Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

LEGE umeuchuna sio.....no sweat leo nitakuota
 
SEASON 2


SEHEMU YA 26


ILIPOISHIA SEHEMU LIYOPITA
“ Elibariki nadhani unahitaji mapumziko .Kesho asubuhi tutafahamu kinachoendelea” akasema Mathew .Jaji Elibariki hakusema kitu akajitahidi kusimama na kisha aketembea kuelekea katika chumba chake.

“ Anitha hata wewe pia unahitaji mapumziko ,siku imekuwa ndefu sana,mambo mengi yametokea usiku huu ,tupumzikena tujiandae kwa ajili ya siku ya kesho,ila kitu kimoja ambacho sikutaka kukwambia mbele ya Elibariki ni kwamba sina hakika kama mkewake atakuwa salama.Nilimsogelea karibu ilikuchukua ile bahasha nikasikia namna alivyokuwa akihangaika kuvuta hewa.Tusubiri hadi siku ya kesho tutapata taarifa nini kimetokea ,kama ni mzima ama amefariki “

“ maskini Elibariki.Namonea huruma sana.Amepatwa na majanga mengi mfululizo “akasema Anitha
“Kesho tutaanza kuifanya kazi taarifa ile ya madaktari kubaini ukweli wake.Vile vile nitawasiliana na rafiki zangu wa huko nje ili waweze kunisiadia kutambua kilichomo ndani ya zile karatasi zilizoibwa ikulu” akasema Mathew na kila mmoja akaenda chumbani kupumzika.



ENDELEA………………

Saa kumi alfajiri madaktari katika hospitali kuu ya taifa walikamilisha upasuaji waliokuwa wakimfanyia Flaviana ili kuondoa risasi na kujaribu kuokoa maisha yake.Bado Dr Joshua alikuwepo pale hospitali akisubiri kutaarifiwa kuhusiana na hali ya mwanae.Flaviana alitolewa katika chumba cha upasuaji na kupelekwa katika chumba cha uangalizi maalum.Dr Joshua akataarifiwa kuhusu kumalizika kwa upasuaji ule halafu wakaongozana na Dr Marcelo kuelekea ofisini kwake.
“ Mheshimiwa rais upasuaji umemalizika na wamefanikiwa kuziondoa risasi tatu alizokuwa amepigwa Flaviana.Risasi moja ilimpata pajani,nyingine mbili zilimpata kifuani lakini hazikufika katika moyo .Hata hivyo madaktari wamejitahidi sana kuzuia kuendelea kuvuja kwa damu .Madaktari wamefanya kila waliloweza kulifanya kuokoa uhai wa Flaviana na kwa sasa kila kitu tukiweke katika mikono ya mwenyezi Mungu yeye ndiye mwamuzi wa kila jambo lakini bado tunaendelea kumuangalia kwa karibu sana” akasema Dr Marcelo

“Dr Marcelo sina neno la kusema kutosha kuwashukuru nini nyote kwa msaada huu mkubwa mlionisaidia.Utanifikishia shukrani zangu kwa madaktari wote waliopambana kuokoa uhai wa mwanangu.Pamoja na hayo kuna jambo nimekuwa nikilifikiria.”

“ jambo gani Mheshimiwa rais?
“ Ninafikiria kumuhamisha Flaviana na kumpeleka nje ya nchi.Unanishauri vipi kuhusu hilo?

“ Wazo lako sibaya mheshimiwa rais lakini hata hapa tunao uwezo wa kumuangalia mwanao.Kwa hali yake ya sasa sina hakika kama anafaa kusafirishwa .Nakushauri mheshimiwa rais muache hapa hapa ili aendelee kupewa uangalizi .Tunao madaktari wenye ujuzi wa kutosha ”
Dr Joshua akafikiri kidogo a kusema
“ Sawa Dr Marcelo ninakubaliana na ushauri wako .Tumuache hapa hapa nchini kwa siku kadhaa halafu kama hakutakuwa na mabadiliko nitampeleka nje ya nchi kwenye hospitali kubwa na bora zaidi “ akasema Dr Joshua na kuagana na Dr Marcelo akaingia garini akiwa na Dr Kigomba

“ Kigomba nilikuwa nafikiria kumpeleka Flaviana nje ya nchi lakini Dr Marcelo amenishauri kwamba haitafaa kwa sasa ,ngoja tusubiri kidogo na kama hali yake haitakuwa na mabadiliko basi tutampeleka nje ya nchi.Kwa hiyo anza kulifanyia jambo hili maandalizi”akasema Dr Joshua

“ Sawa Dr Joshua.Nitalifanyia kazi jambo hilo .” Akasema Dr Kigomba ambaye alionekana mchovu sana

“ Kitu kingine ambacho nataka nikuweke wazi ni kwamba pamoja na yote yaliyotokea na yatakayotokea biashara ile lazima ifanyike.Hakuna cha kuweza kutuzuia kuifanya biashara ile.Leo hii ninakwenda kuzungumza na wale jamaa ili waanze kuandaa fedha na kuzihamishia katika zile akaunti za nje.Tukisha hakikisha kwamba pesa imeingia katika akaunti zile tutawakabidhi mzigo wao ili tuachane kabisa na jambo hili na tuangalie mambo mengine kwani tayari biashara hii imeanza kuingiwa na vikwazo vingi.Vizingiti vimekuwa vingi mno na maadui wanaongezeka kila uchao.Hatutakiwi kuendelea kulivuta sana jambo hili ” akasema Dr Joshua
“ Uko sahihi Dr Joshua biashara hii lazima tuifanye haraka sana . Kila siku linaibuka jambo jipya.Tukivuta sana muda tutajikuta siku moja tunashindwa kabisa kuifanikisha kwa hiyo wakati ni sasa kama unavyoshauri”akasema r KIgomba

“ Kitu kingine ambacho nataka usisahau ,naomba uendelee kumchunguza Peniela.Ukumbuke lisemwalo lipo .Nataka tuwe na uhakika kwamba Peniela hana mahusiano yoyote na Elibariki.kama atakuwa na mahusino naye basi itakuwa rahisi sana kwetu kumpata Elibariki.Mtu aliyetoa taarifa za kunonekana kwa Elibariki nyumbani kwa Peniela ni mtu mwenye uhakika na hatupaswi kuzipuuza taarifa hizo.Tunatakiwa tuzifanyie kazi.” Akasema Dr Joshua
“ usijali mzee,leo hii hii ninaanza kulifanyia kazi hilo jambo.”akasema Dr Kigomba aliyeonekana kujawa na usingizi .Walifika katika makazi ya rais na kwa kuwa alikuwa amechoka sana akaingia chumbani kwake kujipumzisha.


*******



Kumepambazuka na siku mpya imeanza.Taifa limeamshwa tena na habari nyingine mpya ya shambulio lililopelekea vifo vya watu wanne pamoja na Flaviana mtoto wa rais kujeruhiwa kwa risasi.Magazeti mengi yaliandika kuhusiana na tukio lile .Wengine walilihusisha tuko lile na ujambazi baada ya mtu mmoja miongoni mwa wale waliofariki kugundulika kwamba ni jambazi sugu.
Peniela aliamka asubuhi na mapema kama kawaida yake na kuanza kujiandaa kwa ajili ya mizunguko ya siku.Siku hii alikuwa ameipanga kwa ajili ya kushughulikia suala la kupata hospitali ambayo John Mwaulaya atafanyiwa upasuaji.Baada ya kuoga akachukua simu na kumpigia Dr Joshua ili kumsisitiza na kumkumbusha kuhusu suala lile
“ Hallow Peniela” akasema Dr Joshua kwa uchoovu.Bado alikuwa na usingizi mwingi

“ Dr Joshua bado umelala? Sauti yako inaonyesha ni ya uchovu sana” akasema Peniela
“ Bado nimelala Peniela.Nimechoka sana”

“ Pole sana Dr Joshua.Siku nyingine sintakuchosha namna hii.” Akasema Peniela
“ Hapana peniela hukunichosha bali nimekesha hospitali”

“ Hospitali? ! Peniela akashangaa

“Ndiyo Peniela.Ina maana hujasikia kilichotokea? akauliza Dr Joshua
“hapana Dr Joshua sijasikia chochote,.nini kimetokea?

“ Mwanangu Flaviana amepigwa risasi jana usiku .”

“ What ?! peniela akastuka
“ Flaviana amepigwa risasi jana usiku na hali yake si nzuri.Nimekesha hospitali na nimerudi asubuhi hii ndiyo maana unaona ninaongea kichovu hivi” akasema Dr Joshua
“ Ouh my God ! Pole sana Dr Joshua.Pole sana.Anaendeleaje kwa sasa?

“ Ahsante sana Peniela.Kwa sasa hali yake si nzuri hata kidogo japokuwa amefanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi lakini bado hali yake si nzuri.Bado yuko katika uangalizi maalum.”

“dah ! Pole sana jamani.Nani lakini aliyefanya jambo hili? Akauliza Peniela
“ Ni mtu ambaye huwezi kumdhania kabisa”
‘ Mmekwisha mfahamu? Akauliza Penny

“ Ndiyo tumemfahamu na kwa sasa jeshi la polisi linamsaka kila kona ya nchi.Ni mumewe jaji Elibariki”

“ Elibariki ?!!..Peniela akastuka sana

“ Ndiyo .Ni Elibariki aliyefanya shambulio hilo” akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua mna hakika kwamba ni Elibariki ndiye aliyefanya shambulio hilo?
“ Tuna kila ushahidi wa jambo hilo na kwa sasa vyombo vyote vya dola vinamsaka na tuna imani haitafika jioni ya leo kabla hajatiwa nguvuni.”

“ Mhh ! nimestuka sana kusikia kwamba Elibariki ndiye aliyefanya kitendo hicho.Japokuwa simfahamu vyema lakini anaonekana ni mtu mpole na ambaye huwezi kumdhania kama anaweza kufanya kitendo kama hicho.Pole sana dr Joshua”
“ Ahsante sana Peniela nimekwisha poa.”
“ Natamani ningekuwa karibu yako nikufariji katika wakati huu mgumu ulio nao”akasema Peniela
“ Ahsante sana Peniela kwa kunijali.Ndiyo maana nikakupa ilenyumba.Kama ungekuwa pale ingekuwa rahisi kwangu mimi kuja na kulala pale lakini hutaki kuishi pale sijui kwa nini”
“usijali Dr Joshua kuna mambo nayaweka sawa halafu nitahamia katika ile nyumba.Hata mimi sipendi kukaa mbali na wewe” akasema Peniela

“ Nitafurahi sana Peniela kama nitakuwa na uwezo wa kukupata kila pale ninapokuhitaji.Unajua hizi kazi zetu zinahitaji faraja kubwa kwa hiyo kila pale ninapokuwa nimechoka ninahitaji mtu wa kuniliwaza na katika dunia hii yote nimekuchagua wewe peke yako na ndiyo maana niko tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili yako Peniela”
“ Ahsante sana Dr Joshua umekuwa unanijali sana na umedhihirisha unanipenda kweli.Nakuahidi hata mimi nitakupenda daima.”
“ Nafurahi kuisikia ahadi hiyo Peniela.”
Kikapita kimya kifupi Peniela akauliza

“ Dr Joshua najua kwamba uko katika matatizo laini naomba kukuuliza vipi kuhusu lile suala la hospitali? Umelifanyia kazi tayari?
“ ouh samahani sana Peniela.Sikuwa nimelifanyia kazi kutokana na mambo yaliyotokea lakini naomba unipe kama dakika kumi hivi nizungumze na daktari mkuu wa ile hospitali yetu halafu nitakufahamisha.Samahani sana kwa kuchelewa kulifanyia kazi suala hili” akasema dr Joshua
“ Usijali dr Joshua” akajibu Peniela na kukata simu na kuitupa kitandani huku akionekana kuwa na mawazo mengi

“ hapana si kweli kabisa.Elibariki hawezi akafanya jambo kama hilo la kutaka kumuua mke wake.Nina hakika hiki ni kitu kimepangwa na Dr Joshua na wenzake ili waweze kumkamata kirahisi Elibariki.I wont let that happen.I must save him,.” Akachukua simu yake na kuzitafuta namba za simu za Mathew akampigia.
“ hallow Mathew habariza asubuhi? Akauliza Peniela

“ habari za asubuhi nzuri ,unaendelaje?
“Ninaendelea vizuri sana.Ninaweza kuongea na elibariki?
“ Ok subir naomba unipe kama dakika mbili nimpelekee simu”
“ Ahsante sana Mathew.” Akajibu Peniela na kukata simu

“ dr Joshua ni mtu mwenye roho ya kishetani sana na kuanzia sasa inanibidi niwe naye makini mno.Kama ameweza kumuua mke wake basi kwake kuutoa uhai wa mtu ni kitu kidogo sana.Kwa nini anamtesa Elibariki kiasi hiki? Akawaza Peniela na simu anayotumia k uwasiliana na rais ikaita

“hallo dr Joshua” akasema Peniela

“ Peniela tayari nimekwisha wasiliana na daktari mkuu wa pale anaitwa Dr Henry sibowa.Ukifika onana naye tayari nimekwisha mueleza kila kitu “
“ nashukuru sana dr Joshua.Narudia tena kukupa pole kwa matatizo makubwa yaliyokupata .Niko pamoja nawe katika wakati huu mgumu”
“ Nashukuru sana Peniela.Nitakufahamisha baadae nini kinaendelea” akasema Dr Joshua na kukata simu

“ Kuna ule msemo unaosema kwamba kila jambo hutokea kwa sababu maalum.Inawezekana hata tukio hili la kushambuliwa Flaviana limet okea kwa sababau maalum.Sifurahii jambo hili lakini yawezekana ikawa ni mipango ya Mungu ili niweze kuwa na Elibariki.Ninampenda Elibariki na ikitokea kama mke wake akafariki basi nafasi yangu kwake ni kubwa sana.Ni mwanaume ambaye ninataka kuanza naye maisha mapya baada ya kuondoka Team SC41.” Akawaza Peniela na kuchukua tena simu akampigia Mathew
“ hallow Peniela” ikajibu sauti ya upande wa pili ambayo aliitambua ilikuwa ya Elibariki
“ Elibariki my love,uko salama? Unaendelea vizuri? Akauliza Peniela

“ Ninaendelea vizuri Peniela.Vipi wewe unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri sana japokuwa kuna matatizo yametokea jana usiku”
“ tayari ninazo taarifa za kilichotokea jana” akasema Peniela

“ Unazo taarifa za kilichotokea jana?
“ Ndiyo tayari ninazo na ninakupa pole sana kwa mkeo kushambuliwa.”

“ Ahsante sana Peniela.Mke wangu alishambuliwa na sifahamu hadi hivi sasa hali yake inaendelaje? Akauliza Elibariki

“ yuko hospitali na hali yake si nzuri.alfanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi jana usiku nab ado yuko katika uangalizi maalum”

“ Thank you Lord.” Akasema Elibariki
‘ Elibariki did you shoot her? Akauliza peniela

“ Peniela!! Jaji elibariki akashangaa

“ Swali gani hilo unaniuliza ? I think You know me better that anyone,do you think I can shoot my wife? Akauliza jaji Elibariki

“ tell me its not true and I’ll believe you” akasema Peniela

“ Ahsante kwa kuniamini.Siwezi kufanya jambo kama hilo.Kilichotokea ni kwamba nilimpigia simu Flaviana jana usiku na kuomba kuonana naye.Kuna kitu Fulani nilikua nakihitaji toka kwake.Sikujua kama kuna watu walikuwa wanamfuatilia ambao nahisi walifahamu kwamba anakuja kuonana na mimi na ndipo lilipotokea shambulio lile na Flaviana akapigwa risasi.Ni kweli mimi na Flaviana kwa siku za hivi karibuni tumekuwa na tofauti kubwa lakini katu siwezi kuinua silaha na kumpiga risasi.Yule ni mkewangu nasiwezi kumfanyia jambo kama hilo” akasema Elibariki

“ Pole sana Elibariki.Nadhani hizi ni njama za wale wanaoitafuta roho yako usiku na mchana.Naomba Elibariki kwa sasa utulie tu ndani na usionekane kabisa huku nje kwa sababu taarifa zilizosambaa na ambazo zimelifikia jeshi la polisi ni kwamba wewe ndiye uliyepanga shambulio lile na hivi sasa jeshi la polisi liko katika msako mkali kukutafuta kwa hiyo hali si nzuri huku nje”

“ Kwa hiyo kibao kimenigeukia mimi? Elibariki akashangaa

“ Ndiyo Elibariki.kwa sasa wewe ndiye unayesakwa ukituhumiwa kuhusika na shambulio lile”
“ Ahsante sana kwa taarifa hiyo Peniela.Nitazingatia ushauri wako” akasema jaji Elibariki

“ Elibariki ninahitaji sana kukuona.Najua uko katika wakati mgumu na unahitaji sana faraja.When will I see you? Akauliza Peniela

“ Peniela kwa sasa itakuwa ngumu kidogo kuniona lakini nakuahidi kwamba baada ya mambo kutulia nitatafuta nafasi mimi na wewe tutaonana.Peniela pamoja na matatizo yote yaliyotokea lakini bado uko moyoni mwangu bado umeitawala akili yangu kwa hiyo usijali,tuzidi kuombeana uzima na siku moja tutaonana” akasema jaji Elibariki
“ nashukuru sana Elibariki.Nakupenda sana na tafadhali kuwa mwangalifu.Nitakuwa nikiwasiliana nawe mara kwa mara kujua hali yako” akasema peniela na kukata simu

“ Afadhali sasa ninasikia faraja baada ya kuongea na Elibariki.Ninamuonea huruma sana kwa mambo yanayomkuta.Nitajitahid kufanya kila linalowezekana ili kumsaidia.Kwa sasa ngoja nishughulikie kwanza suala la John .Halafu nimekumbuka kitu,kwa mujibu wa Amos nikwamba leo ndiyo siku ambayo atanikutanisha na Dr Kigomba .Natakiwa nijiandae.” Akawaza Peniela

“ Nasikitika sana kwa kugeuka kuwa chombo cha kuwastarehesha watu lakini mambo haya yote yatakwisha muda si mrefu sana .Tuko katika hatua za mwishoni kabisa kuikamilisha operesheni yetu na nitaanza maisha mapya .Nataka nianze maisha yangu mapya nikiwa na mwanaume ambaye ninampenda kwa moyo wangu wote Elibariki” akaendelea kuwaza Peniela huku akijiandaa kuelekea hospitali


*******


Hali ya John mwaulaya iliendelea kuimarika siku hadi siku na kwa asubuhi hii ya leo aliamka akiwa na nguvu za kutosha kiasi kwamba aliweza hata kuinua mguu na kukanyaga chini
“ Hizi ni dalili njema sana kwa afya yangu kuboreka namna hii.sitaki kufa mapema kwa sababu kuna mambo mengi bado natakiwa kuyafanya kwa Peniela.Lazima kabla ya kufa nihakikishe kwamba maisha yake yanakuwa ya kawaida tena.Hilo ndilo jambo kubwa ambalo ninaweza kulifanya ili kuyajenga tena maisha yake kwa sababu ni mimi ndiye niliyeyaharibu.Pen……….” John akakatishwa mawazo yake na Josh aliyeingia mle chumbani
“ karibu Josh” akasema John
“ mzee nimekuja kukutaarifu kwamba ninakwenda kuifanya ile kazi uliyoniagiza jana nikaifanye leo ya kumteka Jason yule wakili wa Peniela “ akasema Josh

“ Ouh Good.Kumbe unakumbu kumbu sana .Hakikisha unampata leo na atueleze ni alifahamuje kama Elibariki yuko pale kwa Peniela na kwa nini aliamua kuripoti polisi .?.Kitendo kile kingehatarisha usalama wa Peniela na hata wa kwetu sote.Lazima tuifahamu sababu ya yeye kufanya vile “akasema John
“ Usijali mzee nitampata leo na atatueleza kila kitu” akasema Josh ,kijana ambaye kwa hulka yake si muongeaji sana.Josh akageuka na kuanza kupiga hatua kutoka mle ndani na alipofika mlangoni John akamuita akageuka
“ Josh please make him talk” akasema John na Josh akaitika kwa kichwa kuonyesha kukubaliana na John.

“ Josh ni kijana mtiifu sana na anajua kuifanya kazi yake vyema.Huyu naye nitahakikisha ninamuacha sehemu nzuri pia naye awe na maisha mazuri.” Akawaza John

“ lakini huyu Jason aligundua vipi kama Elibariki yuko pale kwa Peniela? Ninahitaji sana kujua.Ninahisi Josh ataifanya kazi yake vyema na tutafahamu kila kitu.Nimemkumbuka Peniela ngoja niwasiliane naye asubuhi hii nijue maendeleo yake” akawaza John halafu akabonyeza kitufe cheusi chini ya kitanda chake akaingia kijana mmoja mwenye taaluma ya udaktari na ambaye ndiye amekuwa akimuhudumia John kwa muda mrefu .John akamuomba ampatie simu na akampigia Peniela

“ Hallow baba” akasema Peniela

“ Hallow Peniela unaendeleaje? Akauliza John
“ Ninaendela vizuri sana baba .Vipi wewe hali yako?

“ hali yangu nzuri na kila siku ninazidi kupata nguvu’
‘ Nafutahi kusikia hivyo.Kwa hivi sasa ninaelekea hospitali kuonana na daktari kwa ajili ya kufanya maandalizi ya ule upasuaji” akasema Penny
“ Ouh Peniela nakushukuru sana kwa namna unavyonishughulikia.”

“ usijali john,lazima nihakikishe kwamba unapona na unarejea katika hali yako”

“ ahsante sana ,vipi Elibariki anaendeleaje? umefanikiwa kuwasiliana naye?

“ Nimewasliana naye asubuhi hii na hali yake ni nzuri lakini bado yuko katika matatizo makubwa

“Matatizo gani tena?akauliza John
Peniela akamsimulia kila kitu,John akasikitika sana.
“ Penny ninachoweza kukushauri kwa sasa usiwaze sana kuhusu Elibariki nina uhakika mahala aliko yuko salama na nitaangalia baadae namna ya kumsaidia.”

“ Ahsante sana baba,nitashukuru kwa sababu ninampenda Elibariki na yuko katika wakati mgumu sana.Kuna jambo nimekuwa nikilifikiria”

“ jambo gani penny?

“ Wewe una mtandao mkubwa wa watu unaofahamisha nao,kwa nini basi tusimuhamishe Elibariki na kumpeleka nje ya nchi? Nadhani ni jambo ambalo tunatakiwa tulifanye” akasema Peniela

“ Hilo si wazo baya.Naomba uniachie suala hilo nilifanyie kazi halafu nitakupa majibu kama tunaweza tukamuondoa Elibariki hapa nchini”
“Nitashukuru sana baba kama utanisaidia kwa hilo” akasema Peniela na kukata simu
“ Kwa Peniela siwezi kusema hapana.Lazima nimsaidie kumuondoa Elibariki hapa nchini.Uwezo huo ninao ” akawaza John


*******



Jaji Elibariki baada ya kumaliza kuongea na Peniela simuni akatoka na kumfuata Mathew jikoni ambako alikuwa akiandaa mlo wa asubuhi
“ Karibu Elibariki.Anasemaje Peniela? Akauliza Mathew

“ Kuna jambo ameniambia limenistua kidgo”
“ Amekwambia nini?

“ Amesema kwamba taarifa zimesambaa kwamba mimi ndiye niliyefanya shambulio lile la jana nikishirikiana na mtandao wa majambazi na kuua watu wanne pamoja na kumjeruhi Flaviana kwa risasi.Kwahiyo kwa hivi sasa jeshi la polisi linanisaka katika kila kona ya nchi hii.I have no where to run.Mathew nimeogopa sana.Maisha yangu yatakuwaje? Unadhani jeshi la polisi watashindwa kufuatilia na kugundua kwamba niko hapa? Akauliza jaji Elibariki.Mathew akatabasamu kidogo na kuendelea na kazi zake

“ Relax Eli..Relax..”

“ Mathew this is a serios matter.!!..jeshi lapolisi kwa sasa nguvu yao yote wameielekeza kwangu.Ninatafutwa kila kona.Unadhani nitaweza kuwa na amani tena? Akauliza Elibariki.Mathew hakujibu kitu akaendelea na kazi zake
“ Mathew can you stop what you are doing and to me?
"Nimekwishakusikia Elibariki.Ninakuelewa na ndiyo maana nikakwambia kwamba relax.Ngoja kwanza tupate kifungua kinywa halafu tuanze kupanga kazi za leo”
“ Mathew ,kifungua kinywa ni muhimu kuliko maisha yangu? Look,I’m sorry about yesterday.najua labda umekasirika kwa kitendo nilichokifanya jana kwa kuachia ile risasi na kuhatarisha uhai wetu lakini wewe ndiye tumaini langu.Tafadhalinaomba unisikilize” akasema Elibariki
“ Elibariki ,this is a war and we have to fight back kwa hiyo lazima tujipange vizuri mapambano yetu.Hili ni suala dogo sana na muda si mrefu litafika mwisho kwa hiyo usihofu” akasema Mathew na kuendelea kuandaa kifungua kinywa .Jaji Elibarii akarejea chumbani kwake alikuwa amekasirika sana kwa namna Mathew alivyolichukulia suala lile

“ Sijui Flaviana ana hali gani huko aliko,nitamani sana kufahamu anaendeleaje lakini siwezi.Maisha yangu yamebadilika na ninaishi kama mfungwa” akawaza.
Dakika ishirini baadae wote wakajumuika pamoja katika mlo wa asubuhi na baada ya hapo wakangia katika chumba cha kazi.
“ Ok Elibariki sasa tunaweza kuongea ” akasema Mathew
“ Mathew ni kama vile nilivyokwambia kwamba tayari taarifa zimesambaa kila kona ya nchi kwamba ni mimi nidye niliyepanga shambulio la jana na kwa hivi sasa jeshi la polisi linanisaka katika kila kona ya nchi.”
“Elibariki nadhani nguvu ya watu hawa wanaokutafuta umeiona na kwa sasa wameamua hata kulitumia jeshi la polisi kukutafuta .Wewe ni mtu hatari sana kwao na kuendelea kwako kuwa hai unawanyima usingizi.Kitu tunachotakiwa kukifanya ni kupambana nao.Tutaanza kwanza kuifanyia kazi taarifa ile ya kuhusiana na kifo cha Dr Flora .katika taarifa hii kumeorodheshwa majina ya madaktari waliofanya uchunguzi huo.Tutalipitia jina moja moja na tuhakiki kama ni kweli walishiriki katika uchunguzi huo na tutapata jibu .Mimi na Anitha tutaifanya kazi hii leo na mpaka jioni ya leo tutakuwa na majibu kuhusiana na taarifa hii kama ni ya kweli ama vipi na baada ya hapo tutajua nini kitafuata.” Akasema Mathew
“ Kuhusu zile karatasi zilizoibwa ikulu ambazo tumeshindwa kuzielewa nimemtumia rafiki yangu mmoja yuko katka chuo kikuu kimoja cha sayansi nchini Israel na baadae ninategemea kupata majibu kuhusiana na nini kilichoandikwa ndani ya karatasi zile kiasi cha kuzifanya ziwe na thamani kubwa kiasi kile.Mpaka jioni ya leo tutakuwa na majibu yote na tutajua nini kitafuata.Kwa hiyo usihofu Elbariki tutapambana nao.” Akasema Mathew
“ Ahsanteni sana Mathew na Anitha.Ninawaomba mtakapokuwa katika mizunguko yenu msisahau kutafuta habari kamili kuhusu maendeleo ya mke wangu.”

“ Tutajitahidi Elibariki lakini kwa wakati huu lazima tujiandae kwa lolote lile litakalotokea” akasema Mathew


TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SEASON 2


SEHEMU YA 27

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Kitu tunachotakiwa kukifanya ni kupambana nao.Tutaanza kwanza kuifanyia kazi taarifa ile ya kuhusiana na kifo cha Dr Flora .katika taarifa hii kumeorodheshwa majina ya madaktari waliofanya uchunguzi huo.Tutalipitia jina moja moja na tuhakiki kama ni kweli walishiriki katika uchunguzi huo na tutapata jibu .Mimi na Anitha tutaifanya kazi hii leo na mpaka jioni ya leo tutakuwa na majibu kuhusiana na taarifa hii kama ni ya kweli ama vipi na baada ya hapo tutajua nini kitafuata.” Akasema Mathew

“ Kuhusu zile karatasi zilizoibwa ikulu ambazo tumeshindwa kuzielewa nimemtumia rafiki yangu mmoja yuko katka chuo kikuu kimoja cha sayansi nchini Israel na baadae ninategemea kupata majibu kuhusiana na nini kilichoandikwa ndani ya karatasi zile kiasi cha kuzifanya ziwe na thamani kubwa kiasi kile.Mpaka jioni ya leo tutakuwa na majibu yote na tutajua nini kitafuata.Kwa hiyo usihofu Elbariki tutapambana nao.” Akasema Mathew

“ Ahsanteni sana Mathew na Anitha.Ninawaomba mtakapokuwa katika mizunguko yenu msisahau kutafuta habari kamili kuhusu maendeleo ya mke wangu.”

“ Tutajitahidi Elibariki lakini kwa wakati huu lazima tujiandae kwa lolote lile litakalotokea” akasema Mathew


ENDELEA…………………….


Josh kijana ambaye kwa haiba yake anaonekana ni kijana mpole sana,aliwasili katika jengo zilimo ofisi za kampuni ya uwakili ya Jason.Alichukua takribani dakika mbili hivi kablaya kushuka akiangalia hali ya usalama ilivyo eneo lile na kama kulikuwa na kamera zozote za ulinzi zilizofungwa .Aliporidhika kwamba eneo lilikuwa salama akafungua mkoba wake akatoa uturi mzuri na kujipulizia akajiangalia na kuhakikisha yuko katika muonekano mzuri akashuka garini.Kwa yeyote ambaye angemuona Josh asubuhi hii lazima angedhani ni kijana anayefanya kazi nzuri na yenye maslahi mazuri kwa namna alivyovaa na hata namna anavyotembea kwa kujiamini.Aliingia ndani ya ofisi zile na kupokelewa na mwanadada mmoja aliyevaa mavazi yaliyomkaa vyema.
“ habari yako kaka” akasema yule mwanadada

“ habari nzuri dada yangu ,habari za hapa?

“karibu sana.Nikusaidie nini?

“ Ninahitaji kuonana na wakili Jason”

“ Una miadi naye siku ya leo?

“ Hapana sina miadi naye lakini nina tatizo ambalo ninahitaji kuonana naye”

“ sawa kaka lakini Jason ana matatizo binafsi na leo ni siku ya nne Jason hajafika hapa kwa hiyo kama una tatizo la kisheria na unahitaji msaada unaweza ukashughulikiwa na mawakili wengine walioko hapa ambao nao wamebobea pia katika masuala ya kisheria” akashauri yule mwanadada.Josh akafikiri kidogo na kusema

“ Lini Jason atarudi ofisini kwake? Ninahitaji kumuona yeye tu”

“ Hatuna uhakika kwa kweli lini atarudi na wala hajatuambia chochote.Unaweza ukatuachia mawasiliano yako ili atakaporejea basi tukutaarifu kama shida yako inamuhitaji yeye pekee” akasema yule dada.Josh akafikiri na kusema
“ Basi isiwe taabu nitakuwa nikija mara kwa mara kumtafuta na siku moja ninaweza kumbahatisha” akasema Josh na kugeuka akaanza kuondoka.Alipofika mlangoni akageuka na kurejea tena kwa yule dada
“ samahani dada unaweza ukanielekeza nyumbani kwake ili nikaonane naye? Akasema Josh na yule dada bila kuwa na wasi wasi wowote akamuelekeza Josh nyumbani kwa Jason.
Ilimchukua Josh zaidi ya saa moja kufika nyumbani kwa Jason.Akashuka garini na kubonyeza kengele ya getini .Baada ya dakika mbili mlango mdogo wa geti ukafunguliwa na kijana mmoja aliyekuwa amevalia nadhifu kabisa na ilionekana kama vile alikuwa akihitaji kutoka

“ habari yako kaka” akasema Josh

“ habari nzuri sana,karibu”
“ Ahsante sana.Ninaitwa josh ,nimeelekezwa kwamba hapa ni nyumbani kwa wakili Jason”
“ Ndiyo mimi.karibu sana” akasema Jason
“ Ahsante sana Jason.Nimefika ofisini kwako nilikuwa na shida ya kiofisi nikaambiwa kwamba una siku kama nne hivi hujaonekana pale kazini.Niliambiwa kama nina shida ninaweza kumpata wakili mwingine lakini shida yangu mimi ilikuwa ni wewe tu.Sina imani kabisa na wakili mwingine zaidi yako” akasema Josh na kumfanya Jason atabasamu

“ karibu ndani Josh” akasema Jason na Josh akaingia ndani akakaribishwa katika sebule kubwa.

‘ Jason samahani kama nimekatisha shughuli zako naona ulikuwa katika mkao wa kutoka lakini kama hutajali ninaomba unisikilize japo kwa dakika tano tu”

“ usijali Josh.Una tatizo gani?

“ Ninafanya kazi katika kampuni moja ya madini ambayo ina migodi yake mitatu katika mkoa wa geita lakini ofisi yake kuu iko hapa Dar es salaam.Kampuni yangu imekuwa na mgogoro na serikali kuhusiana na baadhi ya vipengele Fulani viliyomo katika mkataba wa uchimbai wa madini.kwa sasa tunafikiria kuifikisha serikali mahakamani kwa kosa la kukiuka mkataba.li tuweze kushinda kesi hii tunahitaji wakili ambaye ni mahiri na ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja kama ulivyo wewe.Kesi uliyoisimamia ikamalizika hivi karibuni ya yule msichana ,imetudhihirishia kwamba wewe ni wakili ambaye utatufaa sana katika kesi hii.Kwa hiyo Jason nimekuja kukuomba uwe wakili wetu katika kesi hii na kama hutajali basi tuongozane hadi ofisini kwetu kwani wakurugenzi wetu wanakusubiri kwa hamu ili uweze kuelezwa kwa kina kuhusiana na jambo hili.Je uko tayari kwa kazi hii Jason? Kumbuka ni kazi yenye maslahi manono sana” akasema Josh.Jason akamtazama Josh kwa makini na kusema

‘ Nadhani nikishauona mkataba huo na vipengele ambavyo vina utata ninaweza nikasema jambo lakini siwezi kutoa tamko lolote kabla ya kuupitia mkataba huo.” Akasema Jason
“ Ok vizuri Jason.kama hutajali tunaweza kuongozana asubuhi hii hadi ofisini kwetu na ukaupitia mkataba huo kwa umakini mkubwa” akasema Josh

“ Ok sawa tunaweza kuongozana” akasema Jason halafu wakatoka kila mmoja akaingia katika gari lake wakaondoka Jason akilifuata gari la Josh
Moja kwa moja walielekea hadi nyumbani kwa john Mwaulaya.Geti likafunguliwa wakaingia ndani
“ Jason karibu sana hapa ni nyumbani kwa mkurugenzi wetu mkuu na ndipo mikataba yote muhimu huwa inahifadhiwa.Tukitoka hapa tutaelekea ofisini ” akasema josh na kumshangaza kidogo Jason kwani hakutegemea kama wangekuja hapa nyumbani kwa mtu badala ya ofisini kama walivyokuwa wamekubaliana.waliingia sebuleni Josh akamuomba Jason aketi sofani na amsubiri kwa dakika moja ili akamtaarifu mkurugenzi wake kwamba wamefika.Baada ya dakika mbili Josh akarejea na kumuomba Jason amfuate ,wakapanda ghorofani.Josh akaufungua mlango mmoja akaingia na kumkaribisha Jason.katika chumbakile kulikuwa na meza na viti viwili.Josh akamuomba Jason aketi kitini wakati wakimsubiri mkurugenzi wake.Mara tu Jason alpoketi kikatokea kitu ambacho hakukitarajia.Josh alichomoa bastora na kumuelekezea.Jason akabaki akishangaa

“ Josh..Wh..what’s going on? Akauliza Jason huku akitetemeka

“ Give me your phone and everything” akasema Josh na kwa haraka Jason akatoa simu yake na kila kitu akaviweka mezani Josh akavichukua.

“ Josh kuna nini? Kwa.n…” Jason maneno yakashindwa kutoka.
“ Jason naomba unisikilize kwa makini sana.Nimekuleta hapa kuna mambo ninayotaka kuyafahamu toka kwako.Kama hutanieleza ukweli hutatoka humu ndani salama.” Akasema Josh huku ile sura yake ya upole ikiwa imebadilika na sasa alikuwa ana sura ya kikatili ya kiuaji.Jason akazidi kutetemeka.Ilikuwa ni m ara yake ya kwanza kuelekezewa bastora.

“ Josh..tafa.fadhali naomba uniambie ..unataka nini? Nitakueleza kila kitu unachokihitaji lakini tafadhali naomba usinidhuru” akaomba Jason.

“ Nitarejea baada ya dakika mbili.” Akasema Josh na kutoka akaufunga ule mlango na kuelekea moja kwa moja katika chumba cha John mwaulaya
“ Mzee tayari ile kazi nimeikamilisha.Jason nimempata kwa wepesi sana na yuko hapa ndani katika chumba cha mahojiano”

“ Good ! Josh wewe nikijana hodari sana.Ahsante sana.Umeshaanza kumuhoji?
“ Hapana mzee bado sijaanza kumuhoji”

“Please make him talk” akasema John mwaulaya.Josh akaiwasha luninga moja kubwa kati ya luninga zatu kubwa zilizokuwa ukutani na John akaweza kuona kila kinachoendelea katika chumba kile cha mahojiano.Jason alikuwa amekaa kitini akitetemeka kwa uoga

“ He’s scared.Atatueleza kila kitu” akasemaJosh na kisha akatoka na kueleka chumbani kwake akabadili nguo na kuchukua baadhi ya vitu ambavyo huvitumia katika kumtesa mtu wakati wa mahojiano halafu akaingia tena katika chumba alimo Jason ambaye alipomuona tu akatetemeka sana na kuema

“ josh ..josh ..Please don’t hurt me..Nitakueleza kila kitu unachokihitaji” akasema Jason.Josh hakujibu kitu akavipanga vifaa vile vya kutesea mezani na kuzidi kumuogopesha Jason

“ Jason mimi si mtu mkatili kama unavyodhani na hata sura yangu haionyeshi kama mimi ni mkatili lakini huwa ninalazimishwa kuwa katili pale ambapo mtu ninayemuhoji akanidanganya au akashindwa kutoa ushrikiano kwa hiyo naomba usinilazimsihe niwe mkatili.Ninaoma unieleze ukweli wa kila nitakachokuuliza” akasema Josh
“ Nitakueleza ukweli wa kila kitu Josh ila tafadhali naomba usinitese”akasema Jason.Josh akamtazama na kusema
“ Unamfahamu jaji Elibariki?

‘ Ndiyo ninamfahamu.Nilimfahamu wakati wa kesi ya Peniela kwani yeye ndiye aliyekuwa akiisikiliza kesi ile.Baada ya kesi kukamilika tukawa marafiki”

“ Good.”akasema Josh halafu akamtazam tena jason kwa makini na kumuuliza

“ jaji Elibariki alinusurika kuuawa na watu wasiojulikana hivi majuzi na mpaka sasa hajulikani alipo,unafahamu mahala aliko?
Jason akakaa kimya ,akashindwa kujibu

“ Jason unafahamu mahala aliko jaji elibariki hivi sasa? Akauliza tena Josh
“ hapana sifahamu mahala aliko” akajibu Jason
“ Unataka kunilazimisha nianze kukutesa mapema Jason.Naomba usinidanganye tena.Jana kuna taarifa imeripotiwa polisi kwamba jaji Elibariki yuko kwa Peniela na wewe ndiye uliyeipeleka taarifa hiyo polisi,kwa nini ulifanya hivyo na ulifahamuje kama jaji Elibariki yuko kwa peniela?
Swali lile likamtoa jasho Jason.
“ Sikuwa nikifahamu mahala Elibariki alipo hadi nilipozipata taarifa hizo jana jioni kwa Mathew nilipokuwa nyumbani kwake baada ya kutoka kumzika Noah kijana aliyeuawa katika shambulio lile alilonusurika Elibariki.Mathew ndiye aliyenitaarifu kwamba Elibariki yuko kwa peniela.Nilikasirika sana kusikia kwamba Elibariki yuko kwa Peniela na nilitaka kumuondoa pale na ndiyo sababu nikaenda kutoa taarifa hizi polisi.” Akasema Jason

“ Huyu mathew ni nani? Alijuaje kama Elibariki yuko kwa Peniela? Akaulizia Josh na Jason akasita kidogo kujibu

“ Jason naomba tafadhali usinilzimishe niwe mkali.Nijibu huyu Mathew ni nani?

“ Nilimfahamu mathew kupitia Elibariki kwani ni marafiki wakubwa na Elibariki ndiye aliyenipigia simu Mathew kumfahamisha kwamba yuko kwa Peniela.”
“ Mathew anafanya kazi gani? Akauliza Josh
“ hapanasifahamu kazi yake kwani nimekutanishwa naye na jaji Elibariki kwa hiyo sifahamu kazi yake lakini kwa mujibu wa Elibariki Mathew aliwahi kufanya kazi katika idara ya ujasusi miaka ya nyuma kidogo na akaacha baada ya familia yake kuteketea kwa moto ”
John mwaulaya aliyekuwa akifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea kupitia Luninga akastuka sana kwa kauli ile ya Jason na kubonyeza kitufe cheusi kilichokuwa chini ya kitanda chake na daktari wake akatokea mara moja.

“ Martin Mpigie simu Josh” akasema John na bila kuchelewa martin akachukua simu na kumpigia Josh

“ hallow Martin” akasema Josh
“ Josh mzee anataka kuongea nawe “ akasema martin na kumpatia simu John.
“ Hallo mzee” akasema Josh

“ Josh muonyeshe huyo jamaa zile picha za jana za wale watu wawili tulizozinasa katika kamera nyumbani kwa Peniela .Muulize kama Yule mwanaume ndiye Mathew ” akasema John na Josh akatoka mle chumbani akaenda kuchukua simu yake na kumuonyesha Jason picha ya Mathew na Anitha iliyochukuliwa katika kamera nyumbani kwa Peniela.Jason akastuka sana baada ya kuona picha zile.

“ Watu hawa ni akina nani? Wana mahusiano gani na Peniela? Kwa nini wanataka kufahamu kuhusu Mathew? Akawaza Jason
“ Unawafahamu watu hawa wawili? Akauliza Josh
“ Ndiyo. huyu mwanaume ni Mathew na huyu mwanamke anaitwa Anitha rafiki yake” akasema Jason. John Mwaulaya akatokwa na jasho.Kuna kitu alikikumbuka.

“ Ndiyo maana baada ya kuona sura ile kumbu kumhu zilikuja kama nimewahi kuiona mahala ile sura.? Sasa nimemkumbuka vizuri.Aliposema kuhusiana na familia yake kuteketea kwa moto ndipo nimekumbuka nimekumbuka kuhusu lile tukio la moto lililotokea kipindi kile.Mathew alinusurika kipindi kile katika shambulio tulipowashambulia kikosi cha makachero waliokuwa wakitaka kumkamata mwanamama gaidi aliyeingia nchini.Ni yeye pekee aliyenusurika katika shambulio lile na haikuishia pale bali tuliiteketeza na familia yake yote ili tuweze kumkamata kirahisi lakini alitoweka na sikuwahi kupata taarifa zake tena hadi leo hii nilipomuona kwa Peniela.Amenistua sana kwani huyu ni mu hatari sana japokuwa sina hakika kama anafahamu ni team SC41 ndio waliofanya shambulio lile baya na kuwaua wenzake wote.Japokuwa ni miaka imepita lakini bado Mathew anaendelea kuwa ni mtu hatari sana kwetu na hatakiwi kabisa kukaa karibu na Peniela wala kuzoeana naye.Lazima tahadhari za haraka zichukuliwe ili kumuweka Penny mbali watu hawa waliomzunguka.Ninahisi labda Mathew anataka kumchunguza Peniela na anamtumia Elibariki katika kumchunguza Penny.Hapana lazima tufanye jambo haraka sana” akawaza John na kubonyeza kile kitufe cheusi cha kengele ya kuita wasaidizi wake na Martin akaingia mara moja mle ndani.

“Martin mpigie simu Josh,ninahitaji kumuona haraka sana “ akasema John na Martin akampigia simu Josh akamtaarifu kwamba John anahitaji kumuona haraka.Kutokana na mwito ule wa haraka Josh akatoka mbio katika kile chumba akaelekea chumbani kwa John.Kosa alilolifanya Josh ni kuacha kila ktu pale mezani ikiwamo simu yake .

“ Lazima nitafute msaada wa haraka sana,vinginevyo ninaweza kuuawa.Watu hawa wanaonekana wana mahusiano na Peniela na inaonekana wanafuatilia kila kitu kinachoendelea pale kwa Peniela na ndiyo maana wameweza kuzipata picha za Mathew na Anitha kupitia kamera walizozitega pale kwa Peniela.Ni Peniela pekee anayeweza kuniokoa toka kwa watu hawa kwani nina hakika anawafahamu.Kwa bahati nzuri ninazifahamu namba zake kwa kichwa.” Akawaza Jason na kwa haraka akachukua simu ya Josh iliyokuwa mezani akaandika namba za Peniela na kupiga simu ikaanza kuita
“ c’mon Peniela pick up the phone..!! akaomba Jason na mara simu ikapokelewa

“ hallo Josh” akasema Peniela na kumstua Jason
“ Kumbe Peniela anazifahamu hadi namba za simu za Josh.Kumbe hawa ni watu wake.Peniela ninani hasa? Akawaza Jason

“ Hallow Josh” akaita tena peniela
“ peniela,its me Jason.”

“ Jason?!!! Peniela akapatwa na mshangao mkubwa sana.

“ Ndiyo Penny.”
“ Imekuaje uko na simu ya Josh?! Akaulzia Peniela

“ Peniela please help me.Nimetekwa na huyu anayeitwa Josh “

“ what? Akauliza Peniela kwa mshangao

“ Peniela tafadhali naomba unisaidie nimetekwa na kuletwa katika hili jumba ,ninaulizwa maswali mengi kuhusiana na Mathew na Elbariki.Sina hakika kama nitatoka salama ndani ya jumba hili.Josh ametoka kidogo amesahau simu yake nimepata mwanya wa kukupiga.Please help me Peniela.” Akasema Jason .wakati akiongea na Peniela Jason hakuwa na habari kwamba alikuwa akionekana kupitia luninga kubwa iliyokuwamo chumbani kwa Joh mwaulaya.

“ Josh what have you done? Unawezaje kusahau simu? Ona anachokifanya Jason” akasema John.Josh akatupia jicho luningani na kumuona Jason akiongea na simu
“ ouh my God !! akasema Josh na kutoka mbio akarejea kule chumbani alikomuacha Jason.aliufungua mlango na kuingia ndani kwa kasi,akamvamia Jason na kuanza kumshushia kipigo kikali.Alikasirishwa sana kwa kitendo cha Jason kuchukua simu yake na kumpigia Peniela.Jason alilala sakafuni damu nyingi ikimvuja kutokana na kipigo kile kikali.Josh akachukua kila kilichokuwa mezani akatoka akiwa amefura kwa hasira.Mara simu yake ikaita.Alikuwa ni Peniela.Josh akasita kupokea.Simu ikaendelea kuita ikamlazimu aipokee
“ hallo Josh hebu niambie Jason umempeleka wapi? Akauliza Peniela kwa ukali

“ Peniela there is an explanation” akasema Josh
“ Explanation ? Sitaki maelezo yoyote nataka uniambie kwa nini umemteka Jason? Kwa nini unamtesa Jason” Akauliza peniela kwa ukali

“ I’m just following orders Peniela” akasema josh
“ orders from who? john? Tafadhali naomba mpe simu john niongee naye.!! Akaamuru penny

“ Penn….” Josh akataka kusema kitu lakini Penny akamzuia

“ Nimesema mpe simu John” akasema Peniela.Josh akakimbia hadi chumbani kwa John na kumpatia simu
“ Peniela anataka kuongea na wewe”
“ Ouh my God ! mambo yameharibika ! akasema John na kuchukua ile simu

“ hallo peniela”
“ John nahitaji kujua jason umemchukua kwa ajili gani?

“ Peniela samahani sikukutaarifu toka mapema kwamba nitamchukua Jason wa ajili ya mahojiano .Kikubwa nilichotaka lukifahamu kutoka kwake ni kwamba kwa nini alitoa taarifa polisi kwamba Elibariki yuko pale kwako? Mtu kama huyu ni wa kukaa naye mbali sana kwani akifahamu siri yako yoyote ile lazima ataitoa kwa polisi.tafadhali penny naomba usiwe na urafiki na watu kama Jason.Ni watu wabaya sana.Watu wanaokuzunguka ambao unawaita ni watu wako wa karibu si watu wazuri hata kidogo.Nimegundua vile vile Elibariki ana mahusiano na mtu mmoja anaitwa Mathew ambaye nimemfahamu ni mtu hatari sana kwetu.Ninahisi atakuwa anakuchunguza na anamtumia Elibariki kupata taarifa zako.Mwisho wa siku atafahamu kwamba wewe ni Tweam SC41 na akiligundua hilo tutakuwa na kaziya ziada ya kufanya kwa hiyo Peniela nakuomba tafadhali sana angali bado mapema achana kabisa na hawa watu.” Akasema John Mwaulaya
“ Is that all? Umemaliza? Akauliza Peniela

“ Penn…” akasema John lakini Peniela akamkatisha

“ naomba unisikilze vizuri sana John. Kwa miaka hii yote umeyaongoza maisha yangu na kuyapeleka ulivyotaka wewe.Sijawahi kukulalamikia hata siku moja kwa nini umeyafanya maishayangu yakawa hivi.Umeniingiza team SC41 ambako nimekuwa kama chombo cha starehe huku nikiwafaidisha ninyi na hao wamarekani.Nimefanya kila ulichoniamuru hata kiwe cha hatarikiasi gani.Maisha yangu hayako sawa na wanawakewengine,siruhusiwi kuwa na mpenzi wala familia na yote hayo nimeyavumilia na sijawhai kulalamika lakini kwa hili mlilolifanya leo mmevuka mipaka na kuanza kuingilia hadi watu wangu wa muhimu sana.jason na Elibariki ni watu wangu wa muhimu sana ambao hata mnifanye nini siwezi kuachana nao,narudia tena siwezi kuachana nao.Ni watu ambao wamenisaidia hadi leo hii niko huru na mnanitumia katika kazi zenu.Nilipatwa na matatizo na kunusurika kufungwa lakini ninyi nyote mliniacha na kunitenga kama siyo mwenzenu lakini ni Jason na Elibariki ndio waliosimama pamoja nami katika kipindi chote cha matatizo wamepambana na hatimaye nikaachiwa huru.hawa ni watu wangu wa muhimu sana na mkimuumiza mmoja wao mjue mmeniumiza mimi pia.Kwa mara ya kwanza ninahisi kuumizwa sana na maamuzi yako john.I’m deeply hurt.” Akasema Peniela

“ Peniela nimefanya hivi kaa ajili ya usalama wako na wa kwetu pia.Nielewe kwamba watu hawa si wazuri hata kidogo na unatakiwa kuanza kuepukana nao.Kama Jason ameweza kudiriki kwenda polisi na kutoa taarifa za kuonekana kwa Elibariki nyumbani kwako na nyumba yako ikazingirwa na polisi unadhani anaweza kushindwa kutoa taarifa zako akigundua kwamba wewe ni Team SC41? Lazima atakuripoti tu.Peniela ..”

“ John No! sitaki kabisa watu wangu wa karibu waguswena mtu yeyote yule.Nimekwisha kwambia kwamba ukimgusa Elibariki au Jason basi utakuwa umenigusa na mimi pia kwa hiyo ninasema naomba Jason aachiwe haraka sana.”

“ Peniela calm down. Hili ni suala ambao unatakiwa ulifikirie kwa umakini mkubwa.Angalia kwa sasa tuko katika hatua za mwishoni kabsia za kukamilisha operesheni yetu kwa hiyo hatuhitaji tena kikwazo cha aina yoyote ile.Elibariki ambaye unasema kwamba unampenda anashirikiana na Mathew mtu hatari sana,unadhani ni kwa nini Elibariki anatafuta ukaribu na wewe? Ni kwa sababu anatumiwa na Mathew kukuchuguza ”
“ John shitaji maongezi yoyote nawe ninachohitaji ni Jason aachiwe huru .Nataka nisikie toka kwako kitu kimoja tu, Jason anaachiwa huru ama haachiwi? Akaliza Peniela kwa ukali.John Mwaulaya akaonekana kukereka sana na kauli ile ya Peniela
“ Peniela naomba usisahau mtu unayeongea naye ni nani kwako? Akasema John kwa ukali
“ Ni nani kwangu? Ni mtu katili asiye na hata chembe ya huruma,mtu mwenye moyo wa kishetani” akasema Peniela bila kuogopa.John mwaulaya akavuta pumzi ndefu na kusema

“ Peniela kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nimetukanwa na mtu tena si mtu baki bali mtu ambaye nimemlea kama mwanangu kwa miaka mingi.”

“ John sijakutukana nakueleza ukweli,hujawahi kuniudhi kama ulivyoniudhi leo.Kitendo cha kumchukua Jason na kuanza kumtesa bila hata ya kunishirikisha mimi kwanza kimeniumiza sana.Endapo Josh asingesahau simu yake na Jason akaitumia kunipigia basi maisha yake yangekuwa hatarini mko tayari hata kumuua kama hatawapa taarifa mnazotaka.How could you do this to me John? Sitaki maongezi zaidi nataka Jason aachiwe mara moja”

“ Peniela huna mamlaka ya kuniamuru chochote.Mimi ndiye ninayepaswa kukuamuru na ninakuamurukwamba kuanzia sasa sitaki ukaribu wowote na Elibariki.Mahusiano yake nawe yamekufa rasmi kuanzia sasa” akasema John kwa ukali

“ Huwezi kuniamuru niachane na Elibariki John.Yule ni rafiki yangu ni mpenzi wangu na kama ukitaka kumdhuru basi anza na mimi kwanza.”

“ Peniela narudia tena kukuonya naomba unisikie ninachokwambia na usiende kinyume na ninachokuamuru.Wewe ni binti mdogo sana na huwezi kushindana na mimi hata kidogo” akasema John

“ what are you going to do John? Are you going to kill me? Try.Come and kill me.I’ll destroy you John.I swear I will destroy you.!! Akasema Peniela kwa hasira.
“ Peniela this is my last warning.Sintakuvumilia kabisa kwa maneno yako unayonitolea.Usinidharau kwa vile unaniona niko kitandani .Naomba usinilazimishe nikuchukie Peniela.” Akafoka John
“ John naomba usinilazimishe na mimi nipambane na wewe. Mimi ndiye niliyeyashika maisha yako kwa sasa kwa hiyo utafanya kile takachokuamuru John.Natoa dakika thelathini Jason awe ameachiwa ,na kama hutafanya hivyo nitasahau kama wewe umenilea toka nikiwa mdogo na nitakuweka katika kundi la maadui zangu .I will destroy you John.Kumbuka una dakika thelathini za kumuachia Jason .Chaguo ni lako”
“ Peniela unacheza na moto wewe mtoto.Mimi huwa sichezewi namna hiyo na watoto.I’m a devil sasa usitake kuuona ushetani wangu.Nakuonea huruma sana kukuadhibu kwa sababu bado ninakupenda sana.”
“ Ungekuwa unanipenda usingenifanyia mambo kama haya uliyonifanyia.Umeniingiza katika kundi lako na ukayaharibu maisha yangu.Umenivurugia ndoto zangu zote za maisha ,umenifanya nikawa mtumwa wako,nikakufanyia kazi zako kwa kuutumia mwili wangu ,Maisha yangu yamekosa amani,yamekosa furaha,kila siku ninaishi katika hatari kubwa.Nimechoka John .Ninasema nimechoka .I need my freedom back na ninajua hutaweza kuniachia huru kwa sababu mnautegemea mwili wangu katika kufanikisha mipango yenu.” Akasema Peniela
“ Don’t try me Peniela !! akasema John kwa ukali huku akianza kuvuta pumzi kwa shida

“ You have thirty minutes to free Jason .Mkimuachia nataka anipigie simu na aniambie kwamba ameachiwa.baada ya nusu saa bila kupokea simu yake nitajua mmepuuza agizo lagu na mtaona nitakachowafanyia” akasema Peniela na kukata simu.JohnMwaulaya kwa hasira akairusha simu ileukutani ikavunjika .Alianza kuhema kwa taabu sana.Josh akamuita daktari anayemuhudumia na kwa haraka akamuwekea kifaa mdomoni cha kumsaidia kupumua.Hali yake ilibadilika ghafla.


******


“ Sijawahi kukasirika kama nilivyokasirka leo.Kitendo cha kumteka Jason na kwenda kumtesa ni kitendo ambacho kimenikasirisha na kuniumza sana.Jason ni mtu wangu wa karibu na ninamthamini sana.Amenipigania kwa kila namna na hadi leo hii niko huru.Yeye na Elibariki walisimama na mimi wakati ule dunia yote imenitenga.Hawa ni watu wangu ambao niko tayari kuyaweka hatarini maisha yangu kwa ajili yao.Nafahamu kwa sasa mimi na Jason tuna matatizokidogo kutokana na kuwagonganisha na Elibariki lakini hii haijaiondoa thamani yake kwangu.Bado ni mtu muhimu sana kwangu na ndiyo maana alipopata nafasi ya kupiga simu akanipigia mara moja akifahamu kwamba ninaweza kumsaidia.Siwezi kumuacha Jason ateseke.Ninajua lazima watamtesa sana ili awape taarifa na husan taarifa za Mathew kwan ndiye anayeonekana kuogopwa sana na John.”akawaza Peniela akiwa garini akitokea hospitali

“ Nimekuwa mtumwa wa Team Sc41 kwa miaka mingi na sasa nimechoka.Wamenitumia wanavyotaka na sasa wanaanza kuingia hadi kwa watu wangu wa muhimu.Wanataka kunipangia hadi marafiki.Nitaishi vipi bila ya kuwa na marafiki ? Watu wangu wa muhimu watanielewaje? Akajiuliza peniela

“ lazima mambo haya yafike mwisho.Endapo hawatamuachia Jason katika muda niliowapa Iswear lazima nitapambana nao vibaya sana.Nadhani Team SC41 wakati wake umefika.” Akawaza Peniela akasimamisha gari pembeni ya bara bara akachukua simu na kumpigia Mathew
“ hallow Peniela habari yako?akasema Mathew baada ya kupokea simu
“ habari nzuri sana Mathew.Ninaomba unisaidie niongee na Elibariki” akasema peniela

“ kwa sasa siko nyumbani ,nimetoka kidogo nitakaporejea nitampatia simu utawasiliana naye’ akasema Mathew

“ ok Mathew ahsante sana” akajibu Peniela na kukata simu


JOHN MWAULAYA ANAINGIA KATIKA MGOGORO NA PENIELA,NINI HATIMA YAO,JASON ATAACHiWA? TUKUTANE KATIKA SEHEMU IJAYO YA SIMULIZI HII
 
SEASON 2


SEHEMU YA 28

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Nimekuwa mtumwa wa Team Sc41 kwa miaka mingi na sasa nimechoka.Wamenitumia wanavyotaka na sasa wanaanza kuingia hadi kwa watu wangu wa muhimu.Wanataka kunipangia hadi marafiki.Nitaishi vipi bila ya kuwa na marafiki ? Watu wangu wa muhimu watanielewaje? Akajiuliza peniela
“ lazima mambo haya yafike mwisho.Endapo hawatamuachia Jason katika muda niliowapa Iswear lazima nitapambana nao vibaya sana.Nadhani Team SC41 wakati wake umefika.” Akawaza Peniela akasimamisha gari pembeni ya bara bara akachukua simu na kumpigia Mathew

“ hallow Peniela habari yako?akasema Mathew baada ya kupokea simu
“ habari nzuri sana Mathew.Ninaomba unisaidie niongee na Elibariki” akasema peniela

“ kwa sasa siko nyumbani ,nimetoka kidogo nitakaporejea nitampatia simu utawasiliana naye’ akasema Mathew

“ ok Mathew ahsante sana” akajibu Peniela na kukata simu


ENDELEA………………


Hali ya John Mwaulaya ilibadilika sana baada ya kumaliza kuongea na Peniela simuni.Alikuwa akivuta pumzi kwa shida hali iliyomlazimu daktari wake amuwekee kifaa cha kumsaidia kupumua.

“ Martin, is he going to be ok? Akauliza Josh aliyekuwa na wasi wasi mwingi na haliya John

“ I don’t know” akajibu Martin kijana ambaye ana taaluma ya udaktari na ambaye amekuwa akimuhudumia John mwaulaya kwa kindi kirefu

“ Tutafanya nini sasa? Akauliza Josh
“ Subiri kwanza usikate tamaa mapema,baada ya muda atarejea katika hali yake ya kawaida’ akasema Martin.
Pamoja na kuvuta pumzi kwa shida lakini John mwaulaya alionekana kutaka kusema jambo,akamfanyia josh ishara asogee karibu halafu akakitoka kile kifaa cha kumsaidia kupumua
“L.e..le….uhhpphh..” akashindwa kuongea na kukirudisha tena kifaa kile mdomoni.Baada ya sekunde kadhaa akakitoa tena na kujitahidi kuongea

“ Let…hi..him..gooo..!! akasema John huku akinyoosha kidole katika luninga iliyokuwa ikimuonyesha Jason aliyekuwa amelala chini baada ya kipigo kikali alichopewa na Josh baada ya kutumia simu yake kuwasiliana na Peniela

“ Are you sure John ? akauliza Josh kwa mshangao kidogo.John Mwaulaya akamfanyia ishara ya mkono kwamba amuache Jason aende zake.Josh akaonekana kama vile hakubaliani na kitendo kile John akamfanyia ishara amsogelee akatoa kile kifaa cha kumsaidia kupumua akasema
“ Mpigie Pen..nniela..mwambie tum..tu..tumemuachia Jas..’ akasema John kwa taabu,martini akakirudisha kifaa kile mdomoni mwa John

“ Umesikia alichokwambia Josh? Go do it ! John hahitaji kuongea tena mida hii.Go Josh” akasema Martin na Josh akatoka mle chumbani akaelekea katika chumba alimo Jason.Akamtazama alivyokuwa amelala pale chini
“ Una maisha marefu zaidi ya paka kenge wewe.Leo ningekufanyia kitu kibaya sana umshukuru Peniela.bila yeye sijui kama ungetoka humu una meno yote”akawaza Josh huku akimtazama Jason kwa hasira sana. Akamuendea pale chini na kumpiga teke la mgongo.
“ Inuka paka we! Akasema kwa ukali na kumuinua Jason aliyekuwa akivuja damu akamtazama kwa hasira na kusema

“ Una bahati sana .Tunakuachia uondoke lakini ukithubutu kufumbua mdomo wako na ukasema chochote kuhusiana na kilichotokea leo ,nakuhakikishia kwamba haitatuchukua dakika thelathini sisi kufahamu na hautakuwa na sehemu ya kukimbilia kwani tutakusaka katika kila kona na tutakupata.Nikikupata nitakufanyia kitu kibaya sana,nitakuondoa jino moja moja kwa kutumia hili koleo” akasema Josh huku akimuonyesha jason kifaa kile kidogo

“ Nitakukata sikio moja moja na kukumwagia tindikali.Nitakukata kiuongo kimoja kimoja and you will die slowly but in great pain.kwa hiyo jihadhari sana usifanye jambo lolote lile kinyume na maagizo ninayokupa.Tumeelewana? akauliza Josh kwa ukali
“ N..dn..ndiyo..” akajibu Jason huku bado damu ikiendelea kumtoka mdomoni.Josh akamrejeshea vitu vyake vyote halafu akamuamuru ainuke wakatoka mle chumbani wakaelekea nje.

“ Ingia katika gari lako uondoke haraka sana,na tafadhali yafanyie kazi yale niliyokueleza.Ukienda kinyume chake litakapokupata hakuna anayeweza kukusaidia tena.keep your mouth shut” akasema Josh .Jason akaingia katika gari lake na kuliwasha kabla hajaondoka Josh akamwambia asubiri.Akachukua simu yake na kumpigia Peniela

“ hallo Josh,nategemea simu hii itakuwa ni ya kunifahamisha kwamba mmemuacha Jason na hajaumizwa” akasema Peniela mara tu baada ya kupokea simu

“ Peniela ongea na mtu wako huyu hapa” akasema Josh na kumpa Jason simu

“ hallo peniela’ akasema Jason

“ Jason ! are you ok? Akaulizaa peniela.Jason akamtazama Josh aliyekuwa katika dirisha la gari akimuangalia
“ ndiyo peniela.I’m ok.Wameniruhusu niondoke” akasema Jason

“ Wamekutesa? Wamekuumiza ? akauliza Peniela
“ hapana hawajanitesa ,walikuwa wakiuliza tu maswali “
“ Ok good.Naomba usiende nyumbani kwako.Nenda moja kwa moja nyumbani kwangu nisubiri pale mimi niko njiani ninaelekea huko .tafadhali fanya hivyo Jasoni kwa usalama wako” akasema peniela

“ sawa peniela nitafanya hivyo” akajibu Jason na kisha akamrejeshea Josh simu yake.

“ hallo peniela,kuna ktu ambacho ninataka kukueleza”
“ Kitu gani josh?

“ Hali ya John si nzuri toka ulipoongea naye simuni.Anavuta pumzi kwa shida sana”

“ Josh naomba usiniambie habari hizo kwa sasa.Sina chochote cha kufanya kwa sasa “akasema Peniela

“ peniela,John ndiye kongozi wetu na baada ya Osmund kufariki John hana tena msaidizi.Wewe ndiye ambaye tunakutegemea “

“ Josh please ,nina mambo mengi ya kufanya kwa sasa.Naomba uniache kwanza nitakupigia simu baadae.Jitahidini kufanya vile muwezavyo kumsaidia” akasema Peniela na kukata simu.

“ John amekwisha nitoka kabisa akilini na sitaki hata kusikia habari zake.Ninachokifikiria kwa sasa ni namna ya kuwalinda watu wangu wa karibu,Elibariki na Mathew wasidhuriwe na mtu yeyote.Kama ikitokea akapoteza maisha its ok.Amezoea kutoa roho za wenzake na yeye zamu yake imefika.John ni mtu ambaye amenilea toka nikiwa mdogo na amenifikisha hapa nilipo lakini ni mtu mkatili sana na hafai kuonewa huruma.Binafsi ameniharibia maisha yangu na kunipotezea kabisa mwelekeo mzima wa maisha yangu.Amenichefua zaidi baada ya kuanza kuwaandama na watu wangu wa karibu .Kwa sasa kuna kitu kimoja tu ninachokifikiria kukifanya….” Akawaza Peniela
“ Sijui jason atanielewaje kuhusiana na tukio hili .Watu ninaoshirikiana nao wamemteka na kumtesa sana.Hakuna kitu cha kuficha tena hapa kwani kila kitu kiko wazi.Tayari amekwishagundua kwamba ninashirikiana na akina Josh ambao wamemteka na kumtesa .Tayari amekwisha fahamu kwamba nina mahusiano na watu hatari.Taswira yangu kwake imekwishabadilika na sina namna nyingine ya kufanya kumfanya aniamini tena zaidi ya kumweleza ukweli mimi ni nani. Siwezi kuendelea kujificha kwani tayari nimekwisha fahamika.Hii yote imesababishwa na akina John kufanya mambo kwa kukurupuka bila kutumia akili.Nadhani mwisho wa Team SC41 umekaribia sana.”akawaza Peniela na kuongeza mwendo wa gari kuelekea nyumbani kwake kumuwahi Jason
Alifika nyumbanikwake na kulikuta gari la Jason liko nje.Akashuka garini haraka na kwenda kugonga mlango wa gari la Jason ambaye alipomuona Peniela akashusha kioo na kumstua sana Penny baada ya kuona damu nyingi ikimvuja.
“ Ouh my God Jason!..akasema Peniela kwa mshangao akafungua geti haraka haraka wakangiza magari ndani.Jason akashuka huku akichechemea.Peniela akamfuata na kumkumbatia

‘ Oh Jason jamani Pole sana” akasema Peniela Jason hakujibu kitu.Peniela akamshika mkono na kumuongoza hadi chumbani kwake akamvua koti na shati vilivyokuwa vimeloana damu akamshika mkono akamuingiza bafuni.

“ peniela you dont have to do this” akasema Jason
“Jason please let me do this” akasema Peniela huku akiufungua mkanda na kumvua Jason suruali halafu akafungua maji na kumuogesha .Kisha maliza zoezi hilo akachukua kisanduku cha dawa akampaka dawa katika majeraha yote aliyoyapata kutokana na kipgo cha Josh

“ Thank you penny’akasema Jason

“ Please Jason you don’t have to thank me” akasema peniela
“ lazima nikushukuru Peniala.Umeniokoa .Bila wewe watu wale wangenitesa na kuniua.Umeyaokoa maisha yangu” akasema Jason

“ Jason Pole sana kwa kitendo ulichofanyiwa na wale watu.Naomba ufahamu kwamba nimeumizwa sana na kitendo hiki.Hawakutakiwa wakufanyie jambo kama hili ” akasema Peniela huku akimtazama Jason kwa huruma

“ Usijali peniela mimi ndiye niliyefanya ujinga wa kwenda polisi na kutoa taarifa za Elibariki kuonekana nyumbani kwako.Utanisamehe sana kwa jambo hili la kijinga nililolifanya .Niliposikia kwamba Elibariki yuko hapa kwako niliingiwa na wivu mkubwa na niliumia moyoni kwa nini awepo hapa na ndiyo maana nikalazimika kwenda kutoa taarifa polisi kwa lengo la kulipiza kisasi .Peniela naomba unisamehe pia kwa tuko lile nililolifanya siku ile la kusababisha ugomvi mkubwa na Elibariki hapa nyumbani kwako ugomvi uliosababisha nimpige Elibariki na chupa kichwani.Nilishindwa kudhibiti hasira zangu na kufanya kitendo kile cha kijinga ambacho ningeweza hata kusababisha kifo cha Elibariki na ningekuingiza wewe katika matatizo makubwa.Lakni yote haya niliyoyafanya yamesababishwa na pendo wangu mkubwa nilionao kwako.Ninakupenda sana Peniela na ninasika wivu mkubwa kukuona ukiwa na mwanaume mwingine hasa hasa Elibariki”akasema Jason.Peniela akamtazama akamuonea huruma sana.
“ Pole sana Jason.Hukutakiwa kufanya vile ulivyofanya .Hata hivyo nimekwisha kusamehe Jason kwa sababu wewe ni mtu wangu wa karibuna wa muhimu sana.Tumekuwa marafiki kwa muda mrefu na hatujawa kukorofishana.Umesimama na mimi dunia nzima iliponitenga nilipopata matatizo kwa hiyo wewe ni mtu ambaye una nafasi kubwa sana ndani ya moyo wangu .Kuhusiana na kilichotokea leo kuna mambo mengi sana ambayo tunatakiwa kuyaongea na kuyaweka sawa.Kuna masuala ambayo mnatakiwa kuyafahamu lakini kabla ya yote kuna mahala tunatakiwa kwenda.Unafahamu anakoishi Mathew? Akauliza peniela

“ Ndiyo ninapafahamu ” akajibu Jason

“ Ok jiandae tunaelekea huko”akasema Peniela

” Tunaenda kufanya nini huko kwa Mathew? Akauliza Jason

“ Kuna mambo ambayo mnatakiwa kuyafahamu.”akasema Peniela
“ peniela kabla hatujaelekea huko kuna jambo nataka niulize.Watu wale ni akina nani? Unahusiana nao kivipi? Akauliza Jason
“ Usijali kuhusu hilo Jason.Utafahamu kila kitu lakini kwa sasa naomba ujiandae tuelekee kwa Mathew.”akasema Peniela akafungua kabati lake la nguo na kutoa trakisuti nyeusi na kumpatia Jason avae kwani nguo zake zote zilikuwa zimetapakaa damu.Kisha vaa wakatoka wakaingia garini na kuondoka kuelekea kwa Mathew.Mara tu baada ya kuliacha geti Peniela akachukua simu na kumpigia Mathew

“ Hallow Peniela” akasema Mathew

“ Mathew ninaelekea nyumbani kwako,uko wapi?
“ Unakwenda nyumbani kwangu? Mathew akashangaa
“ Unapafahamu nyumbani kwangu? Akauliza Mathew
“Sipafahamu ila niko na Jason ndiye anayenipeleka huko” akasema Peniela

“ Unakwenda kufanya nini?

“ Ninahitaji kuonana nanyi nyote.Kuna mambo ambayo nataka kuongea nanyi” akasema Peniela
“ Penela kwa sasa bado niko katika mizunguko yangu ya kikazi ukifika nisubiri usiondoke,sintakawia sana”akasema Mathew

“ sawa Mathew” akasema Peniela na kukata simu
“ Unamfahamu Mathew? Akauliza Jason

“Ndiyo ninamfahamu yeye na Anitha pia ” akasema Peniela na kumshangaza Jason.Hakujua kama tayari Mathew na peniela wanafahamiana
“ Peniela ni msichana hatari na nimemuogopa sana.Sikuwahi kuhisi hata siku moja kama anaweza kuwa na mahusiano na watu hatari kama wale.lakini watu wale ni akina nani? Shughuli zao nini nini? Ni majambazi? Akajiuliza Jason
“ hapana sina hakika kama wale jamaa ni majambazi.Inaonekana shughuli zao ni zaidi ya ujambazi.wale hawaonekani kama ni majambazi.Ninahisi wanaweza kuwa ni mtandao unaojihusisha na madawa ya kulevya.Ninaweza kuamini hivyo kutokana na jumba lile kubwa walimonipeleka .Lilikuwa ni jumba la kifahari sana ambalo kwa pesa ya ujambazi si rahisi kulijenga .Lazima watakuwa wakijishughulisha na biashara haramu na kama ni hivyo basi hata Peniela naye atakuwa akijihusisha na mtandao huu na ndiyo maana ni binti ambaye anaishi maisha ya hali ya juu sana na akaweza kumiliki yale maduka makubwa mawili ya nguo ambayo hata hivyo yalifilisika alipopata matatizo ya ile kesi ya mauaji.Pamoja na kumalizika kwa kesi yake na kukuta biashara zake zote zimefilisika lakini bado Peniela hajatetereka kiuchumi na anaishi bado maisha ya hali ya juu.Nilitegemea kwamba baada ya kutoka gerezani atakuwa katika hali mbaya kiuchumi na nilikwishajipanga kumsaidia lakini haonekani kabisa kuyumba na maisha yake yanaendelea kama kawaida.Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusiana na suala hili kwamba ni wapi Peniela anakopata pesa za kuendesha maisha yake na leo hi nimepata jibu.Nimeanza kumuogopa sana” akawaza Jason
“ Ninampenda sana Peniela lakini kwa tukio la leo sina hakika kama peniela ni mwanamke anayenifaa.Ukimuona namna alivyo huwezi kumdhania kama anaweza kuwa na mahusiano na watu hatari kama wale.Ninajilaumu hata kwa nini nilifahamiana naye.” Akawaza Jason huku akimtazama Peniela kwa jicho la wizi .

“ Ninaanza kuingiwa na hisia kwamba huenda hata kifo cha edson Peniela akawa anahusika.Suala hili linatakiwa lifanyiwe uchunguzi.Ninakubaliana kabisa na ule usemivusemao kwamba umdhaniaye siye ndiye. Akaendelea kuwaza jason
Safari ilikuwa ya kmya kimya na mara chache waliongea pale Jason alipomuelekeza Peniela njia za kupita hadi walipofika nyumbani kwa Mathew
“ wow ! the house is so big like a palace”akasema Peniela.Mlinzi ambaye hulinda jumba la Mathew tayari alikwisha pewa taarifa za wageni wale akawafungulia geti wakaingia ndani.

“ The house is so beautiful” akasema Peniela akitabasamu na kuufurahia uzuri wa jumba lile la Mathew.Walikaribishwa sebuleni na mlinzi ambaye alipewa maelekezo kwamba awahudumie kwa vinywaji wageni wale.
Sauti za kufungwa kwa milango ya gari zikamstua jaji Eliabriki akafikiri kwamba Mathew na Anitha wamerejea.Akatoka chumbani kwake na kuelekea sebuleni.Alistuka mno baada ya kukutanisha macho na Peniela .Alitamani kuamini kwamba ile ilikuwa ni ndoto lakini haikuwa ni ndoto bali ni kitu cha kweli alichokuwa akikishuhudia.Peniela alikuwa sebuleni akiwa na jason hasimu mkubwa wa Elibariki.Mara tu alipokutanisha macho na Jason wote wakabaki wakishangaana .
“ Penela my love!..akasema jaji Elibariki .Pemiela akainuka na kwenda kumkumbatia kwa furaha kubwa.
“ Ouh Elibariki I missed you so much my love” akasema Peniela.Kama ilivyokuwa kwa Elibariki Jason naye alibaki akishangaa kwani hakutegemea kama angekutana na Elibariki pale nyumbani kwa Mathew.
‘ what is he doing here? Akauliza Eliariki kwa ukali huku akimtazma jason kwa hasira
“ peniela whats going on? Why is this bastard here ? Naye Jason akauliza kwa hasira
“ Hey guys..its time now to stop your childish things..You have to stop fighting .What are you fighting for ? akauliza Peniela kwa ukali

“ I hate this bstard so much” akasema Jason

“ I hate you too ..Sikupendi sana Jason” akasema jaji Elibariki huku akitaka kumfuata Jason.Peniela akamzuia
“ Elbariki stop.!!..Do you want to keep on fighting because of me? Ok fine keep on fighting and kill each other” akasema Peniela na kuondoka akaenda kuketi sofani.Jaji Elibariki na jason wakabiki wanatazamana kwa hasira.

“ Nimewaachia uwanja mpigane.Mbona hampigani?akauliza Peniela
“ If I see you near Peniela again I swear in heaven and earth I’m going to kill you” akasema jaji Elibariki na kumfuata peniela pale sofani akakaa pembeni yake.
“ Peniela I’m so sorry .sikutegemea kama ningekutana na huyu kijana hapa.” Akasema jaji Elibariki.Jason akakasirika na kuinuka

“ Elibariki nimekuvumilia sana na sintavumilia tena dharau nyingine yoyote toka kwako.Unadhani ninakuogopa? Akaulizia Jason huku akimsogelea jaji Elibariki.Peniela akamfuata na kumshika mkono
“ Jason naomba ukae na sitaki mtu yeyote aongee zaidi yangu” akasema Peniela kwa ukali.Wote waili Jason na Elibarii wakabaki kimya

“ nawashangaa sana mnapoendelea kupigana kila siku na kutishiana maisha kwa sababu yangu.Mimi ni nani kwenu?Chombo cha kuwastarehesha hadi mfikie hatua ya kutaka kutoana uhai? Akauliza peniela kwa ukali
“ Ninyi nimarafiki na hamna haja ya kugombana.Ni aibu kubwa mkisikika waheshimiwa kama ninyi mnagombana kwa sababu ya mwanamke.” akasema Peniela.
“ Ni huyu ndiye aliyeanza haya yote kwa kuvamia mapenzi ya wat…”akasema jaji Elibariki na akakatishwa na Peniela

“ Elibariki stop.Nimesema sitaki mtu yeyote aongee zaidi yangu” akafoka Peniela

“ Mimi na wewe nani aliyevamia mwenzake.Unajua nimetoka wapi na Peniela? Wewe una mke wako rudi katika ndoa yak……………”akasema Jason lakini akakatishwa na Penny
“ Jason Stoop ! nimesema hiki ni kikaochangu na nyote mnatakiwa make kimya”akasema peniela.akawatazama mashababi wale ambao kila mmoja alikuwa amefura kwa hasira akimtazama mwenzake kwa chuki

“ Ninyi nyote hampaswi kuchukiana wala kugombana.Mnayepaswa kunilaumuna kunichukia ni mimi kwa sababu ndiye niliyekubali kulala nanyi nyote wawili.Hakuna kati yenu aliyefahamu kwamba mwenzake anatembea na mimi hadi siku ile mlipokutana.Kwa maana hiyo basi mnatakiwa mkae na mmalize tofauti zenu.Nimewakutanisha hapa makusudi kabisa ili muweze kumaliza tofauti zenu ninyi wenyewe.Mnatakiwa muongee na muelewane na baada ya hapo kuna jambo kubwa ambalo nataka kuwaambia.kwa sasa nitaondoka na kuwaacha ninyi peke yenu na nitakaporejea nataka muwe mumemaliza tofauti zenu na ndipo tutakapoweza kukaa na kuongea.Siwezi kuongea nanyi sasa hivi wakati ambao kila mmoja wenu amefura hasira kama simba.” Akasema peniela na kuchukua mkoba wake.

“ peniela siwezi kuendelea kukaa hapa.Ninaondoka pia”akasema Jason
“ jason you cant go anywhere.Kaeni hapa na mmalize tofauti zenu ninyi wenyewe.Ninyi ni marafiki na hampaswi kugombana .Be like men ! …akasema peniela na kutoka mle sebuleni akaingia garini na kuondoka.Akiwa garini akachukua simu yake na kumpigia Mathew
“ hallow Mathew ,nimekwisha fika kwako na nimeondoka ila nitarejea baadae kidogo nina maongezi makubwa na Elibariki pamoja na Jason.Kuna mambo ambayo nahitajiku yaweka sawa kati yao’ akasema Peniela

“ sawa Peniela hata sisi tutarejea nyumbani muda si mrefu kwani shughuli yetu tuliyokuja kuifanya tunatarajia kuikamilisha muda si mrefu” akasema Mathew na kukata simu

“ Kuna ulazima wa kufahamu john anaendelaje? Akajiuliza Peniela
“ hakuna haja.sitaki kujua anaendelea vipi.Akili yangu imenituma katika kitu kimoja tu na ambacho ndicho ninakwenda kukifanya.Its time to take down Team SC41.Hakuna aliywahi kufikiria kitu hiki lakini mimi ninakwenda kukifanya.Najua ni hatari lakini sintakata tama I’ll die trying.Nimegundua kwamba bila kufanya hivi sintakuwa huru na sintakuwa na maisha ya kawaida” akawaza Peniela halafu akazitafuta namba za simu za Captain Amos akampigia

“ hallow Peniela” akasema Captain Amos

“ hallow amos.habari yako?
“ habari nzuri peniela ,vipimaendeleo yako?
“Ninaendela vizuri Amos.Nimekupigia kutaka kufahamu kuhusu ule mpango wa kunikutanisha na Dr Kigomba.Maandalizi yanakwendaje? akaulizia Peniela
“ Kila kitu kinakwenda vizuri sana Peniela na jioni ya leo nitakukutanisha naye.Kwa sasa ninaandaa sehemu ya kukutania na nitakutumia ujumbe baadae kukujulisha sehemu ya kukutania.Kitu ambacho ni cha muhmu wakati wa kuonana usionyeshe kama unanifahamu.Utajifanya kwamba ni mara ya kwanza mimi na wewe tunaonana.Kitu kingine ni kwamba jitahidi jambo hili liende kwa haraka kwani muda wowote Dr Joshua anaweza akamkabidhi Dr Kigomba ule mzigo.kwa hiyo lazima tufanye haraka sana kujenga mahusiano ya haraka”
“ usijali Amos.Kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa.Huna haja ya kuwa na wasi wasi na mimi” akasema Peniela na kukata simu


*******


Jaji Elbariki na Jason waliendelea kukaa pale sebuleni hakuna aliyetaka kumsemesha mwenzake.Baada ya kama dakika kumi na saba toka Peniela aondoke jaji Elibariki akasema

“ Ok Jason,nimeamua kujisusha .Lets talk like men.” Akasema jaji Elibariki

“ You want to talk? Sina muda wa kuongea nawe Elibariki” akasema Jason
“ Jason lets be like men.Lets talk about this !” akasema jaji Elibariki
“ Ok unataka kuniambia nini? Akauliza Jason
“ Peniela yuko sahihi.Hatuhitaji kugombana.Binafsi sikuwa nikifahamu kama nawewe unampenda Peniela .Nilianza kumpenda peniela wakati wa kusikiliza kesi yake na baada ya kesi kumalizika ndipo nilipooanza kuwa na ukaribu naye na hakuwahi kunieleza chochote kuhusu wewe.Yeye alichoniambia nikwamba hakuwa na mpenzi kwani mpenzi wake alikuwa Edson pekee.Nilimweleza ninavyompenda na alinikubalia tukawa wapenzi.Nilistuka sana siku ile nilipokuona umetokea ghafla mle ndani wakati tukifanya mapenzi.Nilistuka zaidi pia uliponieleza kwamba Peniela ni mpenzi wako.Sote wawili hatukuwa tukifahamu kwamba tulikuwa tunatembea na mwanamke mmoja.Kwa maana hiyo baadaya kuligundua hili ni wakati wetu sasa wa kusameheana na kusahau yaliyopita.Hatuna haja ya kugombana kwani sote tumedanganywa kwa hiyo hata tukigombana hatutapata mshindi.” akasema jaji Elibariki.Maneno yale ya jaji Elibariki na sauti ya upole aliyoitumia kidogo vikamfanya Jason atulize hasira .Akakohoa kurekebisha koo na kusema
“ Nimefahamiana na Peniela kwa muda mrefu kidogo na wakati huo bado alikuwa katika mahusiano na Edson.Baada ya kupatwa na matatizo yake nikasimama pamoja naye kama rafiki.Baada ya kesi kumalizka na akashinda kwa kuwa tayari nilikuwa na hisia za kumpenda mrefu niliamua kuitumia vizuri nafasi hiyo na kumueleza hisia zangu.Peniela akanielewa na akanikubalia kwamba tuwe wapenzi na hakuwahi kunieleza kama ana mahusiano na mtu mwingine yeyote.Siku ilenilipowakuta mkifanya mapenzi na ukatokea ule ugomvi,Peniela alinipigia simuna kunifahamisha kwamba kuna mtu yuko ndani kwake na mtu huyo amekuwa akimsumbua sana kwa muda mrefu akimtaka kimapenzi.Alinambia kwamba niwahi haraka kwa kuwa mtu yule hakuwa na nia njema na alikuwa na wasi wasi kwamba mtu yule angeweza hata kumbaka.Nilifika haraka sana na kukuta kwamba ni wewe ,nilikasirika sana na ndipo ugomzi ule ukatokea.Jana baada ya kutoka katika msiba wa Noah,nilipata taarifa toka kwa Mathew kwamba uko salama na uko kwa Peniela.Nilisikia wivu mkubwa na ndipo nikaenda kutoa taarifa kituo cha polisi na kuwafahamisha kwamba uko pale” akasema Jason na kumstua sana Elibariki

“ It was you? Jaji Elibariki akashangaa

“ yes it was me”akasema Jason
“ ouh my God I cant believe this” akasema jaji Elibarii
“Utanisamehe sana Elibariki kilichonifanya nikafanya jambo lile ni kutawaliwa na wivu na hasira .Sikujua kama kwa kufanya vile nitahatarisha maisha yako”akasema jason.jaji elibariki akakaa kimya kidogo akainama na baada ya sekunde kadhaa akainua kichwa na kusema.
“ katika watu wote ambao ningewadhania sikuwahi kufikiri kama ungeweza kufanya kitu kama kile Jason”
“ Tusameheane Elibariki,nililfanya vile kutokana na hasira na wivu tu.” Akasema Jason

“ Ok tusahau yaliyopita” akasema Elibariki

“ nashukuru sana Elibariki.Ni kweli hatuna sababu ya kupigana kama alivyosema Peniela.Hakuna kati yetu aliyefahamu kama tuna mahusiano na mwanamke mmoja.Wa kulaumiwa hapa ni Peniela” Akasema Jason

“ kweli kabisa Jason.Kuna jambo nimeliona baada ya kuniambia kwamba Peniela alikupigia simu na kukufahamisha kwamba kuna mtu ambaye anataka kumbaka na ukaja ukanikuta mimi.Sikuwahi kutaka kutenda kitendo kama hicho na wala sikuwahi kumlazimisha kimapenzi Peniela.Mimi na yeye tulikubaliana kuwa wapenzi kwa mioyo yetu yote na wala hakukuwa na shinikizo lolote toka kwangu kumtaka anikubali.Kuna picha ninaipata hapa kwamba peniela alitembea na sisi sote wakati akijua kwamba ni marafiki na zaidi ya yote alitaka tukutane uso kwa uso.Ninakumbuka siku ile alitaka tufanye mapenzi sebuleni kumbe lengo lake ni ili utukute pale.” akasema jaji Elibariki
“ Mimi alivyonipiigia simu aliniambia kwamba nikifika nipite moja kwa moja ndani milango iko wazi” akasema Jason

“ Umeona Jason. ! Ni wazi peniela alitaka jambo lile litokee yaani mimi na wewe tukutane,tugongane ,alitaka utukute mimi na yeye tukiwa sebuleni tukifanya mapenzi.Alitaka tugombane,tuchukiane na alifanikiwa lengo lake kwani tuligombana na nusura nipoteze maisha.kwa nini lakini alifanya hivi?kwa nini alitaka mimi na wewe tugombane?akauliza jaji elibariki

“ Elibariki Peniela ni msichana hatari sana,na leo nimelifahamu hilo”
“ Umefahamu kitu gani?akauliza jaji Elibariki

“ Sote hatukuwa sahihi kuhusiana na mtu tuliyekuwa tukimpigania kiasi cha kutishiana kutoana uhai.”
“ kwa nini unasema hivyo Jason? Akauliza Elbariki

“ Peniela hayuko kama vile tunavyomchukulia.Ni mtu hatari sana”akasema Jason
“ Jason bado sijakuelewa.Hebu nifafanulie nifahamu” akasema jaji Elibariki
Jason akamueleza jaji Elibariki kila kitu kilichotokea

“ dah ! ninahisi joto kali.maneno uliyonieleza ni mazito sana.”akasema jaji Elibariki na kusimama akaenda katika friji akachukua maji baridi akanywa na kurejea tena sofani
“Peniela ! Nimemuogopa sana”akasema jaji Elibariki.Akawaza tena kidogo na kusema

“ Ninaweza kukubalina nawe Jason kwamba peniela ana mambo mengi sana tofauti na tunavyomfahamu.Baada ya maelezo hayo kuna kitu nimekikumbuka,wakati nikiwa palekwake kuna nyakati alikuwa akipigiwa simu na hakutaka kupokea mbeleyangu.Alikuwa akitoka na kwenda kuongelea mbali.Hakutaka nisiyasikie maongezi yake.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu alikuwa anakificha.”akasema jaji Elibariki

“ Ninavyohisi mimi wale jamaa watakuwa wakijihusisha namadawa ya kulevya kwa sababu jumba lille alikonipeleka Josh si jumba la kawaida.Ni jumba la kifahari sana.kama si madawa ya kulevya basi watu wale watakuwa wakijihusisha na biashara za haramu .Ninahisi vile vile kwamba hata kifo cha Edson,Peniela atakuwa akihusika.” Akasema Jason
“ Hapana.Katika kifo cha Edson Peniela hahusiki kabisa.tayari wahusika wamefahamika” Akasema jaji Elibariki

“ mmekwisha wafahamu? Akauliza Jason kwa mshangao
“ Ndiyo tayari tumekwisha wafahamu lakini bado kuna uchunguzi unaendelea ili kupata taarifa zenye uhakika zaidi “akasema elibariki
“Ni akina nani hao? Akauliza Jason
“ Ni jambo lenye maelezo marefu na ninadhani tusubiri atakapokuja Mathew ndiye atakayekuelezea kila kitu.” Akasema jaji Elibariki
“Sikuwa na taarifa hizo kabisa.Nilidhani kwamba baada ya ugomvi ule kutokea kila kitu kilisimama’akasema Jason
“ hapana Jason.Mambo yaliendelea.Akina Mathew waliendelea kufanya kazi na wamepiga hatua kubwa kuna mambo ambayo yamegundulika na ambayo akina Mathew wanayafanyia kazi.Mathew anaweza kukufafanulia vizuri zaidi kama bado utahitaji kuendelea na operesheni ile tuliyoianza”

“ Niko tayari Elibariki.Niko tayari kuendelea nayo.Nina hamu sana ya kutaka kumfahamu kwa undani peniela ni nani ,na wale jamaa anaoshirikiana nao ni akina nani.”

“ basi kama ni hivyo tumsubiri Peniela jioni atakaporejea kwani ameahidi kuja kuzungumza nasi jambo kubwa,sijui ni jambo gani hilo analotaka tulizungumze” akasema jaji Elibariki.

“ Yawezekana labda anataka kuja kuongelea kilichotokea asubuhi ya leo kwani nilimuuliza kuhusiana na watu wale akaniambia kwamba ataniambia baadae kila kitu .Atanipa ukweli kamili”

“ basi itakuwa vyema tukiendelea kumsubiri.so are we ok now? Akasema jaji Elibariki

“ yes we’re ok.Sisi ni wanaume na hatupaswi kugombana kwa sababu ya mwanamke”
‘ Ahsante sana Jason.nashukuru sana. “ akasema jaji Elibariki,akasimama wakashikana mikono.walimaliza tofauti zao na urafiki ukarejea tena.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
SEASON 2
SEHEMU YA 29
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ hapana Jason.Mambo yaliendelea.Akina Mathew waliendelea kufanya kazi na wamepiga hatua kubwa kuna mambo ambayo yamegundulika na ambayo akina Mathew wanayafanyia kazi.Mathew anaweza kukufafanulia vizuri zaidi kama bado utahitaji kuendelea na operesheni ile tuliyoianza”
“ Niko tayari Elibariki.Niko tayari kuendelea nayo.Nina hamu sana ya kutaka kumfahamu kwa undani peniela ni nani ,na wale jamaa anaoshirikiana nao ni akina nani.”
“ basi kama ni hivyo tumsubiri Peniela jioni atakaporejea kwani ameahidi kuja kuzungumza nasi jambo kubwa,sijui ni jambo gani hilo analotaka tulizungumze” akasema jaji Elibariki.
“ Yawezekana labda anataka kuja kuongelea kilichotokea asubuhi ya leo kwani nilimuuliza kuhusiana na watu wale akaniambia kwamba ataniambia baadae kila kitu .Atanipa ukweli kamili”
“ basi itakuwa vyema tukiendelea kumsubiri.so are we ok now? Akasema jaji Elibariki
“ yes we’re ok.Sisi ni wanaume na hatupaswi kugombana kwa sababu ya mwanamke”
‘ Ahsante sana Jason.nashukuru sana. “ akasema jaji Elibariki,akasimama wakashikana mikono.walimaliza tofauti zao na urafiki ukarejea tena.

ENDELEA……………….

Saa tisa za alasiri Mathew na Anitha wakarejea nyumbani baada ya mzunguko mrefu wa siku.Walikuwa wakiifanyia uchunguzi ile taarifa ya kuhusiana na kilichosababisha kifo cha Dr Flora ,iliyotolewa na madaktari bingwa toka hospitali kuu ya taifa.Sebuleni waliwakuta Jaji Elbariki na Jason ambaye uso wake ulikuwa umevimba na una majeraha.Wote wakashangaa
“ Jason nini kimetokea? Umepata ajali? Akauliza Mathew
“ Hapana Mathew si ajali.Nilipata matatizo kidogo nitakusimulia” akasema Jason.
“ Elibariki umeshindaje? Akauliza Anitha
“ Nimeshinda salama kabisa.Poleni na mizunguko” akasema Elibariki
“ Ahsante sana.Tunashukuru tumerejea salama”
“ Mmefanikiwa kupata habari zozote kuhusiana na mke wangu? Akauliza Jaji Elibariki
“ Tulikuwa katika hospitali kuu ya taifa ambako mkeo amelazwa lakini hatukufanikiwa kumuona kwani ulinzi ni mkali sana katika wadi aliyolazwa.Lakini kwa mujibu wa taarifa tulizozipata ni kwamba hali ya mkeo bado si nzuri ingawa ulifanyika upasuaji wa kuondoa risasi mwilini lakini bado hali yake haijawa nzuri na bado anapumua kwa msaada wa mashine .Tuzidi kumuombea kwani kwa sasa anahitaji sana sala zetu” akasema Mathew.Elibariki akainamisha kichwa.Akazama mawazoni.
“ Elibariki najua hiki ni kipindi kigumu sana kwako lakini usijali tuko pamoja.Tutamuombea Flaviana na Mungu atasikia maombi yetu na atamponya.” Akasema Anitha
“ Ahsanteni sana.”akasema Elibariki
“ peniela alikuja hapa? Akauliza Mathew
“ ndiyo alikuja hapa ,mimi ndiye niliyemleta” akasema Jason
“ Alisema kwamba kuna jambo anataka kuja kutuambia ni jambo gani hilo? Aliwadokeza chochote? akauliza Mathew
“ hapana hakutueleza jambo lolote alisema atarejea baadae jioni” akasema Elibariki
“ ok Good.Tumsubiri tuone anataka kutueleza kitu gani.” Akasema Mathew na kuchukua chupa ya maji baridi akanywa alisikia joto sana.
“ Mambo yamekwendaje huko? Akauliza Elibariki
“ Nadhani tuelekee katika chumba cha kazi,kuna mambo ya kujadili “akasema Mathew na wote wakainuka na kuelekea katika chumba cha kazi
“ Jason karibu sana .Kwa muda mrefu tumekukosa katika vikao vyetu na ninadhani Elibariki amekwisha kuelezea kwa undani mahala tulikofikia hadi hivi sasa kuhusiana na ile kazi mliyotupa ya kuchunguza kuhusu mauaji ya Edson,kwa hiyo tunaweza tukaendelea na mambo mengine”akasema Mathew
“Hapana Mathew.Jason bado hajafahamu chochote kinachoendelea kuhusiana na ile kazi tuliyowakabidhi” akasema Elibariki
“ What?! Hafahamu chochote? you guys don’t contact? Akashangaa Mathew
“ Mathew kuna mambo ambayo hatukuwa tumeyaweka wazi kwenu kuhusu mimi na Jason” akasema jaji Elibariki akamtazama Mathew kisha akaendelea
“ kwa sasa hatuna tena sababu ya kulificha jambo hili ni bora tukaliweka wazi kwenu ili mlifahamu”akasema Elibariki akarekebisha koo na kuendelea
“ kwa siku za hivi karibuni mimi na Jason tulikuwa katika mgogoro na hatukuwa na maelewano baina yetu .Kilichotokea ni kwamba…..”akashindwa kuendela na kuwatazama akina Mathew.
“ elibariki tueleze kuna tatizo gani? Akauliza Mathew
“ Kilichokuwa kimetokea ni kwamba sote wawili mimi na Jason tulijikuta tukigongana kwa mwanamke mmoja,Peniela” akasema na kuwatazama akina Mathew huku akiona aibu kidogo
“ Hicho ni kitu cha kawaida kwa wanaume.Nini kikatokea baada ya kugongana? Akauliza Mathew
“ Sote wawili mimi na Jason hatukujua kama kila mmoja ana mahusiano na Peniela.Mimi nilimfuata kwa wakati wangu na Jason naye alimfuata kwa wakati wake.Kilichotokea siku ile tulipogongana ni kwamba Peniela alinipigia simu nikiwa katika msiba wa mama mkwe na kuniambia kwamba ananihitaji sana.Ni usiku ule ambao mlikwenda kufanya uchunguzi wa kilichomuua mama mkwe.Nilipofika kwake akaniomba tufanye mapenzi na kwa kuwa hata mimi nilikuwa na hamu naye sikukataa,tukafanya mapenzi.Kwa kuwa alikuwa na hamu sana na mimi hakutaka hata tuende chumbani akataka tufanyemapenzi sebuleni.Wakati tukifanya mapenzi mara ghafla akaingia Jason na kutukuta tukifanya mapenzi.Uliibuka ugomvi mkubwa kati yetu kila mmoja akimtuhumu mwenzake kumchukulia mwanamke wake.Ugomviule ukapelekea Jason anipige chupa ya kichwa na ndiyo hili jeraha mnaloliona hapa kichwani.Nilipoteza fahamu na niliporejewa na fahamu niliwakuta watu Fulani sebuleni kwa peniela ambao wakaondoka na peniela na wawili kati yao wakanipeleka hospitali.Toka siku ule mimi na Jason hatukuwa katika maelewano na hatukuongea hadi leo hii.”akasema jaji Elibariki na kuwatazama akina Mathew .
“ Imekuwaje leo mkakutana na kumaliza tofauti zenu?akauliza Mathew
“ Kilichotokea leo ni kwamba peniela ametukutanisha mimi na Jason na kututaka tumalize tofauti zetu” akajibu jaji Elibariki
“ peniela again? Huyu huyu aliyewagonganisha na sasa amewakutanisha na kuwataka mpatane? Mathew akashangaa
“Ndiyo.Kuna jambolililompelekea akafanya hivyo”akajibu Jason
“ jambo gani?akauliza Mathew
“ Ilikuwa hivi” akasema jason
“ baada ya ugomvi ule mimina Elibariki hatukuwa tena na mawasiliano yoyote hadi niliposikia kupitia vyombo vya habari kwamba amenusurika katika shambulio na hajulikani yuko wapi.Ni wewe Mathew uliyenifahamisha kwamba Elibariki yuko kwa Peniela.Kwa kuwa bado nilikuwa na ugomvi naye nilikasirika sana na sikutaka kabisa kumuona akiwa na Peniela hivyo wazo lililonijia haraka haraka ni kwenda kutoa taarifa polisi ili Elibariki aondolewe pale kwa Peniela.Sifahamu nini kilitokea lakini leo asubuhi kuna kijana mmoja anaitwa Josh alinifuata nyumbani kwangu akidai kwamba kampuni yao inanihitaji kuwafanyia kazi ya uwakili.Nilikubaliana naye na tukaongozana hadi katika jumba moja kubwa ambalo alidai kwamba mkurugenzi wake ndipo anaishi.Tulipofika pale nikageuziwa kibao nikafungiwa katika chumba na kuanza kuhojiwa maswali kuhusiana na kwa nini nilipeleka taarifa polisi kwamba Elibariki yuko kwa Peniela na maswali mengine wakiniuliza kama ninakufahamu Mathew na walitaka kujua pia unafanya kazi gani n.k .Baadae Josh akanionyesha picha zilizochukuliwa katika kamera iliyofungwa kwa siri nyumbani kwa Peniela.Katika picha ile niliwaona wewe na Anitha mkiwa mmeambatana na Peniela usiku mkiingia ndani.Nikagundua kwamba watu wale walikuwa na mahusiano ya karibu na Peniela.Yule kijana Josh aliondoka ghafla na kuiacha simu mezani nikautumia mwanya huo kumpigia simu peniela na nakumuomba aniokoe kwani niliamini anawafahamu watu wale.Ktendo kile kilimuudhi sana Josh akanishushia kipigo kikali na ndiyo haya majeraha mnayoyaona.Dakika kumi baadae nikaachiwa niende zangu lakini kwa sharti kwamba nisimweleze mtu yeyote kilichotokea na endapo nikienda kuripot kwa vyombo vya usalama basi watafahamu na wataniua.Peniela aliniomba nisiende nyumbani kwangu bali niende nikamsubiri nyumbani kwake.Nilifanya hivyo na kwenda nyumbani kwake nikamsubiri akaja akanitibu haya majeraha na kisha akanitaka nimlete huku akanikutanisha na jaji Elibariki akatutaka tumalize tofauti zetu na kwamba atakaporejea jioni kuna jambo kubwa anataka kutueleza. Kwa hiyo basi tumeongea na tumemaliza tofauti zetu na tunamsubiri atakaporejea ili atueleze alichotaka kutueleza.”akasema Jason
“ Pole sana Jason kwa kilichokupata.Hata hivyo ninafurahi sana kuona mkiwa mmemaliza tofauti zenu .Hivi ndivyo wanaume wanavyomaliza mambo yao.”akasema Mathew kikapita kimya kifupi Elibariki akasema
“ Mathew nadhani Peniela anahitaji kufanyiwa uchunguzi mkubwa kwani anaonekana kuwa na mambo mengi.Anaonekana kuwa na siri kubwa.”
“ Suala la Peniela tutalijadili baadae lakini kwa sasa Jason anahitaji kufahamishwa kilichotokea ili tweze kwenda sawa .Ni kwamba mpaka hivi sasa tumekwisha piga hatua na tayari tumefahamu ni kwa nini Edson aliuawa .” Akasema Mathew na kumsimulia Jason kuhusiana na walichokigundua katika kufuatilia kifo cha Edson.
“ kwa hiyo Jason,hapo ndipo tulipofikia hadi hivi sasa kuhusiana na kifo cha Edson.Kwa hiyo kwa sasa tnaweza kwenda pamoja” Akamalizia Mathew
“ Poleni sana kwa kazi kubwa na ngumu mliyoifanya hadi mkagundua suala hili zito.Sikuwa nikitegemea kabisa kama jambo hili litakuwa namna hii” akasema Jason
“ Ndivyo hivyo lilivy😵k tuachane na hayo kwa kuwa sasa wote tunakwenda katika mstari mmoja basi tuendelee na pale tulipokuwa tumeishia.” Akasema Mathew
“ Kuhusu majibu ya zile karatasi bado sijapokea chochote kutoka kwa wale washirika wangu
Wa kule Israel ambao niliwaomba wanisaidie kutafuta kilichoandikwa katika zile karatasi.Nadhani bado hawajapata jibu na pindi wakipata jibu watanifahamisha.Kuhusu ile ripoti ni kwamba taarifa hii haina ukweli wowote.Orodha hii ya madaktari walioorodheshwa hapa si ya kweli na tumefuatilia kila sehemu hadi wizara ya afya na hawana madaktari bingwa wenye majina haya.Kwa maana hiyo basi tayari tumekwisha pata uhakika kwamba taarifa ilehaina ukweli wowote na ni taarifa ya kutunga.Hii ina maana tulikuwa sahihi kwamba dr Flora aliuawa kwa sindano ya sumu kama taarifa yetu ilivyokuwa ikionyesha.Kitendo cha Dr Joshua kuikubali taarifa hii ya uongo na kukataa taarifa ya kweli tuliyompatia kinatufanya tuamini kwamba inaweza kuwa anafahamu ama alishiriki katika kupanga kifo cha mke wake.Ukianza kuangalia namna mlolongo wa mambo yalivyokwenda tunalazimika kuamini kabnisa kwamba haiwezekani mambo yote haya yakafanyika bila ya rais kufahamu. Hatuna ushahidi wa moja kwa moja kumuingiza rais katika mambo haya lakini tunalazimika kuamini kwamba lazima atakuwa anafahamu ama ameshiriki.” Akasema Mathew
“ Guys endapo ikigundulika kwamba rais ameshiriki katika jambo hili nini kitafanyika? Akauliza Jason
“ kama ikigundulika kama rais ameshiriki katika jambo hili ni kitu kimoja tu kitakachofanyika.We’ll take him down.”akasema Mathew
“ Hii si kazi rahisi.Kumuondoa madarakani rais sijambo dogo”akasema Jason
“ Linavyoonekana si jambo dogo lakini ni jambo dogo kama tukiwa na ushahidi wa utosha wa kumtia hatiani.Kuwa rais si kwamba uko juu ya sheria.Ukivunja sheria za nchi lazima ushughulikiwe kama wahalifu wengine.kwa hiyo jamani kazi kubwa iliyoko mbele yetu ni kuhakikisha kwamba tunapata ushahidi wa kutosha kuthibitisha kwamba Dr Joshua anahusika katika jambo hili na hadi hapo tutakuwa na nguvu ya kumuondoa .Ninachowaomba kuanzia sasa ni kujiandaa kwani tunakoelekea si kuzur hata kidogo.Tunakwenda katika shimo la moto na kifo kwa hiyo kila mmoja wetu ajichunge na amchunge mwenzake.Sote tukiwa kitu kimoja na kuifanya kazi hii kwa umoja wetu basi tunaweza kulimaliza suala hili lakini akitokea mwenzetu mmoja akaenda kinyume na sisi basi tutakwama na tutakuwa tumejitengenezea hatari kubwa”akasema Mathew
“ Mathew mimi siogopi kitu na katika suala hili nipo tayari kwa lolote” akasema jaji Elibariki
“ What about you Jason?akauliza Mathew
“ Hata mimi siwezi kupingana na ninyi wenzangu kwani sote lengo letu ni moja tu.Kuhakikisha haki inatendeka.Hata hivyo suala hili ni pana sana na linahitaji watu wengine wa kutusaidia.Sisi peke yetu hatuwezi .” akasema Mathew
“ Unayosema ni ya kweli Jason.Pindi tutakapofanikiwa kuwa na ushahidi wa kutosha wa kumtia hatiani Dr Joshua kwa vitendo hivi basi tutatafuta uungwaji mkono lakini kwa sasa tuelekeze nguvu katika kutafuta ushahidi wa kutosha kuweza kumtia hatiani Dr Joshua.” Akasema Mathew
“ Vipi kuhusu peniela? Naye suala lake linakuwaje? Peniela ana mahusiano na wale jamaa ambao kama hisia zangu ni za kweli basi watakuwa wakijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya ama biashara nyingine haramu.Tunatakiwa naye pia tumchunguze.”akasema Jason
“ Suala la Peniela ni suala la tofauti kidogo na lenyewe litashughulikiwa kwa namna yake peke yake.Tumuweke pembeni kwa sasa na tushughulike na suala hili kubwa kwanza”akajibu Mathew
“ Ni suala la tofauti? Akauliza Jason kwa mshnagao kidogo
“ Ndiyo Jason.Ninamfahamu Peniela na suala lake liko tofauti kidogo na wala watu hao anaoshirikiana nao si wauza madawa ya kulevya.”akasema Mathew
“ kama si wauzaji wa madawa ya kulevya ni akina nani basi? Akauliza jaji Elibariki
“ kwa kuwa yeye mwenyewe amesema kwamba atakuja jioni ya leo kwa ajili ya kuzungumza nasi basi tumsubiri na atakapofika tutajua anatakakutueleza jambo gani “akasema Mathew
Baada ya maongezi yale jason akaomba atumie gari la Mathew kwenda nyumbani kwake mara moja kwani gari lake aliliacha kwa Peniela.

******

Ni saa kumi na mbili za jioni,Peniela yuko mbele ya meza iliyoshehehi vipodozi vya kila aina akimalizia kuuremba uso wake.Jioni hii alikuwa amependeza kuliko kawaida.Uzuri wake uliongezeka mara dufu.Alivalia gauni jekundu refu lililoenda sambamba na umbo lake jembamba.Yatosha kusema kwamba kama ni kutoa maksi basi peniela usiku huu angezoa maksi zote mia kwa namna alivyokuwa amependeza.Akajitazama tena katika kioo kikubwa akatabasamu
“ I’m so pretty.Ninamshukuru Mungu kwa kunipendelea uzuri huu na ni uzuri huu ambao umekuwa ni kama ua lenye harufu nzuri ambalo huwavutia nyuki kulitembelea na kuling’ang’ania.Pamoja na uzuri huu sina maisha ya kawaida kama wenzangu.Uzuri huu umenifanya niishi maisha mabovu na yasiyokuwa na hata chembe ya furaha ndani yake .Msichana mwenye uzuri kama wangu anatakiwa aishi maisha mazuri akiwa na mume bora na familia yenye furaha .”alipowaza kuhusu suala la familia mara akamkumbuka jaji Elibariki.
“ Sijui Elibariki na Jason watakuwa katika hali gani hivi sasa.Niliwakutanisha makusudi kabisa ili wamalize tofauti zao.Ninataka kuongea nao wakati hawana tofauti na kwa pamoja tunaweza kusaidia katika kuimaliza team SC41.Nimekwisha dhamiria kukimaliza kikundi hiki kwa hiyo siwezi kufanya jambo hili peke yangu ninahitaji waku wa kunisaida , watu ambao ninawaamini nao si wengineni Elibariki na Jason.Nikifanikiwa kuimaliza Team SC41 basi nitakuwa huru na maisha yangu na nitakuwa na jaji Elbariki mwanaume ninayetaka kuanza naye maisha mapya.Ndiye mwanaume ninayempenda.Sijali kama ana mke au hana yeye ndiye mwanaumeambaye ninataka kuishi naye na lazima niwe naye”akawaza peniela halafu akachukua mkoba wake mwekundu na kujitazama tena katika kioo.
“ Kila kitu kimekaa vizuri.its time now to go” akawaza na kutoka akaingia garini akaondoka kuelekea mahala alikoelekezwa na Amos ili akutane na katibu wa rais dr Kigomba.
“ Hii ni kazi yangu ya mwisho ninakwenda kuifanya kwa kutumia mwili wangu na baada ya kuikamilisha basi nitakuwa huru kuishi maisha ya kawaida kama wengine.Baada ya kazi hii hakutakuwa tena na Team SC41” akawaza peniela akiwa garini
“Natamani kufahamu John anaendeleaje lakini nafsi yangu inakataa kabisa.Ili niweze kujiweka huru natakiwa kwanza kumchukia John mwaulaya na ndipo nitakapoweza kupambana naye vizuri na hatimaye kuimaliza Team Sc41.Najua ni kikundi chenye nguvu lakini nitajitahdi kwa kila namna niwezavyo kuweza kukimaliza kikund hiki nandiyo maana ninawahitaji sana Elibariki na Jason katika jambo hili”akawaza Peniela.
“ Sijawahi kukutana na Dr Kigomba ana kwa ana lakini ni namfahamu kwa sura.Hata hivyo hawezi kunitisha kwani nimekwisha kutana na watu wenye nguvu na wakutisha zaidi yake .Kama nimefanikiwa kumtia Dr Joshua mikononi siwezi kushindwa kumuweka Dr Kigomba mfukoni na akajisahau kabisa.Mimi ndio Peniela na usiku wa leo atanifahamu vizuri”akaendelea kuwaza Peniela .
Hoteli Silvano ni moja kati ya hoteli kubwa za kitalii jijini dare s salaam.Ni hoteli ambayo hutumiwa na watalii wenye uwezo mkubwa kifedha kwani inasemekena ndiyo hoteli inayoongoza kwa kuwa na gharama za juu sana hapa nchini.katika hoteli hii ndiko Peniela na Dr Kigomba watakutana.Geti la kuingilia hotelini hapa lilikuwa wazi peniela akaingia na kuelekea katika maegesho akaegeshagari na kuvuta pumzi ndefu kabla ya kushuka.
“ Hii ni kazi ya mwisho ninakwenda kuifanya” akawaza Peniela na kisha akafungua mlango wa gari akashuka na kuelekea moja kwa moja mapokezi.Katika mlango wa kuingilia ndani ya hoteli alisimama kijana mmoja nadhifu aliyevaa suti iliyompendeza sana akamsalimu Peniela kwa adabu na kumkaribisha ndani.Peniela akatabasamu kwa mapokezi yale mazuri na moja kwa moja akaelekea mapokezi ambako alijitambulisha na bila kupoteza muda kijana mmoja akaitwa na kuombwa aongozane na Peniela kumpeleka sehemu anakotakiwa kuelekea.
Hoteli ilikuwa kimya sana na kwambali katika baa ya hotelini hapo kulisikika muziki wa ala uliokuwa ukiwaburudisha wageni.Peniela alipelekwa hadi ghorofa ya tano na kukaribishwa katika chumba kikubwa na kizuri.Hakukuwa na mtu yeyote ndani ya chumba kile alikuwa peke yake.Baada ya dakika kumi mlango ukafunguliwa wakaingia watu wawili peniela akawatambua mara moja.Walikuwa ni Captain Amos na Dr Kigomba.Dr Kigomba alionyesha mshangao mkubwa baada ya kukutana na Peniela .
“ hallow peniela”akasema Captain Amos akimpa mkono Peniela.
“ naitwa Amos mimi ndiye ambaye nimekuwa nikiwasiliana nawe katika simu” akasema Captain Amos
“ Nafurahi sana kukufahamu Amos” akasema peniela
“ Ninaitwa dr Kigomba.Mimi na Amos ni marafiki wakubwa” akasema Dr Kigomba.
“ Nafurahi kukufahamu dr Kigomba .Nadhani ninyi nyote hatujawahi kuonana “ akasema peniela
“ Hapana hatujawahi kuonana na hata mawasiliano yako nilipata taabu sana kuyapata” akasema captain Amos.
“ Ok vizuri.Uliniambia kwamba unashida kubwa na mimi.Ni shida gani hiyo?akauliza Peniela bila kuchelewa.Hakutaka kupoteza muda
“ Peniela nimekuita tukutane hapa lakini si mimi mwenye shida.Huyu mwenzangu ndiye mwenye shida na wewe.kwa maana hiyo basi nitawaacha ninyi peke yenu muweze kuongea na akueleze ana shida gani” akasema Captain Amos na kuinuka akatoka nje akawaacha mle chumbani Dr Kigomba na Peniela.

NINI KITATOKEA HUMO CHUMBANI ? PENIELA ATATIMIZA AZMA YAKE? TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
SEASON 2
SEHEMU YA 30
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ hallow peniela”akasema Captain Amos akimpa mkono Peniela.
“ naitwa Amos mimi ndiye ambaye nimekuwa nikiwasiliana nawe katika simu” akasema Captain Amos
“ Nafurahi sana kukufahamu Amos” akasema peniela
“ Ninaitwa dr Kigomba.Mimi na Amos ni marafiki wakubwa” akasema Dr Kigomba.
“ Nafurahi kukufahamu dr Kigomba .Nadhani ninyi nyote hatujawahi kuonana “ akasema peniela
“ Hapana hatujawahi kuonana na hata mawasiliano yako nilipata taabu sana kuyapata” akasema captain Amos.
“ Ok vizuri.Uliniambia kwamba unashida kubwa na mimi.Ni shida gani hiyo?akauliza Peniela bila kuchelewa.Hakutaka kupoteza muda
“ Peniela nimekuita tukutane hapa lakini si mimi mwenye shida.Huyu mwenzangu ndiye mwenye shida na wewe.kwa maana hiyo basi nitawaacha ninyi peke yenu muweze kuongea na akueleze ana shida gani” akasema Captain Amos na kuinuka akatoka nje akawaacha mle chumbani Dr Kigomba na Peniela.

ENDELEA…………………
Kimya kikatawala mle chumbani walimobaki Dr Kigomba na Peniela.Uzuri wa peniela ulimchanganya sana Dr Kigomba na kumfanya ababaike namna ya kumuanza.Hakuwahi kukutana ana kwa ana na peniela na hakufikiri kama anaweza kuwa ni mwanamke mzuri kiasi hiki.
“ Amos alikuwa sahihi Peniela ni binti mwenye uzuri usio wa kawaida.Sikuwahi kukutana naye ana kwa ana na kuushuhudia uzuri wake.Ana uzuri ambao siwezi kuuelezea.Siwezi kukubali kumkosa mrembo huyu,lazima nimpate.Nashukuru Dr Joshua kwa kunipa jukumu la kumchunguza Peniela kwa amenikutanisha na malaika.” Akawaza Dr Kigomba .Peniela naye alikuwa ametulia akiwa na glasi yake ya wine akinywa taratibu akimsubri Dr Kigomba aanzishe maongezi.
“ Nimegundua Kigomba tayari ameanza kuniogopa.Nimeiona sura yake namna anavyohangaika kutaka kunianza.Hii ni dalili nzuri kwangu kwamba kazi yangu itakuwa rahisi sana.Ngoja nimsubiri aanzishe maongezi “ akawaza Peniela akiendelea kunywa wine taratibu sana.Dr Kigomba akakohoa kidogo na kurekebisha tai yake akasema
“ maisha yanakwendaje Peniela?
“ maisha yanakwenda vizuri sana.Kila kitu kinakwenda vizuri na ninamshukuru Mungu”
“ Vizuri sana.kazi zinakwendaje?
“ Kazi nzuri tu.Ninaendelea vizuri.Vipi kwa upande wako kazi zinakwendaje? Unafanya kazi hospitali gani? Akauliza Peniela na kumfanya Dr Kigomba acheke kidogo
“ Peniela mimi si daktari wa kutibu magonjwa bali ni daktari wa ssheria.Kuhusu kazi yangu mimi ni katibu wa rais “
“ Wow ! “ Peniela akajifanya kushangaa sana
“ Kumbe niko na mtu mkubwa hapa bila kuelewa.Katibu wa rais ni mtu mzito.Nimefurahi sana kukutana nawe Dr Kigomba”
“ Hata mimi nimefurahi sana kukutana nawe peniela.” Akasema Dr Kigomba
“ Amos naye anafanya kazi gani?
“ Amos naye pia anafanya kazi ikulu kama daktari wa familia ya rais.”
“ Ouh ! Kumbe leo nina bahati sana ya kukutana na watu wazito .”akasema Peniela huku akiachia tabasamu kubwa.Baada ya kimya kifupi Dr Kigomba ambaye alikwisha anza kumzoea peniela akauliza
“ Peniela unajishughulisha na nini sasa hivi baada ya matatatizo yako kumalizika?
“ Unazungumzia yale matatizo ya kesi ? akauliza peniela
“ Ndiyo.Tena naomba nichukue nafasi hii kukupa pole kwa matatizo yale”
“ Ahsante sana Dr Kigomba nimekwisha poa.Ninamshukuru Mungu kesi ilimalizika salama ,mahakama haikunikuta na hatia na ikaniachia huru.Baada ya kesi kumalizika nimerejea tena katika maisha ya kawaida na nimekutana na changamoto nyingi za kimaisha mfano kabla ya kwenda gerezani nilikuwa na maduka makubwa mawili ya nguo na….” kabla hajaendelea dr Kigomba akaingilia kati
“ Niliyafahamu maduka yako,mke wangu alikuwa anapenda sana kununua nguo toka katika maduka yako”
“ ouh kumbe ulikuwa ukiyafahamu maduka yangu.Kwa hiyo baada ya kesi kumalizika nimekuta maduka yangu yamefilisika ,biashara zangu karibu zote zilikufa kutokana na watu kutokuwa waaminifu kwani wengi waliamini kwamba ningefungwa maisha gerezani au kuhumumiwa kifo.Hivi sasa ninajipanga upya ili niweze kuzifufua tena biashara zangu zote” akasema Peniela
“ Pole sana Peniela.Wanadamu hawana wema hata kidogo.lakini usijali kuhusu hilo.Kwa vile sasa uko huru kila kitu kitarejea kama kilivyokuwa awali na hata zaidi ya awali.watu wa kukusapoti na kukushika mkono tupo na mimi nitakuwa mmoja wao katika kuchangia maendeleo yako.Watu waliofanya kitendo kile cha kukusingizia kesi walifanya kitendo kibaya sana lakini serikali ipo na siku moja watabainika tu”akasema Dr Kigomba
“ Mwanaharamu huyu angejua kama ninamfahamu zaidi ya anavyojifahamu wala asingethubutu kuongea upuuzi wake huu mbele yangu.Natamani hata nimvamie nimng’oe pua yake” akawaza Peniela halafu akauliza
“ Dr Kigomba ulisema kwamba una shida na mimi.Ni shida gani hiyo? Akauliza Peniela kwani hakutaka kuendelea kusimuliana hadithi za maisha
“ Uhhm..ni kweli peniela nilikuwa nahitaji sana kukuona na sikujua ningekupata vipi ndiyo maana nikamuomba Amos anisaidie niweze kukupata kwani yeye anafahamiana na watu wengi na angeweza kupata mawasiliano yako.Nashukuru sana hukupuuza wito wake na umekuja kunisikiliza na inaonyesha ni namna gani ulivyo mstaarabu na mwenye adabu”akasema Dr Kigomba
“ Siku zote sina tabia ya dharau na Amos aliniomba kiustaarabu sana nije nionane nanyi na nikaona ni vyema nikavunja ratiba zangu na kuja kukusikiliza” akasema Peniela.Dr Kigomba akafikiri kidogo na kusema
“ peniela nimekuita hapa kwa jambo moja kubwa.”
“ Ndiyo nakusikia Dr Kigomba” akasema peniela huku akimkazia macho
“ Uuhm… Peniela kilichonifanya nitake kukutana nawe usiku huu hapa ni kwamba nimevutiwa nawe,na ninataka mimi nawe tuwe marafiki.kwa ufupi ninahitaji kuwa na uhusiano na wewe.Umenivutia sana Peniela na nimeshindwa kuvumilia kwa hiyo nimekuita hapa ili kukueleza jambo hilo.Ninakupenda sana Peniela na ninataka uwe mpenzi wangu”akasema Dr Kigomba.Peniela akanywa wine kidogo halafu akamtazama Dr Kigomba na kutabasamu
“ Kigomba I can see you have a wedding ring” akasema Peniela huku akicheka kidogo.Dr Kigomba akatabasamu kidogo na kusema
“ To be honest I have a wife and kids and..”
“ kama una mke na watoto unahangaika nini Dr Kigomba? Akauliza Peniela
“ Unajua katika ndoa huwezi ukapata kila kitu unachokihitaji kwa hiyo kama huwezi kupata kitu unachokihitaji basi unaruhusiwa kutoka kwenda kutafuta nje.Ninahitaji mapenzi motomoto ninahitaji vitu vingi ambavyo mke wangu hawezi kunifanyia.Siwezi kuelezea sana jambo hili lakini naomba tu ufahamu kwamba ninakuhitaji sana Peniela.Nitakupatia kila kitu unachokihitaji katika maisha yako.If you need a house,a car au kitu chochote kile nieleze nitakupatia.” Akasema dr Kigomba
“ Dr Kigomba kwa nini unataka kumfanyia hivyo mke wako? Kwa nini unataka kumsaliti na kuvunja kiapo chenu cha ndoa? Akauliza Peniela
“ Ouh Peniela ,naomba tusijadili kuhusu mambo hayo na tujadili kuhusu mimi na wewe.Peniela ninakuhitaji sana uwe mpenzi wangu na nitakufanyia kila kitu unachokihitaji katika katika maisha yako.”
“ Dr Kigomba nashind………….” Akataka kusema peniela lakini Dr Kigomba akamuwahi
“ Peniela kwani una mchumba? Akauliza Dr Kigomba
“ hapana sina mchumba kwa sasa.Mpenzi wangu niliyekuwa naye alikuwa ni edson na akauawa.baada yake sina tena mchumba” akasema Peniela
“ kama ni hivyo kwa nini basi usinipe nafasi hiyo Peniela ? Nipe nafasi ya kukutunza,kukuenzi na kuyafuta majeraha yote ya nyuma uliyoyapata.Ninastahili kabisa nafasi hiyo Peniela.Tafadhali naomba usininyime nafasi hii ya kukuonyesha upendo ”akasema Dr Kigomba
“ Sina muda mrefu wa kuzungushana na huyu paka shume ambaye hata kutongoza hajui,ngoja nimkubalie tu ili niokoe muda kwani natakiwa kuonana na akina Elibariki usiku huu” akawaza Peniela
“ Dr Kigomba umeniweka katika wakati mgumu sana kiasi kwamba ninashindwa kusema hapana kwa ombi lako.Hata hivyo kwa hali niliyo nayo hivi sasa baada ya kuyamaliza yale matatizo ,ninahitaji sana msaada.Ninahitaji sana mtu ambaye anaweza akanikwamua hapa nilipo na kuniwezesha kusimama tena.kwa kuwa umeonyesha kutaka kunisaidia ili niweze kurejea katika maisha yangu ya kawaida basi mimi sina namna nyingine zaidi ya kuridhia ombi lako.Nitakuwa mpenzi wako na nitakutimizia kile ulichokikosa kwa mkeo lakini naomba unihakikishie kwamba hautaniingiza katika matatizo mengine na mkeo wala familia yako.Sihitaji tena matatizo yoyote yale” akasema Peniela.Dr kigomba akainuka na kumfuata peniela pale sofani alikokuwa amekaa.Alikuwa na furaha ya ajabu,furaha ya ushindi wa kumpata kimwana yule ambaye uzuri wake uliyafanya mapigo ya moyo wake yaende mbio.
“ Peniela ahsante sana kwa kunikubalia ombi langu,Huwezi kujua ni furaha kiasi gani niliyonayo moyoni mwangu kwa kunikubalia kuwa mpenzi wako.Ninajiona ni mwanaume mwenye bahati sana kukupata mwanamke mrembo kama wewe.Nakuahidi kwamba sintakuletea matatizo yoyote yale na badala yake nitafanya kila jitihada kuhakikisha kwamba unakuwa na maisha bora zaidi kuliko yale ya awali .Nitakufanyia mambo makubwa ambayo hukuwahi kuyafikiria,I’ll make you a queen.Peniela sisiti kufanya jambo lolote lile kwa ajili yako na usisite kuniambia chochote kile unachokihitaji na nitakufanyia.Ila kuna jambo nataka unihakkishie”
“ Jambo gani Dr Kigomba?
“Ninataka unihakikishie kwamba ni kweli hauna mahusiano na mwanaume mwingine yeyote yule? Kama unaye naomba uniambie ili nijue kwamba nina ingia katika mahusiano na mtu ambaye ana mahusiano na mwanaume mwingine.Mimi pia ni mume wa mtu na nimekuweka wazi kuhusu suala hili na hata pete ya ndoa hii hapa sijaitoa kwa hiyo naomba na wewe uwe wazi kwangu kama kuna mtu ana mahusiano na wewe hata kama ni mume wa mtu nitaelewa.”akasema Dr Kigomba
“ Dr kigomba kwa nini unasisitiza kutaka kufahamu jambo hilo la mahusiano ? Nimekwisha kwambia kwamba sina mahusiano na mtu yeyote yule.Au huniamini?” Akasema peniela
“peniela usinielwe vibaya kusisitiza kulifahamu jambo hili kwa sababu unajua tunaingia katika mahusiano kwa hiyo lazima tufahamiane vizuri.Nitahitaji kuja nyumbani kwako mara kwa mara kwa hiyo sihitaji kukusabishia matatizo ya aina yoyote ile kama una mpenzi wako nahata mimi sihitaji kujisababishia matatizo yoyote.Kwa hiyo ninataka unithibitishie kwamba ni kweli hauna mchumba na uko peke yako”
“Niko peke yangu.Thats all I can say” akasemaPeniela
“ Nashukuru kwa kunihakikishia hilo” akasema Dr Kigomba huku akiendelea kumuangalia Peniela kwa matamanio.Peniela akaligundua hilo naye akajilegeza .Dr Kigomba akamsogelea karibu zaidi
“ Peniela unataka nikufanyie kitu gani? Akauliza kwa sauti ya taratibu halafu akaupitisha mkono wake shingoni mwa Peniela ambaye hakuonyesha kustuka wala kuuondoa.Kigomba akafurahi sana moyoni kwani alichokuwa akikitaka sasa anakaribia kukipata
“ Tell me Peniela unahitaji kitu gani nikufanyie? Akauliza Dr Kigomba na kuusogeza mdomo wake karibu na mdomo wa Peniela.Taratibu Peniela akauinua mkono wake na kuupeleka maeneo nyeti ya Dr Kigomba na kusababisha mvurugano eneo hilo.
“ I want this.I miss this so much”akasema Peniela kwa sauti laini huku akiishika ikulu na kumfanya Dr Kigomba azidi kuchanganyikiwa.Peniela hakutaka kupoteza muda akaanza manjonjo yake .Dr Kigomba naye hakutaka kubaki nyuma naye akaaka kuonyesha umahiri wake katika sekta hii naye akaanza manjonjo yake.Baada ya dakika kumi hali ikazidi kuwa mbaya Dr Kigomba akamuinua peniela na kumpeleka kitandani na bila kuchelewa mchaka mchaka ukaanza.Ulikuwa ni mtanange mkali kwani kila mmoja akitaka kumuonyesha mwenzake ujuzi wake.Mpaka wanamaliza mzunguko mmoja Dr Kigomba alikuwa hoi akihema kwa kasi.Mchaka mchaka aliokimbizwa na peniela haukuwa mdogo.
“ peniela nimekuvulia kofia.Sijawahi kukutana na mjuzi kama wewe katika haya mambo.Nilikuwa sahihi kukutaka mtu kama wewe kwani ndiye unayenifaa.Umenionyesha vitu adimu ambavyo sijawahi kuonyeshwa.Ahsante sana peniela .Sema chochote ukitakacho nami nitakusikiliza na kukitekeleza” akasema Dr Kigomba huku jasho likiendelea kumtiririka.Peniela akatabasamu
“ Nilijua tu,lazima atachanganyikiwa .Mpaka hapa nadhani kazi yangu imekamilika.Nimeuvaa uhusika vizuri na tayari Kigomba ameingia mfukoni.” Akawaza peniela huku akimuangalia Kigomba na kutabasamu
“ Kigomba hata mimi ninashukuru sana kwa raha ulizonipa .Umenipeleka mbio sana.Ngoma hii unajua kuicheza vizuri.”akasema Peniela
“ peniela I’m serious,niambie chochote unachokitaka nikufanyie ili niwe na uhakika kwamba nitakuwa nawe siku zote.Hata ukisema nimuache mke wangu kwa ajili ya kuwa nawe niko tayari” akasema dr Kigomba.Peniela hakujibu kitu akatabasamu
“ Say something Peniela.Neno lako ni amri kwangu” akasema Kigomba
“ Kigomba ninachokihitaji toka kwako ni hiki ulichonifanyia leo.Hicho ndicho ninachokihitaji zaidi kwani ndicho nilichokikosa zaidi’ akasema peniela na Kigomba akamvuta kwake akamkumbatia na kumbusu.
“ Peniela nitakufanyia mambo makubwa sana.naomba uniamini’ akasema Dr Kigomba
“ Ninakuamini Dr Kigomba.Nisigeweza kuuachia mwili wangu kama sikuamini.”akasema Peniela.
“Ahsante sana peniela kwa kuniamini.Usiku wa leo umekuwa ni wa kipekee sana kwangu.”
“ Hata mimi pia usiku huu umekuwa mzuri na umenikutanisha na mtu mkubwa sana katika nchi hii.Nafurahi kukutana nawe.Nadhani sasa baada ya kufahamiana na kuufungua ukurasa wetu mpya basi niruhusu niondoke na tutapanga tena siku na mahali pa kukutana.”
“ peniela kwa nini tusilale leo hapa hapa hotelini? Bado nina hamu sana na wewe’
“ Hapana Dr Kgomba kwa leo haitawezekana kwa sababu sikuwa nimejiandaa kwa kuja kulala.Nina hakika hata wewe pia hukuwa umejiandaa kama leo hii utakuja kulala hapa kwani hukujua kama ningeweza kukukubalia ombi lako.Go back to your wife.Tutapanga siku nyingine ya kukutana na tutakesha usiku mzima nikikuonyesha vitu ambavyo hujawahi kuviona.Next time nataka tukutane kwangu na utakuwa wangu kwa usiku mzima” akasema peniela
“ Natamani sana siku hiyo ifike haraka peniela”akasema Dr Kigomba
“ Vipi kuhusu kesho unaweza kupata nafasi ?
“ Siwezi kukosa nafasi kwa ajili yako Peniela.Niko tayari kuahirisha kila kitu kwa sababau yako”
‘ basi usijali jiandae kwa usiku wa kesho.I’ll be yours for the whole night” Akasema peniela na kumbusu Dr Kigomba halafu akainuka na kwenda kuvaa nguo zake na kisha akamuaga Dr Kigomba akaondoka.
“ Dr Kigomba amechanganyikiwa kabisa mzee wa watu hadi ananitamkia kwamba yuko tayari kumuacha mkewe kwa ajili yangu.Hivi mimi nina kitu gani ambacho kila mwanaume ninayetembea naye ananing’ang’ania na hataki tena kuachana na mimi? akajiuliza Peniela akiwasha gari lake na kuondoka pale hotelini
“ Yawezekana labda kuna kitu nimebarikiwa nacho kinachowachanganya sana hawa wanaume.Hata hivyo ninashukuru mpango wangu umekwenda vizuri sana kama nilivyokuwa nataka.Dr Joshua ,Dr Kigomba wote katika mifuko yangu kwa hiyo kilichobaki hapa ni kuimaliza kazi yangu.Lakini kabla ya yote natakiwa usiku huu nikaonane na Elibariki na Jason.Ngoja kwanza nimpigie simu Mathew” akawaza Peniela na kuchukua simu akampigia Mathew
“ hallow Peniela,habari yako?
“ habari nzuri Mathew.”
“Peniela uko wapi mbona hutokei? Mathew na Jason wanakusubiri mpaka wamekata tamaa kwamba hutakuja tena” akasema Mathew
“ Niko njiani ninakuja nilikuwa na udhuru kidogo.Are they ok? Akauliza Peniela
“ Una maanisha nini kwa swali hilo Peniela? Akauliza Mathew
“ Nina maanisha hawana matatizo yoyote,je wanaongea ?
“ Hawana tatizo lolote na wanaongea vizuri.Ni marafiki wakubwa hawa “ akasema Mathew
“ Ahsante sana Mathew.Niko njiani ninakuja naomba mnisuburi” akasema peniela na kukata simu
“ Ahsnate Mungu kwa Elbariki na jason kupatana.Sasa mipango yangu itakwenda vizuri kama ninavyotaka.Elibariki na Jason ninawahitaji sana katika jambo hili.Halafu kuna kitu nimekuwa nikijiuliza sana bila kupata jibu huyu Mathew ni nani ? Anafanya kazi gani? Kwa nini Elibariki na Jason wanamuheshimu sana ? Nitamuuliza Elibariki anifahamishe kuhusiana Mathew pengine naye anaweza akawa ni mtu wa msaada kwangu katika jambo hili” akawaza Penny
“ natamani sana kujua kama John anaendeleaje lakini kwa namna akivyoniudhi sitaki hata kumsikia.Ngoja kwanza nimalize suala hili la operesheni 26B halafu nitaangalia pengine ninaweza kumsaidia na pengin…………….” Peniela akastuliwa mawazoni na mlio wa simu yake.Alikuwa ni captain amos
“ Halow Amos” akasema Perniela baada ya kupokea simu
“ Peniela good Job.Kigomba amenipigia simu na kunieleza namna alivyochanganyikiwa kwako.Amekiri kwamba hata ile kazi aliyopewa na Dr Joshua ya kukuchunguza haitaki tena yeye anachotaka ni kuwa na wewe tu.Huu ni wakati wetu Peniela wa kuimaliza operesheni 26 B.Endelea kumchanganya Kigomba na nitakuwa nikikufahamisha kila kinachoendelea.” Akasema Captain Amos
“ Usijali Amos.Kigomba tayari nimemuweka mfukoni na ninachosubiri ni kuikamilisha tu operesheni yetu.” akasema Peniela
“ Nitakufahamisha pindi rais atakapomkabidhi Dr Kigomba ule mzigo” akasema Amos na kukata simu.Akaelekea moja kwa moja nyumbani kwake akaoga na kubadili mavazi halafu akaelekea nyumbani kwa Mathew

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………..
 
Cant wait when Penny meets Mathew and company.......Is she going to tell em?how are they going to react?☺☺☺☺☺☺.night night.....
 
Back
Top Bottom