Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah! Too hard!Nasisitiza waandishi wa habari mtengeni Mayalla na waandishi wote wenye vinasaba vya ukabila na wanaoshindwa kusimamia taaluma badala yake wanaishia kujipendekeza kwa kuhofia uhai wao.
Niombe wasomaji wangu muelewe kuwa sina nia mbaya ninapojaribu kuja na uchambuzi wa namna hii. Lengo langu ni kuoneshana kuwa nchi yetu iko hatarini hasa pale taaluma moja ambayo Taifa linawategemea wanaposigana katika jamii nani anayeumia zaidi!
Nakumbuka siku za hivi karibuni gazeti la the Economist lilikuja na habari ambazo Mkuu Pascal aliziita kuwa ni habari za uongo dhidi ya Rais wetu wa Tanzania.
Gazeti ilo liliwahi kuja na habari kuwa "Rais wa Tanzania hapendi kukosolewa"
Gazeti ilo baada ya kuchapishwa Pascal Mayalla alikuja na bandiko la kupinga habari ile huku akionesha jinsi ambavyo sio kweli Rais wetu anapenda kukosolewa.
Alikwenda mbali zaidi akamnukuu Rais wetu kuwa aliwahi kuwaambia wanahabari kuwa yeye anapenda kukosolewe ila akosolewe kwa Staha na kwa hoja.
Pascal Mayalla kwenye andiko lake anatolea mfano kuwa yeye Pascal Mayalla ni moja ya wanahabari ambao waliwahi kumkosoa Rais na Rais alikubali kukosolewa kwa kumjibu huku akimtania.
HOJA.
Kwanza lazma watu mjue kuwa andiko la Pascal kupinga habari ya the Economist ndio iliyoamsha watu na kuanza kufuatilia ni nani na yuko wapi anae ripoti habari hizo katika gazeti la the Economist?
Hapa naomba nieleweke,hata watumishi idara nyeti walianza kufatilia gazeti ilo baada ya kusoma bandiko la Pascal Mayalla hapa JF, na ndipo wakaja kugundua kuwa kumbe mwandishi wa habari zile na nyeti kupitia gazeti lile ni ndugu yetu Erick Kabendera.
Kwanini walifuatilia,kiukweli kilichoandikwa na mwandishi huyo wa habari kilikuwa na ukweli wa 100%ingawa huyu Ndugu Mayalla alikipinga kwa lengo la kujipendekeza kwa msukuma mwemzake.
Je, Pascal Mayalla alijua tangu awali kuwa Kabendera ndie anayeandika habari nyeti na kuziripoti The Economist na alishindwa kumuita kama mdogo wake na kumpa onyo?
Kimsingi kifungo cha Kabendera nadhani ni furaha kwa Mayalla kwani alimjua tangu awali na alishindwa kabisa kumuita na kumuonya ingawa wote wanatoka kanda ya ziwa.
Je, Pascal alijua Erick akifungwa tegemezi wake watalia na kusaga meno na wengine watajitokeza mitandaoni wakimlilia kwa kukosa hata fedha ya kununua Dawa?
Nadhani yote aliyajua ndio maana tangu Kabendera awekwe korokoloni hajawahi jitokeza popote kulaani kukamatwa kwa kijana huyu zaidi inasemekana ndio kwanza anatafuta makala zote zilizoandikwa huko nyuma na kuzisoma na kuzifafanua kwa vijana wa idara nyeti ili kijana azidi kubanwa.
Andiko la Mayalla dhidi ya kumtetea ndugu yake liko hapa JF linaudhi linaumiza kwani humo ndani anawataja wakosoaji wakubwa wa nchi hii ambao leo hii wamegeuziwa rangi ya unga wa ndere wao wanaita unga mweupe sasa huku wakila kuku kwa mirija.
Nasisitiza waandishi wa habari mtengeni Mayalla na waandishi wote wenye vinasaba vya ukabila na wanaoshindwa kusimamia taaluma badala yake wanaishia kujipendekeza kwa kuhofia uhai wao.
Natoa rai kwa Serikali ya Jamhuri kumwachia huru Kabendera. Tusipomdai kwa kiswahili tutawataka kwa kilugha, na hapo ndipo tutakapozuia kiongozi yeyote kuingia mkoa wa Kagera mpaka "omwana weitu mumutaishure.""
Who's Fredrick Kabendera ?
Narudia tena Fredrick Kabendera ni yupi huyo ?
Najipongeza kwa kukacha kusoma mashudu ya paschal Mayalla kwa muda mrefu sasa.Jamaa anaboa sana.
Time will tell,he will never be the President of this country Tanzania.
Aki like unistueKwani Paschal Mayala ndiye Kabander aliyemfungulia kesi ya utakatishaji.
Najua Paschal ni mbumbumbu katika sekta nyingi na huwa namkabili humu lakini siyo kama unavyotaka tuamini katika hili.
Cc:
Pascal Mayalla
Basha wako wa kwanzaWho's Fredrick Kabendera ?
What does Basha mean?Basha wako wa kwanza
Mwandishi wa habari hii ni mfano ya wazandiki waliojaa hapa JF.
Kwanini uone kuwa Eric Kabendera akiandika anakuwa ndio anatumia uhuru wa kujieleza lakini Pascal Mayala akiandika anakuwa anamtetea Msukuma mwenzake?
For sure kwa namna alivokuwa akihakikisha kila makala anaipandisha tena kwa mbwembwe, alikua anamjua kabisa Mwandishi ni nani.Hili hata mimi niliiona.Maandishi ya Paskali ni kama alikuwa na motive fulani behind,na tunaomjua Paskal ukiona anakomalia kitu ujue keshayajua ya nyuma ya pazia,hivyo anaamsha tu dude.Swali ni kuwa,hiki kilichotokea ndio alitaka kitokee?Namuachia mwenyewe.
Huyu Pascal Mayalla ni mkabila sana,mdini na mtu wa kujipendekeza.Inawezekana ni mmoja Wa wale jamaa hua simuelewi pascal
Umenisoma vizuri Mkuu?ndio maana nimeandika kama ni kweli,Nimemaanisha kama nia ilikua kumchongea itamtafuna tuKwani kosa gani kafanya pascal?Hivi hilo gazeti linasomwa na pascal pekee? Hivi nini maana ya uhuru wa maoni na demokrasia? Hebu twambie ni vipi Pascal Kamchongea kaflag?
If it's a genuine questionWho's Fredrick Kabendera ?