Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

Maisha yana siri nzito sana, kiubinadam watu wng tunakutana na mambo ambayo yanabadilisha mtazamo na namna tunavochukulia vitu, ukiangalia toka mwanzo Hadi mwisho unaweza kugundua hili, nadhan kitu kikubwa ni kuangalia ni matari wa namna gani unatakiwa kuuchora ktk maisha yako. Ni vema kuchora mpaka maalumu ambao nafs yako haiwez kuuvuka. Asante sana [mention]LEGE [/mention] kwa huu uzi.
 
Hii ndio stori bora ya muda wote hapa Jf ikifuatiwa na vipepeo weusi.
 
PENIELA
SEASON 1
SEHEMU YA 36
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ripoti ya uchunguzi hii hapa.kwa ufupi tu ni kwamba Dr Flora alichomwa dawa iitwayo Encozynes yenye kiambata kijulikanacho kama Spinolin.Dawa hii hutumiwa na watu wenye matatizo ya shinikizo la damu lakini ni kwa kiwango kidogo sana.Mgonjwa akipewa dawa hii kupita kiwango chake basi husababisha kifo ndani ya muda mfupi kutegemea na kiwango alichopewa.Kwa hiyo tunatakiwa tuchunguze ni nani aliyemchoma dawa hiyo na kwa nini alimchoma.Tukimpata mtu aliyemchoma tutakitegua kitendawili hiki”akasema mathew
“ Kwa maana hiyo kuna kila dalili zinazoonyesha kwamba Dr Flora aliuawa kwa kuchomwa kwa makusudi sindano ile .Na hii ni sababu kumekuwa na jitihada kubwa za kutaka kuzuia uchunguzi wa kifo cha Dr Flora usifanyike kwa sababu waliogopa itabainika kwamba aliuawa.” Akasema Jaji Elibariki

ENDELEA……………………

“ Kwa namna jambo hili lilivyotokea na hali halisi ilivyo kuna kila sababu za kunifanya niamini kwamba Dr Flora alichomwa dawa ile kwa makusudi kabisa na aliyemchoma alikuwa na lengo la kumuua.Hebu jiulize ni kwa nini uchunguzi wa kifo cha Dr Flora ulizuiwa na kulikuwa na kila jitihada za kuhakikisha kwamba hakuna uchunguzi unaofanyika? Ni wazi walifahamu kwamba ukifanyika uchunguzi itagundulika kwamba Dr Flora aliuawa.”akasema Mathew
“ kwa hiyo nini kinafuata baada ya hapa? Nimeanza kuogopa Mathew ” akasema jaji Elibariki
“ Kwa upande wangu ,kazi yangu nimeikamilisha.Nilihitajika kupata ukweli wa kilichomuua Dr Flora na tayari nimekwisha upata.Kinachotakiwa hapa ni kuifikisha taarifa hii sehemu husika kwa mheshimiwa rais ili aweze kutumia vyombo vyake vya uchunguzi kulifanyia uchunguzi jambo hili.Nguvu yangu mimi inaishia hapa na kwa kuwa jambo hili limefanyika ndani ya ikulu sina nguvu ya kuweza kuingia mle na kufanya uchunguzi.Mheshimiwa rais ana uwezo mkubwa wa kulichunguza suala hili na kujua ni nani aliyefanya kitendo hiki na kuchukua hatua zipasazo” akasema Mathew
“ Mathew nakushukuru sana kwa msaada wako huu mkubwa.Bila wewe tusingeweza kuupata ukweli huu.Nitafanya utaratibu wa kumkabidhi mheshimiwa rais ripoti hii mapema asubuhi ya leo ili aweze kuchukua hatua zipasazo “ akasema jaji Elibariki
“ Jitahidi Elibariki ripoti hii ifike katika mikono husika ili iweze kufanyiwa kazi “
“ Ahsante sana Mathew” akasema jaji Elibariki .
“ Ok Elibariki ,I need to take some rest now.Utanifahamisha baadae utakapokuwa umemkabidhi taarifa hii mheshimiwa rais”akasema Mathew na kutoka mle chumbani akaelekea katika chumba alichokuwamo Anitha .
“ Anitha ninakwenda kupumzika kidogo,jitahidi nawe ukapumzike baada ya kumaliza kazi zako .Usiku ulikuwa mrefu sana.Mambo mengi yametokea usiku wa kuamkia leo.”
“ Pole sana Mathew.Umechoka sana .Hata mimi ninaenda kupumzika muda si mrefu .Nataka kwanza nishughulikie lile suala la ndege alilo omba Dr Michael” akasema Anitha
“ Ok Anitha.Nilisahau kusema ahsante sana.Bila wewe tusingeweza kufanikiwa zoezi lile la kumuokoa mke wa Dr Michael”akasema Mathew na kutabasamu kisha akaondoka na kwenda katika mlango wa chumba cha Dr Michael akagonga na mlango ukafunguliwa
“ Hallow Mathew” akasema Dr Michael
“ Dr Michael mkeo anaendeleaje?
“ Anaendelea vizuri sana Mathew”
“ Sawa Dr Michael ,mimi ninakwenda kupumzika kidogo .Ninachoweza kusema ni ahsante sana kwa msaada wako mkubwa.Bila wewe tusingeweza kufanikiwa kuufahamu ukweli wa kilichomuua Dr Flora.Kwa sasa mnaweza kuendelea kupumzika wewe na familia yako Anitha anaendelea kufanya utaratibu wa kupata ndege na atakapofanikiwa atawafahamisha.”
“ Ahsante sana pia Mathew.Familia yangu iko salama sasa kwa sababu yako .Bila wewe na timu yako tusingeweza kuwa pamoja tena.Sintokushau katika maisha yangu yote.Lakini kuna jambo moja dogo ninahitaji kukuomba.”
“ Omba chochote Dr Michael”
“ Tutahitaji kwenda nyumbani kwetu kuchukua vitu vyetu muhimu kama vile mavazi,nyaraka za kusafiria n.k kwa hiyo tutahitaji ulinzi”
“Usijali Dr Michael,tutawapeleka nyumbani kuchukua kila kitu mnachokihitaji” akasema Mathew na kuondoka akaelekaa chumbani kwake na kujilaza kitandani
.Picha ya matukio yote yaliyotokea usiku ule ikajirudia kichwani
“ Ulikuwa ni usiku mbaya sana.Damu imemwagika na tumempoteza kanali Adolf.Pamoja na hayo tumefanikiwa kupata kile tulichokuwa tukikihitaji.Tumempata mke wa Dr Michael na tumefanikiwa kufahamu kile kilichomuua Dr Flora.Ngoja niipumzishe akili yangu kidogo kabla ya jua kuchomoza “ akawaza Mathew na kufumba macho na hazikupita dakika tano kijiusingizi kikampitia

*******

Ulikuwa ni usiku mrefu sana kwa Jason.hakuweza kupata usingizi usiku ule kwa mawazo mengi yaliyokijaa kichwa chake.Kubwa lililoisumbua akili yake ni tukio lililotokea nyumbani kwa peniela.Picha ya Jaji Elibariki na peniela wakifanya mapenzi katika sofa sebuleni kwa Peniela ilimtesa sana.Picha nyingine iliyokuwa ikimfanya atetemeke na uogopa kila akiikumbuka ni ile ambayo Elibariki alikuwa amelala chini huku damu nyingi ikimtoka baada ya kumpiga na chupa.
“ Mwili wote unanitetemeka sana kila nikilikumbuka tukio lile.Sijui nimeua! ..akawaza Jason
“ Sijui nini kitatokea endapo nitakuwa nimeua.Sielewi nini kilinitokea hadi nikachukua uamuzi ule wa kumpiga Elibariki na chupa.Nadhani ni hasira zilivuka mipaka ndiyo maana nikaamua kuchukua uamuzi ule” akaendelea kukumbuka .Akaumia sana
“ Katika maisha yangu sijawahi kupigana na mtu yeyote yule jana ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kupigana tena na mtu ninayeheshimiana naye sana kama Elibariki.”
Picha ya Elibariki na Peniela ikamrudia tena
“ Sikujua kama Elibariki ni mtu mshenzi namna ile.Ni mtu niliyemuheshimu sana lakini kwa tukio la jana sintomuheshimu kamwe.Siku zote kumbe alikuwa akimtamani Peniela.Kumbe mipango yake yote ya kutaka kumtafuta muuaji wa Edson ni kwa ajili ya kujiweka karibu na Penny.Baada ya kuona juhudi zake za kumpata Peniela zinashindikana akaamua kutumia nguvu.Angejua namna ninavyompenda Peniela katu asingethubutu kufanya vile alivyofanya.” Akainuka na kwenda nje baada ya dakika tatu akarudi tena ndani
“ Natamani nimpigie simu Peniela nifahamu anaendeleaje na nini kilitokea baada ya ugomvi ule.” Akaichukua simu yake na kuzitafuta namba za Peniela akampigia.Simu ya Penny haikuwa ikipatikana.
“ Amezima simu.Inawezekana kukawa na tatizo kubwa lililotokea na ndiyo maana amezima simu yake.Nitamtafuta tena baadae. Sintoweza kukimbia ,kama nitakuwa nimeua basi nitasubiri hapa nije nikamatwe na hatua stahiki zichukuliwe Pamoja na yote bado ninampenda sana Peniela na siku zote ataendelea kuwa ni mwanamkeninayempenda kuliko wote katika hii dunia na kama jaji Elibariki hatakuwa amekufa nitafanya kila linalowezekana mpaka mimi na Penny tuishi pamoja kwani hata yeye mwenyewe amekwisha onyesha kila dalili kamba ananipenda . Ngoja nilale nisubiri kama watakuja askari asubuhi kunikamata kwa mauaji endapo Elibariki atakuwa alifariki baada ya kumpigana ile chupa kichwani.He deserved that” Jason akawaza na kulala kwani macho yalikuwa mazito sana kwa usingizi

******

Kumepambazuka Dar es salaam na kijua tayari kimechomoza.Jaji Elibariki alistuka toka usingizini akatazama saa yake ilipata saa moja na dakika nane.Simu yake ilikuwa imezima haikuwa na chaji.Alihitaji kuwasiliana na mke wake Flaviana akatoka mle chumbani na kuelekea sebuleni ,akamkuta Noah
“Noah,habari za asubuhi ? Unaendeleaje na jeraha? akauliza
“ Habari za asubuhi nzuri,ninaendelea vizuri .Vipi wewe unaendeleaje?
“ Hata mimi ninaendelea vizuri japokuwa nasikia maumivu kwa mbali.Watu wote bado wamelala?
“Ndiyo bado wamelala.Wamechoka sana kwa kazi ya jana usiku”
“ yah ! kazi ya jana haikuwa ndogo.Noah unaweza ukaniazima simu yako nahitaji kumpigia mke wangu simu yangu haina chaji hata kidogo ” akasema Elibariki.Noah akampatia simu yake akaziandika namba za Flaviana akampigia
“ Hallow “ akasema Flaviana
“ Hallow Flaviana ,samahani nimetumia simu nyingine kukupigia simu yangu imekwisha chaji” akasema Elibariki
“Eli,uko wapi? Are you ok? Akauliza Flaviana
“ I’m ok Flaviana.Unaendeleaje?
“ Ninaendelea vizuri sana.Vipi wewe unaendeleaje? Akauliza Flaviana
“ Ninaendelea vizuri pia.Kuna habari gani hapo msibani ?
“ Ratiba imeshatolewa na leo kutakuwa na zoezi la kumuaga mama ambalo litafanyika katika viwanja vya ukombozi ili kuwapa nafasi watu wengi waweze kumuaga.Kesho tutaelekea kijijini kwa mazishi.Vipi kuhusu lile suala umefikia wapi?”
“ Flaviana ninahitaji kuonana nanyi wewe na Anna asubuhi hii .Naomba tukutane pale kwenye mgahawa wa Maria Stella.Utanikuta ninakusubiri pale.Tafadhali kuweni makini sana”
“kwani kuna nini Eli mbona unaniogopesha?
“Ni kuhusiana na lile suala .Kuna mambo ambayo nahitaji kuwafahamisha.” Akasema Elibariki na kukata simu.
“Noah kuna jambo lingine ambalo naomba unisaidie. Nahitaji kufika sehemu fulani asubuhi hii lakini siko na gari langu.Nahitaji kuongea na Mathew ili kama kuna uwezekano aniazime gari lake moja linifikishe sehemu Fulani nikaonane na mke wangu.”
“ Mathew bado anapumzika mida hii lakini usihofu nitakupeleka mimi” akasema Noah
“ Noah utaweza kuendesha gari na maumivu uliyonayo?
“Usijali Elibariki,nitaweza kuendesha.Maumivu ni vitu tulivyovizoea ”akasema Noah na kuinuka wakaingia katika mojawapo ya gari la Mathew wakaondoka na kuelekea moja kwa moja katika mgahawa unaomilikiwa na dada mmoja aitwaye Maria stella.Noah akamuacha Elibariki pale akarejea.Baada ya dakika kama ishirini hivi toka awasili pale mgahawani Flaviana na Anna wakatokea .Walikuja na gari la kukodi.Flaviana akastuka baada ya kumuona mume wake akiwa na jeraha kichwani
“Eli umefanya nini hilo jeraha ? Akauliza
“ Ni katika purukushani za jana.Kulikuwa na kazi nzito”akasema jaji Elibariki.
“Pole sana mpenzi wangu.Najuta ni kwa nini nilisababisha ukaingia katika jambo la hatari kama lile.Usiku kucha wa leo sijaweza kupata usingizi hata kidogo nikifikiria kama utakuwa salama”akasema Flaviana
“ Usihofu mke wangu,ilikuwa ni kazi ya hatari sana lakini namshukuru Mungu imemalizika na niko salama”
“Pole sana shemeji”akasema Anna
“Nimekwisha poa Anna” akasema Jaji Elibariki halafu akafika muhudumu na kuwahudumia supu halafu Flaviana akauliza
“kwa hiyo umelala wapi leo?
“ Ilinilazimu kulala sehemu salama kutokana na hali ilivyokuwa.”akasema
“ Ile kazi haikuwa rahisi lakini nashukuru Mungu imekwisha salama na tayari tumegundua nini kimemuua Dr Flora”
“ Ouh thanks God”akasema Flaviana
“Mmegundua ni nini? akauliza Anna
“ Tulifanikiwa kuingia katika hospitali ile ya jeshi tukaanza kufanya uchunguzi lakini wakati tukiendelea,ukanipigia simu ikatulazimu kuondoka haraka sana lakini tuliondoka na sampuli kadhaa ambazo tulikwenda kuzifanyia uchunguzi katika maabara nyingine.Katika uchunguzi huo ilibainika kwamba Dr Flora alichomwa dawa iitwayo Encozynes ambayo hutumiwa na wagonjwa wa shinikizo la damu.Natumai hata Dr Flora alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu”akasema Mathew
“ Ndiyo alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu kwa muda mrefu”akasema Flaviana
“ Dawa hiyo ina kiambata kiitwacho Spinolin ambacho huweza kusababisha madhara kwa mgonjwa endapo itatumika kwa kiwango kikubwa na ndiyo maana dawa hii hutumika katika kiwango kidogo sana.”akanyamza kidogo halafu akaendelea
“ Vipimo vinaonyesha kwamba Dr Flora alichomwa kiasi kikubwa cha dawa hii hatari na hivyo kusababisha kifo chake ghafla”
Anna akainama akashindwa kuyazuia machozi kumtoka.Flaviana naye michirizi ya machozi ikaonekana mashavuni pake.
“Ladies please not now.Tafadhali msianze kuangua kilio humu mgahawani ”Jaji Elibariki akatoa angalizo
“ They killed my mother”akasema Anna
“ Anna please futa machozi.Huu si wakati wa kulia tena.Ni wakati wa kuutafuta ukweli wa jambo hili”akasema Elibariki.Baada ya Flaviana na mdogo wake kufuta machozi akaendelea
“ Kutokana na majibu haya kuna mambo ambayo lazima tujiulize.Kubwa ni kwa nini uchunguzi wa kifo cha Dr Flora uzuiliwe? Nyote ni mashahidi juhudi kubwa zimefanyika ili kuhakikisha kwamba mwili wa Dr Flora haufanyiwi uchunguzi ili kubaini ni kitu gani kimemuua.Waliokuwa wakifanya juhudi ili jambo hili lifanyike ni wazi walielewa kilichokuwa kinaendelea.Jambo lingine la kujiuliza ni je dawa hii ilichomwa kwa uzembe au mchomaji alidhamiria kufanya alichokifanya? Majibu ya maswali haya ni magumu kwetu sisi kuyafahamu kwa hiyo ripoti hii anatakiwa apewe mheshimiwa rais yeye atatumia vyombo vyake kufanya uchunguzi wa jambo hili na kulipatia jawabu.” Akasema Jaji Elibariki
“ Dr Kigomba lazima atakuwa anajua kuhusu jambo hili”akanong’ona Anna
“ Unasemaje ana? akauliza Elibariki
“Dr Kigomba lazima atakuwa akilifahamu suala hili.Yeye ni katibu wa baba na ndiye niliyemsikia akipiga simu akitoa amri madaktari wanaofanya uchunguzi kwa mwili wa mama wakamatwe haraka sana.Lazima ni yeye atakayekuwa amemuua mama” akasema Anna na macho yake yakaonyesha hasira za wazi.
“Nakubaliana nawe Anna kwamba huyo Dr Kigomba anaweza akawa anahusika katika suala hili lakini lazima jambo hili lichunguzwe kuanzia mzizi wake.Kama ni kweli Dr Flora alichomwa dawa ile kwa makusudi kwa lengo la kuutoa uhai wake basi lazima kutakuwa na watu wengi wanaohusika na suala hili.Dr Kigomba hawezi kuwa peke yake.Unatakiwa ufanyike uchunguzi wa kina ili kuwabaini wote waliohusika katika suala hili aidha kwa uzembe au kwa makusudi. ” Akasema jaji Elibariki.
“ Moyo wangu unakataa kabisa kuhusu ushauri wako Elibariki ,kwa nini suala hili tusilifanye wenyewe na kuubaini ukweli? Akasema Flaviana
“Flaviana ushauri wako ni mzuri na tungeweza kulifanya suala hili sisi wenyewe kama tungeweza lakini hili ni suala kubwa zaidi ya unavyolifikiria.Huu ni uchunguzi wa kifo cha mke wa rais,huyu si mtu mdogo.Kama aliuawa basi ni kwa sababu nzito na kuifahamu sababu hiyo kunahitaji vyombo vya usalama.Kwa hiyo basi naomba ukubali tumuachie mheshimiwa rais suala hili atumie vyombo vyake vya usalama vifanye uchunguzi na kuufahamu ukweli wa jambo hili” akashauri jaji Elibariki.Flaviana akakubaliana na mawazo ya mume wake na bila kupoteza muda wakaingia katika gari na kuelekea moja kwa mojakatika makazi ya rais.
Asubuhi hii katika makazi ya rais kulikuwa na pilika pilika nyingi.Ni siku ya kumuaga mke wa rais Dr Flora .Flaviana hakupoteza muda akaomba kuonana na baba yao kisha wakiambatana na jaji Elibariki wakaingia katika chumba cha maongezi.
“ Pole sana mheshimiwa jaji.Ilikuwa ni ajali? ” Dr Joshua akampa pole jaji Elibariki baada ya kumuona na jeraha kichwani
“ Ahsante sana mheshimiwa rais.Haikuwa ajali bali mkwaruzo mdogo tu,nilijigonga mahala” akasema Jaji Elibariki
“ Flaviana mbona tumeitana asubuhi asubuhi namna hii kuna nini? Akauliza Dr Joshua
“Baba kuna taarifa tunataka kukupatia.Ni kuhusiana na kilichosbabisha kifo cha mama”
“ Ouh Flaviana,nilikwisha kueleza toka jana kwamba nitalifanyia uchunguzi suala hili na hivi tunavyoongea tayari madaktari wako katika uchunguzi.Kabla ya mwili kupelekwa viwanja vya ukombozi kwa kuagwa tayari tutakuwa tumepata majibu nini kilisabisha kifo cha mama yenu.Msihofu wanangu tutafahamu tu muda si mrefu nini kilimuua mama yenu.” Akasema Dr Joshua
“ Baba tayari tunafahamu nini kilimuua mama “
“Mmefahamuje” akauliza Dr Joshua kwa mstuko kidogo
“ Unakumbuka jana nilikufahamisha kwamba nimemuomba mume wangu anisaidie kufanya uchunguzi wa siri?
“Ndiyo nakumbuka”
“ Basi Elibariki na jopo lake walifanikiwa kuufanya uchunguzi huo kwa siri licha ya amri ya kuusimamisha iliyotolewa na ripoti yake ni hii hapa” akasema Flaviana na kumkabidhi Dr Johua bahasha yenye ripoti.
“ Mheshimiwa jaji pole sana kwa misuko suko.Jana alinifuata mwenzako akiwa na mdogo wake na kunieleza mambo mazito ambayo sikuwa nikiyafahamu.Kwa kuwa ndiyo kwanza niliyasikia ninahitaji muda wa kuyachunguza zaidi na kuubaini ukweli.Ripoti yenu inasemaje? Mmegundua ni kitu gani kilimuua Dr Flora? Akauliza Dr Josha akimuelekezea macho jaji Elibariki
“ Mheshimiwa rais ,uchunguzi tulioufanya unaonyesha kuwapo kwa sumu aina ya Spinolin .Hiki ni kiambata kinachopatikana katika dawa aina ya Encozynes inayotumiwa na watu wenye shinikizo la damu.Dawa hii hutumiwa katika kiwango kidogo sana na endapo ikitumika katika kiwango kikubwa inaweza kusababisha kifo.Uchunguzi unaonyesha kuwapo kwa kiwango kikubwa cha spinolin dalili kwamba Dr Flora alichomwa kiwango kikubwa cha dawa hii na hivyo kusababisha kifo chake.Maelezo ya kitaalamu zaidi namna dawa hiyo inavyofanya kazi yapo ndani ya hiyo bahasha”akasema Jaji Elibariki.Uso wa Dr Joshua ukabadilika .Akamtazama jaji Elibariki kwa muda wa kama sekunde Arobaini hivi halafu akasema
“ Nashukuru sana mheshimiwa jaji.Good job.Taarifa hii imenistua sana na ninaombeni mnipe muda niwezekulifanyia kazi ili kuwabaini wote waliofanya kitendo hiki” akasema Dr Joshua.
“ Baba hiki kitu kilicho wazi kabisa.Watu waliofanya hivi wanajulikana kabisa.Dr Kigomba ndiye aliyetoa amri uchunguzi wa kifo cha mama usifanyike.Anatakiwa akamatwe na awataje wenzake”akasema Anna huku akilia.Dr Joshua akamfuata na kumbembeleza
“ Anna nyamaza usilie.Najua umeumizwa sana kwa jambo hili.Natamani sana ningefanya kama hivyo unavyoshauri nifanye lakini mambo hayaendi namna hiyo.Uchunguzi wa jambo hili ni mkubwa .Naombeni mniachie suala hili nilishughulikie .Nina watu wangu ambao wanaweza wakaifanya kazi hii kwa umakini mkubwa.Yeyote ambaye amehusika katika suala hili lazima apate adhabu stahili.”akasema Dr Joshua
“ Flaviana na Anna ,tafadhali naombeni mliache suala hili katika mikono ya mzee ili alishughulikie kama alivyoahidi. “ akasema Jaji Elibariki.Flaviana na mdogo wake wakakubali kuliacha suala lile katika mikono ya rais
“ Muda unakwenda kwa kasi,nendeni mkajiandae mtaongozana na msafara kuelekea hospitali kuufuata mwili .” akasema Dr Joshua na wanae wakatoka kwenda kujiandaa.Dr Joshua akabaki chumbani amesimama akiwaza.Halafu akachukua simu na kuzitafuta namba fulani akapiga
“ Hallo Mr president” ikasema sauti ya upande wa pili
“ Dr Kigomba,mambo yamebadilika.Wale jamaa walifanikiwa kufanya uchunguzi na wakagundua kila kitu”
“ What ?!! Dr Kigomba akashangaa
“ Hapa nilipo nimeishika bahasha yenye maelezo ya kuhusiana na kilichomuua Flora.Umefanyika uzembe mkubwa sana na tusipofanya juhudi za haraka kila kitu kitaharibika.”
“ Ok mzee usijali,we’re going to fix this.Hivi tunavyoongea Amos anatengeneza ripoti ya kifo cha Flora.Ikishapatikana ripoti hiyo,ikatae taarifa waliyokuletea,na uwaonyeshe ripoti ya kwetu ambayo itaonekana imetoka hospitali kuu ya taifa na uchunguzi umefanywa na madaktari bingwa.Baada ya hapo tutaangalia namna nyingine ya kufanya”akasema Dr Kigomba
“ Ok good plan.lakini kuna jambo lingine.”
“ Jambo gani mzee?
“ Tunatakiwa tumuondoe Amos katika picha.Yule ni hatari sana kwetu kwani yeye ndiye aliyemchoma Flora sindano ile.”
“ Una maana tumuue?
“ yah.Kuendelea kuwa hai ni jambo la hatari kubwa sana kwetu”
“ Ok nimekuelewa mzee” akasema Dr Kigomba.
‘One more thing”
“Nakusikiliza Mzee’
“ Keep an eye on my daughters.Wanatakiwa wachunguzwe nyendo zao,wanahusiana na nani ,wanaongea na nani na wanaongea nini.Hawa nao wanaweza kuwa ni hatari kubwa sana kwetu.Endapo itaonekana kwamba wanaweza wakasababisha hatari sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kuwaondoa katika picha pia.Mtu mwingine ni jaji Elibariki.Yeye ndiye aliyeshughulikia uchunguzi huu ukafanyika.Huyu ndiye nyoka mwenye sumu kali sana.Huyu naye inatakiwa itafutwe namna ya kumuondoa haraka sana.Tayari anafahamu kilichotokea na hatujui amekwisha mueleza nani .Kabla ya kuanza na Amos,anza kwanza na Jaji Elibariki.“
“ Ok nimekuelewa mzee,nitalifanyia kazi hilo suala “
“ Kigomba ,naomba utambue kwamba hii ni nafasi ya mwisho ninakupa.Please don’t mess up.”
“ I wont mr President” akasema Dr Kigomba na Dr Joshua akakata simu.Alikuwa akiangalia juu ya dari akiwa na mawazo mengi sana.
“ Suala hili linaanza kufuka moshi.Inatubidi kuwahi mapema kuuzima moto ule kabla haujaanza kuwaka na kusambaa .Ukiwaka moto huu hautazimika na utatuunguza wengi.I wont let that happen.kwa gharama zozote zile lazima nihakikishe ninalizima suala hili” akawaza Dr Kigomba na kutoka mle katika chumba maalum cha maongezi ya faragha cha mheshimiwa rais

******

Jiji la Dare s salaam limeamshwa na habari kubwa ya kifo cha kanali Adolf.Karibu magazeti yote yaliandika kuhusiana na habari ile lakini hakuna hata gazeti moja lilioandika habari ya kweli kuhusiana na nini kilisababisha kifo cha kanali Amos.
Akiwa bado kitandani ,Peniela alisikia kitu kama mlio wa simu na alipofumbua macho ni kweli ile simu anayotumia kuwasiliana na rais ilikuwa inaita.
“ Joshua anataka nini asubuhi yote hii?akajiuliza huku akiunyoosha mkono na kuichukua simu ile
“ Hallo Dr Joshua”
“ Hallow Penny.Bado umelala?
“ Bado asubuhi sana Dr Joshua”akasema Penny.Dr Joshua akacheka kidogo na kusema
“ Ok Peniela.Nimekupigia kukutaarifu kwamba leo inafanyika shughuli ya kumuaga mke wangu katika viwanja vya ukombozi na kesho tutamzika kijijini kwao.Nimemkabidhi Kareem jukumu zima la kukuhamisha siku ya leo.Nitawasiliana nawe tena baada ya kurejea kesho kutoka katika mazishi”
“Ahsante sana Dr Joshua.Nakutakia safari njema hapo kesho.Nina hamu sana ya kuongea nawe mambo mengi lakini tutaongea ukisharudi” akasema Peniela
“Usijali malaika wangu ,hata mimi nina mambo mengi sana ya kuongea nawe.Kwa heri kwa sasa”akasema Dr Joshua na kukata simu
Hazikupita hata dakika tano toka akate simu,kengele ya getini ikalia akaamka na kwenda kufungua akakutana na kareem
“ Kareem karibu sana “ akasema Penny na kumkaribisha Kareem ndani
“ Penny ,mheshimiwa rais amenikabidhi mimi kazi ya kuhakikisha leo unahamia katika lile kasri.Nimekuja mapema namna hii nataka tuelekee katika maduka ya fenicha na uchague kila kitu unachokihitaji kiwepo ndani ya ile nyumba .Hutakiwi kuchukua kitu chochote toka huku kwako hata nguo.Kila kitu utanunua kipya..”akasema Kareem.Penny hakujibu kitu akabaki akitabasamu akaelekea chumbani kwake akaoga na kujiandaa kwa ajili ya mizunguko ya siku ile.Alikusanya baadhi ya vitu vyake vidogo vidogo na bila kulisahau kasha alilopewa na John Mwaulaya.
“Hii yote ni katika kuhakikisha kasha hili linakuwa salama.”akawaza huku akilishika kasha lile akalipakia katika sanduku lle kubwa na kulikokota akatoka mle chumbani.Kareem akamsaidia kulibeba sanduku lile hadi katika gari ,Penny akafunga milango yote ya nyumba yake kisha akaingia garini na kuondoka”
“Safari ya kuelekea katika maisha mapya imeanza.” Akawaza akiwa garini.
RAIS WA JAMHURI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DR JOSHUA AMEIPOKEA RIPOTI YA UCHUNGUZI ULIOFANYWA KWA SIRI NA AKINA MATHEW NINI KITAWATOKEA WATOTO WAKE ANNA NA FLAVIANA PAMOJA NA JAJI ELIBARIKI? PENIELA TAYARI AMEHAMIA KATIKA NYUMBA ALIYOPEWA NA DR JOSHUA .MWISHO WA PENIELA SEASON ONE..

.
 
SEASON 2

SEHEMU YA 37

“ Ahsante sana kijana wangu lakini kuna jambonataka nikuweke wazi.Nimekueleza jambo hili lakini tafadhali sana naomba usimweleze Peniela kwani ndiyo yalikuwa makubaliano yangu na John na sikuwahi hata mara moja kuyavunja kwa kumueleza Peniela kwa hiyo naomba na wewe usithubutu kumweleza chochote.Iko siku John mwenyewe atamueleza “ akasema Bi Bernadetha

“ Nimekuelewa bibi na sintafanya hivyo.Nitakachofanya nitamueleza tu kwamba nimekuja kukutembelea na kukuta unaumwa na nitamsisitiza kwamba aje akutembelee.” akasema Mathew kisha akamuaga Bi Bernadetha na kuondoka

“ John Mwaulaya ni baba yake Peniela??..akajiuliza Mathew akiwa garini
“ Hapana hainiingii kabisa akilini eti John Mwaulaya awe ni baba yake Peniela halafuakatae mwanae kumfahamu.Hili ni jambolisilowezekana.Kama kweli ni baba yakena hakutaka peniela afhamu na badala yake akatambulishwa kwake kama mfadhili basi kuna kitu alikuwa anakificha na ambacho lazima nikifahamu.Amakweli dunia imekuwa ndogo sana.Hatimaye mimi na John mwaulaya tunakwenda kukutana tena uso kwa uso.This time I’ll be the one making him talk.” Akawaza Mathew



ENDELEA…………………

Abiria waliokuja na ndege ya shirika la ndege la Emirates walianza kutoka nje ya uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere.Peniela akiwa ameongozana na Jacob na Francis tayari walikuwapo hapo uwanjani wakiwasubiri wageni wao waliofika na ndege hii.Mikononi mwao kila mmoja alikuwa na picha mbili za wageni wanaowasubiri kwani hawakuwahi kukutana nao hata mara moja.Ni Peniela aliyekuwa wa kwanza kumtambua mmoja wa wageni wale waliokuwa wakiwasubiri.Nickson Strawberry alitambulika kwa urahisi kutokana na mtindo wake wa nywele .Alikuwa na nywele ndefu alizozikusanya kwa nyuma na kuzifunga.

“ That’s Nickson “ akasema Peniela na kumuita Nickson akasimama akageuka na kutmazama Peniela, akamfuata.

“ hallow Nickson.karibu sana Tanzania” akasema Peniela

“ Ahsante sana.” Akajibu Nickson

“ Naitwa Peniela na hawa ni wenzagu Jacob na Francis” Peniela akafanya utambulisho mfupi
“ Peniela !.akashangaa Nickson
“ wewe ndiye Peniela?! Akasema Nickson na kumkumbatia Peniela kwa furaha
“ Nimefurahi sana kuonana nawe Peniela” akasema Nickson kisha akawaita wenzake akawatambulisha.Alikuwepo Joe Levernsky mmarekani mweusi ,alikuwepo pia Bill beherds,Stanley Phoenix,Alexander Piscat na Edwin Washington.Kisha salimiana wakaelekea katika maegesho wakaingia katika magari mawili waliyokuja nayo akina Peniela na kuondoka
“ Nilitegemea kumuona Osmund hapa uwanjani.Yuko wapi?akauliza Nickson aliyekuwa amekaa kiti cha mbele pembeni ya Peniela

“ Osmund? Peniela akashangaa

“ Ndiyo” akajibu Nickson

“ Ina manaa hamna taarifa? Peniela naye akashangaa

“ taarifa gani penela?

“ Kuhusiana na Osmund”
“ Hatuna taarifa zozote kuhusiana na osmund.Tulipopanga safari hii yeye ndiye tuliyekuwa tukiwasiliana naye kwani ndiye aliyekuwa akiongoza team SC41 badala ya John lakini kwa siku kama tatu hivi hapatikani simuni hivyo ikatulazimu kwenda nje ya taratibu za team Sc41 na kuwataarifu vijana ofisi kuu dare s salaam kuhusu ujio wetu.Mara nyingi safari kama hizi hufanyika kwa siri.Yuko wapi Osmund? akauliza Nickson

“ Nini kinaendelea katika Team SC41? Kama tukio linaweza likatokea huku Tanzania na ninyi makao makuu msilifahamu basi ni hatari sana.Inaonekana wazi kwamba hakuna mawasiliano kati ya ofisi ya Dar es salaam na ofisi kuu Marekani.Ninaamini Team SC41 Tanzania ina watu wengi ambao wangeweza kuwapa taarifa.Kwa nini washindwe kutuma taarifa za matukio yanayotokea huku ? akauliza Peniela
“ Unayosema Penielani ya kweli kabisa.Toka John mwaulaya alipoanza kuumwa kumekuwa na tatizo katika ofisi ya Dar es salaam.Alimteua Osmund lakini bado hali ilikuwa ile ile.lakini usijali tumekuja kuweka mambo sawa na kila kitu kitakwenda vizuri sana.Kuna taarifa gani ya kuhusiana naOsmund? Akauliza Nckson.Peniela aliyekuwa akiendesha akapunguza mwendo na kusimama katika foleni kisha akasema
“ Osmund amefariki dunia”

“ Osmund amefariki dunia? Lini ?Akashangaa Nickson

“ Ndiyo tena si Osmund pekee bali na Dr Burke ambaye alitumwa kuja kufuatilia hali ya ugonjwa wa John .” akawema Peniela na kumstua sana Nickson ,aliyebaki anamtazama Peniela hadi pale gari zilipoanza kusogea

“ Peniela taarifa hizi ni ngeni kabisa kwetu.Hatukuwa tukifahamu chochote kilichotokea.Hapa ndipo unapokuja ukweli kwamba John mwaulaya alikuwa na nafasi kubwa sana katika team SC41.Kabla hajaumwa mambo kama haya hayakuwepo kabisa.Hakuna mtu yeyote aliyekamatwa hadi hivi sasa kuhusiana na mauaji hayo? Akauliza Nickson

“ Hapana.hakuna aliyekamtwa hadi hivi sasa “ akajibu Peniela.Nickson akainama akafikiri halafu akainua kichwa na kusema

“ Peniela kuna tatizo kubwa Team Sc41 Tanzania.Kuna kitu kinachoendelea hapa kwa sababu haiwezekani watu wawili wote team SC41 wauawe kwa wakati mmoja.Lazima tulifanyie uchunguzi suala hili ili tufahamu ukweli.Ninahisi kuna kitu hakiko sawa ndani ya team SC41 na hii ni hatari sana” akasema Nickson

“ Unahisi Dr Burke na Osmund waliuawa na mtu toka ndani ya team SC41? Akauliza Peniela

“ Sina hakika bado kama ni mtu toka ndani ya team SC41 lakini mazingira ya vifo hivyo yanatia shaka sana kwani inaonekana wazi waliuawa na mtu aliyekuwa na sababu Fulani.Lakini tutafahamu kila kitu baada ya kufanya uchunguzi wa kina.” Akasema Nickson
“ Ninajiuliza endapo tusingekuja,tusingetaarifiwa kuhusu kifo cha Osmund na Dr Burke? Huu ni udhaifu mkubwa sana umeonekana katika Team Sc41.Kuna kazi kubwa inatakiwa kufanyika kuisuka upya team SC41. Ahsante sana Peniela kwa taarifa hizi.kazi yetu itakuwa kubwa sana tofauti na nilivyokuwa nikitazamia.Team SC41 tanzania inatakiwa isukwe upya ili iwe imara kama ilivyokuwa mwanzo.Tukiachana na hayo vipi hali ya John mwaulaya? Akauliza Nickson

“ hali ya John si nzuri hata kidogo.kwa siku kadhaa hapo kati kati hali yake ilikuwa nzuri na wote tukawa na matumaini kwamba muda si mrefu atapona lakini ghafla hali yake ilibadilika na mpaka leo bado si nzuri.Anahitaji matibabu makubwa,kuna rafiki zake madaktari wanaweza wakaingia muda wowote kwa ajili ya kuja kumfanyia upasuaji” akasema Peniela
“ hakuna haja tena ya hao madaktari.Tumekuja na madaktari bingwa wawili kwa ajili tu ya kuja kuangalia ukubwa wa tatizo la John na kumpatia tiba.John anatakiwa kupatiwa tiba toka kwa madaktari wanaotambuliwa na Team SC41 .Usijali atapona tu” akasema Nickson na safari ikaendelea kimya kimya
“watuhawa wanataka kuisuka upya Team SC41 ili iwe na nguvu kama zamani Wakati nikiwa katika mikakati ya kuisambaratisha.Nimekwisha azimia kulifanya hilo na lazima nihakikishe linafanikiwa.Halafu kuna kitu nimekikumbuka kuhusiana na mauaji ya Dr Burke na Osmund.Nina hakika kabisa John alihusika katika vifo vya Dr Burke na osmund.Hawa jamaa wakifanya uchunguzi wao na kugundua kwamba John alishiriki sijui watafanya nini,nahisi wanaweza hata wakamuua.” Akawaza peniela huku safari ikiendelea.
Josh alimtaarifu kwamba kila kitu kuhusiana na mahala pakufikia wageni wale kilikuwa kimekamilika,Peniela akawapeleka kwanza hotelini kila mmoja akapata chumba chake halafu wakaondoka tena kuelekea nyumbani kwa John Mwaulaya ambako walipokelewa na Josh na moja kwa moja wakapelekwa chumbani kwa John mwaulaya ambaye alifurahi kuonana tena na watu wale baada ya muda mrefu.Kisha salimiana wote wakatoka na kuelekea katika sebule ya John Mwaulaya kwa ajili ya maongezi.Nickson ndiye aliyeongoza kikao kile kifupi

“ Peniela ,Josh,Jacob na Francis,kwa niaba ya wenzangu wote napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana kwa mapokezi yenu mazuri.Sina haja ya kurudia kujitambulisha tena kwani tayari sote mnatufahamu kwa hiyo basi nitakwenda moja kwa moja katika mambo makuu yaliyotuleta hapa.’ Akasema Nickson
“ jambo kubwa la kwanza lililotuleta hapa ni kuhusiana na operesheni 26B.Hii ni operesheni muhimu sana kwetu kwa hiyo tmelazimika kuja na kuifuatilia kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kwamba inakwenda kama inavyotakiwa na inakamilika.Tulimpa maelekezo Osmund kwamba ndani ya mwezi huu tunatakiwa tuwe tumeikamilisha operesheni hii na kuipata package hiyo muhimu sana kwa marekani na dunia kwa ujumla.Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari ni kwamba mawasiliano kati ya Dr joshua na wanunuzi wa package hiyo yamekwisha anza na muda wowote wanaweza wakafikia makubaliano.Tayari akaunti za benki zimekwisha funguliwa ambako wanunuzi hao wanatakiwa kuweka kiasi kikubwa sana cha fedha na kisha watakabidhiwa mzigo wao.Kwa gharama zozote zile hatutaki jambo hili litokee kwa hiyo lazima tuhakikishe tunaipata hiyo package.kwa hiyo nahitaji kusikia toka kwenu mmefikia wapi hadi hivi sasa? Akauliza Nickson

“ Nadhani peniela anaweza akajibu vizuri zaidi swali lako kwani yeye ndiye kiongozi mkuu katika operesheni 26B” akasema Josh
“ Ni kweli kama alivyosema Josh.Mimi ndiye niliyekabidhiwa jukumu la kuhakikisha kwamba tunaipata pachage hiy😵peresheni hii ilisimama kwa muda wa kama mwaka mmoja hivi baada ya mimi kuingia matatizoni lakini baada ya matatizo kumalizika operesheni imeendelea tena na ninapenda kukuthibitishia kwamba tumepiga hatua kubwa tayari.Ili kujiweka katika hatua nzuri ya kuipata package hiyo tayari nimejenga uhusiano wa kimapenzi na rais Dr Joshua pamoja na katibu wake .Vilevile tunaye captain Amos.Huyu ni mshirika mkubwa wa rais katika bashara hii na yeye ndiye ambaye ananipa taarifa za kila kinachoendelea kwa hiyo ushirikiano baina yetu ni mkubwa na tunachoshubiri kwa sasa ni siku ambayo package hiyo itatolewa ikulu kisha tuichukue.” Akasema peniela
“ Hongera sana peniela.Umefanya kazi kubwa na nzuri.Sisi tutakuwa nyuma yako kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda vizuri.Tutapata wasaa mzuri wa kujadili kwa upana kuhusiana na namna bora tunavyoweza kulikamilisha jambo hili hapo baadae.”akasema Nickson.

“ Nickson kuna jambo nataka kuuliza .Hiyo package ina nini ndani yake? Nimeyatoa mhanga maisha yangu kwa ajili ya kitu ambacho sikifahamu.Nadhani ni wakati mzuri sasa wa mimi kufahamu kitu ambacho nimekuwa nikihangaikia kwa muda huu mrefu ni kitu gani hasa.” Akauliza peniela
“ peniela wewe ni teamSC41 na ukiwa ndani ya kikundi hiki unakuwa ni kama askari mpambanaji,ukiambiwa fanya kitu Fulani basi unakifanya bila kuhoji.Sintaweza kukueleza kwa sasa kwani ni nje ya taratibu za team SC41.Una swali lingine?”akasema Nickson.Peniela akatingisha kichwa ishara kwamba hana tena swakli lingine lakini moyoni alikuwa amekasirika sana

“ Tuendelee.Jambo la pili lililotuleta hapa ni kuhusiana na afya ya John Mwaula.Kama mnavyofahamu ni kwamba John Mwaulaya hawezi kutibiwa katika hospitali za serikali wala haruhusiwi kuonekana nchini marekani kwa hiyo anatakiwa kutibiwa na madaktari walio ndani ya team SC41 pekee na ndiyo maana katika ujio huu tumeambatana na madaktari bingwa wawili wa mambo ya mishipa ya fahamu na kazi iliyowaleta hapa ni kumuhudumia John.”akasema Nickson

“ jambo la tatu ambalo tutalifanya tukiwa hapa ni kuhakikisha Team SC41 inasukwa upya na inarejea kuwa na nguvu kama zamani kabla John hajaanza kuumwa na jambo la mwisho kabisa tutahakikisha mwili wa Dr Burke unarejeshwa nyumbani kwa mazishi.Hayo ndiyo mambo ambayo tuyafanya katika kipindi ambacho tutakuwa hapa Dar es salaam.” Akasema Nickson.Sebule yote ilikuwa kimya.Nickson akaendelea

“ Nadhani mpaka hapo tumeelewana kwa hiyo kinachofuata sasa hivi sote tutaelekea kupata chakula cha mchana na baada ya hapo madaktari watarejea hapa kwa ajili ya kuanza kumfanyia John uchunguzi na wengine tutaelekea katika ofisi kuu ya team SC41 Tanzania tutasalimiana na watu wote pale na shughuli itaanzia hapo.Tukisha pata chakula cha mchana madaktari watarejea hapa ili waendelee kumfanyia uchunguzi John wakati sisi tukiendelea na kazi nyingine.Ninachoomba toka kwenu ni ushirikiano wenu mkubwa kwani bila ninyi hakuna tutakachoweza kukifanikisha.Kipindi hiki kifupi tutafanya kazi usiku na mchana hadi tuhakikishe kwamba tumefanikisha mambo yote.” Akasema Nickson

“ Nickson ninashukuru sana kwa ujio wenu huu ambao utakuwa na faida sana kwetu sote na team SC41.Ninashukuru sana kwa kuwaleta madaktari kwa ajili ya kuangalia afya ya John.Kwa kuwa jioni ya leo tutakuwa pia na kikao kikubwa kujadili kwa upana kuhusu mambo haya yote hususan operesheni 26B basi kwa mchana huu sintaweza kupambatana nanyi kuna jambo la muhimu na kwenda kulishughulikia ambalo linahusiana pia na operesheni yetu.Jacob na Francis watawapeleka katika ofisi kuu na mtakutana na watu wengine wote huko” akasema Peniela.
“ sawa peniela hakuna tatizo.Tutaonana jioni ya leo” akasema Nickson kisha wakaagana na kuondoka na kuwaacha Josh na peniela
“ Kazi imeanza.Wiki hii itakuwa ni wiki ngumu sana kwa Team SC41.Mambo mengi yatafanyika ndani ya wiki hii” akasema Josh,Peniela akamtazama kwa makini na kusema
“ Josh kuna kitu nataka kukuuliza na tafadhali naomba unipe jibu la kweli” akasema Peniela

“ Uliza chochote Peniela nakuahidi nitakueleza ukweli” akasema Josh.Peniela akamtazama na kuuliza
“ nani alimuua Dr Burke na Osmund?
Swali lile likamstua sana Josh.Alibabaika akasindwa ajibu nini

“ Naomba unijibu Josh.Nani alimuua Osmund na Dr Burke? Uko karibu sana na John muda wote na John hakuwa akimtaka kabisa Dr Burke aje na nina hakika ni yeye ndiye aliyetoa amri Dr Burke auawe .Kwa kuwa yeye hawezi kuifanya kazi hiyo lazima alimtuma mtu toka ndani ya team SC41.Niambie nani alifanya mauaji yale? Nina hakika unafahamu.” akasema Peniela.
“ Kwani kuna nini Peniela? Dr Burke na Osmund wamekwisha fariki na suala hili liko mikononi mwa polisi wakilifanyia uchunguzi”

“ Unawaona watu hawa waliokuja? Tayari wamehisi kwamba kuna mtu ndani ya Team SC41 ndiye aliyefanya mauaji yale na wanaanza uchunguzi wao mara moja na nina hakika lazima watampata na wakimjua nadhani unafahamu kitu watakachomfanyia.Josh kama unamfahamu mtu aliyefanya mauaji yale tafadhali nieleze” akasema Peniela.Sura ya Josh ilibadilika na alionekana kuogopa sana..
“ Peniela its me” akasema Josh.Peniela akamuangalia kwa mshangao mkubwa.

“ katika watu wote sikutegemea kama ni wewe ambaye unaweza ukafanya kitendo hiki” akasema peniela

“ Peniela nilifanya kwa kuwa John aliniomba nifanye.Siku zote nimekuwa mtiifu kwa John na hata aliponituma nikaifanye kazi hii sikusita kufanya hivyo.John alidai kwamba Dr Burke alikuwa na lengo la kumuua na tulitakiwa kumuwahi.Kama tusingemuwahi Burke basi angemuua John.Tafadhali Peniela kama kuna lolote unaloweza kunisaidia katika hili naomba unisaidie” akasema Josh.Peniela akainama akafikiri kidogo na kusema
“ Kwa kuwa ni John ndiye aliyekutuma nitakusaidia,tutatafuta namna ya kuweza kulitatua jambo hili.” Akasema Peniela.


*****


“Lazima leo nionane uso kwa uso na John mwaulaya.Lazima ukweli kuhusiana na Peniela ujulikane leo.Jason anapafahamu nyumbani kwa John kwani ndiko alipelekwa siku aliyotekwa”akawaza Mathew baaad ya kutoka katika kituo cha kulele watoto yatima alikolelewa Peniela.Akachukua simu akampigia Jason.
“ habari za asubuhi Jason” akasema Mathew baada ya Jason kupokea simu
“ habari nzuri sana Mathew.Habari za toka jana? Akauliza Jason

“ habari nzuri Jason.Uko wapi mida hii?
“ kwa sasa niko ofisini kwangu.”

“ Jason nahitaji kuonana nawe.Nielekeze mahala ofisi yako ilipo ili nikufuate hapo” akasema Mathew na Jason akamuelekeza mahala iliko ofisi yake .

“Kwa mara ya kwanza bada ya miaka mingi hatimaye nakwenda kukutana ana kwa ana na John Mwaulaya mtu ambaye aliiteketeza familia yangu.Kwa leo sintamfanya lolote kwani ninakwenda kwa ajili ya suala la Peniela lakini safari nyingine nitamfuata rasmi kwa ajili yangu na ninahisi huo utakuwa ndio mwisho wake.Kwa kumpa salamu tu,leo lazima aeleze ukweli wote kuhusiana na Peniela.Wakati ule John ndiye aliyekuwa na nguvu na kunifanya hadi nikaikimbia nchi yangu lakini safari hii mambo yamebadilika na mimi ndiye mwenye nguvu kuliko yeye.He will talk “ akawaza Mathew na mara simu yake ikaita.Alikuwa ni rafiki yake wa kutoka nchini Israel ambaye alimtumia zile karatasi zilizoibwa ikulu zilizokuwa zimeandikwa fomula za kisayansi
“ hallow Yash “ akasema Mathew

“ Mathew habari za Dar es salaam?
“ habari za huku nzuri sana .habari za huko?
“ Hata huku kwema tu” akajibu yash
“ Mathew tayari nimeikamilisha ile kazi uliyoniomba nikusaidie.Samahani imechukua muda kidogo lakini ilinilazimu kukutana na wanasayansi wakubwa ili kuweza kutambua kilichoandikwa katika zile karatasi.Nimekutumia kila kitu katika anuani yako ya barua pepe utasoma na kuelewa kila kitu”akasema Yash
“ Ahsante sana yash kwa msaada wako mkubwa.” Akajibu Mathew

“ Mathew karatasi zile umezitoa wapi? Akauliza Yash

“ Kuna jambo nalichunguza kwa sasa na ndani ya uchunguzi huo nikazipata karatasi hizo.Kwa nini umeuliza hivyo Yash?
“ nimeuliza hivyo kwa sababu ya ukubwa wa kitu kilichoandikwa ndani ya zile karatasi.Kama ni kitu hicho kipo kweli basi ni kitu cha hatari kubwa sana lakini kama hakipo basi karatasi hizo ni za kutunza sana kwani ni hatari mno na sijui zimefikaje huko.”
“ unaweza ukanipa japo kwa ufupi ni kitu gani hicho ? Akauliza Mathew

“ Nimekufafanulia kila kitu katika barua pepe niliyokutumia.” Akasema Yash
“ Ahsante sana Yash”

“ Mathew ,nitakupigia tena simu jioni ili tuongee vizuri zaidi” akasema Yash na kukata simu

“ Nini kimeandikwa katika zile karatasi kiasi hata cha kumstua Yash ? Lazima kitakuwa ni kitu kikubwa na kizito na ndiyo maana akina Edson walitaka kuziuza kwa mabilioni ya pesa” Akawaza Mathew akiwa njiani kuelekea ofisini kwa Jason
Aliwasili katika ofisi za Jason wakasalimiana na bila kupoteza wakati Mathew akauliza

“ Jason unaweza kupakumbuka nyumbani kwa John Mwaulaya ulikopelekwa siku ile”

“ Ndiyo ninapakumbuka.” Akajibu Jason

“ Ninaomba unipeleke” akasema Mathew
“unataka kwenda nyumbani kwa John mwaulaya? Jason akashangaa
“ Ndiyo nataka kwenda kuonana na John Mwaulaya.Kuna mambo ambayo anatakiwa kuyaweka wazi kuhusiana na Peniela”
“ mambo gani hayo Mathew? John ni mgonjwa unadhani anaweza akakueleza chochote kwa hali aliyonayo ? akauliza Jason
“ He will talk.Take me there” akasema Mathew.Jason huku akiwa na wasi wasi akavaa koti lake na kutoka wakaingia katika gari la Mathew na kuondoka kuelekea nyumbani kwa John Mwaulaya.Safari ilitawaliwa na maongezi machache sana hadi walipofika katika jumba la John mwaulaya.

“ Hapa ndipo nyumbani kwa John mwaulaya” akasema Jason
“ Wow ! jumba kubwa na la kifahari.Hawa watu ni kweli wanalipwa pesa nyingi sana kama alivyosema peniela.” Akasema Mathew na kisha akasimamisha gari katika geti .

“ Shuka kabonyeze kengele “ akasema Mathew.Jason akashuka na kwenda getini akabonyeza kengele mara tatu halafu akasuburi.Baada ya dakika tano mlango wa geti ukafunguliwa .Aliyeufungua alikuwa ni Josh ambaye alipatwa na mstuko mkubwa alipoonana uso kwa uso na Jason.Kwa sekunde kadhaa walibaki wanatazamana.
“ Jason !!..akasema Josh
“ What brings you here? Akauliza Josh.Jason akafumbua mdomo kutaka kusema kitu lakini akasita baada ya kusikia mlango wa gari unafunguliwa hakujibu kitu akageuka baada ya kusikia mlango wa gari ukifunguliwa,akashuka Mathew.Josh alimtazama vizuri sana na kuikumbuka ile sura.Ni yule mtu aliyeonekana katika kamera za nyumbani kwa Peniela.Akaingiwa na woga

“ hallow “ akasema Mathew
“ Josh .Naitwa Josh “ akasema Josh na kumpa mkono Mathew

“ Josh naitwa Mathew” akasema Mathew
“ Karibuni sana.Niwasidie nini? akauliza Josh
“ Nahitaji kuonana na John Mwaulaya.”
“ John Mwaulaya? Nani kawaambia John anaishi hapa? Akauliza Josh
“ Josh naomba usinipotezee muda wangu.Utatupeleka kwa John mwaulaya au nitumie nguvu? Akasema Mathew huku akipeleka mkono mahala iliko bastora yake.Josh akaogopa akafungua geti Mathew akamwambia Jason aingize gari ndani .Jason akalitambua gari la Peniela lililokuwamo mle ndani.
“ Peniela yuko hapa? Akauliza Jason
“ Ndiyo yupo”akajibu Josh

“ Ok vizuri sana.Tupeleke aliko John” akasema Mathew na Josh akaanza kuwapandisha ghorofani kilipo chumba cha John mwaulaya.Ndani ya chumba cha John alikuwemo Peniela na Dr martin ambaye amekuwa akimuhudumia John mwaulaya kwa muda mrefu.Mlango ukafunguliwa akaingia Josh akiwa amefuatana na Mathew na Jason.Wote mle chumbani wakastuka sana.

“ Mathew ! Jason !..akasema peniela kwa mshangao na kumfanya John Mwaulaya ageuze shingo yake na kutazama mlangoni.
“ mungu wangu ! akasema John mwaulaya kwa sauti ndogo .Naye pia alikuwa ameogopa sana.Mathew akasogea hadi karibu na kitanda cha John Mwaulaya akamtazama kwa macho makali sana.Peniela akaogopa
“ John mwaulaya,hatimaye tumeonana tena uso kwa uso .” akasema Mathew
“ Mathew what are you doing here? Akauliza Peniela

“ peniela nimekuja kuonana na John Mwaulaya.Nimefurahi sana kukukuta na wewe hapa ili usikie kile ambacho ninataka John akieleze mbele yako”

“ Mathew ,John is sick and he cant talk” akasema Peniela kwa wasi wasi.

“ he will talk” akasema Mathew.

“ Mathew !!..what are you doing? Akasema peniela huku akipiga hatua kumuendea Mathew.Jason akamzuia.
“ John mwaulaya,japokuwa imepita mika ming lakini nina hakika sura hii bado unaikumbuka vizuri sana.kama umeisahau nitakuja siku nyingine kukukumbusha lakini kwa leo nimekuja kwa ajili ya jambo moja tu, Peniela.” Akasema Mathew na kumstua kidogo Peniela.John mwaulaya alikuwa anatetemeka.
“ Ulimpeleka Peniela usiku katika kituo cha kulelea watoto yatima na ukadai kwamba umemchukua toka kwa mama yake na ukataka alelewe pale.Ulimwambia mama mwenye kile kituo kwamba peniela ni mwanao lakini hukutaka afahamu kama wewe ni baba yake na badala yake ukajiita mfadhili wake.Umemfanyia Peniela mambo mengi mabaya na kuyaharibu kabisa maisha yake,umemuingiza katika Team SC41 na umezifuta kabisa ndoto za maisha yake na mmekuwa mkimtumia kwa kazi zenu kwa manufaa ya serikali ya marekani.Ninataka mbele ya Peniela uungame ukweli wewe ni baba yake mzazi? Akauliza Mathew kwa ukali.Peniela alipigwa na butwaa asiamini kile alichokisikia .Akamkazia macho John mwaulaya kusikia atatoa jibu gani.

“ John answer me!!..akafoka Mathew

“ Sifahamu chochote juu ya hayo unayoyasema” akasema John kwa sauti ndogo.

“ John nitazame vizuri machoni.Nina uhakika na ninachokisema na sina utani hata kidogo.” Akasema Mathew na kumuinamia John
“ John nitazame vizuri machoni.I’m a monster kwa hiyo naomba usiniudhi.Nataka useme ukweli kwamba wewe ni baba yake mzazi Peniela? Akasema kwa ukali Mathew

“ I don’t know anything” akajibu John kwa sauti ndogo .

“ John this is the last chance ..are you Peniela’s father? Akauliza Mathew kwa ukali.John akajibu kwa kumfanyia ishara kwamba haelewi chochote.Mathew akakasirika na kuchomoa bastora yake.Peniela akaogopa sana
“ Mathew what are yo doing? Akauliza lakini Mathew hakumjali

“ Mathew unataka kufanya nini? Akauliza Peniela kwa wasi wasi
“ I’ll count to three and if you cant answer me I’m going to kill you John ! akasema kwa ukali Mathew

“ Mathew No ! Don’t do that !! akasema Peniela huku akilia
“ Jason hold her” Mathew akamuamuru Jason amshike Peniela ili asimsogelee.

“ Three…..!!!akaanza kuhesabu Mathew huku amemuelekezea John bastora
“ Two ….!!!!
“ Mathew noo!!!!..dont do that !!..akapiga kelele peniela.
“ On………..” Kabla Mathew hajamaliza kutamka John Mwaulaya akasema
“ Ok ok..I’ll tell you..put your gun down” akasema John mwaulaya aliyekuwa akitetemeka
“ ok tell her the truth! akasema kwa ukali Mathew huku akimtazma John kwa macho ya hasira
John akamfanyia ishara peniela asogee karibu na kuanza kumsimulia kilichotokea kuhusiana na wazazi wake.Alisimulia mkasa mzima uliotokea na kupelekea kuwaua wazazi wote wa peniela.Peniela alibubujkwa na machozi mengi.John akamgeukia Mathew
“ Hiyo ndiyo historia ya Peniela.Nilishindwa kabisa namna ya kumueleza nikiogopa kumuumiza na ndiyo maana nilitaka afahamu kuhusu yeye baada ya mimi kufariki dunia.Nilijua lazima atanichukia sana akifahamu kwamba mimi ndiye niliyewaua wazazi wake.Nilimuwekea kila kitu kuhusiana na historia yake katika makasha matatu ikiwamo na picha za wazazi wake.” Akasema John.Peniela alimuangalia kwa hasira huu machozi yakimtoka.

“Leo nilikuja kwa ajili ya Peniela.Safari ijayo nitakuja rasmi kwa ajili yangu.Jiandae “ akasema Mathew na kutoka Peniela akamfuata

“ Mathew thank you so much.Umenisaidia nimefahamu jambo kubwa sana.Sikuwa nikifahamu chochote kuhusiana na wazazi wangu.John amenificha siri hii kwa miaka mingi.I hate that bastard so much.”akasema Peniela

“ Elibariki aliniomba nikusaidie kuufahamu ukweli kuhusiana na asili yako na ninashukuru ukweli umedhihiri.Naomba ukweli huu usivuruge mipango yetu.”

“hakuna kitakachovurugika Mathew.I’m a very strong woman.Kila kitu kitakwenda kama tulivyokipanga.hata hivyo nina swali nataka kukuuliza.”

“ Uliza Peniela”

“ Ulipomuelekezea John bastora na kuanza kuhesabu,ulidhamiria kumpiga risasi kama asingesema chochote ?
Mathew akatabamu kidogo na kusema

“ No ! I just wanted him to talk”

“ ahsante Mathew.Ahsante sana.Tutaonana jioni .Mwambie Elibariki nashukuru sana kwa kunijali.Bila yeye kuwa na mawazo haya nisingeufahamu ukweli kuhusu wazazi wangu“ akasema peniela na kurejea tena ndani akakuta hali ya John mwaulaya imebadilika ghafla.Ikawalazimu wawaite haraka wale madaktari wawili waliokuja toka marekani kwa lengo la kuja kuangalia afya yake.


MCHAKATO WA KUIPATA PACKAGE MUHIMU UMESHIKA KASI NA KILA UPANDE UNAJIANDAA KUIPATA NINI KITATOKEA ? FLAVIANA MKE WA JAJI ELIBARIKI BADO YUKO MAHUTUTI HOSPITALI NINI HATIMA YAKE? NINI HATIMA YA JOHN MWAULAYA? KIKUNDI KIDOGO CHA WATU WENYE NGUVU NA USHAWISHI KIKIONGOZWA NA RAIS MSTAAFU KINAPANGA KUMUONDOA MADARAKANI DR JOSHUA NA WANAFIKIRIA KUMPENDEKEZA JAJI ELIBARIKI KUWANIA NAFASI HIYO JE WATAFANIKIWA LENGO LAO ? MWISHO WA SIMULIZI YA PENIELA SEASON 2..TUKUTANE TENA KATIA SEASON 3 HIVI KARIBUNI

..
 
Back
Top Bottom