Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
2009-03-16 08:16:00
Pinda : Audit bus terminal performance
By Beatus Kagashe
THE CITIZEN
Prime Minister Mizengo Pinda has ordered the Controller and Auditor General (CAG) to do a performance management audit at the Ubungo Bus Terminal (UBT) and the Kariakoo market to establish the truth about revenues collected and their contracts.
Mr Pinda said the bus terminals and the major markets would be good sources of income if well managed. Smart Holding Co Ltd has been contracted to collect revenue at UBT since 2004 and they are paying Sh1.5 million per day.
.
Kinje au Kinjikitikile, ambaye hafanani na kingunge hata kidogo, (naomba wakapime DnA)
Kingunge: Kweli familia yangu inatoza kodi Stendi Ubungo
Asema kama mkataba ni feki Jiji walaumiwe![]()
![]()
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru.
![]()
Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT).
![]()
![]()
![]()
![]()
.....Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, amesema kama mkataba wa kukusanya ushuru katika Kituo Kuu cha Mabasi Ubungo (UBT) ni mbovu ambao kampuni ya familia yake inahusika nao, basi wa kulaumiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam...............
mimi nimechoka na hii nchi. serekali ya Tanzania imefanikiwa kiasi kikubwa sana kuwatia upumbavu raia wake. waziri mkuu anaonekana mtu wa maana kwa kufuatila hilo suala. sasa na afuatilie hao mafisadi wanaoiba mabilion ,sio hizo kesi za mitaani.Kingunge: Kweli familia yangu inatoza kodi Stendi Ubungo
Asema kama mkataba ni feki Jiji walaumiwe![]()
![]()
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru.
![]()
Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT).
![]()
![]()
![]()
![]()
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, amesema kama mkataba wa kukusanya ushuru katika Kituo Kuu cha Mabasi Ubungo (UBT) ni mbovu ambao kampuni ya familia yake inahusika nao, basi wa kulaumiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Kampuni ya Smart Holdings ambayo ina uhusiano na mwenasiasa huyo iliingia mkataba na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kukusanya mapato kituo hicho cha mabasi yaendayo mikoani.
Hata hivyo, mkataba huo ulizua utata baada ya kubainika kuwa una harufu ya ufisadi, jambo lililoifanya serikali kuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuanza kufanya ukaguzi.
Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam, Kingunge alisema kama mkataba wa Halmashauri ya Jiji na kampuni hiyo ni feki basi wa kulaumiwa ni yule aliyetangaza tenda, yaani Jiji.
Kingunge alikiri kuifahamu kampuni hiyo na kuongeza kuwa kampuni hiyo iliomba kazi kama walivyofanya watu wengine na ilifuata vigezo vyote vilivyowekwa na Jiji.
Alisema Jiji lina watalaamu wake na kwamba kama walikubali kusaini mkataba mbovu, basi kampuni hiyo haina makosa yoyote.
Tayari Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG), imeanza kufanya uchunguzi wa mapato katika kituo hicho na Soko Kuu la Kariakoo kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu hivi karibuni, Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, alisema timu kutoka ofisi yake imeishaanza kazi hiyo.
Alisema wameanza kufanya kazi hiyo kutokana na maagizo waliyopewa na Waziri Mkuu Pinda wakati alipofanya ziara katika Stendi ya Ubungo mapema mwaka huu.
Aliongeza kuwa ameipa timu hiyo hadidu za rejea na kwamba kazi hiyo itafanyika haraka na ripoti yake itakabidhiwa kwa Waziri Mkuu.
Mapema mwaka huu, Pinda alisema kuna mkataba mbovu wa kukusanya mapato unaonukia ufisadi katika kituo hicho.
Mkataba huo ulifanywa kati Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Mkandarasi, kampuni binafsi ya Smart Holdings, inayomilikiwa na familia ya Kingunge ambaye Mbunge wa Kuteuliwa na Rais.
Mkandarasi huyo alipewa zabuni ya kukusanya mapato kituoni hapo na amekuwa akifanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka mitano sasa.
Kwa mujibu wa Meneja wa kituo hicho, Fadhili Izumbe, katika mkataba huo mkandarasi anatakiwa kulipa Sh. milioni 1.5 kwa siku kwa Halmashauri ya Jiji hata kama atakusanya mapato ya Sh. bilioni 1 kituoni hapo.
Waziri Mkuu alishuhudia ufisadi huo alipotembelea kituo hicho mapema mwaka huu ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo katika Jiji la Dar es Salaam.
Pinda alishangazwa na kushtushwa na utendaji mbovu wa uongozi wa UBT, mkataba huo na namna mkandarasi huyo alivyopatikana.
Waziri Mkuu alihisi kuwepo kwa ufisadi kituoni hapo, baada ya kusomewa taarifa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Abubakari Kingobi, kuhusu hali ya utendaji wa uongozi wa UBT, ukusanyaji wa mapato, mkataba wa mkandarasi na maendeleo ya kituo hicho.
Aliwauliza Halmashauri ya Jiji jinsi walivyompata Mkandarasi huyo na vigezo vilivyotumika kumpata.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Kingobi alipoulizwa maswali kadhaa na Waziri Mkuu hakuweza kujibu lolote, badala yake akamwita Meneja wa UBT, Izumbe ambaye naye hakutoa majibu, badala yake aliishia kusema: Aah!
Katika taarifa yake, Izumbe alisema kwa mujibu wa mkataba, mkandarasi huyo hutoa Sh. milioni 1.5 kwa Halmashauri ya Jiji kwa siku, taarifa iliyomshangaza Pinda na kumfanya ahoji kuwa hata wakikusanya Sh. bilioni moja kwa siku watalipa Sh milioni 1.5 tu kwa Jiji?
Kutokana na utata huo, Pinda aliiagiza Halmashauri ya Jiji na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuupitia upya mkataba huo ili kuondoa maswali yasiyokuwa na majibu.
Kituo hicho kwa siku kinahudumia mabasi zaidi 400, teksi 100, watu zaidi ya 2,000, maduka ya vinywaji (Baa na Grosari), maduka ya kawaida, hoteli, vioski, gereji, ambavyo vyote hulipa ada za viwango mbalimbali.
Kingunge: Kweli familia yangu inatoza kodi Stendi Ubungo
Asema kama mkataba ni feki Jiji walaumiwe![]()
![]()
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru.
![]()
Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT).
![]()
![]()
![]()
![]()
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, amesema kama mkataba wa kukusanya ushuru katika Kituo Kuu cha Mabasi Ubungo (UBT) ni mbovu ambao kampuni ya familia yake inahusika nao, basi wa kulaumiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Kampuni ya Smart Holdings ambayo ina uhusiano na mwenasiasa huyo iliingia mkataba na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kukusanya mapato kituo hicho cha mabasi yaendayo mikoani.
Hata hivyo, mkataba huo ulizua utata baada ya kubainika kuwa una harufu ya ufisadi, jambo lililoifanya serikali kuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuanza kufanya ukaguzi.
Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam, Kingunge alisema kama mkataba wa Halmashauri ya Jiji na kampuni hiyo ni feki basi wa kulaumiwa ni yule aliyetangaza tenda, yaani Jiji.
Kingunge alikiri kuifahamu kampuni hiyo na kuongeza kuwa kampuni hiyo iliomba kazi kama walivyofanya watu wengine na ilifuata vigezo vyote vilivyowekwa na Jiji.
Alisema Jiji lina watalaamu wake na kwamba kama walikubali kusaini mkataba mbovu, basi kampuni hiyo haina makosa yoyote.
Tayari Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG), imeanza kufanya uchunguzi wa mapato katika kituo hicho na Soko Kuu la Kariakoo kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu hivi karibuni, Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, alisema timu kutoka ofisi yake imeishaanza kazi hiyo.
Alisema wameanza kufanya kazi hiyo kutokana na maagizo waliyopewa na Waziri Mkuu Pinda wakati alipofanya ziara katika Stendi ya Ubungo mapema mwaka huu.
Aliongeza kuwa ameipa timu hiyo hadidu za rejea na kwamba kazi hiyo itafanyika haraka na ripoti yake itakabidhiwa kwa Waziri Mkuu.
Mapema mwaka huu, Pinda alisema kuna mkataba mbovu wa kukusanya mapato unaonukia ufisadi katika kituo hicho.
Mkataba huo ulifanywa kati Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Mkandarasi, kampuni binafsi ya Smart Holdings, inayomilikiwa na familia ya Kingunge ambaye Mbunge wa Kuteuliwa na Rais.
Mkandarasi huyo alipewa zabuni ya kukusanya mapato kituoni hapo na amekuwa akifanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka mitano sasa.
Kwa mujibu wa Meneja wa kituo hicho, Fadhili Izumbe, katika mkataba huo mkandarasi anatakiwa kulipa Sh. milioni 1.5 kwa siku kwa Halmashauri ya Jiji hata kama atakusanya mapato ya Sh. bilioni 1 kituoni hapo.
Waziri Mkuu alishuhudia ufisadi huo alipotembelea kituo hicho mapema mwaka huu ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo katika Jiji la Dar es Salaam.
Pinda alishangazwa na kushtushwa na utendaji mbovu wa uongozi wa UBT, mkataba huo na namna mkandarasi huyo alivyopatikana.
Waziri Mkuu alihisi kuwepo kwa ufisadi kituoni hapo, baada ya kusomewa taarifa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Abubakari Kingobi, kuhusu hali ya utendaji wa uongozi wa UBT, ukusanyaji wa mapato, mkataba wa mkandarasi na maendeleo ya kituo hicho.
Aliwauliza Halmashauri ya Jiji jinsi walivyompata Mkandarasi huyo na vigezo vilivyotumika kumpata.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Kingobi alipoulizwa maswali kadhaa na Waziri Mkuu hakuweza kujibu lolote, badala yake akamwita Meneja wa UBT, Izumbe ambaye naye hakutoa majibu, badala yake aliishia kusema: "Aah!"
Katika taarifa yake, Izumbe alisema kwa mujibu wa mkataba, mkandarasi huyo hutoa Sh. milioni 1.5 kwa Halmashauri ya Jiji kwa siku, taarifa iliyomshangaza Pinda na kumfanya ahoji kuwa hata wakikusanya Sh. bilioni moja kwa siku watalipa Sh milioni 1.5 tu kwa Jiji?
Kutokana na utata huo, Pinda aliiagiza Halmashauri ya Jiji na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuupitia upya mkataba huo ili kuondoa maswali yasiyokuwa na majibu.
Kituo hicho kwa siku kinahudumia mabasi zaidi 400, teksi 100, watu zaidi ya 2,000, maduka ya vinywaji (Baa na Grosari), maduka ya kawaida, hoteli, ‘vioski', gereji, ambavyo vyote hulipa ada za viwango mbalimbali.
Naam! Huo mradi ni wa Mheshimiwa KNM na familia yake Kinje na mama yake wakiwa ndo wakurugenzi, pamoja na ule Ubungu Bus Terminal hususana mabango yote ya matangazo pale terminal. Alipewa tender hiyo on a plater na kijana wake Ndugu Mukama kwa baraka za Ngwilizi (enzi hizo).
Hii ni baada ya Chacha Kiguha kuzikusanya tani yake na kutowalipa City sehemu yao ya mgao na akaingia mitini. Mzee Chacha tunaye huku US anatanua tu.