#COVID19 Pascal Mayalla: Viongozi wa Umma wajitokeze kuchanjwa, wasiopenda wakae kimya

#COVID19 Pascal Mayalla: Viongozi wa Umma wajitokeze kuchanjwa, wasiopenda wakae kimya

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Leo tarehe 02 Agosti 2021, waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari walipata chanjo dhidi ya UVIKO 19 pale Karimjee Dar.

Miongoni mwa waliopokea chanjo ni mwandishi nguli Pascal Mayalla. Katika mahojiano aliongea jambo muhimu sana kuhusu hili zoezi la chanjo.

Amewataka viongozi wote wa umma kujitokeza kuchanja na kama wapo wasiopendelea basi wanyamaze kimya. Kwa sababu chanjo inahusu nchi nzima na wanapaswa kuonyesha uwajibikaji wa pamoja.

Ameenda mbali zaidi kwamba, kama yupo kiongozi anapiga zoezi hili basi ajiweke pembeni yaani ajiuzulu kisha aanze kupinga zoezi hili.

Ninaona ni point muhimu sana katika kuhamasisha kinga dhidi ya UVIKO 19. Lakini pia kwenye kijiwe chetu cha Alkasusu wapo wanaodai Pasco analinyemelea tena jimbo la Kawe.

Lakini yote heri
 
Pasco Pasco wewe !!!

Kwani kua kiongozi maana yake uhuru wako wa uchaguzi HUNA? kwamba kwakua upo ndani ya Chama na serikali. Basi iwe ni lazima kupoteza uhuru wako wa uchaguzi?

Watu mna wivu na roho mbaya sanaaa, Mnataka Kikitokea cha kutokea, basi kitokee kwa wote?

Unachanjwa Poa.... Mwenzio hachanjwi poaaa... ( kila mtu ashinde mechi zake).

Haya mawazo ya Pasco maana yake hata baadae mtatishia kuwaachisha watu kazi ,kisa mnataka kuwalazimisha?

Huu ujinga, Mkome kabisa, mkome mara mia.
 
Hakuna muongozo Wala elimu iliyotolewa Kwa wanaohitajika kuchanjwa. Haijulikani wanaohitajika kuchanjwa wawe na afya Gani,umri Gani,je wakichanjwa waendelee kuvaa barakoa au la? Je wataugua tena au la? Je ambao Bado wanaumwa je wachanjwe? Je ukichanjwa ukapigwe lager au la? Je ukichanjwa Sasa utachanjwa tena ? Kama jibu ni ndio ni lini? Na kwanini uchanjwe tena? Je kwanini ujaze fomu ndipo uchanjwe?Viongozi hawana majibu ya maswali haya. Hakuna muongozo ulio wazi.
 
Wananchi wa Kawe siku zote wanabambikiwa wabunge ..miaka yote toka Hilo Jimbo lianzishwe..
Sijui kama kuna siku watapata mbunge mkazi wa Kawe...
Pasco ni mkazi wa Kawe. Niliwahi kuwa jirani yake
 
Wananchi wa Kawe siku zote wanabambikiwa wabunge ..miaka yote toka Hilo Jimbo lianzishwe..
Sijui kama kuna siku watapata mbunge mkazi wa Kawe...
kwann unaikanyaga katiba
Kama unahuruma nao wambie waende shule ili wachangamke lasivyo wataendeleaga na ngomazao nandoa zautotoni mungu hadi arudi
 
Leo tarehe 02 Agosti 2021, waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari walipata chanjo dhidi ya UVIKO 19 pale Karimjee Dar.

Miongoni mwa waliopokea chanjo ni mwandishi nguli pasco Mayala. Katika mahojiano aliongea jambo muhimu sana kuhusu hili zoezi la chanjo.

Amewatala viongozi wote wa umma kujitokeza kuchanja na kama wapo wasiopendelea basi wanyamaze kimya. Kwa sababu chanjo inahusu nchi nzima na wanapaswa kuonyesha uwajibikaji wa pamoja

Ameenda mbali zaidi kwamba, kama yupo kiongozi anapiga zoezi hili basi ajiweke pembeni yaani ajiuzulu kisha aanze kupinga zoezi hili.

Ninaona ni point muhimu sana katika kuhamasisha kinga dhidi ya UVIKO 19. Lakini pia kwenye kijiwe chetu cha Alkasusu wapo wanaodai Pasco analinyemelea tena jimbo la Kawe....

Lakini yote heri
Hivi Mama hajamteua hata tu kuwa DED?
 
tukachanje kwa uhai wetu, tuache maneno mengi yasiyo na maaana.
chanjo ni salama lkn hulazimishwi kama hutaki kaa kimya wenye akili wachanjwe.
 
Mbona hii Chanjo imeingizwa kwenye Siasa wakati ni jambo muhimu la kutolewa ufafanuzi km anavyofanya Gwajima ambae ni opposer sasa wale proposer wanatakiwa watetee kwa hoja na sio Mipasho
Pascal Mayalla amekuwa mtu wa mipasho tu.akili ameishaiweka mfukoni. Anataka wasiotaka chanjo wanyamaze kwa nini na wanaotaka nao wasinyamaze? Huku ni kuwaza kipumbavu. Kama yeye amechanjwa anaongea kwa nini na wasiochanja nao waongee? Huyu jamaa huwa anasema amesoma sheria lakini sioni kama alielimika.

Katiba inasema kila mtu ana uhuru wa kuongea. Chanjo ni hiyari. Kama kuna wanaohamasisha kuchanja ni kwa nini wasiwepo wenye kuhoji kuhusu huko kuchanjwa? Wameteuliwa wakurugenzi jamaa ameachwa labda teuzi zijazo.
 
Leo tarehe 02 Agosti 2021, waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari walipata chanjo dhidi ya UVIKO 19 pale Karimjee Dar.

Miongoni mwa waliopokea chanjo ni mwandishi nguli pasco Mayala. Katika mahojiano aliongea jambo muhimu sana kuhusu hili zoezi la chanjo.

Amewatala viongozi wote wa umma kujitokeza kuchanja na kama wapo wasiopendelea basi wanyamaze kimya. Kwa sababu chanjo inahusu nchi nzima na wanapaswa kuonyesha uwajibikaji wa pamoja

Ameenda mbali zaidi kwamba, kama yupo kiongozi anapiga zoezi hili basi ajiweke pembeni yaani ajiuzulu kisha aanze kupinga zoezi hili.

Ninaona ni point muhimu sana katika kuhamasisha kinga dhidi ya UVIKO 19. Lakini pia kwenye kijiwe chetu cha Alkasusu wapo wanaodai Pasco analinyemelea tena jimbo la Kawe....

Lakini yote heri
Binafsi brother Pascal Mayalla nimekuelewa sana iyo dhana ya collective responsibility kwa top government officials especially kwa wale wa presidential appointees
 
Wapate wasomi kama Msukuma na Kibajaji?
Ujuavyo hata katiba imepewa majina

#chokochoko(madame tz)
# Ugaidi (polisi tz)

Mwingine MTANZANIA mwema anashauri tupate katiba mpya ili tuondokane na ujinga wa darasa lapili kua wabunge

Ameitwa GAIDi
Kama kweli mungu ndo huyu huyu basi ngoja niendelee na novena yangu
 
Back
Top Bottom