jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Kwa nini hatusikii Netenyahu akipewa warrant ya kukamatwa na mahakama ya ICC kwa uhalifu anaoufanya huko Gaza strip kama ambavyo Putin kafanyiwa?
Hamas walichokifanya ni kizuri au sio?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa nini hatusikii Netenyahu akipewa warrant ya kukamatwa na mahakama ya ICC kwa uhalifu anaoufanya huko Gaza strip kama ambavyo Putin kafanyiwa?
Kumbeeee! Mimi siku zote nadhani Israel ndio mchokozi kujitanua. Kumbe muarabu ndio kima. Basi wacha wachezee kipigo kitakatifu.HISTORIA KWA UFUPI , mwaka 1948 wapalestina walipewa eneo kubwa tu kuliko waisrael ila tamaa ikawaponza wakalitaka eneo dogo la waisrael wakidai wanataka kuwaondoa wayaudi kwenye uso wa dunia , bas mamb yakawa kinyume wapalestina wakapigwa na kuporwa wao eneo , miaka michache baadae wapalestina na waarab wakaanzisha mapambano mapya kwa kuivamia israel ila wakapigwa na kuporwa tena eneo jingine , pia wapalestina wamekuwa wakijichanganya mpk leo wanaanzishaga ugomv hlf wanaishia kuporwa maeneo ba hawajifunzi , kipind waisrael wanapambana kujenga taifa , wapalestina walipambana kuiondoa vizaz vya wayaudi hapo mashariki ya kati huku wakisahau kusau kuwa wao si taifa linalotambuliwa kimataifa
Umeelewa alikisema au ni kuchagua upande tu bila kuelewa?Mimi mkatoliki ila niko upande wa palestine
Kwa walichokifanya Hamas hakuna cha ICC tena Hamas ndio wa kupeleka huko.Kwa nini hatusikii Netenyahu akipewa warrant ya kukamatwa na mahakama ya ICC kwa uhalifu anaoufanya huko Gaza strip kama ambavyo Putin kafanyiwa?
Hata akijadili siriazi haibadilishi kitu!!Mkuu unajadili vita kiutani hivo
Huyo papa tangu aruhusu ndoa za mashoga nilishamtoaga thamani.Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, katika matamshi yake makali tangu kuanza kwa mzozo kati ya Palestina na Israel, ametoa wito wa kuachiliwa kwa Mateka wote waliochukuliwa na wanamgambo wa Hamas na kusema Israel ina haki ya kujilinda.
Mtandao wa DW Swahili umeripoti kuwa akiongea mwishoni mwa hadhara yake ya kila wiki kwa maelfu ya Watu katika uwanja wa St. Peter, Papa Francis ameelezea pia wasiwasi wake juu ya kuzingirwa kwa Israel na Gaza.
"Ninaendelea kufuatilia, kwa uchungu na wasiwasi kile kinachotokea Israel na Palestina, Watu wengi sana wameuawa na wengine kujeruhiwa, naziombea Familia zilizoshuhudia siku ya sikukuu ikigeuka kuwa siku ya maombolezo na ninaomba kwamba Mateka waachiliwe mara moja.”
"Ni haki ya wale wanaoshambuliwa kujilinda, lakini nina wasiwasi mkubwa na mzingiro mzima wa Wapalestina wanaoishi Gaza, ambako pia kumekuwa na wahasiriwa wengi wasio na hatia.”
Jeshi la Israel limefanya mashambulizi ya ndege usiku kucha katika viunga vya ukanda wa Gaza, huku vita vyake dhidi ya kundi la Hamas vikiingia siku ya tano leo Jumatano na zaidi ya Watu 2,200 wameuawa katika vita hivyo kwa pande zote huku vifo vikihisiwa kuongezeka.
Na alivyoruhusu ushoga pia mmekuwa upande wake kama kila anachoongea mnakifuataKwa kauli ya Papa... Tayari wakatoliki wote wako upande wa Israel 😂