Pendekezo: Siku moja WanaJf wote tukutane mahali fulani, siku fulani, haya wote tukubaliane hapa

Pendekezo: Siku moja WanaJf wote tukutane mahali fulani, siku fulani, haya wote tukubaliane hapa

Jambo lisilowezekana na halitowezekana milele.
Watu wako huru kutoa siri za watu,kuvuruga michongo na kukosoa serikali kwa uhuru kisa wako jf kwa anonymous identity.
Hivi unafikiri siku watu wakajulikana kwamba fulani ndo huyu.
Nadhani huo ndio utakuwa mwisho wao.


Acha tuendelee kutojuana hivi hivi kwa usalama.
 
Hilo haliwez kutokea why?
Kuna mapimbi humu wamejipa Sifa zisizo zao[emoji1], kuna mapimbi humu tutategemea wafike eneo la tukio wakiwa na escort ya European cars, new brands cc3000+, matokeo yake unamuona member kashushwa na daladala la nauli mia7 tena kapata siti ya kugombania.

Kuna wale wenzetu jinsia ya kike hawa wanajiona warembo wa JF kumbe kwa ground ni huruma tu kwakweli hawaendani na ID zao, hawana mvuto wala sifa mnazowajaza humu,

Kiufupi suala la kuoanana na wanaJF ni gumu sana, haswa unapofikilia kuonana na yule member aliyekutishia kukufunga sentro, wakati huo ni wewe ndie unastahili kumuonea huruma na kumlisha, bila kutusahau sisi tunaowatukana mabosi zetu humu alafu tuje tuonane live? Hapana bana tuendelee hivi hivi fake Id za vificho humu[emoji3].
 
Impossible! Unataka wengine waondoke na ngeu au wakiwa wamebebwa na defender ya police? Usichukulie poa maoni unayoyatoa ukiwa umejificha! Wengine wanaumia kiasi cha kutaka kukula kichwa! Kuna uadui wa kikabila, kidini, kisiasa! Hivi vitu havijawahi kumuacha mtu salama ukiingia kwenye anga zake!
[emoji23][emoji23]

Naamini hatutofikia huko

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom