Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Kwa ufupi
Kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara

Dar es Salaam. Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.

“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.

Alifafanua zaidi kwamba kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.

Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.

“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.

“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.

Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.

Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.

Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.

“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.

“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.
Hii ni kunyutrolise mambo
 
Askofu Pengo ni irrevant kwa jamii ya sasa iliyojaa vijana wengi,hapaswi hata kuongea,

Muda wake wa kukaa na vijana umeisha,aende Malya kwenye Nyumba za mapumziko ya mapadri waliozeeka au akaombe chumba Vatican

Hizo seminari zina ada kubwa kweli kweli wakati wanaoziendesha ni watoa sadaka,hata hospitali ya bugando,tangu wakabidhiwe gharama zimekuwa Mara mbili,hana moral authority kuongelea elimu na afya
ni kweli
 
Acha ku profess ignorance mbele za watu. Tanzania kuna majimbo makuu 5, sio Dar peke yake, Arusha, Dodoma, Songea, Mwanza. Ukuhani ndani ya kanisa una daraja tatu yaani ushemasi, upadre na uaskofu. Hayo mengine ni taratibu tu za kiutawala.

Nimekuelewa mkuu, swali langu ni moja tu, je mkuu wa kanisa katoliki Tanzania ni nani? tuache mambo ya nani msemaji wa kanisa katoliki kwani hata serikali ya ina Rais na inamsemaji mkuu wa serikali, je msemaji mkuu wa serikali anaweza kuwa mkuu wa serikali? najua system ya serikali na ya kanisa ni inaweza ikawa tofauti au ikashabiliana kwa aina moja, au kanisa katoliki Tanzania halina kiongozi mkuu?

Mfano nimejaribu kutafuta head of catholic church in Uganda nikampata kama ilivyo hapa chini kwenye link, nikatafuka Kenya nikaona pia wanasema somebody njue, je Tanzania hakuna?, tuachane na mambo ya madaraja wengine hatujui, tunachotaka kujua ni kimoja tu je kuna kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Tanzania au hakuna?
bpy3ciz/index.htmlBishop Odama is new head of Catholic Church in Uganda
 
Yote hayo anayasema Pengo leo ni kwa sababu anayetawala sasa ni Mkatoliki ambaye inadaiwa kwa makusudi anaipa Favor ya juu taasisi ya ukatoliki hapa Tanzania.

Kama mtawala angekuwa ni muislamu(Kama kipindi kile cha Kikwete) Askofu Pengo ungemwona yuko busy kila Jumapili kuikosoa serikali na kudai uwepo wa katiba mpya yenye kutoa haki kwa watanzania.
ukweli mtupu pasina shaka
 
Pengo ni archbishop maana yake ni chief or high level leader , na hukaa makao makuu tu, hivyo St peter la dar sio tu jimbo la Dar es salaam bali ni makao makuu ya kanisa katoliki Tanzania, mtu anae kaa makao makuu ndo kiongozi mkuu wa kanisa ila kanisa analosalisha kama mtume . Ndio maana hata niwemuguzi akifikia hatua ya kuwa archibishop atatoka huko aliko aje Dar akisubili pengo kuresign au kufariki yeye arithi, ndio maana hata pengo mwenyewe baada ya Rugambwa kuona hali yake sio nzuri aliteuliwa kuwa archibishop, maana yake alikuwa normal BISHOP kama wengine, na baada ya rugambwa kuresign ndo akamrithi na kuwa cardinal, kutomtambua pengo kama kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Tanzania sio sahihi. Labda twende tukaangalie details za archinishop, bishop & cardinal yana maana gani, pengine wakatoliki waje watueleze kwa undani zaidi.

Kama hulifahamu kanisa takatifu na mfumo wake wa kiuongozi ni heri ukae kimya kuliko kupotosha.

Mfumo wa Kanisa katoliki umegawanyika Kutoka Duniani down to Archdioceses(Majimbo Makuu) yanayoongozwa na Maaskofu Wakuu then Dioceses(Majimbo) yanayoongozwa na Maaskofu wa Jimbo.

Hivyo basi hakuna mfumo wa Kanisa Katoliki katika mipaka ya Kinchi na mdio maana hata Majimbo hayafuati mifumo ya Mikoa ya Kiserikali/Kijiografia.Hivyo basi eneo kua Jimbo Kuu haimaanishi ndio makao makuu ya KK katika nchi.

Askofu Pengo ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam lenye majimbo madogo kama Moro,Tanga n.k.

Kuna majimbo 34 Tanzania,Kati ya hayo matano ni Majimbo Makuu-Arusha,Mwanza,Dodoma,Tabora na Dar es Salaam na haya yote yana Maaskofu wakuu na wanakua na Nguvu katika Jimbo kuu lake tu na kua askofu mkuu haimaanishi ww ndio mkuu wa Maaskofu katika nchi.

Kwa mantiki ya ulichokiandika kua Askofu mkuu ndio kua mkuu wa kanisa nchini,basi utamaanisha Tanzania ina Wakuu wa KK watano maana wote ni Maaskofu wakuu.
Nadhani nimesaidia kuondoa huo utata.

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Nimekuelewa mkuu, swali langu ni moja tu, je mkuu wa kanisa katoliki Tanzania ni nani? tuache mambo ya nani msemaji wa kanisa katoliki kwani hata serikali ya ina Rais na inamsemaji mkuu wa serikali, je msemaji mkuu wa serikali anaweza kuwa mkuu wa serikali? najua system ya serikali na ya kanisa ni inaweza ikawa tofauti au ikashabiliana kwa aina moja, au kanisa katoliki Tanzania halina kiongozi mkuu? mfano nimejaribu kutafuta head of catholic church in Uganda nikampata kama ilivyo hapa chini kwenye link, nikatafuka Kenya nikaona pia wanasema somebody njue, je Tanzania hakuna?, tuachane na mambo ya madaraja wengine hatujui, tunachotaka kujua ni kimoja tu je kuna kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Tanzania au hakuna?
bpy3ciz/index.htmlBishop Odama is new head of Catholic Church in Uganda

Mkuu wa Kanisa Katoliki Tanzania na Duniani ni Papa. Hakuna Askofu mwingne zaidi ya Askofu Mkuu wa Roma yaani Papa anaekua mkuu wa Kanisa katika Nchi yoyote au bala lolote.

Kutoka Papa inafuata level ya Jimbo na Mkuu wa Jimbo ni Askofu mahalia.

Hakuna Cheo cha Mkuu wa Kanisa katoliki Tanzania ila Duniani kote kuna mabaraza ya Maaskofu wa Kila nchi au eneo fulani na huchagua Marais wao ili kupata uongozi unaowaunganisha lakini haimaanishi kua uyo Rais ndio mkuu wa Kanisa bado mamlaka yanabaki kwa Askofu wa Jimbo mahalia.

Shida inayosumbua wengi ni kutaka kuchukua mfumo wa kiutawala wa Dini/Madhehebu mengne kuulazimisha ufiti katika Kanisa Katoliki.

Waandishi wa Habari mara nyingi wamepotoka na kuandika habari fake kwa kuchanganya haya mambo.Hata iyo habari ya Uganda ni matokeo ya kuchanganya huku.

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Kwa Watanzania wenye upeo wa kufikiri KATIBA MPYA ilitakiwa ipewe kipau mbele na Awamu ya 5. Tulitumia hela nyingi sana kwenye Tume ya Warioba na Bunge la Katiba sasa kazi yote iliyofanyika ina maana haikuwa na tija? Kwa hiyo tulichezea rasilimali zetu wenyewe? Basi Rais awawajibishe wote waliohusika kwenye ule mchakato!

Ile Rasimu ya Warioba ingepitishwa na Bunge la Katiba tungejenga Tanzania ya Viwanda katika muda mfupi sana maana kila mhusika angefanyia kazi nafasi yake ipasavyo.

Katiba mpya ingefanya kila kiongozi awe wa siasa au wa kiserikali kuwajibika ipasavyo na akizembea tu anaondolewa kisheria!
 
Nimekuelewa mkuu, swali langu ni moja tu, je mkuu wa kanisa katoliki Tanzania ni nani? tuache mambo ya nani msemaji wa kanisa katoliki kwani hata serikali ya ina Rais na inamsemaji mkuu wa serikali, je msemaji mkuu wa serikali anaweza kuwa mkuu wa serikali? najua system ya serikali na ya kanisa ni inaweza ikawa tofauti au ikashabiliana kwa aina moja, au kanisa katoliki Tanzania halina kiongozi mkuu? mfano nimejaribu kutafuta head of catholic church in Uganda nikampata kama ilivyo hapa chini kwenye link, nikatafuka Kenya nikaona pia wanasema somebody njue, je Tanzania hakuna?, tuachane na mambo ya madaraja wengine hatujui, tunachotaka kujua ni kimoja tu je kuna kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Tanzania au hakuna?
bpy3ciz/index.htmlBishop Odama is new head of Catholic Church in Uganda

Katika Kanisa Katoliki hakuna cheo cha mkuu wa kanisa wa nchi. Waandishi makanjanja ndio wanaopotosha na kuandika hivyo. Hapa Tanzania kwa vile tunaye Kardinali watu hudhani kuwa ndio mkuu wa kanisa. Vp kwa zile nchi ambazo zina makardinali Zaidi ya mmoja?

Kila Askofu wa Jimbo ni mkuu katika Jimbo lake. Huyo Pengo hawezi kwenda Rulenge bila ruhusa ya Askofu Niwemugizi and vice versa. Kila Askofu anawajibika moja kwa moja kwa Baba Mtakatifu. Na hapa Baba Mt sio mtu bali ni ofisi.....kuna idara Vatican inahusika na Maaskofu......na kwa nchi za kwetu "nchi za misioni" mambo yetu yote yanashughulikiwa na idara inaitwa propaganda fide.

Ukisikia Jimbo limepewa hadhi ya Jimbo Kuu basi Askofu wake ataitwa Askofu Mkuu na yale majimbo yaliyo chini yake suffragan diocese yanamwangalia huyu Askofu Mkuu kama muunganishi wao....sio mkubwa wao.

Maaskofu wa nchi wameruhusiwa kuunda mabaraza ndizo hizo episcopal conferences.... na maaskofu huchagua yeyote kati yao kuwa Rais wa hilo baraza.... Niwemugizi amewahi kuwa Rais wa Baraza.....Pengo hajawahi kuwa Rais wa Baraza. Hiki ni chombo tu cha kulisemea kanisa mahalia - a particular church. Kwa sbb wakati mwingine kuna mahitaji maalumu ya kanisa mahalia. Mfano. Sheria ya Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni miaka 16 kwa mwanaume na 14 kwa mwanamke.....Sasa hapa Tanzania sharia za nchi ni kinyume na sharia ya kanisa...basi kanisa katoliki la Tanzania - hilo baraza linaomba kwa hapa Tanzania tufuate utaratibu wa nchi yetu!!!!!! What if mkatoliki wa TZ akiwa nje ya TZ akafunga ndoa akiwa na miaka 16 mwanaume ndoa yake itatambuliwa na kanisa katoliki TZ au la? nakuachia assignment.
 
Mungu akupe maisha marefu Polycarp Cardinal Pengo.
 
Pengo hana mamlaka ya kuwasemea maaskofu wengine. Anayo mamlaka ya kulisemea jumbo la Dar es Salaam.
 
Mzee Pengo sina imani kama unachosema ni kwa utashi wako, nadhani unajitoa tuu ufaham ukijua kabisa unachofanya. Hata mie nakuunga mkono kuwa kauli ya yule askofu ni maoni yke binafsi, ni kweli kabisa, ila je; ni kweli wewe hujui umuhimu kupata katiba inayofuata matakwa ya wananchi !? Ni kweli katiba haina umuhim !? Noooo, sina imani kama huo ndio utashi wako.

Naomba ujue sisi wananchi ambao wewe pia unatuongoza tunahitaji katiba kwa maslahi ya wananchi na kwa dira imara ya taifa kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo.

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Pengo ni archbishop maana yake ni chief or high level leader , na hukaa makao makuu tu, hivyo St peter la dar sio tu jimbo la Dar es salaam bali ni makao makuu ya kanisa katoliki Tanzania, mtu anae kaa makao makuu ndo kiongozi mkuu wa kanisa ila kanisa analosalisha kama mtume . Ndio maana hata niwemuguzi akifikia hatua ya kuwa archibishop atatoka huko aliko aje Dar akisubili pengo kuresign au kufariki yeye arithi, ndio maana hata pengo mwenyewe baada ya Rugambwa kuona hali yake sio nzuri aliteuliwa kuwa archibishop, maana yake alikuwa normal BISHOP kama wengine, na baada ya rugambwa kuresign ndo akamrithi na kuwa cardinal, kutomtambua pengo kama kiongozi mkuu wa kanisa katoliki Tanzania sio sahihi. Labda twende tukaangalie details za archinishop, bishop & cardinal yana maana gani, pengine wakatoliki waje watueleze kwa undani zaidi.
Wewe!!! Kwanini umeamua kupotosha kiasi hiki...??? Ili iweje..? Umetumwa au ni akili zako zimekutuma kuandika haya.. ???
 
Wengi unamaanisha nini?unadhani kila mtu ni kama wewe?
Wengi amemaanisha wale walioshiriki kutoa mawazo yao kwa tume ya warioba ambayo ilileta matokeo ya ile rasimu II. Maoni yaliyoleta ile rasimu ndio maoni ya watanzania wengi, sasa wapi hujamwelewa ? Kama hukumwelewa ni vema usingeandika llte.

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Pengo na balozi wa papa hawajakosea.hata yy kasema mtazamo wake binafsi.sio kanisa.kutoa matamko ya jimbo yana utaratibu wake.

Hata kwa jimbo la dsm bado halijatoa msimamo ila aliesema ni pengo.sio jimbo kuu la dsm.

Pia kupitia baraza kuu la maaskofu napo kuna utaratibu wake ambao maaskofu wote wanaketi na kuamua hivyo hata askofu wa iringa ambaye ni rais bado kuna mashart kadhaa huo ndio ukweli kabisa.

Wananchi wanahitaji katiba mpya ila kwa kiwango gani hapo ni utafiti,kanisa linapenda kuona huduma zinatolewa vema
 
Katika Kanisa Katoliki hakuna cheo cha mkuu wa kanisa wa nchi. Waandishi makanjanja ndio wanaopotosha na kuandika hivyo. Hapa Tanzania kwa vile tunaye Kardinali watu hudhani kuwa ndio mkuu wa kanisa. Vp kwa zile nchi ambazo zina makardinali Zaidi ya mmoja?????

Kila Askofu wa Jimbo ni mkuu katika Jimbo lake. Huyo Pengo hawezi kwenda Rulenge bila ruhusa ya Askofu Niwemugizi and vice versa. Kila Askofu anawajibika moja kwa moja kwa Baba Mtakatifu. Na hapa Baba Mt sio mtu bali ni ofisi.....kuna idara Vatican inahusika na Maaskofu......na kwa nchi za kwetu "nchi za misioni" mambo yetu yote yanashughulikiwa na idara inaitwa propaganda fide.

Ukisikia Jimbo limepewa hadhi ya Jimbo Kuu basi Askofu wake ataitwa Askofu Mkuu na yale majimbo yaliyo chini yake suffragan diocese yanamwangalia huyu Askofu Mkuu kama muunganishi wao....sio mkubwa wao.

Maaskofu wa nchi wameruhusiwa kuunda mabaraza ndizo hizo episcopal conferences.... na maaskofu huchagua yeyote kati yao kuwa Rais wa hilo baraza.... Niwemugizi amewahi kuwa Rais wa Baraza.....Pengo hajawahi kuwa Rais wa Baraza. Hiki ni chombo tu cha kulisemea kanisa mahalia - a particular church. Kwa sbb wakati mwingine kuna mahitaji maalumu ya kanisa mahalia. Mfano. Sheria ya Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni miaka 16 kwa mwanaume na 14 kwa mwanamke.....Sasa hapa Tanzania sharia za nchi ni kinyume na sharia ya kanisa...basi kanisa katoliki la Tanzania - hilo baraza linaomba kwa hapa Tanzania tufuate utaratibu wa nchi yetu!!!!!! What if mkatoliki wa TZ akiwa nje ya TZ akafunga ndoa akiwa na miaka 16 mwanaume ndoa yake itatambuliwa na kanisa katoliki TZ au la? nakuachia assignment.

Nimekuelewa vizuri, ateast hata wengine walio nje ya mfumo catholic tunaweza elewa, niko na swali lingine, mfano ukiangalia katika archibishops or bishops wengi, majina yao mengi yanaanza na Rev francis,or Rev Musa, lakini ikifika kwa cardinal wanaanza na His eminence makanga etc, pengine haiwezi ikawa ni unification figure within the Catholic Church and society?.
 
Asiyejitambua huyu! Kauli ile ni msimamo wa Watanzania tulio wengi. Unazidi kupoteza mvuto kwenye jamii ya Watanzania kwa kutokemea maovu ya dikteta uchwara.
mkuu upo sahihi kabisa, japo pia Askofu hakusema ule ni msimamo wa Kanisa, vivyo hivyo aliyosema Pengo nayo siyo msimamo wa kanisa. Ila kiongozi asiyeweza kukemea uovu huyo hafai, sijaisikia sauti ya Pengo juu ya shambulio la Lissu, ni ajabu.
 
Kwa mujibu wa taratibu za kanisa katoliki,askofu pengo sio msemaji wa kanisa,Msemaji ni Rais wa Baraza la maaskofu Tanzania,

Rais wa Baraza la Maaskofu ndio Bosi wa Maaskofu wote nchini na hata askofu pengo anakuwa yuko chini yake, pia kama askofu pengo hakiutumwa na Rais wa Baraza la Maaskofu,na yeye pia hana mamlaka ya kulisemea kanisa katoliki na alichosema ni maoni yake


Ukadinali wake ni kwa ajili ya kupiga kura kumchagua Papa tu,ila yeye akiwa Tanzania kicheo ni Askofu wa Jimbo la Dar es Salaam,anataka watu waone kwamba Ukadinali ndio Ukubwa wa kanisa,Mkubwa wa kanisa ni Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania,na ni askofu wa Iringa Askofu Ngalalekumtwa na anayefatia kwa Cheo ni huyo Niwemugizi, Pengo yuko chini yake Rais wa Baraza

"first among equals" Pengo hamzidi Askofu yeyote kwa cheo,ni sawa na rafiki yangu sheikh mkuu wa mkoa wa Dar ajione mkubwa kuliko mashehe wa mikoa mingine
ASANTE[emoji122] [emoji122]
 
Back
Top Bottom