Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Kukaaa kimya siku zoote yaaani ndo kaja na hili la katiba yoooote yanayotoke kimya!!!! 00
 
Wakati wa Jakaya Kanisa lilishiriki kuishinikiza Serikal kuleta Katiba Mpya japo hapakuwa na Huduma bora, Leo Wanatumia kigezo cha Huduma bora kukataa Katiba Mpya, kweli Mchezaji kwao hutuzwa,
Hongera Rais John Joseph kwa kuungwa Mkono na Kanisa kwa kila jambo

Hapana. JPM haungwi mkono na kanisa. Pengo ni askofu wa dar es salaam. Unapoongelea kanisa katoliki Tz, unaongelea TEC. Sidhani kama TEC imetoa tamko la kumuunga mkono Magufuli.
 

Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.

“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.

Alifafanua zaidi kwamba kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.

Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.

“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.

“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.

Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.

Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.

Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.

“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.

“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.

CHANZO: Mwananchi

Kwa kauli ya Niwemugizi soma zaidi hapa;
Askofu Niwemugizi asema yuko tayari kuitwa mchochezi

Kadinali Pengo huwa namkubali sana huwa ana msimamo thabiti lakini kikubwa zaidi ana uelewa wa hali ya juu sana,
 
Pengo ilibidi atoe maoni yake binafsi kama alivyofanya Niwemugizi, hakupaswa kumwongelea kabisa, akiulizwa amekula maharage ya wapi ataanza kununa bure
 
Samahani naomba kuuliza, hivi kitendo cha Askofu wa jimbo kuu la Dar kujigeuza kuwa msemaji wa baraza la Maaskofu Tanzania siyo utomvu wa nidhamu? Hatakiwi kuwajibishwa? Hivi katika historoa ya Kanisa Katoliki Duniani, imeshawahi kutokea kukawa na Kardinali asiye na impact yoyote kwa jamii na kwa taifa kama tuliyemwona leo kwenye TV? Hivi ni kwanini kuna pengo kubwa sana kati ya Pengo na wananchi?
 
Asiyejitambua huyu! Kauli ile ni msimamo wa Watanzania tulio wengi. Unazidi kupoteza mvuto kwenye jamii ya Watanzania kwa kutokemea maovu ya dikteta uchwara.
Mkuu katiba mpya muhimu lakini sio kipaumbele chetu.

Elimu na Afya pamoja na huduma za jamii kama maji safi ndio vipaumbele. Hata Lowassa na UKAWA waliipa elimu kipaumbele ktk ile kauliu ya ELIMU, ELIMU, ELIMU.

Pia usiwasemee watu kwamba wengi kipaumbele chetu ni katiba kabla ya kura ya maoni. Hivi sasa ukizunguka nchi nzima ukauliza tufute elimu bure na mipango ya maendeleo kisha pesa tuelekeze kwenye kupata katiba mpya utapata kuungwa mkono na angalau 51% ya watanzania wote?
 
Asiyejitambua huyu! Kauli ile ni msimamo wa Watanzania tulio wengi. Unazidi kupoteza mvuto kwenye jamii ya Watanzania kwa kutokemea maovu ya dikteta uchwara.
Hawezi kukemea kama alivyofanya kwenye utawala wa jk. Kwasababu sasa hivi wao kila kitu wanachotaka kutoka serikalini wanapata bila shida yoyote na wala hawahojiwi na mtu. Ndoomana hujasikia hata siku moja kanisa likilaani mambo yanavyokwenda kwa sasa.

Na kama unakumbuka ni lazima aseme hivyo kumbuka kwanini pendo alitukanwa na Gwajima? Kwasababu yeye aliwazunguka wenzake na kwenda kamshauri jk akatae katiba mpya. Na kumbuka wakati jk anahutubia bunge alisemaje? Ameshauriwa na kiongozi mkubwa wa dini kwamba.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Jamani mbona Yule Askofu alisema yale yalikuwa mawazo yake? Sio mawazo ya kanisa, na alisema yuko tayari kuitwa mchochezi mbona mnapotosha?
 
Mkuu katiba mpya muhimu lakini sio kipaumbele chetu. Elimu na Afya pamoja na huduma za jamii kama maji safi ndio vipaumbele. Hata Lowassa na UKAWA waliipa elimu kipaumbele ktk ile kauliu ya ELIMU, ELIMU, ELIMU. Pia usiwasemee watu kwamba wengi kipaumbele chetu ni katiba kabla ya kura ya maoni. Hivi sasa ukizunguka nchi nzima ukauliza tufute elimu bure na mipango ya maendeleo kisha pesa tuelekeze kwenye kupata katiba mpya utapata kuungwa mkono na angalau 51% ya watanzania wote?
Hivi haya ulosema hayana uhusiano wa moja kwa moja na katiba?,hivi hizo Huduma mnazosema ni akina nani zinawahusu?,katiba inalinda utu wa MTU,inasimamia taratibu sahihi za kustawisha utu na maisha ya MTU,sasa ni MTU wa aina gani ambae hata akipewa Huduma bora lkn anafinyangwa utu wake atae furahia Huduma hizo,
 
Ni mtu mwenye akili finyu tu ambaye anaweza kusema katiba mpya si kipaumbele cha nchi. Huwezi kuwa na Serikali bora ambayo inajua fika itaiba kura ili kung'ang'ania madarakani hivyo hata IVURUNDE vipi haina hofu tena kwa wapiga kura maana wanajua watashinda tu. Kutoongwa mkono na 51% ya Watanzania katika kupata katiba mpya haina maana katiba hiyo haina umuhimu. Tatizi ni hao watakaoikataa hiyo katiba mpya kiwango chao cha elimu ni kipi?

Hata vyama vingi wengi hawakuvitaka kama si Baba wa Taifa leo hii baada ya miaka 56 bado tungekuwa na chama kimoja. Imagine madudu chungu nzima ya hawa wahuni na mafisadi ambayo yamewekwa hadharani na vyama vya upinzani tangu tulipoanza rasmi mfumo huo 1992. Fungua akili yako uone mbali zaidi.



Mkuu katiba mpya muhimu lakini sio kipaumbele chetu. Elimu na Afya pamoja na huduma za jamii kama maji safi ndio vipaumbele. Hata Lowassa na UKAWA waliipa elimu kipaumbele ktk ile kauliu ya ELIMU, ELIMU, ELIMU. Pia usiwasemee watu kwamba wengi kipaumbele chetu ni katiba kabla ya kura ya maoni. Hivi sasa ukizunguka nchi nzima ukauliza tufute elimu bure na mipango ya maendeleo kisha pesa tuelekeze kwenye kupata katiba mpya utapata kuungwa mkono na angalau 51% ya watanzania wote?
 
Kwa hiyo hii kauli yako ndiyo msimamo wa kanisa...au nayo ni maoni yako binafsi!?


Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.

“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.

Alifafanua zaidi kwamba kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.

Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.

“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.

“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.

Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.

Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.

Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.

“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.

“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.

CHANZO: Mwananchi

Kwa kauli ya Niwemugizi soma zaidi hapa;
Askofu Niwemugizi asema yuko tayari kuitwa mchochezi
 
Back
Top Bottom