SEASON 2
SEHEMU YA 28
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Nimekuwa mtumwa wa Team Sc41 kwa miaka mingi na sasa nimechoka.Wamenitumia wanavyotaka na sasa wanaanza kuingia hadi kwa watu wangu wa muhimu.Wanataka kunipangia hadi marafiki.Nitaishi vipi bila ya kuwa na marafiki ? Watu wangu wa muhimu watanielewaje? Akajiuliza peniela
“ lazima mambo haya yafike mwisho.Endapo hawatamuachia Jason katika muda niliowapa Iswear lazima nitapambana nao vibaya sana.Nadhani Team SC41 wakati wake umefika.” Akawaza Peniela akasimamisha gari pembeni ya bara bara akachukua simu na kumpigia Mathew
“ hallow Peniela habari yako?akasema Mathew baada ya kupokea simu
“ habari nzuri sana Mathew.Ninaomba unisaidie niongee na Elibariki” akasema peniela
“ kwa sasa siko nyumbani ,nimetoka kidogo nitakaporejea nitampatia simu utawasiliana naye’ akasema Mathew
“ ok Mathew ahsante sana” akajibu Peniela na kukata simu
ENDELEA………………
Hali ya John Mwaulaya ilibadilika sana baada ya kumaliza kuongea na Peniela simuni.Alikuwa akivuta pumzi kwa shida hali iliyomlazimu daktari wake amuwekee kifaa cha kumsaidia kupumua.
“ Martin, is he going to be ok? Akauliza Josh aliyekuwa na wasi wasi mwingi na haliya John
“ I don’t know” akajibu Martin kijana ambaye ana taaluma ya udaktari na ambaye amekuwa akimuhudumia John mwaulaya kwa kindi kirefu
“ Tutafanya nini sasa? Akauliza Josh
“ Subiri kwanza usikate tamaa mapema,baada ya muda atarejea katika hali yake ya kawaida’ akasema Martin.
Pamoja na kuvuta pumzi kwa shida lakini John mwaulaya alionekana kutaka kusema jambo,akamfanyia josh ishara asogee karibu halafu akakitoka kile kifaa cha kumsaidia kupumua
“L.e..le….uhhpphh..” akashindwa kuongea na kukirudisha tena kifaa kile mdomoni.Baada ya sekunde kadhaa akakitoa tena na kujitahidi kuongea
“ Let…hi..him..gooo..!! akasema John huku akinyoosha kidole katika luninga iliyokuwa ikimuonyesha Jason aliyekuwa amelala chini baada ya kipigo kikali alichopewa na Josh baada ya kutumia simu yake kuwasiliana na Peniela
“ Are you sure John ? akauliza Josh kwa mshangao kidogo.John Mwaulaya akamfanyia ishara ya mkono kwamba amuache Jason aende zake.Josh akaonekana kama vile hakubaliani na kitendo kile John akamfanyia ishara amsogelee akatoa kile kifaa cha kumsaidia kupumua akasema
“ Mpigie Pen..nniela..mwambie tum..tu..tumemuachia Jas..’ akasema John kwa taabu,martini akakirudisha kifaa kile mdomoni mwa John
“ Umesikia alichokwambia Josh? Go do it ! John hahitaji kuongea tena mida hii.Go Josh” akasema Martin na Josh akatoka mle chumbani akaelekea katika chumba alimo Jason.Akamtazama alivyokuwa amelala pale chini
“ Una maisha marefu zaidi ya paka kenge wewe.Leo ningekufanyia kitu kibaya sana umshukuru Peniela.bila yeye sijui kama ungetoka humu una meno yote”akawaza Josh huku akimtazama Jason kwa hasira sana. Akamuendea pale chini na kumpiga teke la mgongo.
“ Inuka paka we! Akasema kwa ukali na kumuinua Jason aliyekuwa akivuja damu akamtazama kwa hasira na kusema
“ Una bahati sana .Tunakuachia uondoke lakini ukithubutu kufumbua mdomo wako na ukasema chochote kuhusiana na kilichotokea leo ,nakuhakikishia kwamba haitatuchukua dakika thelathini sisi kufahamu na hautakuwa na sehemu ya kukimbilia kwani tutakusaka katika kila kona na tutakupata.Nikikupata nitakufanyia kitu kibaya sana,nitakuondoa jino moja moja kwa kutumia hili koleo” akasema Josh huku akimuonyesha jason kifaa kile kidogo
“ Nitakukata sikio moja moja na kukumwagia tindikali.Nitakukata kiuongo kimoja kimoja and you will die slowly but in great pain.kwa hiyo jihadhari sana usifanye jambo lolote lile kinyume na maagizo ninayokupa.Tumeelewana? akauliza Josh kwa ukali
“ N..dn..ndiyo..” akajibu Jason huku bado damu ikiendelea kumtoka mdomoni.Josh akamrejeshea vitu vyake vyote halafu akamuamuru ainuke wakatoka mle chumbani wakaelekea nje.
“ Ingia katika gari lako uondoke haraka sana,na tafadhali yafanyie kazi yale niliyokueleza.Ukienda kinyume chake litakapokupata hakuna anayeweza kukusaidia tena.keep your mouth shut” akasema Josh .Jason akaingia katika gari lake na kuliwasha kabla hajaondoka Josh akamwambia asubiri.Akachukua simu yake na kumpigia Peniela
“ hallo Josh,nategemea simu hii itakuwa ni ya kunifahamisha kwamba mmemuacha Jason na hajaumizwa” akasema Peniela mara tu baada ya kupokea simu
“ Peniela ongea na mtu wako huyu hapa” akasema Josh na kumpa Jason simu
“ hallo peniela’ akasema Jason
“ Jason ! are you ok? Akaulizaa peniela.Jason akamtazama Josh aliyekuwa katika dirisha la gari akimuangalia
“ ndiyo peniela.I’m ok.Wameniruhusu niondoke” akasema Jason
“ Wamekutesa? Wamekuumiza ? akauliza Peniela
“ hapana hawajanitesa ,walikuwa wakiuliza tu maswali “
“ Ok good.Naomba usiende nyumbani kwako.Nenda moja kwa moja nyumbani kwangu nisubiri pale mimi niko njiani ninaelekea huko .tafadhali fanya hivyo Jasoni kwa usalama wako” akasema peniela
“ sawa peniela nitafanya hivyo” akajibu Jason na kisha akamrejeshea Josh simu yake.
“ hallo peniela,kuna ktu ambacho ninataka kukueleza”
“ Kitu gani josh?
“ Hali ya John si nzuri toka ulipoongea naye simuni.Anavuta pumzi kwa shida sana”
“ Josh naomba usiniambie habari hizo kwa sasa.Sina chochote cha kufanya kwa sasa “akasema Peniela
“ peniela,John ndiye kongozi wetu na baada ya Osmund kufariki John hana tena msaidizi.Wewe ndiye ambaye tunakutegemea “
“ Josh please ,nina mambo mengi ya kufanya kwa sasa.Naomba uniache kwanza nitakupigia simu baadae.Jitahidini kufanya vile muwezavyo kumsaidia” akasema Peniela na kukata simu.
“ John amekwisha nitoka kabisa akilini na sitaki hata kusikia habari zake.Ninachokifikiria kwa sasa ni namna ya kuwalinda watu wangu wa karibu,Elibariki na Mathew wasidhuriwe na mtu yeyote.Kama ikitokea akapoteza maisha its ok.Amezoea kutoa roho za wenzake na yeye zamu yake imefika.John ni mtu ambaye amenilea toka nikiwa mdogo na amenifikisha hapa nilipo lakini ni mtu mkatili sana na hafai kuonewa huruma.Binafsi ameniharibia maisha yangu na kunipotezea kabisa mwelekeo mzima wa maisha yangu.Amenichefua zaidi baada ya kuanza kuwaandama na watu wangu wa karibu .Kwa sasa kuna kitu kimoja tu ninachokifikiria kukifanya….” Akawaza Peniela
“ Sijui jason atanielewaje kuhusiana na tukio hili .Watu ninaoshirikiana nao wamemteka na kumtesa sana.Hakuna kitu cha kuficha tena hapa kwani kila kitu kiko wazi.Tayari amekwishagundua kwamba ninashirikiana na akina Josh ambao wamemteka na kumtesa .Tayari amekwisha fahamu kwamba nina mahusiano na watu hatari.Taswira yangu kwake imekwishabadilika na sina namna nyingine ya kufanya kumfanya aniamini tena zaidi ya kumweleza ukweli mimi ni nani. Siwezi kuendelea kujificha kwani tayari nimekwisha fahamika.Hii yote imesababishwa na akina John kufanya mambo kwa kukurupuka bila kutumia akili.Nadhani mwisho wa Team SC41 umekaribia sana.”akawaza Peniela na kuongeza mwendo wa gari kuelekea nyumbani kwake kumuwahi Jason
Alifika nyumbanikwake na kulikuta gari la Jason liko nje.Akashuka garini haraka na kwenda kugonga mlango wa gari la Jason ambaye alipomuona Peniela akashusha kioo na kumstua sana Penny baada ya kuona damu nyingi ikimvuja.
“ Ouh my God Jason!..akasema Peniela kwa mshangao akafungua geti haraka haraka wakangiza magari ndani.Jason akashuka huku akichechemea.Peniela akamfuata na kumkumbatia
‘ Oh Jason jamani Pole sana” akasema Peniela Jason hakujibu kitu.Peniela akamshika mkono na kumuongoza hadi chumbani kwake akamvua koti na shati vilivyokuwa vimeloana damu akamshika mkono akamuingiza bafuni.
“ peniela you dont have to do this” akasema Jason
“Jason please let me do this” akasema Peniela huku akiufungua mkanda na kumvua Jason suruali halafu akafungua maji na kumuogesha .Kisha maliza zoezi hilo akachukua kisanduku cha dawa akampaka dawa katika majeraha yote aliyoyapata kutokana na kipgo cha Josh
“ Thank you penny’akasema Jason
“ Please Jason you don’t have to thank me” akasema peniela
“ lazima nikushukuru Peniala.Umeniokoa .Bila wewe watu wale wangenitesa na kuniua.Umeyaokoa maisha yangu” akasema Jason
“ Jason Pole sana kwa kitendo ulichofanyiwa na wale watu.Naomba ufahamu kwamba nimeumizwa sana na kitendo hiki.Hawakutakiwa wakufanyie jambo kama hili ” akasema Peniela huku akimtazama Jason kwa huruma
“ Usijali peniela mimi ndiye niliyefanya ujinga wa kwenda polisi na kutoa taarifa za Elibariki kuonekana nyumbani kwako.Utanisamehe sana kwa jambo hili la kijinga nililolifanya .Niliposikia kwamba Elibariki yuko hapa kwako niliingiwa na wivu mkubwa na niliumia moyoni kwa nini awepo hapa na ndiyo maana nikalazimika kwenda kutoa taarifa polisi kwa lengo la kulipiza kisasi .Peniela naomba unisamehe pia kwa tuko lile nililolifanya siku ile la kusababisha ugomvi mkubwa na Elibariki hapa nyumbani kwako ugomvi uliosababisha nimpige Elibariki na chupa kichwani.Nilishindwa kudhibiti hasira zangu na kufanya kitendo kile cha kijinga ambacho ningeweza hata kusababisha kifo cha Elibariki na ningekuingiza wewe katika matatizo makubwa.Lakni yote haya niliyoyafanya yamesababishwa na pendo wangu mkubwa nilionao kwako.Ninakupenda sana Peniela na ninasika wivu mkubwa kukuona ukiwa na mwanaume mwingine hasa hasa Elibariki”akasema Jason.Peniela akamtazama akamuonea huruma sana.
“ Pole sana Jason.Hukutakiwa kufanya vile ulivyofanya .Hata hivyo nimekwisha kusamehe Jason kwa sababu wewe ni mtu wangu wa karibuna wa muhimu sana.Tumekuwa marafiki kwa muda mrefu na hatujawa kukorofishana.Umesimama na mimi dunia nzima iliponitenga nilipopata matatizo kwa hiyo wewe ni mtu ambaye una nafasi kubwa sana ndani ya moyo wangu .Kuhusiana na kilichotokea leo kuna mambo mengi sana ambayo tunatakiwa kuyaongea na kuyaweka sawa.Kuna masuala ambayo mnatakiwa kuyafahamu lakini kabla ya yote kuna mahala tunatakiwa kwenda.Unafahamu anakoishi Mathew? Akauliza peniela
“ Ndiyo ninapafahamu ” akajibu Jason
“ Ok jiandae tunaelekea huko”akasema Peniela
” Tunaenda kufanya nini huko kwa Mathew? Akauliza Jason
“ Kuna mambo ambayo mnatakiwa kuyafahamu.”akasema Peniela
“ peniela kabla hatujaelekea huko kuna jambo nataka niulize.Watu wale ni akina nani? Unahusiana nao kivipi? Akauliza Jason
“ Usijali kuhusu hilo Jason.Utafahamu kila kitu lakini kwa sasa naomba ujiandae tuelekee kwa Mathew.”akasema Peniela akafungua kabati lake la nguo na kutoa trakisuti nyeusi na kumpatia Jason avae kwani nguo zake zote zilikuwa zimetapakaa damu.Kisha vaa wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea kwa Mathew.Mara tu baada ya kuliacha geti Peniela akachukua simu na kumpigia Mathew
“ Hallow Peniela” akasema Mathew
“ Mathew ninaelekea nyumbani kwako,uko wapi?
“ Unakwenda nyumbani kwangu? Mathew akashangaa
“ Unapafahamu nyumbani kwangu? Akauliza Mathew
“Sipafahamu ila niko na Jason ndiye anayenipeleka huko” akasema Peniela
“ Unakwenda kufanya nini?
“ Ninahitaji kuonana nanyi nyote.Kuna mambo ambayo nataka kuongea nanyi” akasema Peniela
“ Penela kwa sasa bado niko katika mizunguko yangu ya kikazi ukifika nisubiri usiondoke,sintakawia sana”akasema Mathew
“ sawa Mathew” akasema Peniela na kukata simu
“ Unamfahamu Mathew? Akauliza Jason
“Ndiyo ninamfahamu yeye na Anitha pia ” akasema Peniela na kumshangaza Jason.Hakujua kama tayari Mathew na peniela wanafahamiana
“ Peniela ni msichana hatari na nimemuogopa sana.Sikuwahi kuhisi hata siku moja kama anaweza kuwa na mahusiano na watu hatari kama wale.lakini watu wale ni akina nani? Shughuli zao nini nini? Ni majambazi? Akajiuliza Jason
“ hapana sina hakika kama wale jamaa ni majambazi.Inaonekana shughuli zao ni zaidi ya ujambazi.wale hawaonekani kama ni majambazi.Ninahisi wanaweza kuwa ni mtandao unaojihusisha na madawa ya kulevya.Ninaweza kuamini hivyo kutokana na jumba lile kubwa walimonipeleka .Lilikuwa ni jumba la kifahari sana ambalo kwa pesa ya ujambazi si rahisi kulijenga .Lazima watakuwa wakijishughulisha na biashara haramu na kama ni hivyo basi hata Peniela naye atakuwa akijihusisha na mtandao huu na ndiyo maana ni binti ambaye anaishi maisha ya hali ya juu sana na akaweza kumiliki yale maduka makubwa mawili ya nguo ambayo hata hivyo yalifilisika alipopata matatizo ya ile kesi ya mauaji.Pamoja na kumalizika kwa kesi yake na kukuta biashara zake zote zimefilisika lakini bado Peniela hajatetereka kiuchumi na anaishi bado maisha ya hali ya juu.Nilitegemea kwamba baada ya kutoka gerezani atakuwa katika hali mbaya kiuchumi na nilikwishajipanga kumsaidia lakini haonekani kabisa kuyumba na maisha yake yanaendelea kama kawaida.Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusiana na suala hili kwamba ni wapi Peniela anakopata pesa za kuendesha maisha yake na leo hi nimepata jibu.Nimeanza kumuogopa sana” akawaza Jason
“ Ninampenda sana Peniela lakini kwa tukio la leo sina hakika kama peniela ni mwanamke anayenifaa.Ukimuona namna alivyo huwezi kumdhania kama anaweza kuwa na mahusiano na watu hatari kama wale.Ninajilaumu hata kwa nini nilifahamiana naye.” Akawaza Jason huku akimtazama Peniela kwa jicho la wizi .
“ Ninaanza kuingiwa na hisia kwamba huenda hata kifo cha edson Peniela akawa anahusika.Suala hili linatakiwa lifanyiwe uchunguzi.Ninakubaliana kabisa na ule usemivusemao kwamba umdhaniaye siye ndiye. Akaendelea kuwaza jason
Safari ilikuwa ya kmya kimya na mara chache waliongea pale Jason alipomuelekeza Peniela njia za kupita hadi walipofika nyumbani kwa Mathew
“ wow ! the house is so big like a palace”akasema Peniela.Mlinzi ambaye hulinda jumba la Mathew tayari alikwisha pewa taarifa za wageni wale akawafungulia geti wakaingia ndani.
“ The house is so beautiful” akasema Peniela akitabasamu na kuufurahia uzuri wa jumba lile la Mathew.Walikaribishwa sebuleni na mlinzi ambaye alipewa maelekezo kwamba awahudumie kwa vinywaji wageni wale.
Sauti za kufungwa kwa milango ya gari zikamstua jaji Eliabriki akafikiri kwamba Mathew na Anitha wamerejea.Akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni.Alistuka mno baada ya kukutanisha macho na Peniela .Alitamani kuamini kwamba ile ilikuwa ni ndoto lakini haikuwa ni ndoto bali ni kitu cha kweli alichokuwa akikishuhudia.Peniela alikuwa sebuleni akiwa na jason hasimu mkubwa wa Elibariki.Mara tu alipokutanisha macho na Jason wote wakabaki wakishangaana .
“ Penela my love!..akasema jaji Elibariki .Pemiela akainuka na kwenda kumkumbatia kwa furaha kubwa.
“ Ouh Elibariki I missed you so much my love” akasema Peniela.Kama ilivyokuwa kwa Elibariki Jason naye alibaki akishangaa kwani hakutegemea kama angekutana na Elibariki pale nyumbani kwa Mathew.
‘ what is he doing here? Akauliza Eliariki kwa ukali huku akimtazma jason kwa hasira
“ peniela whats going on? Why is this bastard here ? Naye Jason akauliza kwa hasira
“ Hey guys..its time now to stop your childish things..You have to stop fighting .What are you fighting for ? akauliza Peniela kwa ukali
“ I hate this bstard so much” akasema Jason
“ I hate you too ..Sikupendi sana Jason” akasema jaji Elibariki huku akitaka kumfuata Jason.Peniela akamzuia
“ Elbariki stop.!!..Do you want to keep on fighting because of me? Ok fine keep on fighting and kill each other” akasema Peniela na kuondoka akaenda kuketi sofani.Jaji Elibariki na jason wakabiki wanatazamana kwa hasira.
“ Nimewaachia uwanja mpigane.Mbona hampigani?akauliza Peniela
“ If I see you near Peniela again I swear in heaven and earth I’m going to kill you” akasema jaji Elibariki na kumfuata peniela pale sofani akakaa pembeni yake.
“ Peniela I’m so sorry .sikutegemea kama ningekutana na huyu kijana hapa.” Akasema jaji Elibariki.Jason akakasirika na kuinuka
“ Elibariki nimekuvumilia sana na sintavumilia tena dharau nyingine yoyote toka kwako.Unadhani ninakuogopa? Akaulizia Jason huku akimsogelea jaji Elibariki.Peniela akamfuata na kumshika mkono
“ Jason naomba ukae na sitaki mtu yeyote aongee zaidi yangu” akasema Peniela kwa ukali.Wote waili Jason na Elibarii wakabaki kimya
“ nawashangaa sana mnapoendelea kupigana kila siku na kutishiana maisha kwa sababu yangu.Mimi ni nani kwenu?Chombo cha kuwastarehesha hadi mfikie hatua ya kutaka kutoana uhai? Akauliza peniela kwa ukali
“ Ninyi nimarafiki na hamna haja ya kugombana.Ni aibu kubwa mkisikika waheshimiwa kama ninyi mnagombana kwa sababu ya mwanamke.” akasema Peniela.
“ Ni huyu ndiye aliyeanza haya yote kwa kuvamia mapenzi ya wat…”akasema jaji Elibariki na akakatishwa na Peniela
“ Elibariki stop.Nimesema sitaki mtu yeyote aongee zaidi yangu” akafoka Peniela
“ Mimi na wewe nani aliyevamia mwenzake.Unajua nimetoka wapi na Peniela? Wewe una mke wako rudi katika ndoa yak……………”akasema Jason lakini akakatishwa na Penny
“ Jason Stoop ! nimesema hiki ni kikaochangu na nyote mnatakiwa make kimya”akasema peniela.akawatazama mashababi wale ambao kila mmoja alikuwa amefura kwa hasira akimtazama mwenzake kwa chuki
“ Ninyi nyote hampaswi kuchukiana wala kugombana.Mnayepaswa kunilaumuna kunichukia ni mimi kwa sababu ndiye niliyekubali kulala nanyi nyote wawili.Hakuna kati yenu aliyefahamu kwamba mwenzake anatembea na mimi hadi siku ile mlipokutana.Kwa maana hiyo basi mnatakiwa mkae na mmalize tofauti zenu.Nimewakutanisha hapa makusudi kabisa ili muweze kumaliza tofauti zenu ninyi wenyewe.Mnatakiwa muongee na muelewane na baada ya hapo kuna jambo kubwa ambalo nataka kuwaambia.kwa sasa nitaondoka na kuwaacha ninyi peke yenu na nitakaporejea nataka muwe mumemaliza tofauti zenu na ndipo tutakapoweza kukaa na kuongea.Siwezi kuongea nanyi sasa hivi wakati ambao kila mmoja wenu amefura hasira kama simba.” Akasema peniela na kuchukua mkoba wake.
“ peniela siwezi kuendelea kukaa hapa.Ninaondoka pia”akasema Jason
“ jason you cant go anywhere.Kaeni hapa na mmalize tofauti zenu ninyi wenyewe.Ninyi ni marafiki na hampaswi kugombana .Be like men ! …akasema peniela na kutoka mle sebuleni akaingia garini na kuondoka.Akiwa garini akachukua simu yake na kumpigia Mathew
“ hallow Mathew ,nimekwisha fika kwako na nimeondoka ila nitarejea baadae kidogo nina maongezi makubwa na Elibariki pamoja na Jason.Kuna mambo ambayo nahitajiku yaweka sawa kati yao’ akasema Peniela
“ sawa Peniela hata sisi tutarejea nyumbani muda si mrefu kwani shughuli yetu tuliyokuja kuifanya tunatarajia kuikamilisha muda si mrefu” akasema Mathew na kukata simu
“ Kuna ulazima wa kufahamu john anaendelaje? Akajiuliza Peniela
“ hakuna haja.sitaki kujua anaendelea vipi.Akili yangu imenituma katika kitu kimoja tu na ambacho ndicho ninakwenda kukifanya.Its time to take down Team SC41.Hakuna aliywahi kufikiria kitu hiki lakini mimi ninakwenda kukifanya.Najua ni hatari lakini sintakata tama I’ll die trying.Nimegundua kwamba bila kufanya hivi sintakuwa huru na sintakuwa na maisha ya kawaida” akawaza Peniela halafu akazitafuta namba za simu za Captain Amos akampigia
“ hallow Peniela” akasema Captain Amos
“ hallow amos.habari yako?
“ habari nzuri peniela ,vipimaendeleo yako?
“Ninaendela vizuri Amos.Nimekupigia kutaka kufahamu kuhusu ule mpango wa kunikutanisha na Dr Kigomba.Maandalizi yanakwendaje? akaulizia Peniela
“ Kila kitu kinakwenda vizuri sana Peniela na jioni ya leo nitakukutanisha naye.Kwa sasa ninaandaa sehemu ya kukutania na nitakutumia ujumbe baadae kukujulisha sehemu ya kukutania.Kitu ambacho ni cha muhmu wakati wa kuonana usionyeshe kama unanifahamu.Utajifanya kwamba ni mara ya kwanza mimi na wewe tunaonana.Kitu kingine ni kwamba jitahidi jambo hili liende kwa haraka kwani muda wowote Dr Joshua anaweza akamkabidhi Dr Kigomba ule mzigo.kwa hiyo lazima tufanye haraka sana kujenga mahusiano ya haraka”
“ usijali Amos.Kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa.Huna haja ya kuwa na wasi wasi na mimi” akasema Peniela na kukata simu
*******
Jaji Elbariki na Jason waliendelea kukaa pale sebuleni hakuna aliyetaka kumsemesha mwenzake.Baada ya kama dakika kumi na saba toka Peniela aondoke jaji Elibariki akasema
“ Ok Jason,nimeamua kujisusha .Lets talk like men.” Akasema jaji Elibariki
“ You want to talk? Sina muda wa kuongea nawe Elibariki” akasema Jason
“ Jason lets be like men.Lets talk about this !” akasema jaji Elibariki
“ Ok unataka kuniambia nini? Akauliza Jason
“ Peniela yuko sahihi.Hatuhitaji kugombana.Binafsi sikuwa nikifahamu kama nawewe unampenda Peniela .Nilianza kumpenda peniela wakati wa kusikiliza kesi yake na baada ya kesi kumalizika ndipo nilipooanza kuwa na ukaribu naye na hakuwahi kunieleza chochote kuhusu wewe.Yeye alichoniambia nikwamba hakuwa na mpenzi kwani mpenzi wake alikuwa Edson pekee.Nilimweleza ninavyompenda na alinikubalia tukawa wapenzi.Nilistuka sana siku ile nilipokuona umetokea ghafla mle ndani wakati tukifanya mapenzi.Nilistuka zaidi pia uliponieleza kwamba Peniela ni mpenzi wako.Sote wawili hatukuwa tukifahamu kwamba tulikuwa tunatembea na mwanamke mmoja.Kwa maana hiyo baadaya kuligundua hili ni wakati wetu sasa wa kusameheana na kusahau yaliyopita.Hatuna haja ya kugombana kwani sote tumedanganywa kwa hiyo hata tukigombana hatutapata mshindi.” akasema jaji Elibariki.Maneno yale ya jaji Elibariki na sauti ya upole aliyoitumia kidogo vikamfanya Jason atulize hasira .Akakohoa kurekebisha koo na kusema
“ Nimefahamiana na Peniela kwa muda mrefu kidogo na wakati huo bado alikuwa katika mahusiano na Edson.Baada ya kupatwa na matatizo yake nikasimama pamoja naye kama rafiki.Baada ya kesi kumalizka na akashinda kwa kuwa tayari nilikuwa na hisia za kumpenda mrefu niliamua kuitumia vizuri nafasi hiyo na kumueleza hisia zangu.Peniela akanielewa na akanikubalia kwamba tuwe wapenzi na hakuwahi kunieleza kama ana mahusiano na mtu mwingine yeyote.Siku ilenilipowakuta mkifanya mapenzi na ukatokea ule ugomvi,Peniela alinipigia simuna kunifahamisha kwamba kuna mtu yuko ndani kwake na mtu huyo amekuwa akimsumbua sana kwa muda mrefu akimtaka kimapenzi.Alinambia kwamba niwahi haraka kwa kuwa mtu yule hakuwa na nia njema na alikuwa na wasi wasi kwamba mtu yule angeweza hata kumbaka.Nilifika haraka sana na kukuta kwamba ni wewe ,nilikasirika sana na ndipo ugomzi ule ukatokea.Jana baada ya kutoka katika msiba wa Noah,nilipata taarifa toka kwa Mathew kwamba uko salama na uko kwa Peniela.Nilisikia wivu mkubwa na ndipo nikaenda kutoa taarifa kituo cha polisi na kuwafahamisha kwamba uko pale” akasema Jason na kumstua sana Elibariki
“ It was you? Jaji Elibariki akashangaa
“ yes it was me”akasema Jason
“ ouh my God I cant believe this” akasema jaji Elibarii
“Utanisamehe sana Elibariki kilichonifanya nikafanya jambo lile ni kutawaliwa na wivu na hasira .Sikujua kama kwa kufanya vile nitahatarisha maisha yako”akasema jason.jaji elibariki akakaa kimya kidogo akainama na baada ya sekunde kadhaa akainua kichwa na kusema.
“ katika watu wote ambao ningewadhania sikuwahi kufikiri kama ungeweza kufanya kitu kama kile Jason”
“ Tusameheane Elibariki,nililfanya vile kutokana na hasira na wivu tu.” Akasema Jason
“ Ok tusahau yaliyopita” akasema Elibariki
“ nashukuru sana Elibariki.Ni kweli hatuna sababu ya kupigana kama alivyosema Peniela.Hakuna kati yetu aliyefahamu kama tuna mahusiano na mwanamke mmoja.Wa kulaumiwa hapa ni Peniela” Akasema Jason
“ kweli kabisa Jason.Kuna jambo nimeliona baada ya kuniambia kwamba Peniela alikupigia simu na kukufahamisha kwamba kuna mtu ambaye anataka kumbaka na ukaja ukanikuta mimi.Sikuwahi kutaka kutenda kitendo kama hicho na wala sikuwahi kumlazimisha kimapenzi Peniela.Mimi na yeye tulikubaliana kuwa wapenzi kwa mioyo yetu yote na wala hakukuwa na shinikizo lolote toka kwangu kumtaka anikubali.Kuna picha ninaipata hapa kwamba peniela alitembea na sisi sote wakati akijua kwamba ni marafiki na zaidi ya yote alitaka tukutane uso kwa uso.Ninakumbuka siku ile alitaka tufanye mapenzi sebuleni kumbe lengo lake ni ili utukute pale.” akasema jaji Elibariki
“ Mimi alivyonipiigia simu aliniambia kwamba nikifika nipite moja kwa moja ndani milango iko wazi” akasema Jason
“ Umeona Jason. ! Ni wazi peniela alitaka jambo lile litokee yaani mimi na wewe tukutane,tugongane ,alitaka utukute mimi na yeye tukiwa sebuleni tukifanya mapenzi.Alitaka tugombane,tuchukiane na alifanikiwa lengo lake kwani tuligombana na nusura nipoteze maisha.kwa nini lakini alifanya hivi?kwa nini alitaka mimi na wewe tugombane?akauliza jaji elibariki
“ Elibariki Peniela ni msichana hatari sana,na leo nimelifahamu hilo”
“ Umefahamu kitu gani?akauliza jaji Elibariki
“ Sote hatukuwa sahihi kuhusiana na mtu tuliyekuwa tukimpigania kiasi cha kutishiana kutoana uhai.”
“ kwa nini unasema hivyo Jason? Akauliza Elbariki
“ Peniela hayuko kama vile tunavyomchukulia.Ni mtu hatari sana”akasema Jason
“ Jason bado sijakuelewa.Hebu nifafanulie nifahamu” akasema jaji Elibariki
Jason akamueleza jaji Elibariki kila kitu kilichotokea
“ dah ! ninahisi joto kali.maneno uliyonieleza ni mazito sana.”akasema jaji Elibariki na kusimama akaenda katika friji akachukua maji baridi akanywa na kurejea tena sofani
“Peniela ! Nimemuogopa sana”akasema jaji Elibariki.Akawaza tena kidogo na kusema
“ Ninaweza kukubalina nawe Jason kwamba peniela ana mambo mengi sana tofauti na tunavyomfahamu.Baada ya maelezo hayo kuna kitu nimekikumbuka,wakati nikiwa palekwake kuna nyakati alikuwa akipigiwa simu na hakutaka kupokea mbeleyangu.Alikuwa akitoka na kwenda kuongelea mbali.Hakutaka nisiyasikie maongezi yake.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu alikuwa anakificha.”akasema jaji Elibariki
“ Ninavyohisi mimi wale jamaa watakuwa wakijihusisha namadawa ya kulevya kwa sababu jumba lille alikonipeleka Josh si jumba la kawaida.Ni jumba la kifahari sana.kama si madawa ya kulevya basi watu wale watakuwa wakijihusisha na biashara za haramu .Ninahisi vile vile kwamba hata kifo cha Edson,Peniela atakuwa akihusika.” Akasema Jason
“ Hapana.Katika kifo cha Edson Peniela hahusiki kabisa.tayari wahusika wamefahamika” Akasema jaji Elibariki
“ mmekwisha wafahamu? Akauliza Jason kwa mshangao
“ Ndiyo tayari tumekwisha wafahamu lakini bado kuna uchunguzi unaendelea ili kupata taarifa zenye uhakika zaidi “akasema elibariki
“Ni akina nani hao? Akauliza Jason
“ Ni jambo lenye maelezo marefu na ninadhani tusubiri atakapokuja Mathew ndiye atakayekuelezea kila kitu.” Akasema jaji Elibariki
“Sikuwa na taarifa hizo kabisa.Nilidhani kwamba baada ya ugomvi ule kutokea kila kitu kilisimama’akasema Jason
“ hapana Jason.Mambo yaliendelea.Akina Mathew waliendelea kufanya kazi na wamepiga hatua kubwa kuna mambo ambayo yamegundulika na ambayo akina Mathew wanayafanyia kazi.Mathew anaweza kukufafanulia vizuri zaidi kama bado utahitaji kuendelea na operesheni ile tuliyoianza”
“ Niko tayari Elibariki.Niko tayari kuendelea nayo.Nina hamu sana ya kutaka kumfahamu kwa undani peniela ni nani ,na wale jamaa anaoshirikiana nao ni akina nani.”
“ basi kama ni hivyo tumsubiri Peniela jioni atakaporejea kwani ameahidi kuja kuzungumza nasi jambo kubwa,sijui ni jambo gani hilo analotaka tulizungumze” akasema jaji Elibariki.
“ Yawezekana labda anataka kuja kuongelea kilichotokea asubuhi ya leo kwani nilimuuliza kuhusiana na watu wale akaniambia kwamba ataniambia baadae kila kitu .Atanipa ukweli kamili”
“ basi itakuwa vyema tukiendelea kumsubiri.so are we ok now? Akasema jaji Elibariki
“ yes we’re ok.Sisi ni wanaume na hatupaswi kugombana kwa sababu ya mwanamke”
‘ Ahsante sana Jason.nashukuru sana. “ akasema jaji Elibariki,akasimama wakashikana mikono.walimaliza tofauti zao na urafiki ukarejea tena.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……