Pendekezo: Prof. Assad ateuliwe Ukurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari

Pendekezo: Prof. Assad ateuliwe Ukurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari

Kutokana na wizi na ubadhilifu wa bandari yetu napendekeza professor Assad ateuliwe nafasi hiyo
Acha ujinga wewe, sasa hapo umetupa breaking news au umeandika kichwa cha habari cha kupendekeza...
 
Kifupi katiba hairuhusu mtu aliyewahi kuwa CAG kuteuliwa ama kuchaguliwa kushika nafasi yoyote ile ktk utumishi wa umma. CAG ni habari nyingine mkuu. Kasome katiba
 
Hebu rekebisha kichwa cha habari kwanza...
Umetumwa kuja kutukata stimu za mizuka tulizopata asubuhi pale Mjengoni Chamwino.. Ex-CAG ASSAD na huo uDG wa TPA wapi na wapi, unamshusha cheo BABU yetu au sio.
 
CAG vs Mkurugenzi wa Bandari nani zaidi?
 
Katiba haimruhusu Tena kufanya kazi yeyote ya umma...rais akimteua atakuwa amevunja katiba ya nchi...
 
Katiba haikuruhusu Meko kumtumbua Assad b4 kustaafu au kifo. Assad hajastaafu.

njia zipo nyingi tu za kumrudisha. 1. kwa maslahi mapana ya Taifa ana rudi kibabe. Au
2. Kesi ina funguliwa ku challenge kustaafishwa kwake kinyume cha Katiba in 2 months ana shinda ana rudishwa. Huyo Meko alimrudishia hadhi ya Ubalozi Ndg yake Prof. Costa Ricky Mahalu aliye kuwa amevuliwa na JK.
Sidhani Kama mama ataingia huko, kuvunja katiba ni Jambo baya Sana kwa kiongozi...
 
beb2aa5f-b0ea-410b-872b-80de10a08d1e.jpg

ameandika MalisaGJ*

Sio kwamba ripoti hizi zina mpya sana, bali kuna mtu mpya ambaye ameamua kuzifanyia kazi. Zamani zilikua zikisomwa zinawekwa kapuni maisha yanaendelea.

Kuna watu wanadhani hii ndio hasara ya kwanza kwa ATCL. CAG aliyepita Prof.Assad amewahi kuibua hasara kubwa zaidi ya hizi. But who cares?

Mwaka 2015/16 ATCL ilipata hasara ya 94.3Bil. Mwaka 2016/17 hasara ya 109.3Bil, na mwaka 2017/18 hasara ya 113.8Bil.

Kwahiyo hii 60Bil aliyoibua Kichere ni "cha mtoto" someni ripoti za Prof.Assad mtaona hasara ya mabilioni mengi zaidi. Tofauti ni kwamba wakati wa Assad ripoti zilizimwa. Wakubwa hawakupenda serikali "ichafuke". Lakini mama amekua tofauti. Anataka mambo yawekwe hdharani wananchi wajue. Transparency and accountability.

ZZK aliwahi kusema, sio kwamba serikali ya JPM ni safi sana, bali ilijitahidi kuficha taarifa watu wasijue. We unadhani JPM angekuwepo hii ripoti ya CAG ingesomwa kama ilivyosomwa? Thubutu.!

Watu wengi walisema serikali ya JK ilijaa ufisadi, lakini wasichoelewa ni kwamba JK mwenyewe alitaka watu wajue. We unadhani alishindwa kuzuia taarifa ya Richmond, EPA, Escrow etc? Alikua na uwezo wa kuzuia na wananchi wasijue chochote. Na angeondoka madarakani mnamsifia serikali yake ni clean. Lakini JK hakutaka "mapambio fake" aliamua kuweka kila kitu hadharani ili penye makosa paonekane na hatua zichukuliwe.

Serikali ya JPM haikutaka madhaifu yawekwe hadharani. Ndio maana CAG Assad aliibua madudu mengi lakini badala ya kupongezwa, akaonekana eti anaichafua nchi. Si unakumbuka ile kashfa ya 16Bil za jeshi la polisi kununua sare hewa? Iliishia wapi zaidi ya Kange Lugola kusema anajivua nguo na kumuita Prof.Assad muongo.

Bandarini kumejaa ufisadi mkubwa, lakini mkurugenzi wa bandari amekua akisifiwa sana na serikali ya JPM kuongeza mapato. Ndo ujue kuna watu walifanya ufisadi na kujificha kwenye kichaka cha Uzalendo. Leo mama ameagiza apelekewe ripoti ya BOT kuanzia January hadi March. Inadaiwa kuna mabilioni yalichotwa kwa "kisingizio" cha matibabu ya JPM.

Kwahiyo mama ameanza vizuri, lakini asiishie hapa. Mikataba ya miradi yote mikubwa iwekwe wazi. Wananchi wana haki ya kujua. Uwazi na uwajibikaji ni silaha muhimu kwenye utawala bora.!
 
Kutokana na wizi na ubadhilifu wa bandari yetu napendekeza professor Assad ateuliwe nafasi hiyo
Inawezekana tu akapewa hiyo nafasi mbona rais ana stafu halafu anarudi kuwa mkuu wachuo yaan anakuwa chini ya waziri wa elimu hahahaaaaa

Ila nadhani katiba inamzuia kuhudumu tena serikalini kama kishapitia cheo cha CAG sijajua ni kwa nini waliamua iwe hivyo.
 
Inawezekana tu akapewa hiyo nafasi mbona rais ana stafu halafu anarudi kuwa mkuu wachuo yaan anakuwa chini ya waziri wa elimu hahahaaaaa

Ila nadhani katiba inamzuia kuhudumu tena serikalini kama kishapitia cheo cha CAG sijajua ni kwa nini waliamua iwe hivyo.
Swala sio kuwa chini ya Nani, mtu unapokuwa mdhibiti wa hesabu za serikali sheria ina amini unajua muundo na namna ofisi inavyofanya ukaguzi pia sheria ina amini utakuwa una connection kubwa na watu ambao wapo ndani ya ofisi za mkaguzi ambao ndio wa kaguzi hivo unaweza tengeneza njama yakutokaguliwa kwa usahihi, pia ni ngumu watu ambao ni wakaguzi kwene ofisi ulio kuwa ww ndo boss wao kukukagua kwa uhalisia kwa maana ya heshima.
 
Kutokana na wizi na ubadhirifu wa bandari yetu napendekeza Profesa Assad ateuliwe nafasi hiyo
Sawa kabisa .ataibadilisha kabisa .yuko vizuri sana,aisee umefikiria nini mpaka ukaja na wazo zuri hivi!!??
 
Back
Top Bottom