PENIELA SEASON 3
SEHEMU YA 36
MTUNZI 😛ATRICK C.K
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ You devil !! akasema Dr Joshua kwa ukali
“ I’m not a devil Dr Joshua.I’m your angel.Mimi ndiye msaada mkubwa kwako.I’m going to protect you”
“ Protect me ?
“ yes !! I can protect you.Kukuonyesha kwamba mimi ni msaada mkubwa kwako ninakwenda kukuonyesha kitu ambacho you’ve been dying to see. You will thank me “ akasema Rose na kumchukua Dr Joshua wakaelekea ndani.walipoingia sebuleni Rose akawageukia walinzi wa rais
“ Guys you can wait here.We’ll be fine..”akasema Rose.walinzi wale wakaonyesha kutokukubaliana naye
“ Its ok guys.we’llbe fine”akasema Dr Joshua kisha wakaelekea hadi katika chumba alichofungwa Elibariki.Mlango ukafunguliwa na taa ikawashwa.Dr Joshua akapatw ana mshangao mkubwa baada ya kuonana na jaji Elibariki mtu ambaye amekuwa anamuwinda kwa nguvu kubwa usiku na mchana.
ENDELEA………………………
“ Elibariki?!! Dr Joshua akashangaa sana kumkuta Elibariki mle chumbani.Hakuwa ametegemea kabisa kuonana naye ana kwa ana
“ Mr President!! Akasema jaji Elibariki.Hu uso wake ukiwa umejikunja kwa hasira Dr Joshua akamgeukia Rosemary Mkozumi
“ What is the meaning of this Rose? Akauliza kwa ukali
“ Dr JoshuJaji Elibariki ni mtu ambaye ulikuwa unaota kumpata usiku na mchana.Umetumia nguvu kubwa ya vyombo vya dola kumtafuta lakini mpaka sasa hawajafanikiwa kumpata na wasingeweza kumpata kamwe.He wants to talk to you! akasema Rose
“ This man is ..!! akasema kwa ukali Dr Joshua lakini Rose akamzuia
“ Usihamaki Dr Joshua.You have to talk to him.Nakuhakikishia kwamba hutajuta kuzungumza naye” akasema Rose.Uso wa Dr Joshua ulionyesha hasira za wazi
“ hatimaye nimekupata mwanaharamu wewe.Nina hasira nawe sana .Wewe ni chanzo cha matatizo yangu mengi.Ni wewe uliyesababisha hadi mwanangu Flaviana akafariki.Ninakuchukia Elibariki na ninatamani hata nikuvamie na kukuua kwa mikono yangu mwenyewe.” Akawaza Dr Joshua huku akiuma meno kwa hasira halafu akachukua kiti akaketi .
“ Rose sijapendezwa kabisa na hiki ulichokifanya.Huyu mtu ni mhalifu na mida hii anatakiwa awe gerezani.Huyu ni chanzo mwanangu Flaviana kufariki dunia.I hate this man !!.Kwa nini umemuhifadhi hapa kwako?.akasema Dr Joshua kwa hasira
“Dr Joshua kwa nini tusiokoe muda na kuongea mambo ya msingi? Sisi sote hapa tunafahamu kila kinachoendelea na kwamba hayo yote unayoyasema hayana ukweli hata kidogo,Elibarikihahusiki hata kidogo katika kifo cha mkeo wala mwanao.You killed them yourself.” Akasema Rose na Dr Joshua hakujibu kitu akabaki anamtazama kwa hasira
“ Kwa taarifa yako Dr Joshua ni kwamba jaji Elibariki ndiye aliyeniokoa mimi mahala nilikokuwa nimefungwa nikiteswa na aliniokoa kwa dhumuni la kutafuta msaada wangu na msaada aliokuwa anauhitaji ni kuongea nawe.Kuna jambo la muhimu anataka kuzungumza nawe.Tafadhali msikilize” akasema Rose
“ Unataka kunieleza nini? Akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ Dr Joshua ahsante kwa nafasi hii na sitaki kuchukua muda wako mwingi nataka nijielekeze moja kwa moja katika kile ambacho kimenifanya nitake kuonana nawe.” Akasema Jaji Elibariki
“ Kwanza ninataka kuchukua nafasi hii kukupa pole kwa msiba wa mwanao na mke wangu Flaviana.Nimeumia sana kwa msiba ule japokuwa ninatuhumiwa kusababisha kifo kile.Mr President sote tunafahamu kwamba sikuhusika kabisa na kilichotokea usiku ule na wala sikuwa nimelipanga shambulio lile na hata siku moja nisingeweza kumdhuru mke wangu na wewe unafahamu kabisa nani waliomuua Flaviana lakini kwa kuwa una hasira mimi ukaamua kuniangushia kesi ile mbaya ya kusababisha mauaji” akasema Elibariki na Dr Joshua akaendelea kumuangalia kwa hasira.Elibariki akaendelea.
“ Yote haya yalianza baada ya kifo cha Dr Flora.Mazingira ya kifo cha Dr Flora yalimfanya Flaviana aingiwe na shaka na hivyo akaniomba nimsaidie kufanya uchunguzi kubaini nini kilichomuua mama yake.Kwa kushirikiana na wenzangu tulifanikiwa kugundua sababu ya kifo cha Dr Flora kwamba aliuawa kwa kuchomwa sindano ya sumu na hapo ndipo nilipoanza kuwindwa.Nilinusurika kuuawa na nikaokolewa na mwanamke mmoja ambaye simfahamu nikaenda kujificha kwa Pen………”
“ Hebu ngoja kwanza Elibariki,Unasema kwamba uliokolewa na mwanamke.Unamfahamu mwanamke aliyekuokoa? Akauliza Dr Joshua
“ Hapana simfahamu .Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonana naye na sifahamu ni kwanini aliniokoa.”
“ Unaweza ukanielezea muonekano wa mwanamke huyo ? Akauliza Dr Joshua
“ Ni mrefu kidogo,alikuwa na uso mpana na wenye macho madogo.Kingine ninachokikumbuka ambacho kinaweza kunipa urahisi kumtambua hata kama nikikutana naye kesho alikuwa na kovu katika jicho lake la kushoto.Mdom....
“ Wait ….!! Akasema Dr Joshua
“ Mkono wake wa kushoto una kovu la kuungua?
“ Sikuliona kovu hilo lakini alikuwa amevaa glovu mkono mmoja wa kushoto ila shingoni upande wa nyuma alionekana kama vile ana kovu la kuungua “ akasema jaji Elibariki
“ That’s Jesica!!.Ouh my God .I cant believe this.Jessica !!!..akasema kwa mshangao Dr Joshua
“ Unamfahamu? Akauliza Rosemary
“ Ninamfahamu.Anafanya kazi idara ya usalama wa taifa.Aliwahi kuwa mlinzi wangu wakati Fulani nikamuondoa baada ya kutoridhishwa na tabia zake.Ama kweli nimejifunza katika hii dunia usimuamini mtu yeyote Yule.Who sent her to help him??” akasema Dr Joshua.
“ I’ll find her and she will answer to me everything !! akasema Dr Joshua kwa hasira.
“ Endelea na simulizi yako “ Dr Joshua akamwambia Elibariki.
“ Nilipookolewa nilienda kujificha kwa Peniela na baadae nikachukuliwa na Mathew .”
“ Kwa hiyo taarifa za wewe kujificha kwa Peniela zilikuwa za kweli!! Akasema Dr Joshua
“ ni kweli nilijificha kwa Peniela kwa muda halafu nikaenda kujificha kwa Mathew.”
“ Who is Mathew?!!
“ He’s a monster who did this to me !!..akasema Rosemary
“ Mathew ni rafiki yangu ambaye ni mpelelezi wa kujitegemea ambaye ndiye aliyenisaidia katika kufahamu ukweli kuhusiana na kifo cha Dr Flora.Kwa kushirikiana naye tumegundua mambo mengi sana kuhusu wewe na hasa hili kubwa linaloendelea hivi sasa linalohusiana na kirusi Aby.Dr Joshua mambo ya kukuambia ni mengi lakini kwa kuokoa muda ninataka tuongelee mambo yanayotuhusu mimi na wewe.” Akasema jaji Elibariki .Dr Joshua akachomoa kitambaa mfukoni akajifuta jasho.Maneno aliyoambiwa na Elibariki yalimstua sana
“ Mr President ninajua ninatafutwa kila kona kwa agizo lako na endapo nikikamatwa maisha yangu yataharibika kwani nitaozea gerezani.Sitaki hilo linitokee.Nilijifanya jasiri kutaka kushinda nawe lakini hakuna nilichokipata zaidi ya kuwa mkimbizi nikijificha kama Sungura.Nimeinua mikono vita hii imenishinda.Siwezi kupambana nawe mheshmiwa rais kwa hiyo nimekuja kwako kukuomba msamaha sana kwa yale yote niliyokukosea .Nataka unisamehe na unirudishie maisha yangu ya kawaida tena.Nataka unifutie kesi inayonikabili na niendelee na kazi zangu kama kawaida .” akasema jaji Elibariki.Dr Joshua akamtazama akajifuta tena jasho halafu akasema
“ Natamani sana nikuamini tena jaji lakini kwa mambo uliyonifanyia siwezi kukuamini tena.Naomba nikuweke wazi kwamba ninakuchukia sana, sana, tena sana.Wewe ni adui yangu namba moja na lengo langu ni kukukuondoa kabisa katika uso wa hii dunia.Nilikuamini sana Elibariki nikakupa cheo kikubwa cha jaji wa mahakama kuu lakini badala yake ukaanza kunipuuza na hukunisikiliza tena.Sioni namna ya kukuamini tena Elibariki na kwa vile nimekwisha kuona hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutumia nguvu zangu zote nilizonazo kuhakikisha kwamba unapotea katika uso wa dunia.Ni heri ungebaki katika maficho yako kuliko kujitokeza.Umejileta mwenyewe katika mdomo wa mamba na ninakuhakikishia kwamba huu ndio mwisho wako.!! Akasema Dr Joshua kwa ukali.
“ He can be trusted ! akasema Rose
“ What ? Dr Joshua akashangaa
“ Do you trust this guy? Do you know who he is?akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ Yes I do trust him and you have too” akasema Rose.Dr Joshua akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Unanishangaza sana Rose.Huyu mtu hafai kabisa kuaminiwa.Amenifanyia mambo mengi sana ambayo siwezi kumsamhehe hata aseme nini !!
“ Dr Joshua naomba unisikilize.Nimekuleta hapa makusudi kabisa ili uweze kuonana na Elibariki mtu ambaye umekuwa ukiota kumpata usiku na mchana.Huyu ndiye aliyekuwa kikwazo kikubwa katika mpango wako wa kuuza kirusi Aby.Unapaswa ufurahi badala ya kukasirika .Kwa sasa huyu ndiye mkombozi wako.Huyu ndiye anayeweza akasababisha ukaimaliza biashara yako kwa amani na salama”
“ Huyu awe mkombozi wangu??? Rose nashindwa kukuelewa kwa nini unamuamini sana huyu mtu.Hafai huyu kuaminiwa hata kidogo.!!!! Akasema kwa ukali Dr Joshua
“ Ninamuamini kwa sababu ndiye aliyeniachia mimi huru kutoka mahala nilikokuwa nimefungwa.Aliwasaliti wenzake na kuniachia huru kwa lengo la kutaka nikukutanishe naye tu.Hata ukimuangalia machoni anamaanisha kile anachokiongea.Amechoka kukimbia kimbia huku na kule kila siku kujificha.He needs his normal life back na mtu pekee ambaye anaweza akalifanya hilo ni wewe. Elibariki alikuwa anashirikiana na watu ambao walikuwa wanakufuatilia usiku na mchana na ambao wana nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba mpango wako wa kuiuza package ile haufanikiwi.They are dangerous people and I swear kama ukipuuza basi huu utakuwa ni mwisho wako.Wana kila ushahidi wa kuweza kukutia hatiani.Elibariki anafahamu kila mpango wao namna walivyojipanga kukuangusha na anaweza akawa ni msaada mkubwa sana kwako” akasema Rose.Dr Joshua akamtazama tena kwa makini kisha akasema
“ Ni ya kweli hayo anayosema Rose? Watu hao uliokuwa unashirikiana nao ni akina nani? Wamepanga mipango gani kuhusu mimi? Akauliza Dr Joshua
“ Mr President anachokisema Rosemary ni kitu cha kweli kabisa.Nimeshirikiana na wenzangu ambao lengu letu lilikuwa ni kuhakikisha kwanza mpango wako haufanikiwi na pili ni kuhakikisha kwamba unapatikana ushahidi wa kutosha wa kuweza kukutia hatiani kwa kifo cha mkeo Dr Flora.Nimetafakari sana na nikaona kwamba hata kama tukifanikiwa kuizuia mipango yako na kufanikiwa kukufikisha mbele ya sheria ,hakuna faida yoyote ambayo ninaweza nikaipata kwani mimi bado nina kesi ya kujibu ya kusababisha kifo cha Flaviana.Ni wewe pekee ambaye unaweza ukanirejeshea maisha yangu ya kawaida hivyo nikaona njia pekee ni kuwasaliti wenzangu na kuonana nawe,nikuombe msamaha na tuweze kuyamaliza haya mambo.Dr Joshua tafadhali naomba uniamini kwamba haikuwa kazi rahisi kuwasaliti wenzangu na kumuachia huru Rosemary lakini nimefanya hivyo kwa lengo moja tu la kutaka kuishi maisha yangu ya kawaida” akasema jaji Elibariki
“ Jaji una maneno mazuri ambayo yananifanya nitake kukuamini tena lakini bado hujanishawishi nitawezaje kukuamini mtu ambaye nilikupenda kama mwanangu na nikakuamini lakini ukanigeuka na kunifanyia mambo ya ajabu kama uliyoyafanya? Kama nikikuamini leo hii nitakuwa na uhakika gani kwamba hutakuja kunigeuka tena na kunisaliti? Akauliza Dr Joshua
“ Mr President naomba uniamini.Najua bado haitakuwa rahisi kuniamini moja kwa moja lakini naomba nikuhakikishie kwamba I know things that you want to know so badly .I can tell you all the plans they have on you,nitakusaidia hata kuweza kuwapata hao wenzangu wote lakini nitayafanya hayo tu endapo utakuwa tayari kunisamehe na kunirejeshea uhuru wangu,kunirejeshea maisha yangu ya kawaida,kunirejeshea kazi yangu na kulisafisha jina langu.” Akasema jaji Elibariki.Dr Joshua akamtazama kwa zaidi ya dakika moja halafu akamgeukia Rose na kusema
“ Rose naomba tutoke tuongee nje kidogo”
Dr Joshua na Rose wakatoka nje ya kile chumba
“ Rose unaniweka katika wakati mgumu sana na kunitaka nimuamini huyu jamaa tena.Huyu ni mtu mbaya mno !! akasema Dr Joshua
“ Right now this is the only guy you need to trust with your life” akasema Rose
“ Elibariki anafahamu mambo yako yote na vile vile anifahamu mipango yote waliyoipanga akina Mathew juu yako.Tafadhali usiache kumuamini tena jaji.Hautapoteza kitu kama ukimuamini tena.Utafanikiwa katika malengo yako na wabaya wako wote watashindwa. This is your last call Mr President” akasema Rose..Dr Joshua akainama akafikiri kwa kama dakika mbili hivi halafu akasema
“ Ok nitafuata ushauri wako na nitamrejeshea Elibariki uhuru wake lakini anatakiwa aonyeshe kwanza juhudi za kunishawishi nimuamini kwa kuniwezesha kuikwepa mipango yote iliyopangwa na hao jamaa zake na kuwafutilia mbali na kama nikifanikiwa basi nitamuamini lakini kama ananidanganya I’ll kill him...”
“ That’s good.! Akasema Rose
“ What about me .Bado hujanipa jibu lolote lile kuhusu yale tuliyoongea.Kumbuka Elibariki works under my command !! akasema Rose.
“ Kuhusu suala la kwanza, nitakuweka katika mgawo endapo biashara ikifanikiwa kwenda vizuri.Suala la pili ninaomba niondoke nalo nikalitafakari kwanza na kuona namna ninavyoweza kulifanyia kazi na kisha baada ya msiba wa mwanangu kumalizika mimi na wewe tutakuwa na kikao kulijadili suala hili kwa upana wake lakini nakuhakikishia kamba nitakusaidia kwa sababu hata wewe umenisaidia sana kumpata huyu mtu ambaye vyombo vya dola vimeshindwa” akasema Dr Joshua kisha wakarejea ndani
“ Jaji ,nimeongea na Rose na amenishawishi nikubali kukuamini tena.Nimekubali kulifanya hilo na nitakurejesha uhuru wako.Nitaliondoa agizo la kukusaka,na utaendelea na maisha yako ya kawaida lakini kama tu ukiniwezesha kuwapata hao jamaa zako pamoja na kunieleza mipango yote waliyoipanga juu yangu.Endapo ukishirikiana nami vizuri basi unaweza ukafaidika sana badala ya kutaka mapambano na mtu kama mimi na unaishia kutanga tanga kama ndege.Nakuhakikishia kwamba endapo utanisaidia katika hili basi utafurahi mwenyewe.Utakuwa na maisha mazuri sana na utajilaumu kwa nini hukushirikiana nami toka mapema.Pamoja na hayo nataka nikuonye kwamba tayari unafahamu mambo yangu mengi kwa hiyo ninachokitaka kingine ni kuufunga mdomo wako.Sitaki uropoke chochote kama watu wengine ambao niliwaamini lakini kumbe ni wasaliti wakubwa kama akina Amos.Kitu cha mwisho ninachotaka kuwa muwazi kwako ni kwamba kwa sasa kwa kuwa bado sijarejesha imani kubwa kwako sintakupa nafasi ya kupumua. Nitakufuatilia usiku na mchana na kila mahala uendako utaongozana na mlinzi nitakaye mteua mimi na utachunguzwa katika kila unachokifanya,kila simu unayopiga na kila unayeongea naye.Nikiridhika kwamba unafaa kuaminiwa basi nitakuacha uwe huru kufanya unavyotaka lakini kwa sasa hadi hapo baadae you’ll be under my control!! Akasema Dr Joshua
“ Tumeelewana Elibarki?
“ Ndiyo Mr President,tumeelewana.!! Akasema Elibariki.
“ Mfungueni hizo pingu nitaondoka naye ili akahudhurie msiba wa mke wake” akasema Dr Joshua.Rose akampigia simu Fernando mlinzi wake na kumtaka afike mara moja naye hakupoteza muda akafika akamfungua jaji Elibariki pingu alizokuwa amefungwa
“ Take him somewhere to clean up.Hatakiwi kuonekana kama ametoka kifungoni” akasema Dr Joshua halafu wakatoka mle chumbani wakaongozana hadi sebuleni ambako Dr Joshua akakaribishwa kinywaji wakati akimsubiri jaji Elibariki aweze kuoga na kujiweka safi. Rosemary akamchukua Elibariki hadi katika chumba kilichokuwa cha Henry akamuacha mle ili aweze kuoga .Baada ya kuoga akagongewa mlango na kuletewa suti nzuri ya gharama iliyokuwa ya Henry.Elibariki akavaa na kupendeza kisha akashuka ngazi hadi sebuleni alikokuwako Dr Joshua.
“ Now you look like a gentleman.” Akasema Dr Joshua
“ Kwa sasa usijibu chochote endapo ukiulizwa mahala ulikokuwa na kuhusiana na shambulio lile ulilonusurika na lile lililosababisha kifo cha mkeo” akasema Dr Joshua kisha akaongozana na jaji Elibariki hadi katika gari wakapanda na kuagana na Rose wakaondoka.
“ Later tonight,me and you we’ll have a long and serious talk” akasema Dr Joshua na jaji Elibariki akatikisa kichwa kukubaliana naye
“ Elibariki anaonekana kufahamu mambo mnegi sana kuhusiana na kila ninachokifanya.Ameamua kurudi mwenyewe na kuomba msamaha .Kama angelifanya hivi mapema wala tusingefika hapa tulipofika.Tungeweza kupiga hatua kubwa sana na wala asinge hitaji tena hata kufanya kazi.Tatizo la hawa vijana wanatafuta ushujaa lakini matokeo yake ndiyo haya amekosa muelekeo na maisha yake yameharbika.Na kama asingestuka mapema na kuja kuniomba msamaha ningemfutilia mbali toka katika uso wa dunia.” Akawaza Dr Joshua
“ Hawa watu anaoshrikiana nao ni akina nani? Wanaonekana ni watu makini sana na wenye ujuzi wa hali ya juu kiasi cha kuweza kufahamu kila ninachokifanya.Watu hawa hawatakiwi kuachwa hai hata kidogo.NI watu ambao natakiwa kuwaondoa haraka sana “ akawaza Dr Joshua
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………