Paul Mselle: Wenye changamoto ya kucheleweshewa “Passport” wafike ofisini watapata majibu

Paul Mselle: Wenye changamoto ya kucheleweshewa “Passport” wafike ofisini watapata majibu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano, Mrakibu wa Uhamiaji, Paul John Mselle amesema Watu ambao wamekuwa na changamoto ya kudai kucheleweshewa kupata Pasi ya Kusafiria (Passport) wanatakiwa kufika Ofisi za Uhamiaji waelezee changamoto zao.

Amesema hayo wakati akijibu hoja za Wadau wa JamiiForums waliodai kuwa kumekuwa na ucheleweshwaji wa kutolewa kwa Passport kwa zaidi ya miezi mitatu hadi Sita huku baadhi wakidai wamekuwa wakijibiwa kuwa hakuna material ya kuchapisha Pasi mpya.

Mselle amesema “Wafike ofisini, tumesikia hizo taarifa, kuna wakati mtu anaweza kulalamika hata Passport hajaomba, anasikia kutoka kwa Mtu mwingine kuwa kuna shida fulani naya anasema tu bila kuwa na Ushahidi.”

Anaongeza “Nachelea kutoa hayo majibu wanayosema, suala la Passport ni suala tofauti kidogo, wanapofika ofisini watakutana na ufafanuzi mzuri zaidi.”

Kusoma Hoja za Wadau bofya hapa:
~
Miezi mitatu nafuatilia Passport mpya, napigwa kalenda tu, ni kweli UHAMIAJI mmeishiwa material ya kuprinti Passport mpya?
~ Upatikanaji wa Passport kwenye ofisi ya Uhamiaji pale Kibaha Mjini bado ni changamoto
 
Ngoja niende mie

Maana nina safari yangu

Sio muda naenda US kumsalimia Prof Janab wa JF

Kajificha Tandale kwa Mtogole halafu anadai yuko US
 
Angeweza kutoa majibu ya Jumla pia..., kwamba wanayosema ni kweli au sio kweli..., by the way hao waliokuwa wanapewa hayo majibu walipewa wakiwa ofisini au kwenye simu ya upepo ?
 
Mimi nina mwaka wa tatu huu, eti wanataka barua ya shule niliyomaliza darasa la saba mwaka 1983 ndio nipewe passport,

Malipo nimefanya, hatua zote ziko safi, nimeleta barua pia imekataliwa, wanataka barua sasa itoke wizara ya elimu,
Yaani kwa kweli ni shida, kuliwa ni lazima hayo mengine mnajitetea tu,

NB:
Mwaka wat tatu huu sijaipewa
 
Mkoa wa Arusha hakuna aliyefanikiwa kupata passport bila rushwa.
 
Mimi nina mwaka wa tatu huu, eti wanataka barua ya shule niliyomaliza darasa la saba mwaka 1983 ndio nipewe passport,

Malipo nimefanya, hatua zote ziko safi, nimeleta barua pia imekataliwa, wanataka barua sasa itoke wizara ya elimu,
Yaani kwa kweli ni shida, kuliwa ni lazima hayo mengine mnajitetea tu,

NB:
Mwaka wat tatu huu sijaipewa
ulifanikiwa mkuu au bado unapigwa kalenda
 
Back
Top Bottom