Pasipoti za kielektroniki 193,645 zatolewa ndani ya miaka miwili

Pasipoti za kielektroniki 193,645 zatolewa ndani ya miaka miwili

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Idara ya Uhamiaji Tanzania imetoa pasipoti za kieletroniki 193,645 katika miaka miwili ya uongozi wa
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza jijini Dares Salaam, Ofisa Habari wa Idara hiyo, Mrakibu Paul Mselle alisema pasipoti hizo zimetolewa kwa Watanzania waliotaka kusafiri.

"Pasipoti za kielektroniki 193,645 zimeleta mageuzi makubwa, raia wa Tanzania waliohitaji kusafiri nje ya nchi walipata huduma kwa madhumuni mbalimbali,"alisema.

Mselle alisema katika pasipoti za kawaida idara hiyo ilitoa hati hizo za kusafiria 191,822 na kiutumishi 233.

Mselle alisema pasipoti za kidiplomasia zilitolewa 1,582 katika kipindi hicho na pasipoti maalumu ilitoa nane.

Alisema kazi hiyo imefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria Sura ya 42 ya Mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2018.

Pia Mselle alisema wamefanya maboresho ya sheria, kitaasisi, kimuundo na mifumo ya utendaji kazi. Aidha, aliwaomba Watanzania walioomba pasipoti kwenda ofisi za idara hiyo kuzichukua.
 
Idara ya Uhamiaji Tanzania imetoa pasipoti za kieletroniki 193,645 bkatika miaka miwili ya uongozi wa
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.
Ni SAWA ndio lakini je waTanzania walioko kuendana na takwimu za sensa ya mwaka Jana ni kubwa kulingana na hii namba. Passport ni haki ya Mtanzania! Wangeleta namba ya Millioni 10 + ingeeleweka. Hapo Kuna urasimu mkubwa sana.

Na unaposema ndani ya miaka miwili ya Rais una maana gani??
 
Aliekua demu wangu nimemtafutia passport walimsumbua kinoma mpaka kakata tamaa akaamua aolewe hukohuko, yaani kafaya hatua zote mpaka control number kapewa ila wamemuekea ngumu kutokana na rangi yake, Uhamiaji rohombaya sio poa, ndio maana hambariki kwa rohombaya
 
Hii ni aibu kubwa kwa watendaji wa uhamiaji yani katika Watanzania wote hao hata pasi milioni 5 hazijafika watendaji wanapaswa kujipima kama wanatosha wanaendesha mambo kwa mazoea Sana. Hiki ni chanzo kikubwa sana cha mapato kama watendaji wakiondoa ufanyaji kazi kwa mazoea kwanini watu wasipewe pasi za kusafiria maana ni haki ya mtu kamą amekidhi masharti na vigezo. Kwa ufupi tu uhamiaji wamefeli pakubwa Saną katika hili bora wasitoe hizo takwimu zao wakabaki nazo kwenye mashubaka yao maofisini tunashindwa kuiga hata kwa majirani waliofanikiwa kwenye hili tunaona ufahari raia kukosa pasi karne ya 21. Mfano raia milioni 2 wakipewa pasi kwa ada ya 150,000/- : 2,000,000 x 150,000=300,000,000,000 (Bilioni 300)
 
Aliekua demu wangu nimemtafutia passport walimsumbua kinoma mpaka kaolewa hukohuko, yaani kafaya hatua zote mpaka control number kapewa ila wamemuekea ngumu kutokana na rangi yake, rohombaya sio poa kmmk

Hili nchi kuna mijitu mibaguzi na roho mbaya hilo linajulikana mzee baba, na hawa hawa ndio wanamfanya mama yetu aonekane hafai.

Mwenyezi Mungu azidi kumpa afya tele mama samia, hao wenye viburi, roho mbaya na majivuno itafika mwisho wao, wasifikiri watadumu milele kwenye hizo sekta .
 
Ni SAWA ndio lakini je waTanzania walioko kuendana na takwimu za sensa ya mwaka Jana ni kubwa kulingana na hii namba. Passport ni haki ya Mtanzania! Wangeleta namba ya Millioni 10 + ingeeleweka. Hapo Kuna urasimu mkubwa sana.

Na unaposema ndani ya miaka miwili ya Rais una maana gani??
Je utayari wa Watanzania kupata pasipoti ukoje? sawa ni haki ya kila mtanzania lakini unapaswa kupewa hati ya kusafiria pale ambapo una "proof" ya safari sio document ya kupewa uweke kabatini
Then kama huelewi "miaka miwili ya Rais Samia" sina la kuongeza maana inajitosheleza
 
Mreta mada mnazidi kumchafu huyo bibi yenu kwa kumpamba pamba na taharifa zisizo chakachuliwa kwanza,Unakuja kumpongeza kisa passport laki .1.9 wakati tupo watanzania tupo mln 61+?.
Kama kila miaka 2 anaweza kufanya kazi kidogo hivyo si ataondoka madarakani ata kujenga shule yenye vyumba 7 hajamaliza?
 
Idara ya Uhamiaji Tanzania imetoa pasipoti za kieletroniki 193,645 bkatika miaka miwili ya uongozi wa
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza jijini Dares Salaam, Ofisa Habari wa Idara hiyo, Mrakibu Paul Mselle alisema pasipoti hizo zimetolewa kwa Watanzania waliotaka kusafiri.

"Pasipoti za kielektroniki 193,645 zimeleta mageuzi makubwa, raia wa Tanzania waliohitaji kusafiri nje ya nchi walipata huduma kwa madhumuni mbalimbali,"alisema.

Mselle alisema katika pasipoti za kawaida idara hiyo ilitoa hati hizo za kusafiria 191,822 na kiutumishi 233.

Mselle alisema pasipoti za kidiplomasia zilitolewa 1,582 katika kipindi hicho na pasipoti maalumu ilitoa nane.

Alisema kazi hiyo imefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria Sura ya 42 ya Mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2018.

Pia Mselle alisema wamefanya maboresho ya sheria, kitaasisi, kimuundo na mifumo ya utendaji kazi. Aidha, aliwaomba Watanzania walioomba pasipoti kwenda ofisi za idara hiyo kuzichukua.
UPATIKANAJI WA PASSPORT BADO WATENDAJI WENU WANADAI RUSHWA UKWELI BADO KUNA KERO KUBWA
 
Ni SAWA ndio lakini je waTanzania walioko kuendana na takwimu za sensa ya mwaka Jana ni kubwa kulingana na hii namba. Passport ni haki ya Mtanzania! Wangeleta namba ya Millioni 10 + ingeeleweka. Hapo Kuna urasimu mkubwa sana.

Na unaposema ndani ya miaka miwili ya Rais una maana gani??


Kwa takwimu za huyo afisa uhamiaji maana yake kwa mwaka walitoa passport 96,900.kwa wastani


Watanzania tuko milioni 60

Wao kutoa passport kwa Watanzania milioni 10 kwa spidi hiyo itawachukua miaka 103 kwa wao kufikia lengo la kutoa passport milioni kumi

Kuhakikisha Watanzania hata milioni.tano wanapata passport itawachukua miaka 50 kufikia hilo lengo kwa spidi hiyo

Very sad
 
Idara ya Uhamiaji Tanzania imetoa pasipoti za kieletroniki 193,645 bkatika miaka miwili ya uongozi wa
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza jijini Dares Salaam, Ofisa Habari wa Idara hiyo, Mrakibu Paul Mselle alisema pasipoti hizo zimetolewa kwa Watanzania waliotaka kusafiri.

"Pasipoti za kielektroniki 193,645 zimeleta mageuzi makubwa, raia wa Tanzania waliohitaji kusafiri nje ya nchi walipata huduma kwa madhumuni mbalimbali,"alisema.

Mselle alisema katika pasipoti za kawaida idara hiyo ilitoa hati hizo za kusafiria 191,822 na kiutumishi 233.

Mselle alisema pasipoti za kidiplomasia zilitolewa 1,582 katika kipindi hicho na pasipoti maalumu ilitoa nane.

Alisema kazi hiyo imefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti na Hati za Kusafiria Sura ya 42 ya Mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2018.

Pia Mselle alisema wamefanya maboresho ya sheria, kitaasisi, kimuundo na mifumo ya utendaji kazi. Aidha, aliwaomba Watanzania walioomba pasipoti kwenda ofisi za idara hiyo kuzichukua.
Upuuzi mwingine huu! Kwa hiyo passport nazo ni manufaa ya Samia kuwa madarakani? Baadaye mutataja na idadi ya chupi zimeongezeka kwa sababu ya Samia!
 
Mm ni miongoni wa hao waliopata. Na bila rushwa ni vigezo tu vilikamilika. Piga kazi mama kanyaga twende
 
Katika kitengo kilichooza basi ni hiki, uhamiaji, mazee kuna wanaume malaya hii idara, sijui wana shida gani mbwa hawa
Wana tamaa hatari, mm mtu wangu nilikua nataka kumleta huku yaani kafanya process zote mpaka control number kapewa, eti mwisho wanasema hawawezi kuiprint passport wanafkiria demu ni raia wa Omani, hapo nilitoa hela wamekula alaf kimya, dem juzi kaolewa hukohuko, imeniuma sana
 
Wana tamaa hatari, mm mtu wangu nilikua nataka kumleta huku yaani kafanya process zote mpaka control number kapewa, eti mwisho wanasema hawawezi kuiprint passport wanafkiria demu ni raia wa Omani, hapo nilitoa hela wamekula alaf kimya, dem juzi kaolewa hukohuko, imeniuma sana
Wasumbufu ukienda ke mpk wakufunue na wanatumia ubabe, nilikomaa hata kufikia kutaka kutemeshwa kazi, ni washenzi sana hap watu

Japokuwa huyo mtu wako kuolewa kwa sababu kakosa passport kuna kanamna sio sababu ya uhamiaji
 
Wasumbufu ukienda ke mpk wakufunue na wanatumia ubabe, nilikomaa hata kufikia kutaka kutemeshwa kazi, ni washenzi sana hap watu

Japokuwa huyo mtu wako kuolewa kwa sababu kakosa passport kuna kanamna sio sababu ya uhamiaji
Ndio, ameshakaa sana, amevumilia sana, mm siwezi kumlaumu coz ameshakataa posa nyingi akinisubiria, pia kakata tamaa kwa sababu walikua taari wanamsumbua sana
 
Ndio, ameshakaa sana, amevumilia sana, mm siwezi kumlaumu coz ameshakataa posa nyingi akinisubiria, pia kakata tamaa kwa sababu walikua taari wanamsumbua sana
Hii ni mada nyingine! Yuko wapi yeye na wewe uko wapi?
 
Aliekua demu wangu nimemtafutia passport walimsumbua kinoma mpaka kakata tamaa akaamua aolewe hukohuko, yaani kafaya hatua zote mpaka control number kapewa ila wamemuekea ngumu kutokana na rangi yake, Uhamiaji rohombaya sio poa, ndio maana hambariki kwa rohombaya
Uhamiaji ni mapumbavu Sana. Hii ni Haki ya kila mtu, sio wanauliza maswali ya kijinga Sana!
 
Back
Top Bottom