Pamoja na usomi wangu siachi matambiko na mila ng'oo

Jiulize hivi mkuu......Wachina wanaabudu kivyao, wazungu wana wao, wahindi wana wao, waarab wana wao, Africa jee?........ hujiulizi tu?......
Sio nijuilize ,Nisaidie majibu hayo juuu, then ntakupa majibu yangu,nishajiulizaga sana, hebu nitoe tongo tongo ktk maswal hayo, Bila kuruka hata moja, natumia ni mepesi kwako
 
Lazima utambike unajua hata Kwenye uislam nimeiona hii kitu wenyewe wanasema unapokuwa na mtoto kabla hajabalehe bhas mfanyie akhikah sijui km nimeandika Kwa usahihi lakin kitu hiki kinaenda na uchinjaji wa mnyama ni aina ya matambiko bhas mtu wa hv balaa nuksi anasikia tu.
 
 

Attachments

  • VID-20210819-WA0055.mp4
    12.8 MB
Ahsante sana... Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Huyo alikuwa na degree za uchawi anamjua shetani nje ndani na anamjua Mungu nje ndani utasemaje ni student,ameuishi uchawi.
Hio Samwel nenda hadi 31.
Hahahaha
 
Yani ungekuwa unaishi karibu na mimi ningekupa paja la mbuzi ukapike unywe na pombe yenu ya asili tena umwagie kidogo kwe makaburi ya wazee wenu!!! Huu ni moja ya UZI makini kuwahi kuandikwa Jamii forum aisee!!! Yan You have made my day aseeee!!!!nimefurahi mno mno tungekuwa na akili kama yako tungekuwa mbali sana ndugu yangu!!!
Eti unakuta lijitu jeusi kama mm linajifanya linaongea lafudhi ya kiarabu au linajifa lifuasi la ukristo puuuuuuu !!!! Hizi din tuzifate ila tujue tuna za kwetuu !!!asante kwa uzi bora!!!
Sasa subiri watumwa waje utaona
 
Wewe sio muislam, short and clear. Uliyoyaandika kuhusu uislam na pamoja na kusifia ushirikina inaonyesha hujui lolote kuhusu uislam
Wewe huna islamu wowote unafata mkumbo tuuu!!! Hata mm ni mfata mkumbo hizo dini hazi tuhusu!?? Jiulize kabla ya uislam kuingia Afrika kulikua hakuna watu!?? Waliamini nini!!! Kabla wazungu kuja kulikua hakuna watu!?? Wsliamini nini!?? Waafirka amkeni!!!
 
Tatizo Waafrika hamkubari ukwel sijui mlirogwa na nani?

Wewe unajiita muislam wapi na wapi?

Muislam maanake ni wa ukoo wa Islam je wewe ni uko huo?

Mkristu maanake wa ukoo wa Kristu je wewe ni wa ukoo huo?

Acha ujinga sasa
Majinga hayaelewi kitu hayo
 
Kiukweli napenda sana matambiko na kuanudu (kuomba mizimu) ila sijui HOW TO.

Mtu yeyote anaeweza kunipa ABC nitashukuru sana
 
Wewe watoto wako umewaacha wafikishe miaka 18 ndo ukawapeleka kanisani au msikitini??
Ndio kanisani tulikuwa tunaenda wote lakini walipokuwa wakubwa ilibidi waamue wao kama wao kila mmoja kwa wakati wake kumfuata Bwana Yesu kama mwokozi wao (nadhani hii lugha sio ngeni kwako) bila mi kuwepo na sijawai kuwapeleka makaburini kwa Bibi Kinondoni pale. Kaburi la Bi. Mkubwa lipo upande wa kulia na kaburi la Kanumha Pale.

Maana Baba na Mama wote hawapo na Bibi na Babu na mdogo wangu na Shangazi, trip za makaburini itakuwa shida mbona. Mi ndio nacheki nyumba ya Bi. Mkubwa wao watacheki yangu mimi na sio kutambika ili eti dua zao zisaidie kuondoa mizengwe.
 
Kiukweli napenda sana matambiko na kuanudu (kuomba mizimu) ila sijui HOW TO.

Mtu yeyote anaeweza kunipa ABC nitashukuru sana
Ohooo mkuu achana na hiyo kitu ukiona usiku uko nje ya nyumba kwenye ndoto basi wameshakupa uchawi bila kujua utaanza kutafuta minofu ya binadamu.
 
Bonge la uzi, yaani we acha tu! Nilibatizwa nikiwa 18, eti walinicheka na jina langu la nyumbani (bila aibu wanasema jina la kishenzi) nikapewa jina la kizungu nikashangilia kama zuzu!! Tuzingatie mila zetu, tuwaachie za kwao. Mtaniita mpinga Kristu Ila ni ukweli.
 
Mnaokwenda kutambika ujumbe huu unawahusu.Huyu ni mbobezi kwenye mambo ya kiroho ktk Elimu ya ulimwengu usioonekana.
Kama jamaa anajiona mshindi,
Bado tunayo safari ndefu sana,
Mbinguni tutafik kwa Neema tu,
Sio kwa uweza wetu kuzishinda Dhambi,


Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Wewe sio muislam, short and clear. Uliyoyaandika kuhusu uislam na pamoja na kusifia ushirikina inaonyesha hujui lolote kuhusu uislam
Huna haki wala mamlaka ya kuamua nani muislamu au siye.
 
Basi umuache na yeye awafundishe kuabudu kupitia mizimu, na wao wakifikisha miaka 18 watachagua wenyewe kama wanaendelea au lah, kama wa kwako walivyofanya
 
Kamwe narudia kamwe mzungu hawezi kuzaa mtu mweusi. Hivyo kusema kwamba uzao wa Adam na Hawa ndiyo uzao wetu sisi watu weusi ilhali wao walikuwa ni wazungu ni uongo amboa mimi sikubaliani nao kamwe. Mota mada uko sahihi 100%
 
hebu lete andiko
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]yaani nyie watumwa mmekuwa mazuzu kabisa. Eti unataka nikuletee andiko tena bila shaka ni kutoka kwenye bible au quran.


Yaani ni ujinga wa kiwango cha lami mtu akikwambia TAZANI hakuwahi kuwepo, wewe ukamwambia aliwahi kuwepo. Akamwambia ulete ushahidi kama TAZANI aliwahi kuwepo kweli, wewe ukamuwekea CD ya TAZANI kwenye deki ukuoneshe huyo TAZANI ashuhudie[emoji13][emoji13][emoji13]


Ni ujinga wa kiwango cha lami mtu anakwambia SPIDER MAN hakuwahi kuwepo, wewe ukasema aliwahi kuwepo. Akataka ushahidi ukamuwekea CD ya movie ya SPIDER MAN alafu unamwambia angalia pale kwenye dakika ya 18:33 utamuona SPIDER MAN akipaa, na wewe ukauona ni ushahidi unaishikika[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]


Na ji ujnga wa kiwango cha lami vile vile mtu anakwmabia Yesu hajawahi kuwepo na mbingu haipo, wewe unamwambia Yesu alikuwepo na mbingu ipo. Akakwambia umpe ushahidi ukaenda kumfunulia biblia ambapo yapo masimulizi ya Yesu na mbingu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]


Yaani wafia dini mmekuwa makondoo wa Yesu na Mohamad bila hata kufatilia hizo hadithi za vitabuni ziliandikwa na akina nani kwa madhumuni gani.


Shtukeni makondoo nyie[emoji38]
 
Mungu akusaidie umjue Yesu ili uekwepe moto wa milele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…