Ndugu zangu Watanzania,
Hayo ni maneno yaliyotamkwa kwa ujasiri mkubwa sana na Mheshimiwa Paul Makonda Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa CCM Taifa ,ambaye pia ndiye kijana jasiri zaidi kuwahi kutokea katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la sahara,lakini pia ambaye Watanzania wengi wanatamani awe Rais Wa Taifa letu baada ya Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania mama samia suluhu Hasssan kumaliza Muda wake mwaka 2030.
Ambapo Mheshimiwa makonda akiwa mkoani njombe amesema kuwa baada ya kukamilisha ziara yake atarejesha mrejesho kwa Mheshimiwa Amiri jeshi mkuu na Rais wetu Mh mama Samia kuwa niliko pita huko nimeona huyu na huyu hawatufai kuendelea katika nafasi zao maana wameshindwa kazi na kutimiza majukumu yao na wanaichonganisha serikali yako na wananchi.
Amesema kuwa kwa hiyo ukiona umetenguliwa katika nafasi yako na yeye Mheshimiwa makonda alipita katika eneo lako basi ujuwe ni yeye kapelekea hivyo kutokana na kushindwa kwako kwa kazi akikokubaini.kwa hiyo usimlaumu Rais au makamu au nani.
Akasema pia kuwa ni bora watu wamchukie kwa furaha ya wengi ambao ni wananchi na kwamba kilichopandishwa kwa maombi hakiwezi kushushwa kwa Majungu.
Ndugu zangu Watanzania niliwaonyeni sana humu jukwaani watumishi wa umma na viongozi tangia awali kuwa ziara za Mheshimiwa Makonda zichukulieni kwa uzito mkubwa sana,msilete nyodo wala uzembe ,kwa kuwa zitawazoa na kuwatupa nje huko.
Niliwaambia kwa kuwasisitiza sana kuwa Mheshimiwa Makonda huwa hataki mchezo wala kulea uzembe wala kuvumilia ubabaishaji . Mh Makonda ni kiongozi asiyeogopa wala kuona haya kusema ukweli hata kama utamchukia lakini yeye kwake nyeupe ni nyeupe na kijiko ni kijiko tu.
Kaeni mkao wa kula kuvuna matunda yenu kwa kadri ya kazi zenu mnazofanya na kutekeleza kulingana na majukumu yenu.maana wakatii mwingine chama kinachukiwa kwa sababu tu ya uzembe ya watu wachache wanaokuwa wameshindwa kutimiza vyema majukumu yao waliyopewa na kuaminiwa.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
View attachment 2898762View attachment 2898763View attachment 2898765View attachment 2898768