SEASON 2
SEHEMU YA 25
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kigomba naomba uniambie ukweli.Is she dead ? akauliza Dr Joshua
“ No ! but she’s in critical condition.Kuna vijana wetu kama watatu au zaidi wamefariki dunia.”akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akashika kichwa .Alichanganyikiwa.
“ Ok Kigomba I’m on my way there” akasema Dr Joshua na kuingia katika chumba alimo genereli Adam.
“ Adam tutaendelea na maongezi siku nyingine.Kuna tatizo kubwa limetokea.Binti yangu amepigwa risasi ”
“ Is she ok? Akauliza genereli Adam
“ I don’t know.Fanyia kazi hayo mambo tuliyoongea” akasema Dr Joshua
“ Sawa mzee ,nitayafanyia kazi na nitakujulisha kila kitu.Pole sana mheshimiwa rais” akasema Generali Adam.Dr Joshua akatoka kwa kasi mle chumbani na kuwataarifu walinzi wake kwamba wajiandae wanaelekea hospitali,akaingia chumbani kwake kujiandaa
“ Imekuwaje Flaviana akapigwa risasi? Akajiuliza Dr Joshua.Mwili bado ulikuwa unamtetemeka.
“ Ouh Mungu wangu naomba umponye mwanangu huyu.Ninampenda sana binti yangu na siko tayari afariki” akasema Dr Joshua kwa sauti ndogo halafu akatoka na kuingia kuingia garini safari ya kuelekea hospitali ikaanza.
ENDELEA………………
“ Majanga yanazidi kuniandama. Hata wiki mbili hazijapita toka amefariki flora leo hii tena Flaviana naye yuko katika hatari ya kunitoka.Lakini hizi zote ni changamoto za biashara ile ya ile package.Pamoja na yote yaliyotokea na yatakayoendelea kutokea lakini lazima niifaney biashara hii”akawaza Dr Joshua akiwa garini kuelekea hospitali
“ Lakini imetokeaje hadi Flaviana akapigwa risasi ? Kigomba ana kazi kubwa ya kunielezea kuhusiana na jambo hili lilivyotokea na kusababisha mwanangu apigwe risasi.Ouh halafu nimeondoka bila ya kumtaarifu Anna kuhusiana na kilichotokea” akawaza Dr Joshua na akachukua simu yake na kumpigia Anna
“ Hallow Anna uko wapi?” akauliza Dr Joshua baada ya Anna kupokea simu.Anna akasita kidogo kujibu hakutaka baba yake afahamu mahala alipo
“ Anna uko wapi? Akauliza tena Dr Joshua
“ Nimetoka kidogo baba ”
“Uko wapi? Umetoka umekwenda wapi? Akauliza Dr Joshua
“ Nimetoka na Flaviana?!
“ Umetoka na Flaviana?!! Dr Joshua akazidi kushangaa
“Ndiyo baba ,Flaviana aliniomba nimsindikize mahala Fulani kuna mtu anakwenda kuonana naye usiku huu.”
“ Anna tafadhali naomba unieleze ukweli uko wapi? Sikuulizi kwa lengo baya”
“ Baba ni kweli nimemsindikiza Flaviana .”
“ Anna mbona unazidi kunichanganya.Uko na Flaviana muda huu?
“ Hapana siko naye kuna sehemu amekwenda na mimi niko garini ninamsubiri”
“ Anna tafadhali naomba usiondoke hapo ulipo.Nielekeze mahala ulipo ilinitume walinzi wajewakuchukue mara moja”
“ kwani kuna jambo gani baba?Mbona unaniogopesha?
“ Tafadhali niambie Anna uko wapi?
Anna akafikiri kwa sekunde chache na kusema
“ Niko hapa Simbona hoteli ninamsubiri Flaviana” akasema Anna
“ Ok Anna naomba usitoke hapo ulipo na kama uko garini usishuke hadi utakapowaona walinzi nitakaowatuma” akasema Dr Joshua akakata simu na kuwapigia walinzi ili wamfuate Anna pale alipo.Aliogopa kumweleza ukweli Anna akiogopa kumstua
“ kigomba amenieleza tu kuhusiana na Flaviana lakini hajanipa taarifa za Elibariki kama walifanikiwa kumpata au hawakufanikiwa ? Kama hawakufanikiwa kumpata na safari hii basi tutakuwa na wakati mgumu sana.Lakini kwa nini inakuwa vigumu kumpata mtu kama huyu? Hapana imetosha sasa na siwezi kumvumilia.Nitaitumia nguvu yangu kama rais na Elibarii atapatikana ndani ya kipindi kifupi.Nitatumia mtandao mpana wa jeshi la polisi kumtafuta na nitampata.” Akawaza Dr Joshua huku msafara ake ukienda kwa kasi isyo ya kawaida na hatimaye wakawasili hospitali na kupokelewa na dakari mkuu wa hospitali kuu ya taifa akiwa sambamba na Dr Kigomba ambaye alikuwa ameloana damu
“ Daktari mwanangu anaendeleaje? Akauliza Dr Joshua
“ Hali yake haikuwa nzuri wakati tumempokea na kwa sasa ameingizwa katika chumba cha upasuaji na timu ya madaktari wanaendelea kumuhudumia ili kuokoa maisha yake ” akasema daktari mkuu wakati wakiwa njiani kuelekea katika jengo la upasuaji.Dr Joshua aliomba aruhusiwe kuingia katika chumba cha upasuaji ashuhudie kilichokuwa kinaendelea.Akavalishwa mavazi maalum ya kuingilia katika chumba kile na kuingia akiongozana na daktari mkuu.Kazi ya kuokoa uhai wa Flaviana ilikuwa inaendelea na madaktari walikuwa katika heka heka kubwa.
“ Ee Mungu nafahamu mimi si mkamilfu mbele zako na nimekukosea mambo mengi sana makubwa lakini naomba usiniadhibu kwa kunichukulia binti yangu ninayempenda sana.bado ninamuhitaji sana” Dr Joshua akaomba kimya kimya.Machozi yalimlenga kwa kumuona mwanae akiwa kitandani hajitambui akisaidiwa kupumua kwa mashine.Hakutaka kuendelea kukaa mle ndani akatoka .
“ Dr Marcelo naomba mjitahidi kwa kila namna muwezavyo kuokoa uhai wa mwanangu.Sitaki kumpoteza Flaviana “ akasema Dr Joshua
“ mzee tunafanaya kila linalowezekana ili kuokoa uhai wa mwanao.Wewe mwenyewe umeshuhudia namna madaktari wanavyojitahidi na nina hakika watafanikiwa.Tumuombe Mungu atusadie katika jambo hili” akasema Dr Marcelo.
“ nashukuru sana Dr Marcelo.Nina hakika Mungu atasikia kilo changu na kumnusuru mwanangu” akasema Dr Joshua
“ Mzee unaweza tu kwenda kupumzika na sisi tutaendelea kuifanya kazi hii usiku huu na kama kutakuwa na lolote tutakufahamisha” akashauri Dr Marcelo
“ No Marcelo.Nitakesha hapa kufuatilia hatima ya mwanangu.” Akasema Dr Joshua ikamlazimu Dr Marcelo ampeleke sehemu ya mapumziko wakati wakisubiri Flaviana atolewe katika chumba cha upasuaji.Dr Kigomba naye aliambatana naye
“Dr Kigomba naomba unieleze nini hasa kimetokea? Akauliza Dr Joshua wakiwa wamepumzika wakisubiri upasuaji wa Flavina umalizikie.Midomo ya Dr Kigomba ilikuwa mizito kufunguka
“Kigomba tell me what happened? Akauliza Dr Joshua huku akimtazama Dr Kigomba kwa macho makali
“ Dr Joshua nashindwa hata sehemu ya kuanzia kukueleza namna ilivyokuwa” akasema Dr Kigomba
“ Tell me everything !! akasema r Joshua.Kabla Kigomba hajasema chochote akatokea Anna akiwa ameongozana na walinzi.Alikuwa na wasiwasi mwingi sana
“ Baba kuna nini?akauliza anna.Dr Joshua akamshika mkono na kumketisha kitini.
“ Anna dada yako alikupeleka wapi usiku huu ? Akauliza Dr Joshua
“ Aliniomba nimsindikize sehemu Fulani kuna mtu alikuwa anakwenda kuonana naye?
“ hakukwambia ni nani aliyekuwa anakwenda kuonana naye?
“ Hapana hakuniambia kwani kuna nini?akauliza Anna
“ Ulimuona mtu huyo aliyekwena kuonana naye? Akauliza Dr Joshua
“ Hapana sikufanikiwa kuonana naye kwani aliniacha mimi katika gari na yeye akaenda kuonana na mtu huyo” akajibu Anna
“ Alionana naye wapi?
Anna akasita kidogo halafu akasema
“ Mimi aliniacha katika gari na kuniomba nimsubiri akaingia katika gari Fulani la rangi ya bluu na likaondoka.Sijui alielekea wapi na ikanilazimu kuendelea kumsubiri hadi pale uliponipigia simu na kuniomba nisishuke garini.Kuna nini baba? Akauliza Anna
“ Anna dada yako Flaviana amepatwa na matatizo huko alikokwenda”
“ Matatizo?! Anna akastuka sana
“ Ndiyo amepatwa na matatizo “
“ Matatizo gani baba? Is she ok? Akauliza Anna huku sura yake ikishindwa kuuficha mstuko alioupata
“ Dada yako ameshambuliwa na watu wasiojulikana na hali yake si nzuri ,hivi sasa madaktari wanashughulika kuokoa maisha yake kwa hiyo tunatakiw……………….” kabla Dr Joshua hajamaliza Anna akaanguka na kupoteza fahamu.Haraka haraka walinzi wakamuinua na kumpeleka sehemu husika kwa ajili ya kupatiwa huduma ya kwanza
“Nilitegemea jambo kama hili lingeweza kutokea na ndiyo maana sikutaka kumweleza chochote Anna akiwa garini kwani ningehatarisha maisha yake” akawaza Dr Joshua na baada ya sekunde kadhaa akamgeukia Dr Kigomba
“ Kigomba I need to know what happened ? Akasema Dr Joshua
Bado dr Kigomba alikuwa akitetetemeka alishindwa kusema kitu kilichotokea.
“Kigomba,mwanangu Flaviana yuko ndani ya chumba cha upasuaji hivi sasa akipigania uhai wake,naomba tafadhali unieleze nini kimesababisha akapigwa risasi ? Wewe ndiye niliyekukabidhi jukumu zima la kusimamia shughuli ile and you’ve failed me again” akasema Dr Joshua kwa ukali.Dr KIgomba akarekebisha koo lake na kusema
“ Tulimfuatilia Flaviana bila ya yeye kutambua hadi tulipofika Simbona hoteli.Pale alishuka katika gari lakena kuingia katika gari lingine dogo la bluu na kisha gari lile likaondoka pale hotelini.Tuliamini ndani ya gari lilendimo alimo Elibariki hivyo tukaendelea kumfuatilia.Tulilifuata gari lile hadi katika viwanja vya ukombozi.Tuliingiwa na shaka kidogo kuhusu dhumuni lake la kwenda pale.Tulijificha kwa takribani dakika kumi hivi tukisubirikuona kama kuna mtu atashuka lakini hakuna aliyeshuka,tukahisi i labda huenda kukawa na jambo linaendelea pale ndani ya gari.Kwa kuwa muda ulizidi kwenda ilinibidiki kuwatuma vijana wawili waende wakachungulie kilichokuwa kinaendelea mle ndani ya gari .Ghafla tukasikia mlio wa risasi mara tu vijana wale walipolikaribia gari na kijana wetu mmoja kati ya wale wawili akaanguka chini.Tulistushwa sana na kitendo kile ambacho hatukuwa tumekitegemea .Kijana wetu mwingine aliyebaki akapatwa na mstuko na kuanza kupiga risasi hovyo ili kujiokoa.Ghafla naye akapigwa risasi akaanguka chini .Ilitulazimu na sisi kuanza kufyatua risasi mfululizo ili kuwachanganya watu waliokuwapo pale uwanjani ambao hatukujua idadi yao.Nadhani milio ile ya risasi ilimstua Flaviana hivyo akafungua mlango wa gari na kushuka akaanza kukimbia na mara mtu mmoja ambaye tunaamini ni mmoja wa watu wa Elibariki alitoka mafichoni na kuanza kumkimbilia akimuita jina lake .Tulidhani mtu yule ni Elibariki na ndipo vijana wetu walipoanza kumrushia risasi .Mtu yule hakuwa Elibariki kwani alionekana ni mtu mahiri sana katika mapambano na namnaya kujikinga na shambulizi.Risasi zilimpata Flaviana akaanguka chini.Toka ndani ya lilegari akatoka tena mtu mwingineambaye tuliamini ni Elibariki na tukammiminia risasi akaanguka na kufariki pale pale .Risasi zikakoma na tulipokwenda kumuangalia mtu Yule hakuwa Elibariki. Kwa hiyo hatukufanikiwa kumpata Elibariki. Baada ya hapo tukapiga simu polisi na kumchukua Flaviana tukamkimbiza hospitali.Hivyo ndivyo ilivyotokea Dr Joshua.Hakuna aliyetegemea kama kungekuwa na shambulio kama lile.Inaonekana watu wale walifahamu kwamba lazima tutamfuatilia Flaviana na ndiyo maana wakatuwekea ule mtego.Dr Joshua hali hii inazidi kuwa mbaya.Elibariki ni mtu ambaye inabidi tumsake kwa kila namna kabla hajasababisha madhara makubwa kwetu.”akasema Dr Kigomba Dr Joshua akabaki kimya alikosa neno la kusema
“He escaped again” akasema Dr Joshua kwa kwa masikitiko.
“yes he did escape again” akasema Dr Kigomba huku akitazama chini
“ Dr Kigomba we have to clear this mess.Najua polisi lazima watafanya uchunguzi wao kuhusiana na tukio hili na wanaweza wakaingia ndani zaidi na wakagundua kwamba tunahusika nalo kwa hiyo tunatakiwa kufuta nyayo haraka sana.Mzigo wote tutamtupia jaji Elibariki.Tutaliweka jambo hili namna hii. Kwamba Flaviana amekuwa na mahusiano na mwanaume mwingine nje ya ndoa yake na hivyo kupelekea jaji Elibariki na huyo mwanaume kukwaruzana na Elibariki kuhisi kwamba mwanaume huyo ambaye amekuwa na mahusiano na mke wake ndiye aliyepanga shambulio lile lililomtokea na kwa hiyo akaamua kulipiza kisasi kwa mke wake.Akampigia simu na kumuomba wakutane mahali fulani usiku ule.Tutasema kwamba alimpeleka katika viwanja vya ukombozi kwa lengo la kumuua na Flaviana alipohisi hatari alinitumia ujumbe na nikatuma walinzi pamoja na wewe haraka sana eneo la tukio na ndipo lilipotokea shambulio lile.Tukifanya hvyo tuamuangushia mzigo wote Elibariki na atatafutwa katika kila kona ya nchi kwa kitendo hiki na atapatikana tu.Unaonaje kuhusu mpango huu?” akasema Dr Joshua “Ni mpango mzuri sana Dr Joshua.Hii ni njia bora sana ya kumpata jaji Elibariki.” Akasema Dr Kigomba.
“ Naomba umtafute mkuu wa kanda maalum ya Dar es salaam,nahitaji kuongea naye kumpa maelekezo ” akasema Dr Joshua na bila kupoteza wakati Dr Kigomba akampigia simu kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam na kumfahamisha kwamba rais anahitaji kuonana naye
“ hallow mheshimwia rais” akasema kamanda wa polisi wa kanda maalum
“ kamanda,kuna tatizo limetokea na ninadhani tayari umekwisha taarifiwa” akasema Dr Joshua
“ Ndiyo mzee.Nimekwisha taarifiwa kuhusiana natukio hilo na niko njiani kuelekea huko sasa hivi.Nimeambiwa kwamba kulikuwa na mapambano ya risasi kati ya watu wa usalama wa taifa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi,na watu wapatao wanne wamekutwa wamekufa na mwanao Flaviana amejeruhiwa kwa risasi” akasema kamanda wa polisi
“ Ndiyo kamishna .Kwa hivi sasa niko hapa hospitali kuu ya taifa na hali ya mwanangu si nzuri.Madaktari wanaendelea na jitihada za kuokoa uhai wake”
“ Pola sana mheshimwia rais .Tutajitahidi kwa kila tuwezavyo ili tuweze kumpata mtu au kikundi cha watu waliofanya jambohili.”akasema kamanda wa polisi
“ Kamishna ,hakuna haja ya kusumbuka sana kwani tayari tumemfahamu mtu aliyefanya shambulio hilo”
“ Mmekwisha mfahamu? akauliza kamanda wa polisi
“ ndiyo kamishna,huwezi amini mtu aliyefanya hivi ni mume wake ,ni jaji Elibariki”
“ jaji Elibariki?! Kamishna akashangaa
“ Ndiyo kamishna.Ni yeye ndiye aliyefanya jambo hili”
“ Mheshimiwa rais ninapata ugumu kidogo kuhusu jambo hili.Imekuwaje jaji Elibariki afanye shambulio kama hili kwa mke wake?Kwa nini atake kumuua mke wake?
“ Ni hivi kamishna,ndoa ya Flaviana na mumewe kwa siku za hivi karibuni imekuwa katika mgogoro mkubwa.Wamekuwa wakituhumiana kila mmoja akimtuhumu mwenzake kwa kutoka nje ya ndoa.Elibariki alikuwa akikwaruzana sana na mtu ambaye anahisi kwamba ndiye anayeiharibu ndoa yake.Mtu huyo ambaye hatujamfahamu bado inasemakana kwamba ndiye aliyeratibu shambulio lile ambalo Elibariki alinusurika.Baada ya kunusurka jaji Elibariki alitaka kulipiza kisasi na kwa kuanzia alitaka kumuua mkewake na ndiyo maana usiku huu alimpigia simu na kumtaka waonane sehemu Fulani na kisha akamchukua na kumpeleka katika viwanja vya ukombozi . Flaviana alihisi hatari na akanitumia ujumbe ikanilazimu kutuma vijana wa usalama pamoja na katibu wangu Dr Kigomba.Walipofika likatokea shambulio la kustukiza toka katika kundi la Elibariki vijana niliowatuma walianza kupambana ili kumuokoa Flaviana lakini inaonekana Elibariki na kundi lake walikuwa wamejipanga kwa silaha kali na vijana wangu wakazidiwa nguvu na watatu kati yao wakapoteza maisha na Flaviana akajeruhiwa kwa risasi.Elibariki na kundi lake wamefanikwa kukimbia .Ninaomba kamishna kuanzia usiku huu Elibariki aanaze kusakwa katika kila kona ya jiji na hakikisha amepatikana.” Akasema Dr Joshua
“ Sawa mzee nimekuelewa.Ahsante kwa taarifa hizo ambazo zitatusaidia sana katika uchunguzi wetu.Tutaanza msako mkali wa kumtafuta Elibariki kuanzia usiku huu.Na kuna taarifa nimeipokea hivi sasa inasema kwamba mmoja wa watu waliouawa katika tukio hilo ni jambazi sugu ambalo limekuwa likitafutwa sana na polisi kwa wizi wa magari na wizi wa kutumia silaha.Nikiunganisha taarifa hii na maelezo yako tunapata picha kwamba yawezekana Elibariki alimkodisha jambazi huyu ili kumfanyia kazi yake ya kumuua Flaviana”
“ umeona nilichokuwa nakwambaia Kamishna? Elibariki ni mtu hatari sana na tunatakiwa tumpate haraka sana” akasema Dr Joshua
“ Mzee nakuhakikishia kwamba tutafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu na Elibariki atapatikana ndani ya muda mfupi”
“Nashukuru sana Kamishna.Naomba taarifa za mara kwa mara kuhusiana na uchunguzi huu”akasema Dr Joshua na kukata simu na kumgeukia Dr Kigomba
“ Kwa mujibu wa kamishna ni kwamba kuna mtu mmoja amekutwa aneo la tuko amekufa ni jambazi sugu ambaye amekuwa akitafutwa siku nyingi na jeshi la polisi.Hii inadhihirisha wazi kwamba Elibariki anashirikiana na mtandao wa majambazi hatari.Elibariki si mtu wa kuachiwa akatamba,lazima adhibitiwe haraka sana” akasema Dr Joshua
“ Nnakubaliana nawe kwa sababu mapigano yale yalikuwa makali sana na ilionekana kabisa kwamba watu wale walikuwa ni wajuzi sana wa kutumia silaha” akasema Dr Kigomba
“ Nimesahau kukuuliza,ile taarifa aliyokuwa nayo Flaviana mmefanikiwa kuondoka nayo ?akauliza Dr Joshua
“ Hapana Dr Joshua taarifa ile hatukufanikiwa kuichukua .Kutokana na mvurugano uliokuwepo sikukumbuka hata kuchukua taarifa ile.”
“ Ouh mungu wangu ! kama Elibariki akiipata taarifa ile tumekwisha” akasema Dr Joshua
“ Usiwe na hofu mzee,hata kama akiichukua hakuna sehemu ambayo atapita nayo.Kwa sasa Elbariki ni kama mkimbizi na akionekana sehemu yoyote ile atakamatwa kwa hiyo usipate shida kwa Elbariki kuipata ripoti ile”akasema Dr Kigomba
*******
Anitha na Mathew walimsadia jaji Elibariki kushuka garini na kumuingiza ndani.Hakuwa na nguvu za kutembea.Hakuwa amejeruhiwa sehemu yoyote ile lakini tukio lililotoka usiku ule lilimmaliza nguvu kabisa.
“ Ahsanteni sana ndugu zangu” akasema Jaji Elibariki baada ya kuketishwa sofani.
“Mathew ahsante sana bila wewe leo tungekufa.Umepambana sana kutuokoa. Uliponiambia kwamba unahisi Flaviana atakuwa akichuguzwa nilidhani ni kama unatania vile lakini baada ya kushuhudia kilichotokea sasa ninakuamini.Una akili ya ajabu sana” akasema jaji Elibarki kwa sauti dhaifu.Anitha aliyekuwa ameketi sofani naye alionekana amechoka sana na hakutaka kusema chochote.Mathew akavua ile fulana isiyopenya risasi akaitupa pembeni naye akaketi sofani akainamisha kichwa.Alikuwa katika mawazo mengi sana.Picha ya tukio zima ndiyo iliyokuwa imetawala kichwa chake.Alikuwa anakumbuka namna tukio lile lilivyotokea
Waliliacha gari katika zahanati iliyokuwa karibu na viwanja vya ukombozi wakatembea kwamiguu wakipita njia fupi na kuwahi kufika kabla ya gari alimo Flaviana kuwasili.Eneo la uwanja ule lilikuwa na mwangaza hafifu uliotokana na taa za nyumba jirani.Walijibanza katika sehemu inayotumika kama jukwaa na baada ya dakika nne mwanga wa gari ukaonekana.Lilikuwa ni gari alimo Flaviana
“ Mathew hakuna tena muda wa kupoteza,ngoja nikachukue ile ripoti”akasema jaji Elibariki huku akitaka kuinuka
“ Ngoja kwanza Elibariki ,hatuwezi kwenda hadi tuhakikishe kuko salama”akasema Mathew na kisha wakaendelea kujibanza wakisubiri
‘Mathew yawezekana wale jamaa tuliohisi walikuwa wanamfuatilia Flaviana watakuwa wamekata tamaa na wakaamua kurudi,mbona hawatokei tena? akauliza Elibariki
“ Elibariki naomba uwe na subira kidogo.” Akasema Mathew na baada ya kama dakika kumi hivi watu wawili wakaonekana wakiliendea gari lile.Jaji Elibariki akaogopa
“ watu wale ni akina nani ?akauliza jaji elibariki.Mahala walipokuwa wamejibanza hapakuwa mbali na gari alimo Flaviana kwa hiyo kwa kutumia mwangaza ule wa taa za jirani waliweza kuwaona vizuri watu wale
“ Subiri kwanza tutafahamu ni akina nani.Yawezekana wakawa ni miongoni mwa wale ambao wanamfuatilia Flaviana” akasema Mathew
watu wale walifika katika gari lile na kuchomoa bastora wakaanza kugonga dirisha upande wa dereva wakitaka wafunguliwe mlango
“Mathew do something,watu wale watamdhuru mke wangu” akasema Elibarii kwa uoga.
“ subiri kwanza Elibariki.hatuwezi kuwavamia haraka haraka namna hiyo” akasema Mathew
Ghafla ukasikika mlio wa risasi na mtu mmoja katika ile gari akaanguka chini.Bastora aliyokuwa ameishika jaji Elibariki ilikuwa inatoa moshi.Ni yeye ndiye aliyeachia risasi ile.Baada ya mlio ule wa risasi ikaanza kusikika milio ya risasi toka katika kila upande wa uwanja zikielekea kule iliko gari alimo Flaviana.Mlango wa nyuma wa gari ukafunguliwa na Flaviana akatoka
“ Anitha cover me ! “ akasema Mathew na kutoka kwa kasi kumfuata Flaviana aliyekuwa akikimbia huku milio ya risasi ikisikika.
“ Flaviana get down !!..akapiga kelele Mathew akimtaka Flaviana aache kukimbia na alale chini kwani mivumo ya risasi iliongezeka.Ghafla Flaviana akaanguka huku akitoka ukulele alikuwa amepigwa risasi.Mathew akajirusha na kutua karibu na mahala alipoangukia Flaviana.Hatua chache toka mahala alipoanguka Flaviana kulikuwa na bahasha Mathew akainyakua bahasha ile na kuanza kukimbia nayo.
“ twendni tuondoke,hapafai mahala hapa” akasema Mathew
“ Flaviana tunamuacha?akauliza jaji Elibariki
“ Amepigwa risasi” akasema Mathew
“Mathew hapana siwezi kuondoka na kumuacha Flaviana.Lazima tuondoke naye”
“ Elibariki hatuna muda wa kupoteza hapa watu tunaopambana nao wana silaha kali na hatujui wako wangapi.They’re going tokill us.Lets get out of here !! akasema Mathew na kisha wakaanza kukimbia kuondoka.
“Mathew !! akaita Elibariki na kumtoa Mathew katika kumbukumbu ile akageuka na kumtazama
“ Mathew una hakika mke wangu atakuwa salama? Akauliza Elibariki
“ I don’t know Elibariki..” akajibu Mathew
“ Yote haya ni makosa yangu.Kama ningekusikiliza yasingetoeka haya.Nilifanya makosa kuanza kuachia ile risasi ambayo ndiyo imesababisha mke wangu akapigwa risasi.Ouh Flaviana ..!! akasema jaji Elibariki.Alionekana kuchanganyikiwa
“ Sina hakika kama Flaviana atakuwa hai kwani nilikuwa karibu naye na nikasikia namna alivyokuwa akihangaika kuvuta hewa lakini siwezi kumwambia Elibariki kwani nitazidi kumchanganya.Alifanya kosa kubwa kuachia ile risasi,alitakiwa asubiri maelekezo yangu” akawaza Mathew na kisha akaikumbuka ile bahasha ambayo alikuwa nayo Flaviana akaenda garini kuichukua
“ Pamoja na yote yaliyotokea lakini tumefanikiwa kuipata hii taarifa tuliyokuwa tukiitafuta .taarifa ya madaktari bingwa kuhusianana kifo cha Dr Flora.” Akasema Mathew
“ Mathew nahitaji kufahamu Flaviana anaendeleaje.Please help me” Akasema jaji Elibariki
“ Elibariki hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwa sasa.Tunachotakiwa ni kufumba machona kuomba.Anything can happen “ akasema Mathew
“ Mimi na Flaviana tumepitia mambo mengi na ndoa yetu imekumbwa na migogoro mingi lakini sitaki apoteze maisha.Bado anayo nafasi katika maisha yangu.Please Lord save her” akasema jaji Elibariki na michirizi ya machozi ikaonekana machoni pake
“ Elibariki nadhani unahitaji mapumziko .Kesho asubuhi tutafahamu kinachoendelea” akasema Mathew .Jaji Elibariki hakusema kitu akajitahidi kusimama na kisha aketembea kuelekea katika chumba chake.
“ Anitha hata wewe pia unahitaji mapumziko ,siku imekuwa ndefu sana,mambo mengi yametokea usiku huu ,tupumzikena tujiandae kwa ajili ya siku ya kesho,ila kitu kimoja ambacho sikutaka kukwambia mbele ya Elibariki ni kwamba sina hakika kama mkewake atakuwa salama.Nilimsogelea karibu ilikuchukua ile bahasha nikasikia namna alivyokuwa akihangaika kuvuta hewa.Tusubiri hadi siku ya kesho tutapata taarifa nini kimetokea ,kama ni mzima ama amefariki “
“ maskini Elibariki.Namonea huruma sana.Amepatwa na majanga mengi mfululizo “akasema Anitha
“Kesho tutaanza kuifanya kazi taarifa ile ya madaktari kubaini ukweli wake.Vile vile nitawasiliana na rafiki zangu wa huko nje ili waweze kunisiadia kutambua kilichomo ndani ya zile karatasi zilizoibwa ikulu” akasema Mathew na kila mmoja akaenda chumbani kupumzika.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………