Panga la wachezaji Simba linanukia mwishoni mwa msimu huu, kuna majina makubwa

Panga la wachezaji Simba linanukia mwishoni mwa msimu huu, kuna majina makubwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Inadaiwa kuwa uongozi wa Klabu ya Simba un mipango ya kupitisha panga kwa wachezaji wao walioonyesha kushuka kiwango mara baada ya kumalizika kwa msimu huu.

Hilo limeshapangwa lakini kwa sasa wameweka wazi kuwa mawazo yao yote yapo katika kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali wanayoshiriki ikiwemo ligi kuu ambayo wanapambana na Yanga.

Hivyo suala la kuwaongezea mikataba mastaa wao wanaomaliza mikataba litapatiwa majibu mwishoni mwa msimu

Baadhi ya nyota wa Simba ambao wanamaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu na wapo kwenye htari ya kutoongeewa mikataba mipya ni Bernard Morrison, Taddeo Lwanga, Meddie Kagere, Chis Mugalu na Pascal Wawa.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema:

“Ni kweli kuna kundi kubwa la wachezaji wetu ambao wanatarajiwa kumaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu, hatujaanza mazungumzo nao lakini niwatoe hofu Wanasimba kuwa tunajua nini tunapaswa kufanya juu ya hilo na tutahakikisha wachezaji wote tunaowahitaji kwa msimu ujao wanapewa mikataba mipya.”

Chanzo: Global Publishers
 
Chonde chonde,BWALYA WAMUACHE/WASIMUACHE.

WAMUACHE..wasimbugudhi
WASIMWACHE...wamuongezee mkataba ili aendelee kubaki kikosini.

aahh kiswahili hiki!!!
 
Hao wanaoachwa timu yangu Yanga iwachukue watatusaidia kwenye mechi za kimataifa msimu ujao ili tusitolewe tena round ya awali.

Aliyekuambia Yanga ina uhitaji wa makinikia ni nani? Yaani Yanga ya msimu huu imsajili Mugalu, Kagere, Wawa, 😬😬😬

Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi.
 
Kumuacha Morrison itakuwa upumbavu wa hali ya juu sana kuwahi kutokea.Bora angetajwa Bwalya.
Mechi nyingi Bwalya anapoza mpira na back pass nyingi.
Anacheza "soft ball" aina ya mchezo inayofaa kwenye mechi za kirafiki na si za mashindano.
Inadaiwa kuwa uongozi wa Klabu ya Simba un mipango ya kupitisha panga kwa wachezaji wao walioonyesha kushuka kiwango mara baada ya kumalizika kwa msimu huu.

Hilo limeshapangwa lakini kwa sasa wameweka wazi kuwa mawazo yao yote yapo katika kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali wanayoshiriki ikiwemo ligi kuu ambayo wanapambana na Yanga.

Hivyo suala la kuwaongezea mikataba mastaa wao wanaomaliza mikataba litapatiwa majibu mwishoni mwa msimu

Baadhi ya nyota wa Simba ambao wanamaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu na wapo kwenye htari ya kutoongeewa mikataba mipya ni Bernard Morrison, Taddeo Lwanga, Meddie Kagere, Chis Mugalu na Pascal Wawa.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema:

“Ni kweli kuna kundi kubwa la wachezaji wetu ambao wanatarajiwa kumaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu, hatujaanza mazungumzo nao lakini niwatoe hofu Wanasimba kuwa tunajua nini tunapaswa kufanya juu ya hilo na tutahakikisha wachezaji wote tunaowahitaji kwa msimu ujao wanapewa mikataba mipya.”

Chanzo: Global Publishers
 
Fyeka Bwalya.
Fyeka Muzamiru Yassin.
Fyeka yule marasta aliyekakamaa.
Fyeka Wawa.
Fyeka Mugalu.
Fyeka Mhilu.
Fyeka Boco.

Kanoute na Efue wawekwe kwenye matazamio mikataba mifupi.
Lwanga abaki na wengine wabaki.
 
Kumuacha Morrison itakuwa upumbavu wa hali ya juu sana kuwahi kutokea.Bora angetajwa Bwalya.
Mechi nyingi Bwalya anapoza mpira na back pass nyingi.
Anacheza "soft ball" aina ya mchezo inayofaa kwenye mechi za kirafiki na si za mashindano.
Huyu wakuitwa Bwalya aende tu!! Anaikaba team ninaunga mkono hoja yako bro[emoji120][emoji120]
 
Wachezaji wakuachwa kwa mtazamo wangu ni
1:chriss Mugalu
2😛ascal wawa
3:Onyango
5:Bwalha
Hao ni wachezaji wa kigeni,wachezaji wa ndani wakuachwa ni
1:Erasto Nyoni
2:Muhilu
3:Gadiel
Kagere nadhani atapewa mkataba wa msimu mmoja tu unatosha na tumuage kwa upendo kabisa maana yeye ndio mshambuliaji wa kigeni mwenye goli nyingi hadi sasa kuliko mshambuliaji yeyote aliyewahi kucheza kwenye ligi yetu,mnyonge mnyongeni ila haki yake tumpe,kibu bado ni mapema sana kusema ameshindwa kudeliver kile ambacho tunatarajia wanasimba,bado umri unaruhusu chochote kinaweza kutokea,Israel mwenda kashindwa kabisa kuvaa viatu vya kapombe bado ataendelea kuwepo simba ila tutamtoa kwa mkopo timu yeyote kasoro Utopolo fc itayokuwa inamuhitaji,John bocco bado ataendelea kubaki simba maana kilichomkuta bocco ni sawa na kilichomkuta Dube nina imani mambo yatakuwa sawa [emoji1488]
 
Wachezaji wakuachwa kwa mtazamo wangu ni
1:chriss Mugalu
2😛ascal wawa
3:Onyango
5:Bwalha
Hao ni wachezaji wa kigeni,wachezaji wa ndani wakuachwa ni
1:Erasto Nyoni
2:Muhilu
3:Gadiel
Kagere nadhani atapewa mkataba wa msimu mmoja tu unatosha na tumuage kwa upendo kabisa maana yeye ndio mshambuliaji wa kigeni mwenye goli nyingi hadi sasa kuliko mshambuliaji yeyote aliyewahi kucheza kwenye ligi yetu,mnyonge mnyongeni ila haki yake tumpe,kibu bado ni mapema sana kusema ameshindwa kudeliver kile ambacho tunatarajia wanasimba,bado umri unaruhusu chochote kinaweza kutokea,Israel mwenda kashindwa kabisa kuvaa viatu vya kapombe bado ataendelea kuwepo simba ila tutamtoa kwa mkopo timu yeyote kasoro Utopolo fc itayokuwa inamuhitaji,John bocco bado ataendelea kubaki simba maana kilichomkuta bocco ni sawa na kilichomkuta Dube nina imani mambo yatakuwa sawa [emoji1488]
Kagere apewe mkataba wa miezi 6 tu
 
Kumuacha Morrison itakuwa upumbavu wa hali ya juu sana kuwahi kutokea.Bora angetajwa Bwalya.
Mechi nyingi Bwalya anapoza mpira na back pass nyingi.
Anacheza "soft ball" aina ya mchezo inayofaa kwenye mechi za kirafiki na si za mashindano.
Mpira unaangalia mkuu?
Au ndio livescore?
 
Wawa Out
Morrison Out
Kagere Out
Mugalu Out
Kibongo bongo Acha yoyote kasoro nyuma ( Manula na beki zake zote wabaki).
 
Hao wachezaji wa ndani mnapotaja jina mtaje na mbadala wake wa ndani, sio wa nje
 
Back
Top Bottom