Lege inaonekana wewe ni mdau mkubwa wa Riwaya kama mimi. Kwa kweli siwezi orodhesha idadi ya riwaya nilizosoma. Nimeanza kuvutiwa kusoma kipindi nipo darasa la 3. By then nilikua naona mama akisoma sana riwaya za enzi hizo. Nami nikawa nasubiri amalize ili nisome. Kwa kweli nilikuwa na vutiwa sana. Nilikuwa msomaji mzuri kwa sababu kipindi cha magazeti ya sana nilikuwa nawasomea washkaji class. Watu wamekuzunguka hivyo unasoma kwa sauti wote wasikie. Nilikuwa nina library ya hizi riwaya kibao. Nikisafiri kwa basi pale Ubungo lazima ninunue ndani ya basi naburudika bila kuchoka. Zikaja zile za Shigongo, nilikua nakesha kwa utamu. Jamani riwaya ni tamu sana kama unazikubali. Bora nisiangalie movies lakini nisome riwaya yenye msisimko. Mathalani hii riwaya imenikumbusha enzi hizo riwaya za kipelelezi na ukichukulia hakukua na technologies kama simu na computer lakini kila kitu kilikuwa kitavutia.