Paul Makonda yupo mbugani anakula bata

Paul Makonda yupo mbugani anakula bata

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda amepost video fupi katika ukurasa wake wa Instagram akionyesha yupo mbugani akiwa anakula maisha.

Japo hajaeleza kuwa yupo katika mbuga ipi lakini video inaonyesha ni mazingira ya mbugani, na hajaandika chochote kuelezea video hiyo ambayo ameonekana akipata burudani ya muziki.

Wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni ilitoa kibali cha kuchapisha gazetini wito wa kumuita Mahakamani Makonda na kuubandika wito huo katika Makazi yake ya Dar na Kijijini kwao Koromije.

Katika kesi hiyo, Saed Kubenea anaomba kuweza kumshtaki Paul Makonda japokuwa Makonda hajaonekana Mahakamani. Kesi, ambapo Mahakama imesogeza mbele suala hilo hadi Machi 2, 2022.

Makondaa.JPG
 
Aina ya kesi aliyonayo haina nguvu. Kubenea alipaswa kumshinikiza dpp kumfungulia jinai bashite.

Jambo ambalo haliwezekani hata kidogo. Maana ccm ina utamaduni wao kulindana. Na huwezi kumtenganisha huyo Dpp na chama! Wote ni walewale tu. Hata Sabaya ni basi tu imetokea wakamgeuka!
 
Hapo ni tarangire kmaanina!! Huyo aliyempiga picha hakumwambia asije mjini? Akifikiria kuja mjini ataishia kisongo,hata mbauda havuki
 
Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda amepost video fupi katika ukurasa wake wa Instagram akionyesha yupo mbugani akiwa anakula maisha.

Japo hajaeleza kuwa yupo katika mbuga ipi lakini video inaonyesha ni mazingira ya mbugani, na hajaandika chochote kuelezea video hiyo ambayo ameonekana akipata burudani ya muziki.

Wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni ilitoa kibali cha kuchapisha gazetini wito wa kumuita Mahakamani Makonda na kuubandika wito huo katika Makazi yake ya Dar na Kijijini kwao Koromije.

Katika kesi hiyo, Saed Kubenea anaomba kuweza kumshtaki Paul Makonda japokuwa Makonda hajaonekana Mahakamani. Kesi, ambapo Mahakama imesogeza mbele suala hilo hadi Machi 2, 2022.

na hapa yuko mbuga gani ?

Mtoto_wa_kiume_unaogopa_Mahakama%3F_Toka_huko_uliko_jificha_brother._Tutakuweka_makofi!.jpg
 
Masikini na wenye chuki tuendelee kununa, kuvimba na hadi kupasuka. Umasikini ni mbaya sana.

Siyo kila mtu anaye mdiss Makonda, ni maskini wewe! Utuambie kwanza huo utajiri aliupata wapi? Maana miaka michache tu iliyopita alikuwa ni omba omba tu! Kiasi cha kupewa hifadhi na Mzee Samwel Sitta, JK, nk!!

Makonda ni kiburi! Lakini pia ni mjivuni. Hivyo anastahili kabisa kuchukiwa na wale alio wadharau wakati ana yale mamlaka yake ya kupewa.
 
Back
Top Bottom