PayTrade ya tradecarview

PayTrade ya tradecarview

Wasiliana na japanese car auction agent wapo arusha wanadili na minada moja kwa moja ni guarantee kupata gari watumie email yako utatumiwa gari unayotaka na kiwango cha pesa unachotaka .gari japan huuzwa kwa njia za minada kwa kupitia kwenye computer zilizounganishwa moja kwa moja ,minada huanza jumatatu hadi jumamosi .kumbuka huwezi ka access hapa hadi uwe member .

Hawa japanese car auction agent kuwa mwangalifu sana. Lucas nao wapo pale Mikocheni Shoppers Centre, lakini ni watafutaji zaidi kuliko kufanya biashara ya kwali ndio uswahili. Kwa walioishi bongo tu uswahili huo wameuzoea, lakini waliotoka kidogo kuonja wenzetu wanavyofanya biashara hawa wa bongo ni wachovu wa kutafuta pesa kwa mkato na kwa njia mteremko bila kuithamini biashara yao. Ninachoandika nakifahamu na nimeshuhudia watu hao. Ukijiamini ku-deal nao okay, lakini kwangu nimeshawatolea nje.

Tatizo wengi wetu hawana jinsi wala option ya kuagiza gari hivyo inabidi kuwatumia tu mradi upate gari, lakini je ni gari bora unayotazamia au mradi lina sura nzuri kwa nje wakati baada ya muda mfupi unatembea na koleo mkononi huku umeshika usukani.
 
Paytrade ni insuarance inayomilikiwa na wenye mtandao yaani tradecarview, malipo yao si chini ya usd 150 hata kama ni kama unanua gar la cif 200 , ni wazur sana coz unakuwa huna bp, utapeli ulizidi ndo maana wakaanzisha paytrade
 
Tutakuaminije? We bwana acha wizi!

Nimeshazungumza mimi sifanyi biashara ya kuagiza magari ya watu. Nilichofanya kuwasaidia wengine njia ambayo mie nimetumia ambayo haijaniumiza kichwa na nimeridhika nayo. Vinginevyo unaweza kuwatumia Lucas wa Mikochoni ambao wapo tradecarview utalipa pesa pale na utachagua gari online pamoja nao watakusaidia kkulipata haraka na kwa ufanisi, lakini tatizo la ubora litabaki palepale kwa vile tunaangalia picha ya gari bila ukaguzi wa ubora.
 
Paytrade ni insuarance inayomilikiwa na wenye mtandao yaani tradecarview, malipo yao si chini ya usd 150 hata kama ni kama unanua gar la cif 200 , ni wazur sana coz unakuwa huna bp, utapeli ulizidi ndo maana wakaanzisha paytrade

Hapa jamii forums na watanzania kwa vile tumezoea kutapeliana wanafikiri kila mwenye kutoa maoni na mapendekezo mazuri ni kutaka kupata kitu au kutapeli. Sory for that.
 
Acha kuwatisha wenzako,Paytrade is guarnteed.Kuwatumia watanzania ni sawa lakini nimekuja gundua wengi waTz nao wa huko wanaongeza sana cha juu,kwani wengi hulipwa commission na washikaji wanaowapelekea wateja.......for instance niliwahi kuwa na jamaa mmoja tunabrowse hii trade car view website kila kampuni alikuwa anaitoa kasoro,mwisho wa siku akataka anilengeshe kwa mshkaji wake,at the end through my patience and searching nikapata gari usd1500 cheaper tofauti na mshkaji wake wa huko Japan aliyeniunganishia.......sometimes dealing straight na credible companies is better than hawa ndg zetu WaTz walio huko,kwani zimwi likujualo.........:coffee:


Kuna malalamiko mengi na wengi kupoteza fedha zao kwa njia hii. Kwani unafanya biashara na mtu usiyemjua, huna pa kuanzia kufuatia pesa zako. Wengine wanaletewa magari tofauti na waliyoyachagua. Huna hakika na ubora wa gari unayoiona kwenye picha kwa vile mfanya biashara anataka gari litoke nawe huna wa kukuhakikishia kama gari ni salama au kanyagaboya.

Nilikuwa na mpango wa kufanya hivyo, lakini nilisita kwa vile siku hizi ziwezi kuamini sana njia ya kulipa online kiwango kikubwa cha pesa kutokana na wengi kuingizwa majaribuni na kuishia kupata presha. Wenye bahati hubahatika na asiye na bahati ndo hivyo tena. Ujeavyo wauzao magari si kampuni mmoja bali na watu binafsi na makampuni mbalimbali ya car dealers.

Ushauri:
Uzoefu wangu ni bora kumtumia mtu mwaminifu mtanzania aishiye huko Japan ambaye anafanya kazi kwenye moja ya makampuni ya dealership. Kuna mmoja ambaye namfahamu mwaminifu, mwazi na atakutafutia gari unalotaka na kwa kiwango cha kuridhisha. Utaweza kuongea naye kwa simu na kuwa na mawasiliano kwa email naye kwa nini kinatakiwa, na atakupa msaada wa kufaa. Hata wamissionari wanamtumia sana mtu huyo. Mimi mwenyewe nimeagiza gari kutumia yeye alinipa ushauri mzuri, na kunipa tahadhari kwa baadhi ya magari niliyofikiria mazuri kumbe ni bomu tupu. Alinichagulia gari zuri na nilipolichukua bandarini Dar sikuamini na walioona walifikiri ni jipya kwa jinsi alivyokuwa makini katika kufanya uchaguzi makini.

Yeye anafanya dealership kwa hiyo hiyo tradecarview, lakini mimi niliweza kulipa moja kwa moja kwenye kampuni nilikonunua gari kupitia kwake na kwa gharama nafuu. Huyu Kaka namfahamu kwa miaka mingi wakati yupo Tanzania, na sasa ndio yuko Yokohama - Japan.

Anayetaka kuagiza gari kupitia kwa huyu ndugu mtanzania halisi ambaye ni mwaminifu na mcha Mungu,
anipm nimpe contact zake. Siwezi kuanika tu hapa kwa vile hajaniruhusu kufanya hivyo. I'm serious, nawahurumia watanzania wenzangu, pesa yako umeitokea jasho unauchungu nayo. Thanks.
 
Acha kuwatisha wenzako,Paytrade is guarnteed.Kuwatumia watanzania ni sawa lakini nimekuja gundua wengi waTz nao wa huko wanaongeza sana cha juu,kwani wengi hulipwa commission na washikaji wanaowapelekea wateja.......for instance niliwahi kuwa na jamaa mmoja tunabrowse hii trade car view website kila kampuni alikuwa anaitoa kasoro,mwisho wa siku akataka anilengeshe kwa mshkaji wake,at the end through my patience and searching nikapata gari usd1500 cheaper tofauti na mshkaji wake wa huko Japan aliyeniunganishia.......sometimes dealing straight na credible companies is better than hawa ndg zetu WaTz walio huko,kwani zimwi likujualo.........:coffee:

Mimi siishi Japan, na sina nia ya kumtafutia mtu wateja, ila hapa kila kinachowezekana kizuri kusaidiana ni jambo zuri na ndivyo nilivyofanya.

Sina nia ya kumtisha mtu, nilichosema kimetokea ni kweli, kama we umebahatika hivyo si kila mmoja atabahatika. Kumbuka mfanya biashara ni mfanyabiashara tu, anachotaka mali aliyo nayo iuzike na kesho alete nyingine.

Magari yaliyotumika huuzwa 'AS IS" maana yake lolote litakalotokea kama gari ni mbovu mwuzaji hahusiki, ndio maana ya kusema unaweza pata gari zuri au kanyagaboya. Ukweli tuuweke wazi tusiufunike halafu wenzetu wapate hasara ka kila walichotaabikia kwa miaka.

Gari zuri ni lile ambalo mtu mwenye uzoefu analikagua katika mambo ya msingi ya kawaida kuona kama linafaa na linaweza kufanya kazi muda mrefu au la. Huo ndio ukweli wenyewe. Thanks kwa kunielewa, na asiye nielewa ni haki yake. Hapa ni kuelimishana.
 
Hapa jamii forums na watanzania kwa vile tumezoea kutapeliana wanafikiri kila mwenye kutoa maoni na mapendekezo mazuri ni kutaka kupata kitu au kutapeli. Sory for that.

Taratibu baba - mfumo wa kijanja wa nchi umetuaharibu akili hata jambo genuine lazima tuhoji - kwa hoja hii haijalishi unatoa mapendekezo mazuri au vipi lazima machale yatucheze tu
 
sasa sikia usiangaike mie nimeshaagiza mara mbili kwenye hiyo site......kuna jamaa anaitwa patrick ni wakala wa tradecarview Tanzania, ofisi zao zipo pale opposite na shule ya mbezi beach secondary, mitaa ya tangibovu........for more details utanambia
 
sasa sikia usiangaike mie nimeshaagiza mara mbili kwenye hiyo site......kuna jamaa anaitwa patrick ni wakala wa tradecarview Tanzania, ofisi zao zipo pale opposite na shule ya mbezi beach secondary, mitaa ya tangibovu........for more details utanambia


Tatizo linabaki pale pale, maana gari haichunguzwi ubora, unachoweza kufanya pamoja na huyo Patric ni kubrowse mtandaoni na kuchagua mvuto wa gari bila kujua undani wa gari kama litakufaa kwa muda gari.

Tofauti na kumtumia mtu ambaye atalichunguza gari na kukuhakikishia ubora. Haya magari ya "as is" baada ya kutumia pesa nyingi za kulikomboa bandarini utaishia kuliweka juu ya mawe baada ya muda mfupi, kwani wengi wetu Tanzania hatuna uzoefu na ubora wa magari, tunavutiwa na mtindo, mwundo na rangi bila kuangalia ubora.

Nchi zilizoendelea gari huzeeka injini na transmisheni, lakini bodi lake linaonekana lenye mvuto kutokana na kuwa na kiwango cha barabara zote kuwa cha hali ya juu kisichochakaza body la gari.
 
maneno mengi hayavunji mfupa njoo tufanye biashara .chunga pesa na upate unachohitaji kwa ubora unaotaka ,wakati muafaka .arusha no maneno mengi lipa deposit kazi inaanza haraka sana .jaribu leo japanese car auction agent arusha
 
ukishaliwa hela zako uje na karatasi tutakusaidia kuwatafuta hawa jamaa kule japan ila kumbuka hawana ofisi kule ofisi iko kwenye laptop komputa mpakato
 
Back
Top Bottom