Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

Shkamoo LEGE wewe ni kibokooooo.Salute miamia
 
wakuu za kutwa na poleni sana kwakusubilia sana mzigo.nikiwa na nafasi nitakuwa na ubwaga kadili niwezavyo hata kama ni sehem 10 nitafanya hivyo naninapokuwa nimebanwa plz tuvumiliane pia ndio maana najitahidi kwa siku ziwe zinafika sehem 10 na siku mkiona kimyaa msikasirike sana wakuu
 
wakuu za kutwa na poleni sana kwakusubilia sana mzigo.nikiwa na nafasi nitakuwa na ubwaga kadili niwezavyo hata kama ni sehem 10 nitafanya hivyo naninapokuwa nimebanwa plz tuvumiliane pia ndio maana najitahidi kwa siku ziwe zinafika sehem 10 na siku mkiona kimyaa msikasirike sana wakuu
Daaaaaahhhhhhh Mkuuu kwa hio unamaanisha leo umebanwa So sad Mkuu
 
SEASON 2

SEHEMU YA 23

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ jamani kila kitu kinakwenda vizuri.Sasa ni muda wa kujiandaa kwa ajili ya kuelekea huko.Akasema Mathew na kuwachukua Elibariki na Anitha hadi katika chumba ambacho huhifadhi silaha .Akafungua kabati na kutoa fulana nne zisizopenya risasi akawapatia Elibariki na Anitha na moja ikawa kwa ajili ya yule jamaa mwingine watakayemtumia
“ Eli,unaweza kutumia silaha ? Akauliza Mathew

“ Ndiyo ninaweza Mathew , nimewahi kupitia mafunzo katika jeshi la kujenga taifa kwa hiyo ninafahamu kutumia silaha ingawa sijawahi kuingia katika mapambano.” Akasema jaji Elibariki.Mathew akampatia bastora.
“ Ihifadhi hiyo silaha pengine tunaweza kuihitaji” akasema Mathew halafu akaelekea katika chumba alimo Yule jamaa na kumpatia fula moja isiyopenya risasi .
Walipokuwa tayari wakaingia katika gari na kuanza safari wakitanguliwa na Yule jamaa akiwa katika Toyota Carina


ENDELEA…………….



“ Anna jiandae kuna sehemu tunakwenda” Flaviana akamwambia mdogo wake Anna
“ usiku huu? Anna akashangaa

“ Ndiyo kuna sehemu nataka kwenda usiku huu” akasema Flaviana
“Kuna jambo gani la muhimu kiasi cha kutoweza kusubiri hadi asubuhi ? Akauliza Anna ambaye alionekana wazi kwamba hakuwa tayari kuondoka usiku ule.Flaviana akamsogelea na kwa sauti ndogo akasema

“ Elibariki kanipigia simu usiku huu”

“ What ?! Elibariki? Yuko wapi ? Anna akajikuta akiuliza maswali mfululizo
“ Hata mimi sifahamu yuko wapi lakini amenihakikishiwa kwamba yuko sehemu salama” akasema Flaviana
“ Ouh Thank you Lord” akasema Anna
“Umekwishamfahamisha baba kama umeongea na Elibariki? Hata yeye atafurahi sana kusikia kwamba Elibariki yuko mzima .Atafanya mpango wa kwenda kumchukua mahala aliko” akasema Anna
“ Baba nimeongea naye lakini sijamfahamisha chochote kuhusiana na jambo hili na ninaomba usimweleze chochote.Elibariki hataki mtu mwingine yeyote afahamu kuhusiana na jambo hili kwa ajili ya usalama wake .Baada ya Elibariki kunusurika kuuawa sasa nimeanza kuamini yale maneno yake aliyokuwa akisisitiza kwamba kuna kitu kibaya kinachoendelea .” akasema Flaviana
“ Hata mimi shambulio lile limenipa wasi wasi sana .Ninaweza kukubaliana nawe kuhusu jambo hili kwamba kuna kitu kinaendelea chini kwa chini.Unadhani nani anaweza kuwa amefanya shambulio lile?
“ Ni vigumu kufahamu ni nani lakini ninachoweza kuhisi kwa haraka haraka kuna kitu kinachoendela hapa na kama ukikumbuka kuna kitu mama alitaka kutuambia lakini hakuweza kwani alifariki ghafla mchana wa siku ile ambayo alitutaka tuonane naye .Ninahisi kuna jambo kubwa ambalo alitaka kutueleza na kuna hisia zinakuja kwamba huenda jambo hilo alilotaka kutuambia ndilo lillomgharimu uhai wake.Mama alifariki ghafla sana na wewe mwenyewe ulishuhudia sintofahamu iliyokuwepo kuhusiana na sababu ya kifo chake. Elibariki alituambia kwamba wamegundua mama alifariki kwa kuchomwa sindano ya sumu lakini taarifa ile ya madaktari bingwa ambayo baba anaiamini inasema kwamba mama hakufariki kwa sumu.Ukichunguza kwa undani sana masuala haya utagundua kwamba kuna kitu hapa si bure nadhani ndiyo sababu Elibariki hakati tamaa katika jambo hili.Mara ya mwisho nilipooongea naye aliniahidi kwamba hatalala usingizi hadi ukwe liwa jambohili ujulikane na ninahisi hiki ndichokilichotaka kumtoa uhai.Amenitaka nikaonane naye usiku huu kuna jambo anataka kuniambia na nijitahidi niipate ile taarifa ya madaktari bingwa.” Akasema Flaviana

“ Anaitaka ile taarifa? Anataka kuifanyia nini? Akauliza Anna

“ Sifahamu anaitaka kwa ajili gani lakini amesisitiza sana kwamba anaihitaji usiku huu.”
Anna akafikiri kidogo na kusema

“ taarifa yenyewe utaipata vipi wakati anayo baba? Sina hakika kama baba anaweza akakubali Elibariki aipate taarifa ile.”

“ tayari ninayo.Baba amenipatia usiku huu” akasema Flaviana
Anna ambaye tayari alikuwa kitandani akaamka na kujiandaa kisha wakaongozana hadi katika gari la Flaviana wakaondoka.

“ Flaviana unadhani Elibariki alikuwa sahihi kwamba mama aliuawa kwa sumu? Akauliza Anna

“ Siwezi kuwa na uhakika huo Anna lakini ukiangalia namna mambo yalivyotokea unaweza ukakubaliana na jambo hilo kwamba kifo cha mama hakikuwa cha kawaida.Nimekuwa nikilitafakari sana jambo hili .Hebu angalia mama alifariki ghafla na halafu ikatolewa taarifa kwamba usifanyike uchunguzi wowote wa kuhusiana na kifo chake .Hili jambo linashangaza sana kwa sababu haiingii akilini eti mwli wa mke wa rais usifanyiwe uchunguzi kubaini kilichosababisha kifo chake cha ghafla.Hii ni sababu iliyonifanya nimuombe Elibariki anisaidie kufanya uchunguzi ili tuweze kubaini kile kilichosababisha kifo cha mama. Katika uchunguzi uliofanyw ana watu wa Elibariki waligundua kwamba mama alichomwa sindano yenye sumu lakini baadae ikaja tena taarifa nyingine ikisema kwamba mama alikufa kwa shinikizo la damu na hakukuwa na dalili zozote za kuwepo kwa sumu katika mwili wake.Jambo hili linanipa mashaka sana na ninalazimika kuamini kwamba huenda kifo cha mama ni kweli kina mkonowa mtu na kikubwa zaidi kinachonifanya niamini hivyo ni baada ya Elibariki kunusurika kuuawa..Ninajiuliza sana kwa nini Elibariki atake kuuawa sasa hivi? Ni kitu cha kawaida majaji kuwa na maadui wengi na ndiyo sababu wamekuwa wakipatiwa ulinzi lakini kwa niniwatake kumuua sasa hivi? Ukijiuliza swali hili utagundua kwamba lazima kuna kitu kinachohusiana na kifo cha mama.Ninamfahamu Elibariki vizuri akilifuatilia jambo kwa nguvu namna hii lazima kuna sababu maalum.” Akasema Flaviana
“Hata mimi nimekuwa na mawazo kama yako na kilichonifanya niwe na mawazo hayo ni kuhusiana na shambulio la Elibariki.Kitu kingine kinachonipa maswali mengi ni kwamba kwa nini baba amekuwa kimya sana kuhusiana na masuala haya? Kwa masikio yangu nilimsikia Dr Kigomba akitoa amri kwamba watu waliokuwa wakifanya uchunguzi kubaini kilichomuua mama wakamatwe na kudhibitiwa lakini tulipomueleza baba kuhusiana na suala hili amekuwa mzito sana kutuamini na badala yake akadiriki kusema kwamba Dr Kigomba hahusiki kwa namna yoyote ile na suala lolote kuhusiana na kifo cha mama.”akasema Anna

“ Anna unahisi kwamba baba anaweza akawa anafahamu kinachoendelea ? Akauliza Flaviana

“ Siwezi kusema kwamba anahusika moja kwa moja lakini kwa namna alivyolishughulikia jambo hili inanipa mashaka kidogo kuaminikwambahawezi kufahamu kinachoendelea .Inaonekana wazi kabisa kwamba hakulipa ule uzito unaostahili.Aliyefariki ni mke wake na alipaswa kulipa uzito mkubwa sana sana suala hili lakini naona imekuwa tofauti kabisa.Haonekanikujali.haonekani kuumizwana kifocha mama.” Akasema Anna

“ Anna unaweza ukawa sahihi katika hili.Hata mimi japokuwa nilikuwa upande wake kuhusiana na ile taarifa ya madaktari bingwa lakini nilishangazwa zaidi na namna alivyolichukulia suala hili kwa wepesi na kukubali kirahisi maelezo ya Dr Kigomba.Halafu kuna jambo lingine ambalo kwangu mimi naliona kama si la kawaida ,Elibarikiamekuwa akihudhuria katika kila kikao tunachokifanya cha kifamilia.yeye ni sehemu ya familia yetu na ndiyo sababu siku ile nilimuita aje katika kikao kile ili kwa pamoja tuisikie taarifa ya uchunguzi wa kifo cha mama toka kwa madaktari bingwa.Kitu cha kushangaza baba hakuonyesha kufurahi kumuona Elibariki katika kikao kile na ndiyo maana akamtolea maneno yale makali.Kama utakumbuka baada ya kikao aliniita nje na akanifokea sana kwa nini nimemuita Elibariki katika kikao kile .Inaonyesha wazi kwamba hakutaka Elibariki afahamu chochote kuhusiana na taarifa ile.Swali kubwa la kujiuliza hapa ni kwamba kwa nini baba hakutaka Elibariki afahamu chochote kuhusiana na taarifa ile ya kifo cha mama? Binafsi yangu naona kama jambo hili linahitaji kufanyiwa uchunguzi ” akasema Flaviana

“ Tutalichunguzaze Flaviana? Akauliza Anna
“ Hata mimi sielewi lakini kuna haja ya kufanya uchunguzi.Ngoja tukionana na Elibariki usiku huu nitaongea naye kuhusu jambo hili.Yeye anaweza kuwa naushaurimzuri zaidi ” Akasema Flaviana
Waliendelea na safari yao hadi walipofika Simbona hoteli mahala alipoelekezwanaElibariki wakutane ,akapunguza mwendo na kusimamisha gari katika kituo cha basi.Kulikuwa na taksichache eneo lile

“ Hapa ndipo mlipangamkutane?akauliza Anna

“ Ndiyo ! tulipanga tukutane hapa” akasema Flaviana huku akiangaza macho kulitafuta lile gari aliloelekezwa na mara akaliona
“ Anna nitashuka na kuingia katika lile gari la bluu pale mbele.Mle ndimo alimo Elibariki.Utanisubiri hapa hapa,sintakawia sana” akasema Flaviana na kufungua mlango akashuka garini na kuelekea moja kw amoja katika lile gari la bluu akataka kuufungua mlango na kuingia akasita akenda kugonga katika kioo cha dereva.Kioo kikashushwa halafu mtu yule aliyekuwamo ndani ya ile gari akamuamuru afungue mlango wa nyuma na aingie ndaniya gari.Huku akiwa na uoga mwingi,Flaviana akafungua mlango wa nyuma akaingia.Elibariki hakuwamo ndani ya gari

“ Elibariki yuko wapi? Akauliza Flaviana
“ Funga mlango” akaamuru yule jamaa.

“ Wewe ni nani? Elibariki yuko wapi? Akauliza Flaviana kwa wasiw asi
“ Fuata maelekezo uliyopewa.Hukuambiwa uniulize maswali ,kazi yangu ni kukupelekea mahala aliko mtu wako.Kama uko tayari hatuna muda wa kupoteza funga mlango wa gari na nikupeleke huko unakotaka,kama hauko tayari shuka” akasema yule jamaa kwa sautiya ukali.Flaviana akafikiri kidogo halafu akaufunga mlango japokuwa mwili ulikuwa unamtetemeka.Gari likawashwa na kuondoka pale kituoni


******



Ni usiku ulionekena kuwa mgumu sana kwa Dr Joshua.Pamoja na uchovu aliokuwa nao baada ya kufanyishwa kazi nzito na Peniela usiku ule lakini hakuwa na dalilizozote za kupata usingizi.Bado suala la Elibariki liliendelea kukisumbua sana kichwa chake. Alikuwa ameketi sofani chumbani kwake akiwa nasimu yake pembani akisubiri kuwasiliana na Dr Kigomba kuhusiana na zoezi lialoendelea la kumfuatilia Flaviana ili kufahamu mahala alikojificha jaji Elibariki.

“ Toka nimeingia madarakani sijawahi kuwekwa katika wakati mgumu namna hii na mtu yeyote yule zaidi ya Elibariki.Nilikosea sana kumuacha hai mpaka leo .Kama ningejua mapema kwamba Elibariki ana sumu kali zaidi ya nyoka ningek…………….” Alikatishwa mawazoyake na muito wa simu.Haraka haraka akabonyeza kitufe cha kupokelea

“ Hallow Kigomba.Mambo yanakwendaje huko?
“ mambo yanakwenda vizuri,hadimuda huu hakuna tulichokigundua bado.Flaviana ameshuka katika gari lake na ameingia katika gari lingine na likaondoka.Nahisi humo ndimo alimo Elibariki.Tunaendelea kulifuatilia na nitakufahamisha kila kitu baada ya muda mfupi” akasema dr Kigomba

“ Kigomba tafadhali jitahidi kwa kila uwezavyo ili jambo hili limalizike.Sitaki kusikia kosa lolote.Hii ni nafasi ya dhahabu tumeipata na tuitumie vizuri” akasema Dr Joshua

“ usihofu mzee.Mimi mwenyewe nimeamua kuingia kazini na vijana leo ili kuhakikisha kwamba hakuna kosa litakalofanyika.Nitakutaarifu tena baadae kidogo kinachoendela” akasema Dr Kigomba na kukata simu

“ Nina hakika safari hii Elibariki hataweza kuponyoka. “akawaza Dr Joshua baada ya kumaliza kuongea na Dr Kigomba.Akamimina whysky katika glasi na kunywa funda kubwa. Mara akastuliwa na mlio wa simu.Zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu yake na akajiuliza mtu yule ni nani na amezipata wapi namba zake? .Alisita kidogo kuipokea ile simu.Ikaita kwa mara ya kwanza hakuipokea,ikaita kwa mara ya pili akaamua kuipokea
“ hallow “ akasema
“ hallow Dr Joshua” ikasema sauti ya upande wa pili.Dr Joshua akaitambua sauti ile
“ hallow Deus ! akasema Dr Joshua huku uso wake ukiwa na tabasamu
“ hahaha nilidhani hautaweza kuitambua sauti yangu” akasema Deus
“ Siwezi hata siku moja kuisahau sauti yako mtu ambaye uliniachia kijitii.Poel sana nilisikia kwamba ulikuwa unasumbuliwa na miguu na nimepanga kuja kukuona kwa siku za hivi karibuni.Vipi hali yako kwa sasa?
“ Kwa sasa hali yangu inaendelea vizuri sana.Tayari nimekwisha pata tiba naninaendelea vizuri.Nilianguka na kustua mguu wakati nikiwa shambani kufuatilia maendeleo ya mifugo yangu.”
“ usijali Mr Presidnet nitakuja kukutembelea siku za hivi karibuni.Unajua kuna mambo mengiya kujifunza toka kwako kwa kuwa na mimi ninakaribia kumaliza muda wangu wa uongozi kwa hiyo natakiwa kujifunza toka kwenu mlionitangulia namna ya kuishi maisha ya kawaida baada ya kumaliza kuitumikia nchi” akasema Dr Joshua
“ Karibu sana Dr Joshua muda wowote ukiwa na nafasi” akasema Deus ambaye ni rais mstaafu na ndiye aliyemkabidhi ofisi Dr Joshua.Kimya kifupi kikapita halafu Dr Joshua akasema

“ Deus umenistua kidogo kwa simu yako ya usiku huu.” Akasema Dr Joshua
“ usiogope Dr Joshua,nimekupigia muda huu kwanza kukupa pole nyingi sana kwa kifo cha mkeo Dr Flora.Ninamfahamu vizuri Dr \Flora alikuwa na mahusiano mazuri sana na mke wangu kwa hiyo hata sisi tumeondokewa na rafiki muhimu sana wa familia yetu.Sikuweza kufika kwenye msiba lakini mke wangu alikuwepo na aliniwakilisha” akasema Deus
“ Deus nashukuru sana na ninamshukuru Mungu kwa kila jambo.Yeye ndiye mwenye kupanga kila itu kitokee.Ni vigumu sana kuikabili hali hii lakini ninajitahidi” akasema Dr Joshua.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Deus akasema
“ jambo la pili ambalo nimekupigia simu usiku huu ni kutaka tuongee kuhusiana na Package E21.” Akasema Deus na kumstua sana Dr Joshua.Alihisi kama kuna kitu kizito kimempiga kichwani.Kwa sekunde kadhaa akawa ni kama mtu aliyepigwa na butwaa.
“Dr Joshua !!..akaita Deus
“ Hal..hallow deus” akasema Dr Joshua lakini kwa mbali sauti yake ilionekana kutetemeka.

“ Joshua mbona umestuka namna hiyo?akauliza Deus
“ Deus kwa nini unataka tuongelee jambo hilo? Kwa nini leo? Akauliza Dr Joshua

“ Is it safe? Bado iko salama? Akauliza Deus
Dr Joshua akavuta pumzi defu na kuuliza
“ Deus niambie kwa nini unauliza kuhusu jambo hili?
“ Usiogope Joshua,nahitaji tu kujua kama Package E21 iko salama” akasema Deus

“ Kwani kuna tatizo gani Deus ? Akauliza Dr Joshua.
“ Ninataka tu kufahamu kama bado ipo na iko salama” akasema Deus.Dr Joshua akakaa kimya kwa sekunde kadhaa na kusema

“ Deus naomba unieleze kwa nini umenipgia simu? Unataka nini?Ninakufahamu vizurilazima kuna sababu iliyokufanya ukanipigia simu “ Akasema Dr Joshua

“ Dr Joshua kuna ubaya gani kujua kama package iko salama? Mimi nilikabidhiwa na nikaitunza kwa miaka yangu yote kumi halafu nikakukabidhi wewe nikiaminikwamba itaendelea kuwa salama kwa hiyo ni jukumu langu kufahamu kama bado iko salama” akasema Deus na maneno yale yakaonekana kumchukiza Dr Joshua

“ Deus ninakuheshimu mno na ninataka nikueleze jambo moja,wakati wa uongozi wako hakuna aliyekuwa akikuingilia katika kila ulichokifanya.Kwa sasa umekwisha maliza uongozi wako na una pumzika kwa hiyo naomba uendelee kupumzika.Masuala ya Package E21 hayakuhusu tena.Hili ni jukumu langu kwa hiyo naomba usiingilie kazi zangu” akasemaDr Joshua
“ Dr Joshua,siwezi kuacha kufuatilia kuhusu kitumuhimu kama hiki.Wakati wa uongozi wangu niliilinda kama mboniya jicho langu tofauti na wewe unavyotaka kufanya” akasema deus na kumstua sana Dr Joshua.Uso wake ukakunja ndita.
“ Umesema nini Deus? Akauliza Dr Joshau kwa ukali
“ Joshua ninafahamu kila kitu unachotaka kukifanya”
“ Mbona sikuelewi unamaanisha nini? Akauliza Dr Joshua
“ Joshua ninafahamu kuhusu biashara unayotaka kuifanya “
“Biashara gani?

“ Usijifanye haufahamu Joshua.Usisahahu kwamba hata mimi nilikuwa katika nafasi kama yako na ninauwezo wa kufahamu kila kinachoendelea katika uongozi wako.I have lots of connections Joshua” akasema Deus.Dr Joshua akahisi joto kali na kijasho kikaanza kumchuruzika.Alihisi kusikia kizungu zungu.
“ Joshua are you there? Akauliza Deus baada ua Dr Joshua kuwa kimya
“ Unasemaje Deus?
“ Joshua ninarudiaa tena kukukumbusha kwamba ninaifahamu biashara unayoifanya na ninafahamu unataka kuwauzia akina nani.”akasema Deus
“ Kwa hiyo baada ya kugundua hivyo ni kitu gani unakihitaji? Akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ I want you to stop that business as soon as possible.” Akasema Deus kwa ukali

“ Dr Joshua sikuwahi kufikiria kwamba mtu kama wewe unaweza ukafanya kitu hatari kama hiki kwa taifa.Nilikukabidhi package ile nikiamini kwamba utaitunza na kuilinda kama mboniya jicho lako lakini umeingiwa na tamaa ya fedha na unataka kuhatarisha usalama wa taifa.Joshua please don’t do it.Usifanye kabisa jambo hatari kama hilo.Usiitoe ile package mahala ilipo.Pale iko sehemu salama na itaendelea kukaa pale kwa miaka yote.Ni kwa sababu ya unyeti wake ndiyo maana inahifadhiwa ikulu sehemu ambayo anayefahamu ilipo ni rais wa nchi pekee kwa hiyo Joshua narudia tena kukusisitiza kwamba usifanye hicho kitu unachotaka kukifanya.” Akasema Deus kwa ukali

“ who are you Deus to give me orders? Wewe huna mamlaka yoyote kwa sasa ya kuniamuru mimi jambo lolote!!akafoka Dr Joshua

“ Joshua naomba usisahau kwamba I’m a president too..”akasema Deus
“ Ex president. !! akasema kwa ukali Dr Joshua.

“ hauko tena katika uongozi kwa hiyo kwa sasa huna nguvu yoyote ya kuweza kuniamuru chochote” akaendelea kusema kwa ukali Dr Joshua
“ Kitu gani kinakufanya uwe na uhakika huo kwamba siwezi kukuamuru kitu? Umesahau kwamba mimi ndiye niliyekuteua na kukupigania hadi ukashika nafasi hiyo? Kama nilikuwa na nguvu ya kukuweka hapo ulipo ,unadhani sintakuwa na nguvu ya kukuondoa hapo ulipo ? Akauliza Deus

“ Usinitishe huna lolote Deus.I am a president of United republic of Tanzania and you are just a normal citizen so don’t you ever try to interfere anything in my administration ! Wananchi ndio walioniweka hapa na wala si wewe kwa hiyo usinitshe na huwezi kunifanya chochote na tena ninakuonya kwamba usithubutu tena kunipigia simu na kunitolea vitisho. Mimi ni rais na nina uhuru wa kufanya jambo lolote .Package hii haihusiani na raia yeyote wan nchi hii na kuiuza sijavunja sheria wala katiba ya nchi” akasema Dr Joshua kwa ukali huku jasho likimtiririka.

“ Joshua unapata kila kitu unachokihitaji katika maisha yako,na ukimaliza muda wako wa kulitumikia taifa utaishi kwa raha mustarehe na kwa heshima nyingi.Umekwisha fanya mambo mengi mazuri katika nchi hii na watanzania wataendelea kukukumbuka kwa miaka mingi ijayo kwa mambo uliyowafanyia.Tafadhali usiingiwe na tamaa na ukaharibu yale mazuri yote uliyoyafanya kwa sababu tu ya hayo mabilioni ya fedha unayotarajia kuvuna baada ya kuiuza Package E21.” Akasema Deus

“ Deus naomba usitafute ugomvi kati yangu na wewe kwa sababu unaelewa kwamba huwezi kunishinda hata kidogo.” Akasema Dr Joshua
“ Joshua hii ninakupa amri nasi ombi.Nikisikia kwamba unaendelea na biashara hii unayotaka kuifanya basi jiandae kuondoka katika hicho kiti.Siko tayari kuona ukihatarisha usalama wa nchi yetu kwa tamaa zako.Siko tayari kuona maisha ya mamilioni ya watu yakiwa hatarini kwa tamaa zako.Nitakudhibiti kabla hujafanya unavyotaka kufanya and I will take you down Joshua.Kwa heri kwa sasa” akasema Deus na kukata simu.Zilipita kama dakika mbili Dr Joshua bado alikuwa amesimama akiwa na simu yake mkononi.

“ Huyu shetani katokea wapi tena? Aggghhh!!.. kabla hili halijaisha linaibuka hili.” Akajiuliza Dr Joshua na kumimina mvinyo katika glasi akaugugumia wote .
“ Deus amefahamuje kuhusu mpango huu? Akaendelea kujiuliza akamimina tena mvinyo katika glasi

“ Tunaojua kuhusu siri hii ni watu watatu ,mimi,Kigomba na Amos ,ni nani basi kati yetu ambaye atakuwa amempa taarifa Deus? Lazima ni mmoja kati yetu .Nina ni kati ya Kigomba na Amos? Akajiuliza

“ Akili yangu inanituma kwa Amos.Imani inaanza kunitoka kwake.Nahisi ni yeye ambaye anaweza kuwa akitoa habari zetu.Dr Kigomba sina shida naye ni mtu ambaye nimekwisha fanya naye mambo mengi makubwa na ya hatari na hakuna hata siku moja nimewahi kusikia jambo lolote nililofanya naye limevuja.Baada ya kumshirikisha captain Amos mambo ndiyo yameanza kwenda kombo.Nitamfanyia uchunguzi wa kina Amos na kuzifahamu nyendo zake.Nitaweka vijana wa kumfuatilia katika kila jambo analolifanya na ukweli utajulikana tu.Nikifahamu kwamba ni yeye ndiye anayetoa habari zetu basi sintakuwa na huruma naye,nitamzimisha kimya kimya “ akawaza Dr Joshua
“ Deus Amasile Mkozumi ..” akatamka Dr Joshua kwa sauti ndogo

“ Deus ni mtu ninayemuheshimu sana .Ni mtu ambaye wakati wa uongozi wake alifanya mamabo mengi makubwa kwa nchi hii na heshima yake ni kubwa sana .Kwa msaada wake nilifanikiwa kukipata kiti hiki cha urais.Pamoja na mambo yote aliyonifanyia lakini kwa hiki anachotaka kukifanya amepotea njia.Nitaweka kila kitu pembeni na nitapambana naye.Ninamfahamu vizuri Deus ni mtu ambaye akisema jambo hulitimiza.Kama ameahidi kunitoa katika kiti hiki basi atafanya hivyo.Ni mtu ambaye bado ana ushawishi mkubwa sana na anaweza akawashawishi wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na rais na wakaniondoa madarakani.Ni mtu ambaye sipaswi kumpuuza hata kidogo.Nguvu yake katika siasa bado ni kubwa .Kwa maneno aliyoongea japokuwa nilikuwa nikibishana naye lakini yameniogopesha sana.Natakiwa kuchukua hatua haraka sana na kumaliza Deus kabla hajanimaliza.Mimi ni rais wa nchi na nina kila nyenzo ya kuweza kummaliza Deus na wale wote anaoshirikiana nao.Baada ya Elibariki nimepata adui wa pili.Lazima niwamalize wote haraka sana.Nimekaribia mwisho kabisa wa biashara hii kwa hiyo lazima nihakikishe kwamba ninawaondoa wote haraka iwezekanavyo.” Akawaza Dr Joshua na kuchukua simu yake akabonyeza namba Fulani halafu akaiweka simu sikioni

“ General Adam,tafadhali naomba nikuone hapa ikulu usiku huu.” Akasema Dr Joshua na kukata simu

“ I will destroy you Deus,I must destroy you!!! Akasema Dr Joshua kwa hasira na kunywa mvinyo kwa fujo.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
 
SEASON 2
SEHEMUYA 24
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Ninamfahamu vizuri Deus ni mtu ambaye akisema jambo hulitimiza.Kama ameahidi kunitoa katika kiti hiki basi atafanya hivyo.Ni mtu ambaye bado ana ushawishi mkubwa sana na anaweza akawashawishi wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na rais na wakaniondoa madarakani.Ni mtu ambaye sipaswi kumpuuza hata kidogo.Nguvu yake katika siasa bado ni kubwa .Kwa maneno aliyoongea japokuwa nilikuwa nikibishana naye lakini yameniogopesha sana.Natakiwa kuchukua hatua haraka sana na kumaliza Deus kabla hajanimaliza.Mimi ni rais wa nchi na nina kila nyenzo ya kuweza kummaliza Deus na wale wote anaoshirikiana nao.Baada ya Elibariki nimepata adui wa pili.Lazima niwamalize wote haraka sana.Nimekaribia mwisho kabisa wa biashara hii kwa hiyo lazima nihakikishe kwamba ninawaondoa wote haraka iwezekanavyo.” Akawaza Dr Joshua na kuchukua simu yake akabonyeza namba Fulani halafu akaiweka simu sikioni
“ General Adam,tafadhali naomba nikuone hapa ikulu usiku huu.” Akasema Dr Joshua na kukata simu
“ I will destroy you Deus,I must destroy you!!! Akasema Dr Joshua kwa hasira na kunywa mvinyo kwa fujo.

ENDELEA…………………..
Elibariki alikuwa wa kwanza kulitambua gari la Flaviana mara tu lilipowasili Simbona hoteli na kwenda kusimama katika kituo cha mabasi kama alivyokuwa amemuelekeza.
“ Ile pale gari ya Flaviana” akasema jaji Elibariki akiwalekeza akina Mathew.Toka katika sehemu waliyokuwa wameegesha gari lao waliweza kushuhudia kila kitu kilichokuwa kinatokea.
“ Are you sure? Akauliza Mathew
“ yes i’m sure.Ninalifahamu gari la mke wangu “ akajibu Elibariki
Gari la Flaviana likasimama katika kituo cha daladala na baada ya kama dakika mbili hivi mlango wa gari Flaviana ukafunguliwa akashuka mwanamke mmoja ambaye Elibariki akamtambua pia
“That’s my wife Flaviana’ akasema Mathew
“ She’s pretty.” Akasema Anitha na kumfanya Elibariki atabasamu.Mua huo huo zikawasili gari mbili na kuegesha si mbali sana na gari la Flaviana
Kisha shuka garini Flaviana akaelekea moja kwa moja katika gari la bluu aliloelekezwa akagonga katika kio cha upande wa dereva akazungumza na mtu aliyekuwamo ndani.
“ What is she doing? Akauliza Mathew .
Mara Flaviana akafungua mlango wa gari na kuingia ndani na baada ya muda kidogo gari lile likaondoka .
Dakika moja na sekunde kadhaa baada ya gari alilopanda Flaviana kuondoka pale kituoni ,gari mbili zilizokuwa zimeegeshwa karibu na gari la Flaviana nazo zikaondoka.
“ Mmeona zile gari mbili zilizoondoka mara tu baada ya gari alimo Flaviana kuondoka? Ninahisi lazima watakuwa wamemfuatilia Flaviana.Flaviana ni mtu ambaye anamulikiwa sana na watu wanokutafuta Elibariki na ndiyo maana nikaamua kuweka mtego kama ule ili kuhakiki kama kuna mtu atakuwa akimfuatilia Flaviana.Gari zile mbili zimenipa mashaka sana .Twendeni tuzifuatilie ili tujue kama ni kweli Flaviana anafuatiliwa.” Akasema Mathew
“ Mathew,itakuwaje iwapo ni kweli mke wangu anafuatiliwa? Maisha yake yako hatarini” akasema jaji Elibariki kwa uoga
“ Usiogope Elibariki.Tutafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kuweza kumlinda mke wako” akasema Mathew na kuwasha gari wakaanza safari kumfuatilia Flaviana


*******

General Adam aliwasili katika makazi ya rais kuitika wito wa Dr Joshua aliyemtaka afike mara moja usiku ule.Dr Joshua akiwa chumbani kwakealitaarifiwa kuhusu kuwasili kwa generali Adam na kisha akaenda kuonana naye
“ General Adam,karibu sana” akasema Dr Joshua huku akipeana mikono na gererali Adam
“ Nashukuru sana mheshimiwa rais .” akasema Adam na kisha Dr Joshua akamuongoza katika chumba chake cha maongezi ya faragha
“ Mheshimiwa rais ,kwanza pole sana kwa msiba uliokupata wa kufiwa na mkeo.” Akaanzisha mazungumzo Generali Adam
“ Ahsante sana Adam, nimekwisha poa .Yote hii ni mipango ya Mungu.Yeye ndiye mwenye kupanga kila jambo” akasema Dr Joshua halafu Akaka kimya kidogo na kusema
“ General Adam nafahamu nimechukua muda wako wa mapumziko na kukuita hapa usiku huu.Samahani sana kwa hilo” akasema Dr Jsohua
“ Usijali kuhusu hilo mheshimiwa rais.Sisi ni watumishi na muda wote tuko kazini” akasema Generali Adam
“ Nashukuru sana kusikia hivyo General Adam” akasema Dr Joshua halafu akakaa kimya kidogo akavuta pumzi ndefu na kusema
“ General Adam mimi na wewe tumekuwa ni marafiki wakubwa toka tukiwa jeshini na hata baada ya kushika nyadhifa tumekuwa karibu sana na kila pale ninapokuwa na tatizo kubwa hujawahi kushindwa kunisaidia.” Akasema Dr Joshua
“ Ni kweli Dr Joshua.Hata siku moja siwezi kushindwa kukusaidia Dr Joshua .Hata wewe umekwisha nisaidia katika mambo mengi sana.Wewe ni zaidi ya rafiki ” akasema Adam
“ Ahsante sana kwa maneno hayo General Adam .Kama nilivyotangulia kusema ,nimekuita hapa nina tatizo ambalo ninahitaji sana msaada wako .”
“ Usihofu chochote Dr Joshua kama kuna tatizo lolote nitaarifu na kama liko ndani ya uwezo wangu basi nitakusaidia na kama litakuwa nje ya uwezo wangu basi tutaangalia namna ya kulitatua tatizo hilo” akasema Adam
“ Ahsante sana Adam.Naomba pia kile tutakachokiongea hapa kiwe ni siri kubwa kati yako na mimi na asifahamu mtu mwingine yeyote yule na ndiyo maana nikakuita kwa siri usiku huu”
“ Dr Joshua nadhani unaniamni na ndiyo maana ukaniita hapa kwa hiyo usihofu chochote,siri yako itakuwa salama na hakuna yeyote atakayejua” akasema Adam
Dr Joshau akainama akafikiri kidogo na kusema
“ Adam Kazi ya urais ni kazi ambayo watu wengi wanaililia na kufanya kila wawezalo ili waipate lakini ukweli hii ni kazi ngumu sana na yenye changamoto nyingi.Kiti hiki cha urais ni kiti cha moto na huwezi kuamini hayo hadi ukipata nafasi ya kukalia kiti hiki.Unapokalia kiti hiki cha urais unajiona tofauti na raia wengine wa kawaida,unajiona uko juu yao na unaweza ukafanya jambo lolote na hilo ndilo huwafanya viongozi wengi wakapotea njia na kufanya mambo yale ambayo yanaweza yakaenda kinyume na maadili au ya uvunjifu wa sheria za nchi.Hakuna kiongozi ambaye anakalia kiti hiki na akamaliza muda wake wa uongozi akiwa hajafanya hata kosa moja.” akasema Dr Joshua na kukaa kimya kidogo
“ Ukikalia kiti hiki cha urais “ akaendelea
“Unakuwa na marafiki wengi lakini unajenga pia na maadui wengi.Hata mimi nina maadui lakini kuna adui mmoja ambaye ni mwenye nguvu na ametishia kiti changu.Hata mimi ninamuogopa kutokana na nguvu aliyonayo katika chama na ni mtu ambaye alichangia sana kwa mimi kukikalia kiti hiki.Kuna jambo nimelifanya ambalo huyu mtu ana maslahi nalo na tayari ametishia kuniondoa katika kiti hiki.Hilo la kuniondoa katika madaraka kwa kuwashawishi wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na mimi silijali sana kwani muda niliobaki nao katika uongozi ni mfupi lakini mtu huyu ataendelea kuniandama hata nitakapomaliza uongozi wangu kwa kuwa jambo ninalotaka kulifanya lina maslahi kwake.Anataka nisilifanye jambo hilo lakini siwezi kuacha kulifanya jambo hilo kwa sababu litanihakikishia kuishi maisha mazuri sana baada ya kumaliza uongozi wangu.Kazi ya uraisi kwa nchi kama hizi za kwetu ni kazi ambayo ina heshima kubwa lakini isiyokuwa na maslahi makubwa.Nimelitumikia taifa kwa miaka kumi lakini nitakapomaliza nitarejea katika maisha yale yale ya kawaida sana .Japokuwa nitakuwa nikitunzwa na serikali bado maisha yangu hayatakuwa mazuri jinsi ninavyotaka kwa hiyo lazima kabla ya kumaliza kipindi changu cha uongozi basi nijipange ili niishi maisha mazuri baada ya kustaafu.”akanyamaza kidogo na kuendela
“ Lazima nichukue hatua za haraka sana dhidi ya mtu huyo ambaye ninamtaja kama adui yangu namba moja kwa sasa.Njia pekee ya kujihakikishia usalama wangu ni kwa kumuondoa huyo adui yangu toka katika uso wa dunia.Bila kufanya hivyo sintakuwa na amani na maisha yangu na nina hakika ataendelea kuniandama kila uchao” akasema Dr Joshua
“ Pole sana Dr Joshua.Nafasi kama hizi za uongozi lazima ukutane na changamoto nyingi sana.Ni nani huyo adui yako na unapendekeza tumshughulikiaje? akauliza Generali Adam
“ Ndiyo maana nilikwambia kwamba mazungumzo yetu ni ya siri na asifahamu mtu mwingine yeyete kwa sababu mtu huyo ninayemzungumzia ni mtu mkubwa sana hapa nchini na aliwahi kuwa rais wa nchi kwa hiyo jambo kama hili ni siri kubwa sana.” akasemaDr Joshua
“ usihofu kitu mzee.Si mara ya kwanza mimi na wewe kufanya kazi kubwa na za hatari na haijawahi kusikia hata siku moja kwamba kuna siri imevuja.Mimi ni mwaminifu sana kwako mheshimiwa rais.Jisikie huru kunieleza chochote “ akasema Generali Adam
“ Good.Mtu huyo ninayemsema hapa ni rais mstaafu Deus Mliswati” akasema Dr Joshua.Kimya kikubwa kikatanda mle ndani wakabaki wakitazamana.Generali Adam alistushwa mno na taarifa ile.
“ Adam najua umestuka sana kusikia jina la Deus.N i jina kubwa na hakuna mtu asiyemfahamu mtu huyu katika nchi hii.Mimi mwenyewe ni mtu ambaye ninamuheshimu sana Deus na nina deni kubwa kwake kwa mambo makubwa aliyonifanyia.Lakini katika siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.Deus leo hii amegeuka kuwa adui yangu na nisipofanya juhudi za makusudi na za haraka kujilinda basi ataniondoa kwani amekwisha dhamiria kufanya hivyo kwa hiyo lazima nijihami mapema.lazima nimuwahi.Nataka tumuue Deus haraka iwezekanavyo” akasema Dr Joshua.Adam akakuna kichwa chake na kuinama akafikiri kidogo na kusema.
“ dr Joshua hili si jambo jepesi hata kidogo.Yule ni rais mstaafu na kummaliza kama unavyotaka ni jambo gumu kidogo.Una hakika una nia ya dhati ya kutaka kumuua Deus? Hakuna namna mnayoweza kumaliza tofauti zenu? Akauliza general adam
“ Adam hakuna namna yoyote ya kufanya zaidi ya kumuua.Deus is my enemy na nisipomuwahi yeye basi ataniwahi mimi.Siko tayari Deus aniteketeze wakati nina kila sababu ya kuweza kummaliza.Hii ni vita na inanibidi nitumie kila aina ya silaha na mbinu ili kummaliza kwa hiyo sitaki kushindwa nataka nishinde hii vita na kitu pekee kitakachonihakikishia ushdini ni kwa kumuua Deus.Nimekuita hapa kama rafiki na mtu wangu wa karibu unisaidiekatika hili.Hili ni jambo zito, na lenye usiri mkubwa kwa hiyo nahitaji kumshirikisha mtu ambaye ninamuamini na wewe ni mtu ambaye ninakuamini sana ”akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua siku zote nimekuwa mtiifu kwako na nitaendelea kuwa mtiifu lakini kuhusu suala hili ninaomba ulifikirie tena upya kwani linaweza kuwa na athari kubwa kwako na kwetu pia .Deus ni rais mstaafu kwa hiyo kitendo cha kumuua kinaweza kusababisha uchunguzi wa kina ukafanywa na inaweza ikajulikana kama umehusika katika kifo hicho na utakabiliwa na matatizo makubwa sana” akasema Generali Adam
“ Adam tafadhali usiogope.Mimi ni rais wa nchi na nina uwezo mkubwa wa kuzuia huo uchunguzi usifanyike.” Akasema Dr Joshua.Generali Adam aliinama chini alionekana kuzama katika mawazo .
“ Unawaza nini general? Akauliza Dr Joshua
“ nI kuhusiana na jambo hili.Sijawahi kushiriki katika jambo kubwa kama hili hususani la kutaka kumuua rais mstaafu.Hili ni jambo zito kwa hiyo lazima nifikirie kwa makini kabla ya kutoa jibu kama ninaweza kulifanya ama la” akasema Deus
“ Nafahamu hii ni kazi ngumu lakini ina ujira mnono.Mkuu wa majeshi Generali Gosbert maziga anastaafu mwezi ujao na nitakuteua wewe kuwa mkuu wa majeshi.” Akasema Dr Joshua na Generali Adam akainuka kichwa
“ Dr Joshua is this a joke? Akauliza Adam
“ Kwa nini nikufanyie masihara Adam.Nitakuchagua wewe kuwa mkuu mpya wa majeshi.Mimi ndiye mwenye uwezo huo kwa hiyo nakuomba tafadhali nifanyie hiyo kazi na utaona matunda yake.Kabla sijamaliza uongozi wangu nitakuacha katika nafasi kubwa na ya juu kabisa katika jeshi.Hivi ndivyo huwa ninafanya kwa wale watu wangu wote wa karibu ambao hunifanyai kazi zangu na kunifurahisha,huwaweka juu katika nafasi za juu sana” akasema Dr Joshua na kumfanya Adam atabasamu
“ Dr Joshua nimekosa neno la kusema kwa furaha niliyonayo .Usiwe na wasi wasi ninakuahidi kwamba nitaifanya kazi yako.Lakini nitahitaji muda kidogo wa kama siku mbili hivi nitulize akili nitafakari ni kwa namna gani tunaweza kuutekeleza mpango huu mku………………” Adam akanyamaza baada ya simu ya Dr Joshua kuita na sura ya Dr Joshua ikabadilika kidogo baada ya kuliona jina la mpigaji
“ Give me one minute Adam.Its an important call” akasema Dr Joshua na kutoka mle ndani ya kile chumba
“ Hallow Kigomba” akasema Dr Joshau baada ya kupokea simu
“ Dr Jos..Joshu.Jos…..” Kigomba alikuwa anatetemeka na kushindwa kuongea.Hali ile ikamstua sana Dr Joshua
“ Kigomba what happened? Akauliza Dr Joshua kwa wasi wasi mwingi
“ Joshua….jos..” Bado Dr Kigomba alishindwa kuongea.Alikuwa akihema kwa kasi
“ Kigomba niambie nini kimetokea.Naomba utulie tafadhali na unieleze nini kimetokea? Akauliza Dr Joshua .
“ Dr Joshua kuna matatizo makubwa yametokea.” Akasema Kigomba
“ Matatizo makubwa ?!!..Nini kimetokea Kigomba? Dr Joshua akauliza huku mapigo ya moyo yakibadilika na kuanza kwenda kwa kasi kubwa
“ Mwanao Flaviana..!! akasema Kigomba
“ Flaviana amefanya nini?
“ Flaviana amepigwa risasi”
Dr Joshua alikisikia kichwa chake kama kikigongwa na nyundo kubwa.Alishindwa aseme nini.Mwili ulimtetemeka.Ilikuwa ni taarifa iliyomstua sana.Baada ya kama dakika moja akakohoa kidogo na kusema
“ Kigomba tell me it’s a joke” akasema Dr Joshua
“ Its not a joke Joshua.Ni kweli kabisa Flaviana amepigwa risasi na hivi sasa tuko njiani tunamkimbiza hospitali ya taifa” akasema Dr Kigomba
“ Imetokeaje Kigomba? Imekuwaje akapigwa risasi? Akauliza Dr Joshua
“ Dr Joshua sina muda wa kukuelezea kwa sasa.Ninachokuomba amka na uanze safari ya kuelekea hospitali mara moja.” Akasema Dr Kigomba
“ Kigomba naomba uniambie ukweli.Is she dead ? akauliza Dr Joshua
“ No ! but she’s in critical condition.Kuna vijana wetu kama watatu au zaidi wamefariki dunia.”akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akashika kichwa .Alichanganyikiwa.
“ Ok Kigomba I’m on my way there” akasema Dr Joshua na kuingia katika chumba alimo genereli Adam.
“ Adam tutaendelea na maongezi siku nyingine.Kuna tatizo kubwa limetokea.Binti yangu amepigwa risasi ”
“ Is she ok? Akauliza genereli Adam
“ I don’t know.Fanyia kazi hayo mambo tuliyoongea” akasema Dr Joshua
“ Sawa mzee ,nitayafanyia kazi na nitakujulisha kila kitu.Pole sana mheshimiwa rais” akasema Generali Adam.Dr Joshua akatoka kwa kasi mle chumbani na kuwataarifu walinzi wake kwamba wajiandae wanaelekea hospitali,akaingia chumbani kwake kujiandaa
“ Imekuwaje Flaviana akapigwa risasi? Akajiuliza Dr Joshua.Mwili bado ulikuwa unamtetemeka.
“ Ouh Mungu wangu naomba umponye mwanangu huyu.Ninampenda sana binti yangu na siko tayari afariki” akasema Dr Joshua kwa sauti ndogo halafu akatoka na kuingia kuingia garini safari ya kuelekea hospitali ikaanza.

NINI KIMETOKEA NA KUSABABISAH FLAVIANA APIGWE RISASI? TUKUTANE TENA KATIKA SEHEMU IJAYO
 
SEASON 2


SEHEMU YA 25

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kigomba naomba uniambie ukweli.Is she dead ? akauliza Dr Joshua

“ No ! but she’s in critical condition.Kuna vijana wetu kama watatu au zaidi wamefariki dunia.”akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akashika kichwa .Alichanganyikiwa.
“ Ok Kigomba I’m on my way there” akasema Dr Joshua na kuingia katika chumba alimo genereli Adam.
“ Adam tutaendelea na maongezi siku nyingine.Kuna tatizo kubwa limetokea.Binti yangu amepigwa risasi ”
“ Is she ok? Akauliza genereli Adam
“ I don’t know.Fanyia kazi hayo mambo tuliyoongea” akasema Dr Joshua
“ Sawa mzee ,nitayafanyia kazi na nitakujulisha kila kitu.Pole sana mheshimiwa rais” akasema Generali Adam.Dr Joshua akatoka kwa kasi mle chumbani na kuwataarifu walinzi wake kwamba wajiandae wanaelekea hospitali,akaingia chumbani kwake kujiandaa

“ Imekuwaje Flaviana akapigwa risasi? Akajiuliza Dr Joshua.Mwili bado ulikuwa unamtetemeka.

“ Ouh Mungu wangu naomba umponye mwanangu huyu.Ninampenda sana binti yangu na siko tayari afariki” akasema Dr Joshua kwa sauti ndogo halafu akatoka na kuingia kuingia garini safari ya kuelekea hospitali ikaanza.



ENDELEA………………


“ Majanga yanazidi kuniandama. Hata wiki mbili hazijapita toka amefariki flora leo hii tena Flaviana naye yuko katika hatari ya kunitoka.Lakini hizi zote ni changamoto za biashara ile ya ile package.Pamoja na yote yaliyotokea na yatakayoendelea kutokea lakini lazima niifaney biashara hii”akawaza Dr Joshua akiwa garini kuelekea hospitali

“ Lakini imetokeaje hadi Flaviana akapigwa risasi ? Kigomba ana kazi kubwa ya kunielezea kuhusiana na jambo hili lilivyotokea na kusababisha mwanangu apigwe risasi.Ouh halafu nimeondoka bila ya kumtaarifu Anna kuhusiana na kilichotokea” akawaza Dr Joshua na akachukua simu yake na kumpigia Anna

“ Hallow Anna uko wapi?” akauliza Dr Joshua baada ya Anna kupokea simu.Anna akasita kidogo kujibu hakutaka baba yake afahamu mahala alipo
“ Anna uko wapi? Akauliza tena Dr Joshua

“ Nimetoka kidogo baba ”

“Uko wapi? Umetoka umekwenda wapi? Akauliza Dr Joshua
“ Nimetoka na Flaviana?!
“ Umetoka na Flaviana?!! Dr Joshua akazidi kushangaa

“Ndiyo baba ,Flaviana aliniomba nimsindikize mahala Fulani kuna mtu anakwenda kuonana naye usiku huu.”
“ Anna tafadhali naomba unieleze ukweli uko wapi? Sikuulizi kwa lengo baya”

“ Baba ni kweli nimemsindikiza Flaviana .”
“ Anna mbona unazidi kunichanganya.Uko na Flaviana muda huu?
“ Hapana siko naye kuna sehemu amekwenda na mimi niko garini ninamsubiri”

“ Anna tafadhali naomba usiondoke hapo ulipo.Nielekeze mahala ulipo ilinitume walinzi wajewakuchukue mara moja”

“ kwani kuna jambo gani baba?Mbona unaniogopesha?

“ Tafadhali niambie Anna uko wapi?
Anna akafikiri kwa sekunde chache na kusema

“ Niko hapa Simbona hoteli ninamsubiri Flaviana” akasema Anna

“ Ok Anna naomba usitoke hapo ulipo na kama uko garini usishuke hadi utakapowaona walinzi nitakaowatuma” akasema Dr Joshua akakata simu na kuwapigia walinzi ili wamfuate Anna pale alipo.Aliogopa kumweleza ukweli Anna akiogopa kumstua

“ kigomba amenieleza tu kuhusiana na Flaviana lakini hajanipa taarifa za Elibariki kama walifanikiwa kumpata au hawakufanikiwa ? Kama hawakufanikiwa kumpata na safari hii basi tutakuwa na wakati mgumu sana.Lakini kwa nini inakuwa vigumu kumpata mtu kama huyu? Hapana imetosha sasa na siwezi kumvumilia.Nitaitumia nguvu yangu kama rais na Elibarii atapatikana ndani ya kipindi kifupi.Nitatumia mtandao mpana wa jeshi la polisi kumtafuta na nitampata.” Akawaza Dr Joshua huku msafara ake ukienda kwa kasi isyo ya kawaida na hatimaye wakawasili hospitali na kupokelewa na dakari mkuu wa hospitali kuu ya taifa akiwa sambamba na Dr Kigomba ambaye alikuwa ameloana damu
“ Daktari mwanangu anaendeleaje? Akauliza Dr Joshua
“ Hali yake haikuwa nzuri wakati tumempokea na kwa sasa ameingizwa katika chumba cha upasuaji na timu ya madaktari wanaendelea kumuhudumia ili kuokoa maisha yake ” akasema daktari mkuu wakati wakiwa njiani kuelekea katika jengo la upasuaji.Dr Joshua aliomba aruhusiwe kuingia katika chumba cha upasuaji ashuhudie kilichokuwa kinaendelea.Akavalishwa mavazi maalum ya kuingilia katika chumba kile na kuingia akiongozana na daktari mkuu.Kazi ya kuokoa uhai wa Flaviana ilikuwa inaendelea na madaktari walikuwa katika heka heka kubwa.

“ Ee Mungu nafahamu mimi si mkamilfu mbele zako na nimekukosea mambo mengi sana makubwa lakini naomba usiniadhibu kwa kunichukulia binti yangu ninayempenda sana.bado ninamuhitaji sana” Dr Joshua akaomba kimya kimya.Machozi yalimlenga kwa kumuona mwanae akiwa kitandani hajitambui akisaidiwa kupumua kwa mashine.Hakutaka kuendelea kukaa mle ndani akatoka .
“ Dr Marcelo naomba mjitahidi kwa kila namna muwezavyo kuokoa uhai wa mwanangu.Sitaki kumpoteza Flaviana “ akasema Dr Joshua

“ mzee tunafanaya kila linalowezekana ili kuokoa uhai wa mwanao.Wewe mwenyewe umeshuhudia namna madaktari wanavyojitahidi na nina hakika watafanikiwa.Tumuombe Mungu atusadie katika jambo hili” akasema Dr Marcelo.

“ nashukuru sana Dr Marcelo.Nina hakika Mungu atasikia kilo changu na kumnusuru mwanangu” akasema Dr Joshua
“ Mzee unaweza tu kwenda kupumzika na sisi tutaendelea kuifanya kazi hii usiku huu na kama kutakuwa na lolote tutakufahamisha” akashauri Dr Marcelo

“ No Marcelo.Nitakesha hapa kufuatilia hatima ya mwanangu.” Akasema Dr Joshua ikamlazimu Dr Marcelo ampeleke sehemu ya mapumziko wakati wakisubiri Flaviana atolewe katika chumba cha upasuaji.Dr Kigomba naye aliambatana naye
“Dr Kigomba naomba unieleze nini hasa kimetokea? Akauliza Dr Joshua wakiwa wamepumzika wakisubiri upasuaji wa Flavina umalizikie.Midomo ya Dr Kigomba ilikuwa mizito kufunguka
“Kigomba tell me what happened? Akauliza Dr Joshua huku akimtazama Dr Kigomba kwa macho makali

“ Dr Joshua nashindwa hata sehemu ya kuanzia kukueleza namna ilivyokuwa” akasema Dr Kigomba
“ Tell me everything !! akasema r Joshua.Kabla Kigomba hajasema chochote akatokea Anna akiwa ameongozana na walinzi.Alikuwa na wasiwasi mwingi sana

“ Baba kuna nini?akauliza anna.Dr Joshua akamshika mkono na kumketisha kitini.
“ Anna dada yako alikupeleka wapi usiku huu ? Akauliza Dr Joshua

“ Aliniomba nimsindikize sehemu Fulani kuna mtu alikuwa anakwenda kuonana naye?
“ hakukwambia ni nani aliyekuwa anakwenda kuonana naye?
“ Hapana hakuniambia kwani kuna nini?akauliza Anna

“ Ulimuona mtu huyo aliyekwena kuonana naye? Akauliza Dr Joshua
“ Hapana sikufanikiwa kuonana naye kwani aliniacha mimi katika gari na yeye akaenda kuonana na mtu huyo” akajibu Anna
“ Alionana naye wapi?
Anna akasita kidogo halafu akasema

“ Mimi aliniacha katika gari na kuniomba nimsubiri akaingia katika gari Fulani la rangi ya bluu na likaondoka.Sijui alielekea wapi na ikanilazimu kuendelea kumsubiri hadi pale uliponipigia simu na kuniomba nisishuke garini.Kuna nini baba? Akauliza Anna

“ Anna dada yako Flaviana amepatwa na matatizo huko alikokwenda”

“ Matatizo?! Anna akastuka sana

“ Ndiyo amepatwa na matatizo “
“ Matatizo gani baba? Is she ok? Akauliza Anna huku sura yake ikishindwa kuuficha mstuko alioupata
“ Dada yako ameshambuliwa na watu wasiojulikana na hali yake si nzuri ,hivi sasa madaktari wanashughulika kuokoa maisha yake kwa hiyo tunatakiw……………….” kabla Dr Joshua hajamaliza Anna akaanguka na kupoteza fahamu.Haraka haraka walinzi wakamuinua na kumpeleka sehemu husika kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza
“Nilitegemea jambo kama hili lingeweza kutokea na ndiyo maana sikutaka kumweleza chochote Anna akiwa garini kwani ningehatarisha maisha yake” akawaza Dr Joshua na baada ya sekunde kadhaa akamgeukia Dr Kigomba

“ Kigomba I need to know what happened ? Akasema Dr Joshua
Bado dr Kigomba alikuwa akitetetemeka alishindwa kusema kitu kilichotokea.
“Kigomba,mwanangu Flaviana yuko ndani ya chumba cha upasuaji hivi sasa akipigania uhai wake,naomba tafadhali unieleze nini kimesababisha akapigwa risasi ? Wewe ndiye niliyekukabidhi jukumu zima la kusimamia shughuli ile and you’ve failed me again” akasema Dr Joshua kwa ukali.Dr KIgomba akarekebisha koo lake na kusema
“ Tulimfuatilia Flaviana bila ya yeye kutambua hadi tulipofika Simbona hoteli.Pale alishuka katika gari lakena kuingia katika gari lingine dogo la bluu na kisha gari lile likaondoka pale hotelini.Tuliamini ndani ya gari lilendimo alimo Elibariki hivyo tukaendelea kumfuatilia.Tulilifuata gari lile hadi katika viwanja vya ukombozi.Tuliingiwa na shaka kidogo kuhusu dhumuni lake la kwenda pale.Tulijificha kwa takribani dakika kumi hivi tukisubirikuona kama kuna mtu atashuka lakini hakuna aliyeshuka,tukahisi i labda huenda kukawa na jambo linaendelea pale ndani ya gari.Kwa kuwa muda ulizidi kwenda ilinibidiki kuwatuma vijana wawili waende wakachungulie kilichokuwa kinaendelea mle ndani ya gari .Ghafla tukasikia mlio wa risasi mara tu vijana wale walipolikaribia gari na kijana wetu mmoja kati ya wale wawili akaanguka chini.Tulistushwa sana na kitendo kile ambacho hatukuwa tumekitegemea .Kijana wetu mwingine aliyebaki akapatwa na mstuko na kuanza kupiga risasi hovyo ili kujiokoa.Ghafla naye akapigwa risasi akaanguka chini .Ilitulazimu na sisi kuanza kufyatua risasi mfululizo ili kuwachanganya watu waliokuwapo pale uwanjani ambao hatukujua idadi yao.Nadhani milio ile ya risasi ilimstua Flaviana hivyo akafungua mlango wa gari na kushuka akaanza kukimbia na mara mtu mmoja ambaye tunaamini ni mmoja wa watu wa Elibariki alitoka mafichoni na kuanza kumkimbilia akimuita jina lake .Tulidhani mtu yule ni Elibariki na ndipo vijana wetu walipoanza kumrushia risasi .Mtu yule hakuwa Elibariki kwani alionekana ni mtu mahiri sana katika mapambano na namnaya kujikinga na shambulizi.Risasi zilimpata Flaviana akaanguka chini.Toka ndani ya lilegari akatoka tena mtu mwingineambaye tuliamini ni Elibariki na tukammiminia risasi akaanguka na kufariki pale pale .Risasi zikakoma na tulipokwenda kumuangalia mtu Yule hakuwa Elibariki. Kwa hiyo hatukufanikiwa kumpata Elibariki. Baada ya hapo tukapiga simu polisi na kumchukua Flaviana tukamkimbiza hospitali.Hivyo ndivyo ilivyotokea Dr Joshua.Hakuna aliyetegemea kama kungekuwa na shambulio kama lile.Inaonekana watu wale walifahamu kwamba lazima tutamfuatilia Flaviana na ndiyo maana wakatuwekea ule mtego.Dr Joshua hali hii inazidi kuwa mbaya.Elibariki ni mtu ambaye inabidi tumsake kwa kila namna kabla hajasababisha madhara makubwa kwetu.”akasema Dr Kigomba Dr Joshua akabaki kimya alikosa neno la kusema
“He escaped again” akasema Dr Joshua kwa kwa masikitiko.
“yes he did escape again” akasema Dr Kigomba huku akitazama chini
“ Dr Kigomba we have to clear this mess.Najua polisi lazima watafanya uchunguzi wao kuhusiana na tukio hili na wanaweza wakaingia ndani zaidi na wakagundua kwamba tunahusika nalo kwa hiyo tunatakiwa kufuta nyayo haraka sana.Mzigo wote tutamtupia jaji Elibariki.Tutaliweka jambo hili namna hii. Kwamba Flaviana amekuwa na mahusiano na mwanaume mwingine nje ya ndoa yake na hivyo kupelekea jaji Elibariki na huyo mwanaume kukwaruzana na Elibariki kuhisi kwamba mwanaume huyo ambaye amekuwa na mahusiano na mke wake ndiye aliyepanga shambulio lile lililomtokea na kwa hiyo akaamua kulipiza kisasi kwa mke wake.Akampigia simu na kumuomba wakutane mahali fulani usiku ule.Tutasema kwamba alimpeleka katika viwanja vya ukombozi kwa lengo la kumuua na Flaviana alipohisi hatari alinitumia ujumbe na nikatuma walinzi pamoja na wewe haraka sana eneo la tukio na ndipo lilipotokea shambulio lile.Tukifanya hvyo tuamuangushia mzigo wote Elibariki na atatafutwa katika kila kona ya nchi kwa kitendo hiki na atapatikana tu.Unaonaje kuhusu mpango huu?” akasema Dr Joshua “Ni mpango mzuri sana Dr Joshua.Hii ni njia bora sana ya kumpata jaji Elibariki.” Akasema Dr Kigomba.
“ Naomba umtafute mkuu wa kanda maalum ya Dar es salaam,nahitaji kuongea naye kumpa maelekezo ” akasema Dr Joshua na bila kupoteza wakati Dr Kigomba akampigia simu kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam na kumfahamisha kwamba rais anahitaji kuonana naye

“ hallow mheshimwia rais” akasema kamanda wa polisi wa kanda maalum
“ kamanda,kuna tatizo limetokea na ninadhani tayari umekwisha taarifiwa” akasema Dr Joshua

“ Ndiyo mzee.Nimekwisha taarifiwa kuhusiana natukio hilo na niko njiani kuelekea huko sasa hivi.Nimeambiwa kwamba kulikuwa na mapambano ya risasi kati ya watu wa usalama wa taifa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi,na watu wapatao wanne wamekutwa wamekufa na mwanao Flaviana amejeruhiwa kwa risasi” akasema kamanda wa polisi
“ Ndiyo kamishna .Kwa hivi sasa niko hapa hospitali kuu ya taifa na hali ya mwanangu si nzuri.Madaktari wanaendelea na jitihada za kuokoa uhai wake”
“ Pola sana mheshimwia rais .Tutajitahidi kwa kila tuwezavyo ili tuweze kumpata mtu au kikundi cha watu waliofanya jambohili.”akasema kamanda wa polisi
“ Kamishna ,hakuna haja ya kusumbuka sana kwani tayari tumemfahamu mtu aliyefanya shambulio hilo”
“ Mmekwisha mfahamu? akauliza kamanda wa polisi
“ ndiyo kamishna,huwezi amini mtu aliyefanya hivi ni mume wake ,ni jaji Elibariki”

“ jaji Elibariki?! Kamishna akashangaa

“ Ndiyo kamishna.Ni yeye ndiye aliyefanya jambo hili”
“ Mheshimiwa rais ninapata ugumu kidogo kuhusu jambo hili.Imekuwaje jaji Elibariki afanye shambulio kama hili kwa mke wake?Kwa nini atake kumuua mke wake?

“ Ni hivi kamishna,ndoa ya Flaviana na mumewe kwa siku za hivi karibuni imekuwa katika mgogoro mkubwa.Wamekuwa wakituhumiana kila mmoja akimtuhumu mwenzake kwa kutoka nje ya ndoa.Elibariki alikuwa akikwaruzana sana na mtu ambaye anahisi kwamba ndiye anayeiharibu ndoa yake.Mtu huyo ambaye hatujamfahamu bado inasemakana kwamba ndiye aliyeratibu shambulio lile ambalo Elibariki alinusurika.Baada ya kunusurka jaji Elibariki alitaka kulipiza kisasi na kwa kuanzia alitaka kumuua mkewake na ndiyo maana usiku huu alimpigia simu na kumtaka waonane sehemu Fulani na kisha akamchukua na kumpeleka katika viwanja vya ukombozi . Flaviana alihisi hatari na akanitumia ujumbe ikanilazimu kutuma vijana wa usalama pamoja na katibu wangu Dr Kigomba.Walipofika likatokea shambulio la kustukiza toka katika kundi la Elibariki vijana niliowatuma walianza kupambana ili kumuokoa Flaviana lakini inaonekana Elibariki na kundi lake walikuwa wamejipanga kwa silaha kali na vijana wangu wakazidiwa nguvu na watatu kati yao wakapoteza maisha na Flaviana akajeruhiwa kwa risasi.Elibariki na kundi lake wamefanikwa kukimbia .Ninaomba kamishna kuanzia usiku huu Elibariki aanaze kusakwa katika kila kona ya jiji na hakikisha amepatikana.” Akasema Dr Joshua
“ Sawa mzee nimekuelewa.Ahsante kwa taarifa hizo ambazo zitatusaidia sana katika uchunguzi wetu.Tutaanza msako mkali wa kumtafuta Elibariki kuanzia usiku huu.Na kuna taarifa nimeipokea hivi sasa inasema kwamba mmoja wa watu waliouawa katika tukio hilo ni jambazi sugu ambalo limekuwa likitafutwa sana na polisi kwa wizi wa magari na wizi wa kutumia silaha.Nikiunganisha taarifa hii na maelezo yako tunapata picha kwamba yawezekana Elibariki alimkodisha jambazi huyu ili kumfanyia kazi yake ya kumuua Flaviana”
“ umeona nilichokuwa nakwambaia Kamishna? Elibariki ni mtu hatari sana na tunatakiwa tumpate haraka sana” akasema Dr Joshua

“ Mzee nakuhakikishia kwamba tutafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu na Elibariki atapatikana ndani ya muda mfupi”
“Nashukuru sana Kamishna.Naomba taarifa za mara kwa mara kuhusiana na uchunguzi huu”akasema Dr Joshua na kukata simu na kumgeukia Dr Kigomba
“ Kwa mujibu wa kamishna ni kwamba kuna mtu mmoja amekutwa aneo la tuko amekufa ni jambazi sugu ambaye amekuwa akitafutwa siku nyingi na jeshi la polisi.Hii inadhihirisha wazi kwamba Elibariki anashirikiana na mtandao wa majambazi hatari.Elibariki si mtu wa kuachiwa akatamba,lazima adhibitiwe haraka sana” akasema Dr Joshua

“ Nnakubaliana nawe kwa sababu mapigano yale yalikuwa makali sana na ilionekana kabisa kwamba watu wale walikuwa ni wajuzi sana wa kutumia silaha” akasema Dr Kigomba
“ Nimesahau kukuuliza,ile taarifa aliyokuwa nayo Flaviana mmefanikiwa kuondoka nayo ?akauliza Dr Joshua

“ Hapana Dr Joshua taarifa ile hatukufanikiwa kuichukua .Kutokana na mvurugano uliokuwepo sikukumbuka hata kuchukua taarifa ile.”

“ Ouh mungu wangu ! kama Elibariki akiipata taarifa ile tumekwisha” akasema Dr Joshua
“ Usiwe na hofu mzee,hata kama akiichukua hakuna sehemu ambayo atapita nayo.Kwa sasa Elbariki ni kama mkimbizi na akionekana sehemu yoyote ile atakamatwa kwa hiyo usipate shida kwa Elbariki kuipata ripoti ile”akasema Dr Kigomba



*******


Anitha na Mathew walimsadia jaji Elibariki kushuka garini na kumuingiza ndani.Hakuwa na nguvu za kutembea.Hakuwa amejeruhiwa sehemu yoyote ile lakini tukio lililotoka usiku ule lilimmaliza nguvu kabisa.

“ Ahsanteni sana ndugu zangu” akasema Jaji Elibariki baada ya kuketishwa sofani.
“Mathew ahsante sana bila wewe leo tungekufa.Umepambana sana kutuokoa. Uliponiambia kwamba unahisi Flaviana atakuwa akichuguzwa nilidhani ni kama unatania vile lakini baada ya kushuhudia kilichotokea sasa ninakuamini.Una akili ya ajabu sana” akasema jaji Elibarki kwa sauti dhaifu.Anitha aliyekuwa ameketi sofani naye alionekana amechoka sana na hakutaka kusema chochote.Mathew akavua ile fulana isiyopenya risasi akaitupa pembeni naye akaketi sofani akainamisha kichwa.Alikuwa katika mawazo mengi sana.Picha ya tukio zima ndiyo iliyokuwa imetawala kichwa chake.Alikuwa anakumbuka namna tukio lile lilivyotokea
Waliliacha gari katika zahanati iliyokuwa karibu na viwanja vya ukombozi wakatembea kwamiguu wakipita njia fupi na kuwahi kufika kabla ya gari alimo Flaviana kuwasili.Eneo la uwanja ule lilikuwa na mwangaza hafifu uliotokana na taa za nyumba jirani.Walijibanza katika sehemu inayotumika kama jukwaa na baada ya dakika nne mwanga wa gari ukaonekana.Lilikuwa ni gari alimo Flaviana

“ Mathew hakuna tena muda wa kupoteza,ngoja nikachukue ile ripoti”akasema jaji Elibariki huku akitaka kuinuka
“ Ngoja kwanza Elibariki ,hatuwezi kwenda hadi tuhakikishe kuko salama”akasema Mathew na kisha wakaendelea kujibanza wakisubiri
‘Mathew yawezekana wale jamaa tuliohisi walikuwa wanamfuatilia Flaviana watakuwa wamekata tamaa na wakaamua kurudi,mbona hawatokei tena? akauliza Elibariki

“ Elibariki naomba uwe na subira kidogo.” Akasema Mathew na baada ya kama dakika kumi hivi watu wawili wakaonekana wakiliendea gari lile.Jaji Elibariki akaogopa
“ watu wale ni akina nani ?akauliza jaji elibariki.Mahala walipokuwa wamejibanza hapakuwa mbali na gari alimo Flaviana kwa hiyo kwa kutumia mwangaza ule wa taa za jirani waliweza kuwaona vizuri watu wale

“ Subiri kwanza tutafahamu ni akina nani.Yawezekana wakawa ni miongoni mwa wale ambao wanamfuatilia Flaviana” akasema Mathew
watu wale walifika katika gari lile na kuchomoa bastora wakaanza kugonga dirisha upande wa dereva wakitaka wafunguliwe mlango

“Mathew do something,watu wale watamdhuru mke wangu” akasema Elibarii kwa uoga.

“ subiri kwanza Elibariki.hatuwezi kuwavamia haraka haraka namna hiyo” akasema Mathew
Ghafla ukasikika mlio wa risasi na mtu mmoja katika ile gari akaanguka chini.Bastora aliyokuwa ameishika jaji Elibariki ilikuwa inatoa moshi.Ni yeye ndiye aliyeachia risasi ile.Baada ya mlio ule wa risasi ikaanza kusikika milio ya risasi toka katika kila upande wa uwanja zikielekea kule iliko gari alimo Flaviana.Mlango wa nyuma wa gari ukafunguliwa na Flaviana akatoka
“ Anitha cover me ! “ akasema Mathew na kutoka kwa kasi kumfuata Flaviana aliyekuwa akikimbia huku milio ya risasi ikisikika.
“ Flaviana get down !!..akapiga kelele Mathew akimtaka Flaviana aache kukimbia na alale chini kwani mivumo ya risasi iliongezeka.Ghafla Flaviana akaanguka huku akitoka ukulele alikuwa amepigwa risasi.Mathew akajirusha na kutua karibu na mahala alipoangukia Flaviana.Hatua chache toka mahala alipoanguka Flaviana kulikuwa na bahasha Mathew akainyakua bahasha ile na kuanza kukimbia nayo.

“ twendni tuondoke,hapafai mahala hapa” akasema Mathew

“ Flaviana tunamuacha?akauliza jaji Elibariki
“ Amepigwa risasi” akasema Mathew
“Mathew hapana siwezi kuondoka na kumuacha Flaviana.Lazima tuondoke naye”
“ Elibariki hatuna muda wa kupoteza hapa watu tunaopambana nao wana silaha kali na hatujui wako wangapi.They’re going tokill us.Lets get out of here !! akasema Mathew na kisha wakaanza kukimbia kuondoka.
“Mathew !! akaita Elibariki na kumtoa Mathew katika kumbukumbu ile akageuka na kumtazama

“ Mathew una hakika mke wangu atakuwa salama? Akauliza Elibariki
“ I don’t know Elibariki..” akajibu Mathew

“ Yote haya ni makosa yangu.Kama ningekusikiliza yasingetoeka haya.Nilifanya makosa kuanza kuachia ile risasi ambayo ndiyo imesababisha mke wangu akapigwa risasi.Ouh Flaviana ..!! akasema jaji Elibariki.Alionekana kuchanganyikiwa
“ Sina hakika kama Flaviana atakuwa hai kwani nilikuwa karibu naye na nikasikia namna alivyokuwa akihangaika kuvuta hewa lakini siwezi kumwambia Elibariki kwani nitazidi kumchanganya.Alifanya kosa kubwa kuachia ile risasi,alitakiwa asubiri maelekezo yangu” akawaza Mathew na kisha akaikumbuka ile bahasha ambayo alikuwa nayo Flaviana akaenda garini kuichukua

“ Pamoja na yote yaliyotokea lakini tumefanikiwa kuipata hii taarifa tuliyokuwa tukiitafuta .taarifa ya madaktari bingwa kuhusianana kifo cha Dr Flora.” Akasema Mathew

“ Mathew nahitaji kufahamu Flaviana anaendeleaje.Please help me” Akasema jaji Elibariki

“ Elibariki hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwa sasa.Tunachotakiwa ni kufumba machona kuomba.Anything can happen “ akasema Mathew
“ Mimi na Flaviana tumepitia mambo mengi na ndoa yetu imekumbwa na migogoro mingi lakini sitaki apoteze maisha.Bado anayo nafasi katika maisha yangu.Please Lord save her” akasema jaji Elibariki na michirizi ya machozi ikaonekana machoni pake

“ Elibariki nadhani unahitaji mapumziko .Kesho asubuhi tutafahamu kinachoendelea” akasema Mathew .Jaji Elibariki hakusema kitu akajitahidi kusimama na kisha aketembea kuelekea katika chumba chake.

“ Anitha hata wewe pia unahitaji mapumziko ,siku imekuwa ndefu sana,mambo mengi yametokea usiku huu ,tupumzikena tujiandae kwa ajili ya siku ya kesho,ila kitu kimoja ambacho sikutaka kukwambia mbele ya Elibariki ni kwamba sina hakika kama mkewake atakuwa salama.Nilimsogelea karibu ilikuchukua ile bahasha nikasikia namna alivyokuwa akihangaika kuvuta hewa.Tusubiri hadi siku ya kesho tutapata taarifa nini kimetokea ,kama ni mzima ama amefariki “
“ maskini Elibariki.Namonea huruma sana.Amepatwa na majanga mengi mfululizo “akasema Anitha

“Kesho tutaanza kuifanya kazi taarifa ile ya madaktari kubaini ukweli wake.Vile vile nitawasiliana na rafiki zangu wa huko nje ili waweze kunisiadia kutambua kilichomo ndani ya zile karatasi zilizoibwa ikulu” akasema Mathew na kila mmoja akaenda chumbani kupumzika.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………
 
Back
Top Bottom