Papa Francis aikosoa Urusi asema imefanya shambulizi la kinyama Mariupol

Papa Francis aikosoa Urusi asema imefanya shambulizi la kinyama Mariupol

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
PAPA.JPG
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis ameikosoa Urusi kwa kueleza kuwa vita dhidi ya Ukraine ni ishara ya kudidimia kwa hali ya ubinadamu na kwamba imesababisha mateso na majonzi.

Papa Francis (85) hakuitaja moja kwa moja Urusi lakini aliposema kuwa mashambulizi ya Mji wa Mariupol yamekuwa ya kinyama na kusababisha watu kuhamishwa kutoka katika mji huo ni wazi anakosoa mashambulizi yanayoendelea.

“Ninasikiika na kulia kwa watu wan Ukraine hasa wale ambao ni dhaifu, wazee, watoto… ni habari ya kusikitisha kuona watu wakihamishwa katika mji wao,” anasema Papa.

Kulingana na vyombo vya habari vya Urusi, jumla ya raia 46 wamehamishwa kutoka eneo lililo karibu na kiwanda cha chuma kilichozingirwa cha Azovstal katika mji wa bandari wa Mariupol.

Source: English Alarabiya
 
Papa mbona hakuwahi kukemea mateso ya warusi waliyokuwa na wanapewa na wa-Ukraine kule Crimea, Donehsk na Luhahsk?

Kwa Papa maisha ya wa-Ukraine ni bora Sana kuliko ya wa-Russia?

Miaka zaidi ya 10 Russia inalalamika kuhusu warusi kuteswa na Ukraine lakini hakuna aliyeona unatakiwa mjadala ,kwa nini leo?

Papa atulie na hiyo damu inayomwagika ainywe taratibu na mkate kanisani ili furaha yake itimie. Russia anachofanya ni kuhahakikishia usalama warusi nje ya mipaka ya Urusi na kitakachotokea Ukraine dunia itakuja kuisikitikia

Katika hili Papa aache unafiki na kumtumikia Mungu wa kweli ili ajihesabie haki.
 
Kanisa limekuwa lawaimba kwaya saivi nilitegemea kanisa liwe mstari WA mbele kukemea na kutoa misaada ya kiutu mashambulizi na mauwaji yalivyokuwa yanatokea Iraq, Afghanistan, Libya ata Syria Ila sababu Ile ni jamii ya kiislamu na kanisa halioni nafasi ya kupata waumini wapya basi walikaa kimya na kukemea kimya kimya Ila Ukrein sababu wengi ni waothodox na kanisa katoliki linataka kuongeza wafuasi basi linakemea Kwa mbwembwe zote Hadi mfungo WA mwaka huu waliwekwa kwenye maombi ya kwaresma useless kabisaa
 
Kanisa limekuwa lawaimba kwaya saivi nilitegemea kanisa liwe mstari WA mbele kukemea na kutoa misaada ya kiutu mashambulizi na mauwaji yalivyokuwa yanatokea Iraq, Afghanistan,Libya ata Syria Ila sababu Ile ni jamii ya kiislamu na kanisa halioni nafasi ya kupata waumini wapya basi walikaa kimya na kukemea kimya kimya Ila Ukrein sababu wengi ni waothodox na kanisa katoliki linataka kuongeza wafuasi basi linakemea Kwa mbwembwe zote Hadi mfungo WA mwaka huu waliwekwa kwenye maombi ya kwaresma useless kabisaa
Na kwa sababu waliokuwa wanashambulia kule ni wamarekani kanisa likakaa kimya
 
Marehemu baba yangu alisoma seminari tena kipindi hicho walikuwa wanapendekezwa na askofu wa jimbo ambaye alikuwa ni Mmarekani.

Matokeo ya form 4 alifaulu vizuri ila alikataa kuendelea kusoma seminari ili awe padri kitendo kilichomkasirisha hadi askofu maana alimwandaa awe padri.

Aliniambia alikataa kwa sababu mbili, moja mama yake alikataa yeye kuwa padri nyingine ni unafiki wa mapadri kwani maungamo ni siri ila mapadri walikuwa wanatoa siri za maungamo kwa wanafunzi na kisha kuwafukuza. Huyu papa ni mnafiki si ajabu ni pandikizi la usa.
 
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis ameikosoa Urusi kwa kueleza kuwa vita dhidi ya Ukraine ni ishara ya kudidimia kwa hali ya ubinadamu na kwamba imesababisha mateso na majonzi.

Papa Francis (85) hakuitaja moja kwa moja Urusi lakini aliposema kuwa mashambulizi ya Mji wa Mariupol yamekuwa ya kinyama na kusababisha watu kuhamishwa kutoka katika mji huo ni wazi anakosoa mashambulizi yanayoendelea.

“Ninasikiika na kulia kwa watu wan Ukraine hasa wale ambao ni dhaifu, wazee, watoto… ni habari ya kusikitisha kuona watu wakihamishwa katika mji wao,” anasema Papa.

Kulingana na vyombo vya habari vya Urusi, jumla ya raia 46 wamehamishwa kutoka eneo lililo karibu na kiwanda cha chuma kilichozingirwa cha Azovstal katika mji wa bandari wa Mariupol.

Source: English Alarabiya
Putin kushinda vita hii ni ngumu, hizi ni ishara mbaya kwake.
 
Kanisa limekuwa lawaimba kwaya saivi nilitegemea kanisa liwe mstari WA mbele kukemea na kutoa misaada ya kiutu mashambulizi na mauwaji yalivyokuwa yanatokea Iraq, Afghanistan, Libya ata Syria Ila sababu Ile ni jamii ya kiislamu na kanisa halioni nafasi ya kupata waumini wapya basi walikaa kimya na kukemea kimya kimya Ila Ukrein sababu wengi ni waothodox na kanisa katoliki linataka kuongeza wafuasi basi linakemea Kwa mbwembwe zote Hadi mfungo WA mwaka huu waliwekwa kwenye maombi ya kwaresma useless kabisaa
Muslims mna viongozi wenu wa wakuu wa dini wanapoona mnaonewa na kukandamiza kwa nini wasitoe kauli? Mnasubiri kiongozi mkuu wa kanisa katoliki ndiye awasemehe?

Je huko kote unaposema hakukemea una ushahidi wowote wa kuthibitisha kwamba hakufanya hivyo?

Kama kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani ana haki na ni wajibu kwake kulinda waumini wake, hivyo yuko sahihi kukemea pale anapoona wafuasi wa dini yake wanashambuliwa na mabomu.
 
Papa mbona hakuwahi kukemea mateso ya warusi waliyokuwa na wanapewa na wa-Ukraine kule Crimea, Donehsk na Luhahsk?

Kwa Papa maisha ya wa-Ukraine ni bora Sana kuliko ya wa-Russia?

Miaka zaidi ya 10 Russia inalalamika kuhusu warusi kuteswa na Ukraine lakini hakuna aliyeona unatakiwa mjadala ,kwa nini leo?

Papa atulie na hiyo damu inayomwagika ainywe taratibu na mkate kanisani ili furaha yake itimie. Russia anachofanya ni kuhahakikishia usalama warusi nje ya mipaka ya Urusi na kitakachotokea Ukraine dunia itakuja kuisikitikia

Katika hili Papa aache unafiki na kumtumikia Mungu wa kweli ili ajihesabie haki.
Una uhakika hakuwasemea unaweza kuthibitisha?

Unaposema Putin analinda usalama wa Warusi basi na Papa yuko sahihi kutetea waumini wa kanisa lake tena yeye ni mchanganyiko wa watu tofauti tofauti anaowatetea.
 
Anang'ata tuu na kupuliza huyo na usikite ameplan yeye hiyo vita kupitia JESUITS naamin vatikan anaweza kumwondoa rais yeyote akipenda muda wowote kama akienda tofauti na matakwa yake....na kwa hili atakuwepo nyuma ya pazia (VATICAN RULES THE WORLD via USA)
 
Marehemu baba yangu alisoma seminari tena kipindi hicho walikuwa wanapendekezwa na askofu wa jimbo ambaye alikuwa ni Mmarekani.

Matokeo ya form 4 alifaulu vizuri ila alikataa kuendelea kusoma seminari ili awe padri kitendo kilichomkasirisha hadi askofu maana alimwandaa awe padri.

Aliniambia alikataa kwa sababu mbili, moja mama yake alikataa yeye kuwa padri nyingine ni unafiki wa mapadri kwani maungamo ni siri ila mapadri walikuwa wanatoa siri za maungamo kwa wanafunzi na kisha kuwafukuza. Huyu papa ni mnafiki si ajabu ni pandikizi la usa.
Hii kahawa ni chungu mno [emoji846]
 
Kanisa limekuwa lawaimba kwaya saivi nilitegemea kanisa liwe mstari WA mbele kukemea na kutoa misaada ya kiutu mashambulizi na mauwaji yalivyokuwa yanatokea Iraq, Afghanistan, Libya ata Syria Ila sababu Ile ni jamii ya kiislamu na kanisa halioni nafasi ya kupata waumini wapya basi walikaa kimya na kukemea kimya kimya Ila Ukrein sababu wengi ni waothodox na kanisa katoliki linataka kuongeza wafuasi basi linakemea Kwa mbwembwe zote Hadi mfungo WA mwaka huu waliwekwa kwenye maombi ya kwaresma useless kabisaa
Nawewe unashida kichwani, huko kwenye hizo nchi ulizo taja kwanini hukusema misikiti ndio itoe misaada unalaumu kanisa.
 
Back
Top Bottom