Pendekezo:Kikosi maalum cha kupambana na ugaidi

Pendekezo:Kikosi maalum cha kupambana na ugaidi

Tumesikia mmoja wa magaidi huko Garissa alikuwa mtanzania.

Pia tumesikia yule mchinjaji wa ISIS alipita au kujaribu kuingia Tanzania.

ushauri wangu bado ni valid.
 
Tanzania kwa mara nyingine tena inashuhudia tukio la pili la kigaidi ambalo limevuta hisia kutoka jamii mbalimbali za kimataifa.ukiacha tukio la kulipuliwa kwa ubalozi wa marekani utaona tukio la Olasiti linazidi kudhihirisha kuwa Tanzania yaweza kuwa eneo linalotoa mwanya kwa magaidi kupanga na kutekeleza mashambulizi ya kigaidi iwe ndani ya Tanzania au nchi za jirani.
Tumewahi kusikia kuwa mmoja wa waliolipuwa mabomu huko kampala na kuleta madhara kwa wale waliokuwa wakifuatilia fainali za kombe la dunia alikuwa ni mtanzania/aliishi Tanzania.

Kwa maoni yangu watanzania ni wamoja mno nikimaanisha pamoja na matukio kadhaa ya misuguano ya kidini bado wameendelea kusalimiana,kutaniana,kuzikana,kuzungumza na kufanya kazi pamoja.
Lakini kuna kikundi cha watu wachache sana ambao wanataka kuharibu amani ya nchi hii na mataifa kwa ujumla.ni kikundi chenye fedha,wataalamu na mikakati mifupi na mirefu yenye malengo maalumu ambayo hayana tija kwa waislamu,wakristu na wapagani.

Kwa mwelekeo ulivyo tunazidi kuzama kwenye jahazi la ugaidi(wala sio udini)

kuna mtu aliwahi kuleta thread hapa jamvini kwamba ameona kundi la vijana wakiwa kwenye mafunzo ya karate na dini huko njiro Arusha,kuna mtu yoyote anayewafuatilia kujua lengo la mafunzo hayo ni lipi?wakitoka hapo wanaenda wapi?je serikali inafahamu au kuratibu mafunzo ya namna hii?

Kimsingi hoja yangu inataka kujikita katika kuanzishwa kwa kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi(counter terrorism unit) ili kufuatilia nyendo za magaidi nchini.
Hivi karibuni tunaweza kuwa wachimbaji wazuri wa madini ya urani ,sitegemei kama magaidi watakaa mbali na nchi yetu!tusisubiri kufika maeneo ya matukio na kutoa pole bali tujipange kwa kuepusha ugaidi.

Ni vizuri sheria ya ugaidi ikapitiwa vizuri kuona kama inaruhusu/itaruhusu kuundwa kwa kikosi hiki maalumu cha kupambana na ugaidi.
Ni aibu pia kwamba kila wakati tunahitaji msaada wa CIA,FBI ili kufuatilia matukio ya kigaidi ni vyema tukawa na CTU yetu!

Mkuu inaonyesha unaangalia series ya 24.. bado kidogo utasema kwenye mawasiliano tumuweke na clory
 
Hivi vikundi vinavyoashiria kuelekea kuja kuwa magaidi vipo kibao...Hao Panya road, Mbwa mwitu ni hao hao baadae wanakuja kuwa magaidi ikiwa serikali haichukulii kwa umakini makundi haya...Leo hii wadogo wanaitwa panya wakikuwa hao wataitwa Magaidi na roho zao za mauaji zitakuwa zishakuwa sugu..

Pili Katika suala la uhamiaji...Bado watu wauhamiaji hawako makini kabisa sababu mitaani utakuta wahamiaji kibao km wakomoro, wakongo, waarabu wapo ila Balozi au Mwenyekiti wa Serikali za mtaa hajui na hafuatilii hili...

Pia Suala la Ajira kwa vijana limekuwa kikwazo sana hata kijana akiambiwa anapewa kazi yeyote ilimradi maisha yake yanakuwa mazuri yupo tayari...Vijana wasiokuwa na ajira wanaweza pia kuchukuliwa na magaidi kwa kigezo cha kupata maisha bora.

Kuhusu hili suala la Serikali kupeleka vijana wa malizapo shule jeshini....Kijana anapelekwa jeshini...mafunzo yote ya ujasiri anapata, Kijana huyu anakuja mtaani, Japo anaendelea kusoma lkn ajira hana, wala mtaji wa biashara hana.......Je wanamuandaaje kijana huyu kama si kuja kuwa Jambazi, au kuja kuingia katika makundi haya akiwa ashakuwa mtaalamu wa kushika bunduki? Ikiwa wakati mwingine wewe ulosoma unakosa hela, huna kazi, na wengine watoto wa viongozi wanakula hela na kuziita vijisenti...Je kijana huyu hatoingia mwituni?

Naamini waliowengi wanaoingia katika makundi ya kigaidi ni kuwa washachoshwa na maisha, depression ndizo zinazowasababisha hali hii na kujiona hafai ktk ulimwengu na kupelekea kuchukia na wengineo kuona kama hawamuhitaji na wala hawamfai...


Kwa kweli inasikitisha....Yaani nakuwa kama napata taswira mbaya ya Tanzania tunapoelekea..






Tanzania kwa mara nyingine tena inashuhudia tukio la pili la kigaidi ambalo limevuta hisia kutoka jamii mbalimbali za kimataifa.ukiacha tukio la kulipuliwa kwa ubalozi wa marekani utaona tukio la Olasiti linazidi kudhihirisha kuwa Tanzania yaweza kuwa eneo linalotoa mwanya kwa magaidi kupanga na kutekeleza mashambulizi ya kigaidi iwe ndani ya Tanzania au nchi za jirani.
Tumewahi kusikia kuwa mmoja wa waliolipuwa mabomu huko kampala na kuleta madhara kwa wale waliokuwa wakifuatilia fainali za kombe la dunia alikuwa ni mtanzania/aliishi Tanzania.

Kwa maoni yangu watanzania ni wamoja mno nikimaanisha pamoja na matukio kadhaa ya misuguano ya kidini bado wameendelea kusalimiana,kutaniana,kuzikana,kuzungumza na kufanya kazi pamoja.
Lakini kuna kikundi cha watu wachache sana ambao wanataka kuharibu amani ya nchi hii na mataifa kwa ujumla.ni kikundi chenye fedha,wataalamu na mikakati mifupi na mirefu yenye malengo maalumu ambayo hayana tija kwa waislamu,wakristu na wapagani.

Kwa mwelekeo ulivyo tunazidi kuzama kwenye jahazi la ugaidi(wala sio udini)

kuna mtu aliwahi kuleta thread hapa jamvini kwamba ameona kundi la vijana wakiwa kwenye mafunzo ya karate na dini huko njiro Arusha,kuna mtu yoyote anayewafuatilia kujua lengo la mafunzo hayo ni lipi?wakitoka hapo wanaenda wapi?je serikali inafahamu au kuratibu mafunzo ya namna hii?

Kimsingi hoja yangu inataka kujikita katika kuanzishwa kwa kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi(counter terrorism unit) ili kufuatilia nyendo za magaidi nchini.
Hivi karibuni tunaweza kuwa wachimbaji wazuri wa madini ya urani ,sitegemei kama magaidi watakaa mbali na nchi yetu!tusisubiri kufika maeneo ya matukio na kutoa pole bali tujipange kwa kuepusha ugaidi.

Ni vizuri sheria ya ugaidi ikapitiwa vizuri kuona kama inaruhusu/itaruhusu kuundwa kwa kikosi hiki maalumu cha kupambana na ugaidi.
Ni aibu pia kwamba kila wakati tunahitaji msaada wa CIA,FBI ili kufuatilia matukio ya kigaidi ni vyema tukawa na CTU yetu!
 
Naimani watu wakiondoa ule UMIMI, UDINI, baasi tutabadilika na kupambana na hivi vitu....Utamjua mtu anaudini tuu hata kwa comment zake...
Unatakiwa usizungumzie dini yangu NZURI ongelea DINI ZETU nzuri.....
Tukiondoa umimi, uwangu tutafanikiwa...Tukirudia ilivyokuwa enzi za nyuma, Mtu akimuona mwana wa mwenzie anaeonekana anaenda ndivyo sivyo akasaidia kutoa taarifa tukalindana Jirani kwa jirani, ndugu kwa ndugu naamini hivi vitu vitaisha...

Udini wa nini wakati familia zetu zimechanganyika, zimeoana Mke Christian, Mume Muslim, katika familia zetu ni mseto...so hakuna haja ya kuongelea dini yangu....We amini katika kutotenda dhambi zilizokatazwa na kitabu cha dini.....Acha kumsaidia Muumba kuhukumu, Muachie Muumba mwenyewe ahukumu.

Acha kumuona mwana wa mwenzio kiatu, hata ukimkuta anavuta bangi, anafanya uchafu unamuacha hujali...saidia mwana wa mwezio ndipo utajenga TAIFA bora....Huyo mwana wa mwenzio leo hii unayemuona wa nini ndiye atakayekudhuru kesho...

SIPENDI WATU WANAOZUNGUMZIA DINI, KWA KAULI ZA KUKANDAMIZA DINI ZA WENGINE KABISA, kama wewe unaimani yako mafundisho yako ya dini yaamini ila heshimu mafundisho ya wenzio...Unauhakika wewe ni msafiii na hiyo dini yako hali ya kuwa hujafa ukajua huko unapoenda kukoje?





Mkuu unadhani hawa maamuma wanafikiria?
Hebu fikiria mtoa mada amekuja na mada ya kupinga ugaidi suala ambalo lilitakiwa kila mpenda amani aliunge mkono lakini hawa wanalipinga,huoni kuna uwalakini hapo?
 
Haya ndio matatizo ya kuchanganya bangi na kubeli ukateremshia na gongo!
Hii tafsiri ndio umejifunza kanisani sio!?
Mnfnsssssssssss!


Toa yako wewe ambayo ni sahihi...
Nguchiro wwe....Kuwaza kwa kutuia kija.mb i.o ni mbaya san
 
Hiki Kikosi cha Kupambana na Ugaidi (CRT) kipo na kilifadhiliwa na Serikali ya Marekani, labda kiimarishwe zaidi tu.
 

Attachments

  • CRT3.PNG
    CRT3.PNG
    259.2 KB · Views: 145
Back
Top Bottom