Pendekezo: Watumishi wa umma tukatwe mishahara walau asilimia 2 pesa ikasaidie Serikali kupambana na Corona

Pendekezo: Watumishi wa umma tukatwe mishahara walau asilimia 2 pesa ikasaidie Serikali kupambana na Corona

Niliweka uzi kama huu Mods wakautoa haraka sana sijui tatizo lilikua nini au ilikua ni mihemko yao tu
 
Watumishi tayari wapo choka mbaya na nasikia bidhaa zimeanza kupanda bei, hivi tukiuza dreamliner hatuwezi kupata pesa hata ya kununua barakoa?
 
Kwa walimu wabadilishe mrija wa cwt iende wizara ya afya. Korona ikiisha pesa hiyo iende hukohuko iungwe kweny NIHF ..cwt MH Rais JPM huoni chama hiki ni wala jasho la wwnzao tuu?? Tumia mamlaka yako
Asante kwa wazo zuri. Naamini mamlaka husika zitarifanyia kazi. Tunayo serikali makini ya JPM.
 

1586398991180.png
 
Kipindi cha tetemeko kagera hukooo,
Magu aliuliza kwani serikali ndo imeleta tetemekoo??
Nasi watumishi twauliza ..kwani watumishi ndo tumeleta Coronaaa??
 
Wazo lako ni zuri. Ila limejikita kwenye ukweli kwamba Serikali inaweza ikaendelea kukulipa mshahara huo ambao unaupata kwa sasa. Lakini uchumi wa Dunia umeyumba vibaya sana. Wamarekani karibu milioni kumi hawana kazi. Tatizo hili pia linaweza kutokea hapa petu kwani sisi si kisiwa. Utalii ambao unachangia fedha nyingi za kigeni sasa si shwari tena. Na hata sekta ya Madini, Biashara, Usafiri hata zile sekta binafsi zote zinayumba. Je, Serikali inaweza kuhimili vishindo hivi vyote? . Ni wazi itafika mahali hata mishahara inaweza isipatikane na mkaombwa kugawana kidogo kitakachokuwepo. Ndoto ya asilimia mbili itaishia hapo hapo.
 
Kwanza niseme wazo kuwa mimi ni muumini wa ahadi za MwanaTANU. Ambapo msisitizo ni uzalendo kwa nchi.

Nikiwa Mtumishi wa umma huku nikiiona changamoto ya kupambana na covid-19 napendekeza serikali itukate watumishi wa umma wote walau asilimia mbili za mishahara yetu na pesa iende kusaidia mapambano dhidi ya corona. Katika hilo naomba tutangulize uzalendo. Nchi ni yetu na matatizo ni yetu.

Hata hivyo natoa wito kwa watanzania wenzangu wote tukumbuke kuomba risiti tutakaponunua bidhaa madukani jambo ambalo litasaidia kuimalisha uchumi wetu.
Duuuh
 
Back
Top Bottom