PAROKO: Tusikae kimya sasa kusubiri Miaka 10 ijayo Rais wetu aandike Kitabu cha kujutia kuingia mkataba huu mbovu wa Bandari.

PAROKO: Tusikae kimya sasa kusubiri Miaka 10 ijayo Rais wetu aandike Kitabu cha kujutia kuingia mkataba huu mbovu wa Bandari.

escrow one

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2014
Posts
1,473
Reaction score
2,868
Leo ikiwa ni Wiki ya Pili ya Tamko la Maaskofu kusomwa Makanisa yote ya Roman Catholic, nimevutiwa na Maneno aliyoyaongea Paroko mmoja kwenye Ibada " Tusikae kimya sasa kusubiri miaka 10 ijayo Rais wetu aandike Kitabu cha kujutia kuingia mkataba huu mbovu wa Bandari, tumkosoe mapema ili akija kuandika kitabu hicho aseme nilishauriwa ila nilikataa Ushauri"

Amenukuu Maneno yaliyopo kwenye Kitabu cha "My Life, My Purpose" cha Hayati Benjamin Mkapa alipojutia mambo mbalimbali ya Ovyo aliyoyafanya wakati wa Utawala wake ikiwemo kashfa maarufu ya EPA "Wahuni walitumia uaminifu wangu kwa chama kunishawishi nikubali Ninajisikia kuwa nilitumika na kusalitiwa..."

"Kama Wahuni waliweza kumlaghai Rais Mkapa kuingia Mikataba ya ajabu basi hawawezi kushindwa kumlaghai Rais Samia kwamba Mkataba huu una tija"

SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU
 
Nakazia
Akosolewe Tu Baadaye Aandike Kitabu Aseme NilikoselewA Nikakataa

Paroka Namletea Gallons 2 (Za Red Dry Wine ,White Dry Wine)
20230825_174108.jpg
 
Tusikae kimya sasa kusubiri miaka 10 ijayo Rais wetu aandike Kitabu cha kujutia kuingia mkataba huu mbovu wa Bandari, tumkosoe mapema ili akija kuandika kitabu hicho aseme nilishauriwa ila nilikataa Ushauri"
Naunga mkono hoja ✔️!! Haiwezekan yafanyike mamb ya hovyo wanaokosoa hayo mamb ya hovyo wanaitwa.. wasaliti, hawataki maendeleo ya Nchi, wanaleta taharuki, wanavuruga umoja wa kitaifa 🤣🤣🤣🤣 Halafu mwisho wa cku mtu anaandika kitabu na kukiri alifanya makosa? Kwann asikubali wakat anakosolew ili arekebishe makosa? Au unakula kwanza then kuongea badae?
 
Hapa kuna point nzuri sana tuisikilize na kuifanyia kazi
Naunga mkono hoja ✔️!! Haiwezekan yafanyike mamb ya hovyo wanaokosoa hayo mamb ya hovyo wanaitwa.. wasaliti, hawataki maendeleo ya Nchi, wanaleta taharuki, wanavuruga umoja wa kitaifa 🤣🤣🤣🤣 Halafu mwisho wa cku mtu anaandika kitabu na kukiri alifanya makosa? Kwann asikubali wakat anakosolew ili arekebishe makosa? Au unakula kwanza then kuongea badae?
 
Hii nchi itakuja kukaa Sawa kukiwa na uwajibikaji. Hili swala watu wanakosea wanaachwa wanadunda mitaani ni janga kubwa Sana

Leo hii ukimuuliza Kikwete akwambie faida ya gesi ya Mtwara aliyoenda kuichukua kwa mitutu ya bunduki sijui atajibu nini na bado ndio kwanza anajengewa bangaloo pwani baharini aishi kwa Amani. Hawa watu wanatakiwa wawajibishwe kwa matendo yao ili wengine waogope hata kujaribu. Hivi hadi leo ukimuuliza Kikwete hela za Escrow ni za serekali au si za serekali atajibu nini?

Magufuli kaharibu biashara ya korosho kusini yote ikazimika na nchi ikakosa mapato. Kaharibu biashara ya maduka ya kubadilishia fedha leo hii msemaji wa serekali aliyekuwa mstari wa mbele kusifu na kuabudu anasimama mbele ya vyombo vya Habari anasema tumerudisha bilioni 9 zilizonyang'anywa bureau de change, hivyo tu yaani. Just hivyo tu!

Huyo Mkapa anajifanya kujutia kwa kuandika kitabu, hivi Kuna mtu alikuwa mbabe kama Mkapa Enzi zake? Aliambiwa mara ngapi kuhusu ishu ya EPA mnakumbuka maneno yake ya ubabe aliyokuwa anayatoa? Kitabu makaratasi hayo sisi yanatusaidia nini sasa hivi baada ya Ile hela kupigwa?

Tutafanyana wajinga hadi lini hivi?
 
Hii nchi itakuja kukaa Sawa kukiwa na uwajibikaji. Hili swala watu wanakosea wanaachwa wanasunda mitaani ni janga kubwa Sana

Leo hii ukimuuliza Kikwete akwambie faida ya gesi ya Mtwara aliyoenda kuichukua kwa mitutu ya bunduki sijui atajibu nini na bado ndio kwanza anajengewa bangaloo pwani baharini aishi kwa Amani. Hawa watu wanatakiwa wawajibishwe kwa matendo yao ili wengine waogope hata kujaribu.

Magufuli kaharibu biashara ya korosho kusini yote ikazimika na nchi ikakosa mapato. Kaharibu biashara ya maduka ya kubadilishia fedha leo hii msemaji wa serekali aliyekuwa mstari wa mbele kusifu na kuabudu anasimama mbele ya vyombo vya Habari anasema tumerudisha bilioni 9 zilizonyang'anywa bureau de change, hivyo tu yaani. Just hivyo tu!
Wakati haya yanatendeka tunachosikia ni Mapambio, tenzi za sifa na kuabudu tu. Ukisema ukweli unaambiwa unapotosha
 
Leo ikiwa ni Wiki ya Pili ya Tamko la Maaskofu kusomwa Makanisa yote ya Roman Catholic, nimevutiwa na Maneno aliyoyaongea Paroko mmoja kwenye Ibada " Tusikae kimya sasa kusubiri miaka 10 ijayo Rais wetu aandike Kitabu cha kujutia kuingia mkataba huu mbovu wa Bandari, tumkosoe mapema ili akija kuandika kitabu hicho aseme nilishauriwa ila nilikataa Ushauri"

Amenukuu Maneno yaliyopo kwenye Kitabu cha "My Life, My Purpose" cha Hayati Benjamin Mkapa alipojutia mambo mbalimbali ya Ovyo aliyoyafanya wakati wa Utawala wake ikiwemo kashfa maarufu ya EPA "Wahuni walitumia uaminifu wangu kwa chama kunishawishi nikubali Ninajisikia kuwa nilitumika na kusalitiwa..."

"Kama Wahuni waliweza kumlaghai Rais Mkapa kuingia Mikataba ya ajabu basi hawawezi kushindwa kumlaghai Rais Samia kwamba Mkataba huu una tija"

SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU
Sawa sawa
 
Back
Top Bottom