Pendekezo: Kuwe na Daladala VIP kukabiliana na foleni

Pendekezo: Kuwe na Daladala VIP kukabiliana na foleni

Mbona hizo VIP zipo sana kuanzia saa 11 alfajili. Inaelekea unalala sana. Shida kubwa ipo kwa LATRA hawa wanaleta msongamano wa magari jijini. Wanaua route kijinga sana wanatakiwa watengeneze route ndefu mfano Simu 2000 Chalinze ama simu 2000 Bagamoyo. Ukishakuwa na route ndefu unapunguza sana uwepo wa vituo vidogo vidogo vingi ambavyo havina sababu. Hili la VIP route wangelianzisha hawa DART mwendokasi. Wangekuwa na VIP muda wa asubuhi na jioni. Mbezi Kivukoni 3000 na Kimara kivukoni Tshs 2500. Pia wafanye na kariakoo watahudumia hasa.
Hizo nauli ni plates za chakula kwetu sisi wanyonge! Nauli iwe buku tu sio zaidi
 
Wafanye buku bee angalau wengine tuwe tunapumzika ku-drive daily na siku tukikosa pesa ya wese tusiongeze mbanano kwenye daladala.....ninachoona msongamano kwenye daladala unaenda kuwa mkubwa sana kwa sababu hata baby-walker hazitaendesheka kwa hizi bei za mafuta.
 
Wazo zuri sana. Kuna bwana mmoja tulikaa naye jirani alikua na Noah yake kila siku asubuhi saa 12 anachukua abiria wake sita kwenda town, anashusha anaenda zake kazini. Jioni tena saa 11 anarudi home na abiria wake waliokua tayari. Bei elfu 2 one way.
Kwa sababu ilikua ya mtaani na wote tunajuana ilikua na maudhi kidogo. Mfano mtu kachelewa asubuhi anampigia simu jamaa amsubiri, hasa akina mama. Jioni nayo hivo hivyo. Sasa akishakua jirani mnayefahamiana kunakua na ugumu kidogo.
Jamaa akajenga nyumba yake sehemu nyingine kwetu akahama. Watu wanamkumbuka mpaka leo.
Kwa hiyo abiria wapo, tena wengi tu
 
Kujali nauli lazima kwasababu haina maana ikiwa nauli hio itazidi au kukaribia gharama za mafuta atakayotumia kwa gari yake. Pia wengi wanatoka ndani kidogo sio barabara kuu ambapo kufika main road itabidi achukue boda mwisho wa siku atatumia 8000/- kwenda na kurudi ambayo akiweka kwenye gari yake inatosha.
Wengi wanasahau hilo.

Utoke bonyokwa hadi stand kuu na suti yako?

Ushuke Morroco uende TMJ na suti yako kwa boda?

Ofisi nyingi hazipo arround stand.
 
Wengi wanasahau hilo.

Utoke bonyokwa hadi stand kuu na suti yako?

Ushuke Morroco uende TMJ na suti yako kwa boda?

Ofisi nyingi hazipo arround stand.
Yaa, hili nalo ni angalizo....maana unaweza kutumia pesa nyingi zaidi ukaona bora utumie gari lako. Nafikiri waziweke tu ila wawe makini kwenye kupanga nauli zisiende juu sana, labda ziwe kati ya 1,000 na 2000.
 
Kujali nauli lazima kwasababu haina maana ikiwa nauli hio itazidi au kukaribia gharama za mafuta atakayotumia kwa gari yake. Pia wengi wanatoka ndani kidogo sio barabara kuu ambapo kufika main road itabidi achukue boda mwisho wa siku atatumia 8000/- kwenda na kurudi ambayo akiweka kwenye gari yake inatosha.

Mimi walete tu
Nimechoka kubambbiwa kwenye mwendokasi
 
Huu uzi umewalenga Wale wenye magari binafsi, kwa hiyo nauli hata kama itakuwa ni tzs 5,000 bado ni ndogo kwao na wanamudu. Na lengo ni kupunguza Foleni


Point ya msingi ya kuzingatia ni kuwa, Wale wenye magari binafsi, wako tayari kuacha magari nyumbani na kutumia usafiri wa umma ulioboreshwa, bila kujali ghalama ya nauli kuwa kubwa, wao wanachotaka ni ubora wa huduma ya usafiri. Root
Yaani mtu alipe 6000 ambayo ni sawa na lita 2.5 ambayo ni kama km 16 tena asiwe na privacy?
 
Nilikuwa nafikiria zikisajiliwa daladala za VIP ambazo zitakuwa na Air conditioning usafi wa hali ya juu zikapiga ruti mfano Tegeta- Posta kwa Tsh 3,000 na abiria wote level seat hakuna kusimamisha abiria.
Hii ni nzuri sana, ila 3000 ni kubwa sana labda 1000 meaning one way mtu ana uhakika wa 28K kule Morogoro kuna bus mbili ninasafiri kati ya Morogoro na Gairo, hakuna abiria kusimama, na ni nadra kuchukua abiria wa njiani kama ikiwa imeeneza abiria kwenye viti
 
Back
Top Bottom