa majia mwili.
Uhalisia ni kwamba 'Christ' is not a person, 'Jesus' was a person. Christ ni jina lingine la God Christos, likimaanisha the Fire God.
Jesus-Iesus-Zeus aliitwa 'Jesus Christ' baada ya ku_incarnate the cosmic christ.
Christic principle ipo kwenye kila dini ingawa wengi hawalifahamu hilo, na ndio maana tunasema wote tuna muabudu Mungu mmoja.
Hakuna tofauti kati ya Chriatian priest na Mohammedan priest, wote wapo kwenye kapu moja. Vivyo hivyo kwa waafrika, wachina, wahindi, wagiriki, egyptians etc. Christ is cosmic and universal!

Kwa
Egyptians, Christ alikuwa Osiris.
Hindus, Chrishna ni Christ.
Chinese, Fu Hsi ni Christ.
Greeks, Christ anaitwa Zeus, Jupiter the father of Gods.
Germanic edda, Christ ni Balder.
Afrika pia naskia tulikuwa tuna black Christ ingawa sijafanikiwa kufahamu alifahamika kwa ma/jina gani. Na hapa ndipo naiona nguvu ya wakoloni walio tutawala, walipambana kuhakikisha wanatuacha wakavu! Wakavu kiuchumi, wakavu kimaarifa na mbaya zaidi wakavu kiimani!
That's why utakuta mpaka leo tunajifunza maarifa ambayo yanakuwa ni magumu kuendana na uhalisia wetu. Utakuta leo mtu anajifunza chinese meditation kesho kutwa ana recite krisha mantra yaani inakuwa ni vurugu tupu. Sipingani na watu kujifunza maarifa tofauti yenye manufaa, ila nadhani kuna tofauti kubwa ya matokeo kwa wewe utakaye recite 'krisna mantra for success' na yule atakaye enda kijiji kwa babu zake kuomba msaada pale alipo kwama.
All in all we have free will, kila binadamu ana uhuru wa kuchagua kipi kinamfaa.

Jesus Christ.PNG

Hiyo hapo juu ni image pekee yenye uhalisia kuhusu muonekano wa Jesus Christ kwa wale wanaoamini katika Yesu alietokea kwenye kabila la Yuda, na ilipatikana baada ya Sultani wa uturuki kuikabidhi kwa pope Innocent VIII kama ransom ili kaka yake aliyekamatwa na wakristu wa miaka hiyo aweze kuachiwa.
 
Mungu akusaidie umjue Yesu ili uekwepe moto wa milele
Soma kwanza na ujifunze kwa nini Waisrael na wayahudi sio wakristo na hawamkubali Yesu wakati mnasema alizaliwa kule na wao ndio ndugu zake kabisa. Yaani ni babu yao kabisa. Wewe Kalimanzila kutoka Kigoma ndo unajidai unamjua sana Yesu na atakukomboa[emoji3][emoji3]


Waafrika hebu tuache uzwazwa
 
Dini ni mfumo.
Mfumo wa kumtafuta Mwenyezi Mungu.
Mungu ni mmoja hakuna Mungu tofauti na yule alieumba ulimwengu tunaoishi.
Na pia shetani yupo, anaishi ndani ya kila mmoja kama ilivyo Mungu anaishi ndani yetu (Twin souls), a very complicated phenomenon na inahitaji ku
Hiyo picha uongo..

#MaendeleoHayanaChama
 
Kabla sisoma chochote naami maisha yko ni mazuri baada ya kulitambua hilo na kulifanyia kazi...watu wanataka waganga wa kuwapa utajiri lkn wanashindwa kufanya vitu vdogo kama matambiko ambayo ndio ufunguo mkubwa wa mafanikio
 
Kabla sisoma chochote naami maisha yko ni mazuri baada ya kulitambua hilo na kulifanyia kazi...watu wanataka waganga wa kuwapa utajiri lkn wanashindwa kufanya vitu vdogo kama matambiko ambayo ndio ufunguo mkubwa wa mafanikio
Nahitaji maelekezo ili mwaka huu na mimi nianze rasmi..kila siku hua naamini katika mila zetu sema nmekuta kizazi tayari kiko brainwashed na hizi dini za kuja..nisaidie pa kuanzia.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nahitaji maelekezo ili mwaka huu na mimi nianze rasmi..kila siku hua naamini katika mila zetu sema nmekuta kizazi tayari kiko brainwashed na hizi dini za kuja..nisaidie pa kuanzia.

#MaendeleoHayanaChama
Nenda kijijini kwenu tafuta wazee wa kimila waeleze dhumuni lako... lkn pia anza kuwatembelea ancestors wako na kujenga ukaribu nao
 
Mimi na uislam wangu, na uchaga wangu, na usomi wangu siachi matambiko

Huu ndio ukweli unaotusumbua watu weusi, Wazungu wana dini yao, Waarabu wana dini yao, Wahindi wana dini yao, Wachina wana dini yao, na wanaziishi dini zao, ila cc waafrika tulizikataa dini zetu.
Hapa ndo Waafrika tunakosea kabisa. Tunajidai kujua wakati hatujui. Mtu unaamka tu unawaza vitu kichwani ,unaviandika na unataka tuvifuate
Angalau ungefanya utafiti kuhusu unachokiita mizimu ya kiafrika walau utupe sample uliyotumia kufikia conclusion.
Umeishia tu kushambulia imani za watu. Kama imani yako ni bora kuliko zingine, ungeonyesha ni wangapi wamefanikiwa na walifanyaje
Imani nyingi za kiafrika ni za kinafiki,kuoneana kijicho na wivu na kulogana pia
Mizimu ni majini/mashetani. Kutoa kafara ni kulisha mizimu. Haiwezekani mtu akishakuwa marehemu ndo awe na nguvu ya kutuletea mafanikio , mtu ambaye alifariki bila hayo mafanio yoyote. Leo afe aitwe mzimu atuletee utajiri.
Narudia tena ,mizimu ni mahetani wanajifanya ni ndugu zetu waliokufa
Rejea shetani alichosema kwa Yesu, kuwa mali na fahari ni mali yake ,ukimsujudu unapewa mali. Kwa hiyo ukitoa kafara ,hiyo ni umemsudu shetani ,atakuzawadia mali
Fanyakazi kwa bidii huo ndo utajiri halali unapatika
 
Mkuu endelea kuwa na imani yako,ila hivi hujiulizi kwanini watu ambao wanaishi maisha yao ya asili ndo wanaishi miaka mingi mtu kanisa halijui maombi anaomba babu zake na mungu anambariki
 
Shida ni watu kuchanganya dini. Mkristu au Muislamu lakini hapohapo kavaa hirizi au anatambika. Ni vema mtu akafuata dini moja tu, au ya kimila au ya kuletwa.
 
Shida ni watu kuchanganya dini. Mkristu au Muislamu lakini hapohapo kavaa hirizi au anatambika. Ni vema mtu akafuata dini moja tu, au ya kimila au ya kuletwa.
Wakristo wanakatazwa kuombea wazee wao..ila kutwa kuombea wazee wa kizungu kwa mlango wa watakatifu..hapa kiukeli tulipigwa pakubwa


#MaendeleoHayanaChama
 
Mimi na uislam wangu, na uchaga wangu, na usomi wangu siachi matambiko

Huu ndio ukweli unaotusumbua watu weusi, Wazungu wana dini yao, Waarabu wana dini yao, Wahindi wana dini yao, Wachina wana dini yao, na wanaziishi dini zao, ila cc waafrika tulizikataa dini zetu.

UPOTOSHAJI KUHUSU MIZIMU YA KIAFRIKA NA WAAFRIKA JUU YA UTUMWA WA FIKRA

UPOTOSHAJI KUHUSU MIZIMU


Sina haja ya kutoa salam. Kwani najua wengi hampo salama.

Nimeamua kuleta mada hii tata ili kuwafumbua macho walio wengi. Kwanza nakiri kwamba ukweli unashangaza sana. Truth is stranger tha finction. Asilimia 75% ya watu weusi ni watumwa.

Mizimu ni roho za watu ambao ni ndugu zetu waliokufa ambao wamekuwa trapped in 4th dimension na binadamu wa kawaida tupo third dimension. Wao ndio viumbe wa karibu na sisi sana ukizingatia kuna nine dimensions ulimwenguni. Wote sisi ni wasafiri. Na mwisho wa safari yetu ni tisa.

Wengi wa watu weusi wana laana ya asili kwa sababu ya utumwa wa fikra. Lakini silazimishi mtu akiamini kile nachotoa hapa. Kwani wengi wamekuwa trapped by by the matrix system.

Kila jamii zilizo tuzunguka zina miungu yao. Mfano wayahudi (waisraeli) wana mungu wao wa musa aliyetajwa kitabu cha mwazo. Wanasema ni mungu wa haki. Amesemwa ni mngu wa haki kwani ameweka sheria na adhabu kali kwa mwanadamu. Na mungu wa waisraeli ni mungu wa Time (muda) ambaye ameumba vitu. Sikatai.

Pili kuna mungu wa agano jipya chini ya yesu ambaye ni mungu wa upendo. Mungu huyu yupo na anaabudiwa na warumi( warumi ndio wazungu wa sasa hivi au roman empire)

Mungu wa waisraeli, warumi na waarabu ni mungu wa muda hata ukisoma vitabu vyao kila saa wanajisifu wao ndio wana control time.

Kila jamii za kidunia zina miungu yao mfano wahindi wana mungu brahma, kali, vishu na krishna nk., wachina wana budha pamoja na wajapani na watu wote wenye asili ya macho madogo mungu wao ni sanamu lenye tumbo kubwa linaitwa budha.

Waarabu mungu wao ni allah ambaye anawakiliswa na jiwe lipo maka linaitwa black stone jiwe jeusi ambalo lipo al kaba jiwe hilo lilishuka duniani toka kipindi cha adamu na hawa na watu wakienda kuhiji wanalibusu na kusujudia jiwe hilo kwa kulizunguka mara saba. Jiwe hilo linaitwa hajr al aswad.

Ni ibada ya kuabudu sanamu lakini waislamu wengi hawajui ukweli huu. Ndo mana wanipagana vita na kuwauwa watu weusi wenzao kwa makundi kama boko haramu na al shabab. Ni sawa na mawe yanayotumiwa kuchonga sanamu la yesu wa wakrito wakaliabudu. Haina tofauti wote waislamu na wakristo wote wanamuabudu Saturn au Kronos ndo mana waslamu wanaamini biblia ni kitabu cha mungu ambaye ni saturn katika nguzo zao za imani. Nasisitiza mungu wa wakristo ni Saturn pamoja na waislamu ili ujuwe huu ukweli lazima uwe INITIATE. Kawa wewe sio INITIATE utaishi kutoa sadaka na sijda.

Kronos Ndio mungu wa waislamu na wakristo. Na nguvu zake sio kamili kwani mungu halisi hatoi adhabu wala hataki kunyenyekewa ni mungu wa upendo haijalishi unafanya mabaya au hapana yeye yupo tuu wala hawezi kuhukumu kitu. Duniani tupo kwaajili ya kujifunza hivyo hakuna zuri wala baya. Inategemeana na tafsiri ya kile unachokiona nikzuri kwako kinaweza kuwa kibaya kwa mwenzako.

Kwa sasa kuna mawakala wengi sana makanisani na kisikitini wakiwaaminisha kuwa mizimu ni roho chafu za kuzimu ilihali wakijuwa wao wamepokea shahada za ki freemason ambazo ni ibqda za wazungu na hii ipo katika historia ya mqmbabu zao kwamba ndio asili yao wazungu. Wanawatoa watu weusi wenzao katika ukweli ili kulinda maslahi yao ya kidunia.

Wanachofanya hawa watu wazungu ni kututoa katika asili yetu na sisi kufata mambo yao.

Mzimu ni baba au mama yako aliyekufa je baada mzazi wako akifa utamchukia au utamkumbuka kwa wema aliokufanyia kwa malezi mpaka hapo ulipo fika.? Baba na mama yako nao wana wazazi wao ambao nao walisha tangulia mbele za haki mlolongo unaendela hivo. Lengo la ibada ya mizimu ni kutoa shukrani kwa walio tutangukia kwani wao wanatuona ila sisi hawatuoni ila sio kuwa abudu. Kuna tofauti ya kutoa shukranu na kuabudu mfano kujenga kaburi la ndugu au jamaa ni kuonyeaha shukrani fulani.

Wanachofanya watu wa dini mfano wakristo na waslamu kupiga vita mizimu hasara yake hutaiona hapa duniani na pindi utakapo kufa utawakuta ndugu zako na ma bibi na mababu zako ila hawata kupokea kama sehemu yao kwani wakati upo duniani uliwadhihaki na kuwa adui kwao.

Mizimu wanachotaka ni kuwa na hisia za kibinadamu kutowa sadaka mbali mbali kwao ikiwamo za wanyama kwani huwa wametuzunguka na mkikutana kama ukoo huwa wapo na hupenda.

Mizimu inapenda pombe maji au wanyama wanaochunjwa kwa hesma yao kwani ndio life style ya mwanadamu toka enzi watu wanakunywa pombe. Kwa vitu hivo unatengeza conection ya mafanikio yako hapa duniani na ukifa utakuwa na watu watakao kupokea. Ukifa unaenda sehemu ya ugenini lazima uwe na wenyeji walio kutangulia.

Kama ulivyo zaliwa hapa duniani ukapokewa na wazazi wako na ndugu zako na pia utakapo kufa jua kuna wenyeji ambao walisha kutangulia ambao watakupokea. Je hao wenyeji uliwafanyia jambo gani la maana kuonyesha heshima kwao. Wakati bila wao wewe usinge weza kuzaliwa. Kumbuka marehemu babu yako na bibi yako ndio walizaa wazazi wako ambao unawapenda. Na wazazi wako wana wazazi wao ambao wana wapenda na kuwakumbuka cheni ni ndefu sana kurudi nyuma mpaka wewe ukawepo hapo ulipo daganywa na stori za biblia ya warumi na kurani ya waarabu.

Dini zote ambazo mnaziabudu zote zililetwa na watesi wetu na kuwachukua babu na bibi zetu kama watumwa na wameua watu weusi wengi sana. Alafu leo unajifanya mlokole au mkristi safi au muslam safi jua unajidanganya na unaungana na maadui za wazee wetu na kusahau mila.

Ukoo hauishi, kama ulivyo pokelewa hapa duniani na wazazi wako utapokelewa na ahera na mizimu ya waliokutangulia kama ulikuwa unawatoa katika jina la yesu ndonutajua sasa utakapo ishia na mtu akifa kinachobakiwa nae ni kumbukumbu za maisha yake.

Watu weusi ni watumwa wa fikra za historia ipo wazi kuwa tulijishusha chini na kupokea tamaduni za watu wengine hasa waarabu na wazungu. Ili tufanikiwe gundueni tatizo lipo wapi kwanini tuna mali zote lqkini hatuna baraka tupo katika lindi la umaskini na kusalitiana?

Mfano wa wazi ni filamu ya vikings ambapo ragnar alisahau mizumi ya asili kwao kwa kupokea ukristo na mizimu ikamsahau. Ile filamu ni kwaajili ya kutoa fundisho usisahau ulipo toka.

Mimi siabudu mizimu ila natoa shukrani kwa wazee wangu wote waliotangulia mbele za haki ambao bila wao nisinge weza kuzaliwa na baba na mama yangu kwa kutia sadaka ya denge au maji au chochote nachotaka. Kuna mahali nimwekea alter maalumu ila hakuna anaye ishi hapo porini. Ila kwakuwa najua mizimu ipo na mimi inajua nachofanya.

Ombi langu kwako usigombane na mizimu ya watangulizi wako kwani huwezi jua kama wao ni mizimu huenda na wewe ukawa mzimu pia ila ukiwa mzimu wenye maaadui upande wa pili itakuwa ngumu kwako.

Heshimuni tamaduni zenu tukutane mwezi 12 nyumbani. Kuwa kwako mkristo autimatiki unaona waslamu wanaenda motoni wahindi wanaenda matoni na wayahudi pamoja na watoa shukrani kwa mizimu hii ndo mentality wa matrix wana kuwa na Ego kwamba wao dini yao ndo ya haki na wengine wapo dini ya uongo kumbe wote wamepotea.

Wewe unapokesha kumsifia mungu wa waisraeli usije kudhani eti baraka zinakujua kwako hapana zinaenda kwa waisrael na vilevile unavyo msalia mtume na allah baraka zote zinaenda kwa waarabu ndo mana mtu mweusi ni maskini wa mali akili na fikra.

Elimu hii sio ya ku google ni urithi wangu niliopewa. hivo usije kuniambia uislamu au ukristo ni dini ya haki nikikuomba ushahidi ukaniletea maneno kwa biblia imesema au qurani imesema wewe ulikuwepo au wewe ni mwarabu au mrumi.?
Ukikua utatambua ujinga wako.
 
Wakristo wanakatazwa kuombea wazee wao..ila kutwa kuombea wazee wa kizungu kwa mlango wa watakatifu..hapa kiukeli tulipigwa pakubwa


#MaendeleoHayanaChama
Huenda ikawa hivyo. Ndio maana hili mtu akiliona kihivyo ni bora abaki kwenye dini za kimila moja kwa moja. Asiwe nusu mkristu/muislamu na nusu wa kimila.
 
Huenda ikawa hivyo. Ndio maana hili mtu akiliona kihivyo ni bora abaki kwenye dini za kimila moja kwa moja. Asiwe nusu mkristu/muislamu na nusu wa kimila.
Bora tuutafute ukweli mana mimi naamini waafrika dini zao zilikua zina Nguvu sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Katika maisha yangu haiwezi pita mwaka sijaenda kwa Mganga,siwezi kuta maiti hata njiani nisimfunue kumuangalia hata kama kaharibika,nikipita makaburini lazima nikate tawi LA mti na kuweka kwa ndugu zangu waliotangulia

Kanisan pia naenda na nawaombea hta kwenye biblia wanasema wakumbukeni wafu na asili zetu
Naomba mstari wa kwenye biblia unaonsema tuwakumbuke wafu..
 
Back
Top Bottom