Pamoja na wingi wa abiria kwanini Mwendokasi umeshindwa kuongeza mabasi na kuboresha huduma?

Pamoja na wingi wa abiria kwanini Mwendokasi umeshindwa kuongeza mabasi na kuboresha huduma?

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Huu mradi una maswali mengi ambayo binafsi ninakosa majibu. Tunajua na kutambua kwamba kuna gharama za uendeshaji wa mradi, ikiwemo kulipa mishahara wafanyakazi,mafuta, matengenezo n.k Lakini biashara yoyote ambayo ina wateja wengi kiasi kile, Nilitegemea mpaka sasa biashara hii ingekuwa imekua hasa ukizingatia katika route za mwendokasi mfano kutoka Kimara mpaka Gerezani hakuna mpinzani kwasababu route zote za daladala zilifungiwa kupisha mwendokasi pekee kutoa huduma.

Swali fikirishi, inakuwaje biashara yenye wateja wengi kiasi kile tena isiyokuwa na mpinzani inaelekea kufa? Inakuwaje biashara yenye wateja wengi mno badala kukua na kuboresha huduma kwa kuongeza magari ndiyo kwanza inageuka kero na inaelekea kufa sasa? Viongozi wapo, wanashuhudia na hatuoni tamko/juhudi/hatua zinazoonekanazikichukuliwa?

GORz5JGW4AAePsO.jpeg
 
Tanzania nchi yangu nakupenda kwa moyo wote. Tunakulilia Tanzania maana mawakala wa kuhujumu miradi yetu ni wengi kuliko wenye uzalendo wa nchi yetu. Siku zinakuja ambapo kila mmoja atalipia kadiri ya matendo yake
 
Hivi tofauti na uchawa kuimba mapambio, ufisadi, rushwa, wizi na ujambazi ni kipi ambacho serikali ya mboga mboga inafanya kwa usahihi wake 🤔🤔
 
Wakati wa Magufuli akinunua zile ndege niliwahi andika kwanini asinunua mabasi mengi zaidi baada ya ndege.

Kuna msomi mmoja humu anaitwa Pascal Mayalla alitetea sana ununuzi wa ndege nikasema kila msomi na uono wake wacha nikae kimya.
 
Huu mradi una maswali mengi ambayo binafsi ninakosa majibu. Tunajua na kutambua kwamba kuna gharama za uendeshaji wa mradi...
Wizi wa serikali, we angalia huduma za vivuko kigamboni, na huduma ya boat za kwenda zenj, Kampuni binafsi zinafanya vzr Sana, kuliko upuuzi wa serikali, miaka ya 90 kulikuwa na maduka ya serikali ya kuuza sukari na sembe!

Mtu binafsi alikuwa haruhusiwi kuuza hizo bidhaa,mafoleni mskubwa, mateso kwa wananchi.

Na hii mwendokasi kuna pesa nyingi Sana, Ila ndio zinachukuliwa na serikali badala ya kuwekeza, kama ilivyo TTCL,mtu anayetembea, soko lilelie tigo,voda, nk wanapiga faida.

Kwenye mwendokasi, serikali ijitoe kabisa, iwe ya watu binafsi
 
Binafsi nahisi tunashida katika uongozi,Tuna rundo la viongozi
Rais
Makam
Waziri mkuu
Naibu waziri mkuu
Waziri wa uchukuzi makame ndio shida iliyopo hapo sasa.
 
Wakati wa Magufuli akinunua zile ndege niliwahi andika kwanini asinunua mabasi mengi zaidi baada ya ndege.

Kuna masomi mmoja humu anaitwa Pascal Mayalla alitetea sana ununuzi wa ndege nikasema kila msomi na uono wake wacha nikae kimya.
Mpuuzi huyo hana usomi wowote anahaingaika na nchi.
 
Mheshimiwa Rais nipeni management contract ya kuendesha hilo shirika miezi 3 TU kama halitatengeneza faida nitalipa hasara itakayokuwa imejitokeza.

Sijaona sababu ya kuuza au kuingia ubia na mtu Bali right management with right business model ndicho shirika linakosa
 
Sisi watanzania tunasubiri treni za SGR 😃😃😃😃😃😃😃 hii itapunguza foleni njiani.
 
Huu mradi ulianza kufa kabla hata ya kuanza kwasababu ya wakubwa kukosa maono. Kwanza eneo walilolichagua kama karakana ilitosha kueleza mradi ungekufa tu mapema punde tu baaada ya kuanza. Serikali siku zote usema tusijenge mabondeni ila ajabu karakana ikajengwa Jagwani sehemu ambayo uathiriwa na mafuriko kila mwaka.

Dalili nyingine ya kifo cha mradi huu ni kusuasua kwa mfumo wa tiketi, mwanzoni mambo yalikuwa shwari ila baada ya kipindi fulani, mfumo ukakwama kuingia ndani ya kituo cha kugusisha tiketi ukawa mwisho wake. Naomba nieleweke mashine zile zilikuwa na uwezo wa kutambua tiketi ya kughushi na halali ninaamini kuwa tiketi za kughushi zilipata nafasi hivyo faida kutoonekana.

Dalili nyingine ya kifo ilijionyesha waziwazi, baada ya wahusika kushindwa kufanya matengenezo. Mfano mdogo wakati mradi unaanza magari yalikuwa na kamera na mfumo wa kutaja vituo, ila baada ya muda mifumo hiyo ikafa. Sasa kama waendeshaji mambo hayo madogo walishindwa kuweka sawa, matengenezo muhimu wangeweza kweli!

Mwisho Watanzania hatuna utamaduni wa kutunza vitu vyetu, uswahili kwenye vitu visivyohitqji uswahili uturudisha nyuma, ni ngumu sana kuendelea tukiendelea kukumbatia ubabaishaji na uswahili.
 
Mheshimiwa Rais nipeni management contract ya kuendesha hilo shirika miezi 3 TU kama halitatengeneza faida nitalipa hasara itakayokuwa imejitokeza.

Sijaona sababu ya kuuza au kuingia ubia na mtu Bali right management with right business model ndicho shirika linakosa
Usijichanganye mkuu.

Unaweza pewa, lakini baada ya mwezi ukashangaa mapato yote ya hilo shirika yamechukuliwa na serikali kwenda kujenga lelina wewe unataka kufanya matengenezo ya vipuri.

Mambo ya serikalini ni hovyo sana
 
Wakati wa Magufuli akinunua zile ndege niliwahi andika kwanini asinunua mabasi mengi zaidi baada ya ndege.

Kuna masomi mmoja humu anaitwa Pascal Mayalla alitetea sana ununuzi wa ndege nikasema kila msomi na uono wake wacha nikae kimya.
Ila kwa upande mwingine mkuu, Kwanini mradi utegemee fedha za nje ya mradi badala kutegemea mapato yake? Kwa idadi ile ya abiria, nauli juu, hakuna mshindani kwenye route n.k lakini bado mradi umeshindwa kutengeneza faida kuongeza mabasi yake yenyewe?
 
Huu mradi una maswali mengi ambayo binafsi ninakosa majibu. Tunajua na kutambua kwamba kuna gharama za uendeshaji wa mradi, ikiwemo kulipa mishahara wafanyakazi,mafuta, matengenezo n.k Lakini biashara yoyote ambayo ina wateja wengi kiasi kile, Nilitegemea mpaka sasa biashara hii ingekuwa imekua hasa ukizingatia katika route za mwendokasi mfano kutoka Kimara mpaka Gerezani hakuna mpinzani kwasababu route zote za daladala zilifungiwa kupisha mwendokasi pekee kutoa huduma.

Swali fikirishi, inakuwaje biashara yenye wateja wengi kiasi kile tena isiyokuwa na mpinzani inaelekea kufa? Inakuwaje biashara yenye wateja wengi mno badala kukua na kuboresha huduma kwa kuongeza magari ndiyo kwanza inageuka kero na inaelekea kufa sasa? Viongozi wapo, wanashuhudia na hatuoni tamko/juhudi/hatua zinazoonekanazikichukuliwa?

View attachment 2997702
Nimeiona hii picha sehemu fulani nikajua iko edited lkn kumbe ni real?

Cha kushangaza Waziri wa uchukuzi yupo ofisini na anapata amani kwann?

Cha ajabu zaidi, Waandishi wa habari. Baada ya kuonekana picha ningetegemea kumuandama Waziri wa uchukuzi + GM wa shirika la mwendokasi lakini wapo busy na mambo ya kijinga tuu.

Haya mambo yanakera kwa kweli.
 
Huu mradi una maswali mengi ambayo binafsi ninakosa majibu. Tunajua na kutambua kwamba kuna gharama za uendeshaji wa mradi, ikiwemo kulipa mishahara wafanyakazi...
Hiyo picha ni photoshop au? Anyway, wanataka ionekane tumeshindwa ili mwarabu apewe bure! Na nauli itapaa
 
Ila kwa upande mwingine mkuu, Kwanini mradi utegemee fedha za nje ya mradi badala kutegemea mapato yake? Kwa idadi ile ya abiria, nauli juu, hakuna mshindani kwenye route n.k lakini bado mradi umeshindwa kutengeneza faida kuongeza mabasi yake yenyewe?
Ukichimba zaidi ndani utakuta hayo mapato hayabaki shirikani. Yanaingia centeal government ndo yarudi.

Hawa watu kama waliikopa NHIF, Watashindwa kuchukua hela za Hilo shirika
 
Wizi wa serikali, we angalia huduma za vivuko kigamboni, na huduma ya boat za kwenda zenj, Kampuni binafsi zinafanya vzr Sana, kuliko upuuzi wa serikali, miaka ya 90 kulikuwa na maduka ya serikali ya kuuza sukari na sembe!

Mtu binafsi alikuwa haruhusiwi kuuza hizo bidhaa,mafoleni mskubwa, mateso kwa wananchi.

Na hii mwendokasi kuna pesa nyingi Sana, Ila ndio zinachukuliwa na serikali badala ya kuwekeza, kama ilivyo TTCL,mtu anayetembea, soko lilelie tigo,voda, nk wanapiga faida.

Kwenye mwendokasi, serikali ijitoe kabisa, iwe ya watu binafsi
Yani hapo ndipo inaponichosha serikali yani hela inayo nyingi tu kuliko mtu binafsi lakin inashindwa kufanya kitu kidogo tu ambacho inauwezo nacho ila kona kona zitakuwa nyingi mpaka kipatikane
 
Back
Top Bottom