Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 34


MTUNZI 😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ celline siku nyingine ukiingia uwe unabisha hodi ,umenistua sana nilikuwa mbali kimawazo”akasema Rose
“ samahani madam.”akajibu Celline huku akitabasamu
“ madam nimekuja kukutaarifu kwamba lile zoezi limekamilika na mpaka sasa hivi tayari waandishi wa habari wamekwisha anza kuwasili.Kila kitu kitakwenda kama vile ulivyoagiza .Waandishi toka vyombo vyote vikubwa vya habari watakuwepo.kwa hiyo ninaomba sasa uingie ndani na uanze kujiandaa kwa ajili ya kuongea na waandishi wa habari.”akasema Cellne

“ Good Job celline.halafu bado kuna jambo moja ninataka ulifane.Ninataka niwasiliane na Dr Kigomba Yule katibu wa rais.” Akasema Rose

“ Sawa madam ngoja nimtafute simuni halafu nitakupa uongee naye” akasema Celline na kumsaidia Rosemary kunyanyuka akaelekea chumbani kwa ajili ya kujiandaa kuongea na waandishio wa habari




ENDELEA………………………….



Dege la rais linalotajwa kushika nafasi ya pili kwa ufahari barani afrika lilionekana katika anga ya jiji la Dare s salaam.Ni dege aina ya Boeng 747 inayotumiwa na Dr Joshua rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Mara tu alipoingia madarakani Dr Joshau aliidhininisha kiasi kikubwa cha pesa kwa ajii ya kununua dege hili kubwa la kifahari
Uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere ulifurika watu waliokuja kuupokea mwili wa Flaviana mtoto wa rais unaorejeshwa nchini kutokea nchini afrika ya kusini alikopelekwa kwa matibabu .Viongozi mbali mbali wa serikali walikuwepo uwanjani pale kwa ajili ya kuungana na familia ya katika mapokezi ya le ya mwili wa Flaviana.
Taratibu dege lile kubwa la kifahari likaanza kutua kugusa ardhi likienda kwa kasi kubwa na baadae likaanza kureejea taratibu na kusimama.Mlango wa ndege ukafunguliwa na maafisa kadhaa wa usalama pamoja na baadhi ya viongozi wakaingia ndani ya ndege kuonana na rais.Miongoni mwa watu waliongia ndegeni alikuwepo Dr Kigomba katibu wa rais na mshirika wake mkubwa.
“ Pole sana Mr President “ akasema Dr Kigomba mara tu alipoonana na rais

“ Kila kitu kinakwenda vizuri Kigomba? Akauliza Dr Joshua na kisha Kigomba na maafisa wengine wakamuelezea rais namna kila kitu kuhusiana na msiba ule kinavyokwenda na maandalizi yaliyokwisha fanyika.Rais akatoa maelekezo kadhaa na kisha baadhi ya maafisa walioambatana na rais wakaanza kushuka ndegeni na halafu akashuka Anna mtoto pekee wa rais aliyebakia akiwa ameongozana na shangazi yake .Alikuwa amevaa mavazi meusi na macho yake aliyafunika kwa miwani mikubwa ili yasionekane namna yalivyokuwa yamevimba kwa kulia
Baadhi ya ndugu walipomuona Anna wakaangua kilio kikubwa pale uwanjani hali iliyomlazimu Anna naye kujiunga nao kulia .Watu wengi wakiwemo ndugu na marafiki zake walikuja kumpa pole.Baada ya kama dakika kumi hivi Dr Joshua akamaliza kikao kifupi na maafisa wale waliomfata ndegeni , akashuka.Viongozi mbali mbali walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kumpa pole .Dr Joshua akasalimiana nao wote na kisha wakajipanga ili kushuhudia mwili wa Flaviana ukishushwa ndegeni. Taratibu jeneza lenye mwili wa Flaviana likashushwa na kupakiwa katika gari maalum lililoandaliwa kwa ajiliya kuupeleka hospitali .Shughuli uwanjani hapo zikamalizika na Dr Joshua akaingia katika gari lake na kuondoka na msafara wake kuelekea katika makazi yake binafsi ambako ndiko shughuli zote za msiba zingefanyika.Mwili wa Flaviana ukapelekwa kwanza hospitali ambako ungekaa huko wakati taratibu za mazishi zikiendelea.
Katika makazi binafsi ya rais watu walikuwa ni wengi sana.Rais akawasili na kupokewa na vilio vya akina mama ,akasalimiana na watu mbali mbali waliokuja kumpa pole na halafu akaenda kuungana na wazee waliokuwapo pale msibani.Baada ya nusu saa za kukaa na wazee pia kupokea mkono wa pole toka kwa watu mbali mbali, Kareem mmoja wa walinzi ambao Dr Joshua anawaamini sana akamfuata na kumwabia kwamba Dr Kigomba anahitaji kuonana naye katika chumba cha maongezi ya faragha .Dr Joshua akawaomba radhi wale wazee aliokuwa amekaa nao akazunguka mlango wa nyuma na kuingia ndani na moja kwa moja akamfuata Dr Kigomba katika chumba cha maongezi ya faragha.
“ Kigomba mambo yanakwendaje?

“ Dr Joshua samahani kwa kukusumbua lakini imenilazimu kufanya hivyo .Kuna mtu anataka kuongea nawe.Ni mtu muhimu na amesisitiza sana kutaka kuongea nawe sasa hivi.” akasema Dr Kigomba
“ Ninani? Akauliza Dr Joshua
“ Ni Rosemary Mkozumi”

“ Rosemary? Anataka nini ?

“ Atakueleza mwenyewe katika simu lakini kikubwa alichokisema ni kwamba anataka akupe pole kwa matatizo lakini najua lazima kuna suala lingine” akasema Kigomba .Dr Joshua akavuta pumzi ndefu alionekana kushtushwa sana aliposikia Rosemary anataka kuongea naye

“ Mbona umestuka sana Dr Joshua? Akauliza Dr Kigomba

“ That woman is a snake.Yeye na mume wake ni nyoka wenye sumu kali sana.Nimeshangaa sana kutaka kuongea nami wakati mimi na yeye hatuna mazoea ya kupigiana simu na kama ulivyosema lazima kuna jambo anataka kuniambia.Vipi kuhusu Peniela uligundua chochote toka kwake kuhusu mahusiano yake na Elibariki? Kuna maendeleo yoyote yamefikiwa kufahamu mahala alikojificha Elibariki?

“ Mpaka sasa hakuna taarifa zozote za mahala alikojificha Elibariki.Anaonekana amejificha mahala ambako si rahisi kuonekana lakini ninakuhakikishia kwamba lazima atapatikana.Kwa Peniela nilijaribu kumchunguza lakini hakukuwa na dalili zozote kwamba yeye na Elibariki wana mahusiano.Nadhani chanzo cha taarifa hakikuwa na uhakika”
“ Ok good.Hata hivyo lazima tuikamilishe biashara yetu as soon as possible.Kama nilivyokufahamisha awali kwamba Hussein anawasili leo jioni kwa hiyo inabidi ukampokee na kuhakikisha anakuwa salama halafu tujipange ili tuweze kumaliza biashara yetu.Hatutakiwi kuendelea kuchukua tena muda mrefu kwani kadiri tunavyozidi kuchukua muda mrefu ndivyo tunavyozidi kupata athari kwa hiyo suala hili halitakiwi kuchukua zaidi ya siku tatu kuanzia sasa.Nataka baada ya msiba wa Flaviana kumalizika na sisi tuwe tumemaliza biashara yetu .Hakuna tena cha kusubiri kwani jamaa tayari wamekwisha tulipa pesa yote kilichobaki ni kiasi kidogo sana ambacho wanaweza wakakikamilisha muda wowote kwa hiyo anza kufanya maandalizi ya mahala ambako makabidhiano yatafanyika .Iwe ni sehemu tulivu na salama sana.” Akasema Dr Joshua.
“ Sawa Dr Joshua nitashughuilikia kila kitu usijali” akasema Dr Kigomba
“ Tutajadili masuala haya baadae kwa utulivu lakini kwa sasa nataka niongee na huyo Rosemary Mkozumi nisikie anachokitaka” akasema Dr Joshua na Dr Kigomba akachukua simu yake akazitafuta namba Fulani akapiga
“ Hallow Celline ,mheshimiwa rais yuko tayari sasa kuzungumza na madam Rose” akasema Dr Kigomba na kumpatia simu Dr Joshua halafu akatoka nje ya kile chumba kumpa nafasi Dr Joshua
“ Hallow mheshimiwa rais” akasema Rosemary Mkozumi

“ Hallow Rose.Habari za siku nyingi?
“ Habari naweza kusema ni nzuri na si nzuri pia.kwanza pole sana kwa matatizo yaliyokupata wewe na familia yako kwa kumpoteza Flora na mwanao Flaviana” akasema Rose

“ Ahsante sana Rose.Ni mapenzi ya mungu kwa hiyo hatuna budi kukubaliana nayo japo tunaumia.Nimestuka kidogo nilipoambiwa kwamba unahitaji kuzungumza nami” akasema Dr Joshua
“ Ouh Dr Joshua kitu gani kimekustua? Am I an enemy? Akauliza Rose huku akicheka kidogo
“ Hapana si hivyo Rose,unajua mimi na wewe hatuna mazoea ya karibu sana ya kupigiana simu na ndiyo maana nimestuka na kujiuliza maswali mengi kwamba Rose anataka kunieleza jambo gani? akasema Dr Joshua
“ Usiogope Dr Joshua hakuna jambo lolote baya ila ni kweli kama ulivyosema kwamba mimi na wewe hatuna mazoea ya karibu sana ya kupigiana simu lakini from now onwards we’ll be very close friends.” Akasema Rose

“ Nitafurahi sana Rose” akajibu Dr Joshua
“ Dr Joshua samahani sana kwa kukusumbua katika wakati huu wa matatizo lakini dhumuni kuu ni kutaka kuonana nawe.” Akasema Rose

“ Unataka kuonana nami? akauliza Dr Joshua kwa mshangao kidogo
“ Ndiyo ninataka kuonana nawe. Kuna mambo kama mawili matatu hivi ya muhimu sana ambayo nataka kuzungumza nawe ana kwa ana”
“ Ni mambo gani hayo hatuwezi kuzungumza simuni?
“ Hapana Mr President ni mambo mazito ambayo hayafai kuzungumzwa simuni.Mimi na wewe tunapaswa kuonana na kuongea” akasema Rose
Dr Joshua akafikiri kwa sekunde kadhaa na kusema
“ Ok unataka tuonane lini na wapi?
“ We have to meet today.Tuonane leo hapa hapa nyumbani kwangu mida ya saa tisa kama itawezekana” akasema Rose
“ Saa tisa haitawezekana,nina miadi ya kuonana na mtu muhimu sana mida hiyo na halafu niko hapa msibani wageni wengi wanakuja kunipa pole.Vipi jioni ya leo”

“ Sawa Dr Joshua.Tuonane jioni ya leo ila nakuomba usikose kwani ni mambo ya msingi sana ambayo tunataka kuyajadili na ninakuhakikishia utafurahi mwenyewe” akasema Rose

“ Nitafika Rose bila kukosa” akasema Dr Joshua na kukata simu

“ Huyu Rose anataka kunieleza jambo gani? Nimekwisha sikia taarifa za huyu mama anasemekana ni mtu hatari sana na mwenye mtandao mkubwa.Kuna uwezekano akawa tayari amepata taarifa za kuhusiana na package ? Lazima kuna jambo kwani huyu mama hawezi kutaka kuona na mimi hivi hivi kwa suala ambalo halina maslahi kwake.Anyway nitakwenda kuona anaye nimsikie anataka nini.” Akawaza Dr Joshua .
“ Mchana wa leo ninataka kuona na Peniela.Ninahamu sana ya kuonana na Yule mtoto.Toka aliponipigia simu jana nimekesha ninamuota yeye.Huyu msichana ndiye faraja yangu na wakati huu wa matatizo haya ninamuhitaji sana.Nitampigia simu kumtaarifu kwamba tayari nimekwisha rejea” akawaza Dr Joshua na mlango ukafunguliwa akaingia Dr Kigomba
“ Is everything ok Mr President? Akauliza Dr Kigomb
“ Everything is fine.Rose anasema kuna jambo anataka kuongea na mimi na hajanieleza ni jambo gani.Nitakwenda jioni kuonana naye nyumbani kwake” akasema Dr Joshua
“ Sawa Dr Joshua nimepata taarifa kwamba balozi wa India amekuja.Nadhani uende ukaonane naye” akasema Dr Kigomba na Dr Joshua akatoka kwenda kuonana na balozi wa India.



********


Waandishi wa habari kutoka karibu vyombo vyote vikubwa vya habari waliitika wito na kufika kwa wingi nyumbani kwa Rosemary Mkozumi.Ukaguzi ulikuwa mkali sana kuhakikisha kwamba hakuna kati yao aliyekuwa na silaha ya aina yoyote.Waandishi wote walipokewa na kupelekwa bustanini ambako ndiko Rose angefanya nao mkutano
Saa nane na dakika saba Rose akiwa anasukumwa katika kiti cha magurudumu akajitokeza na kuelekea moja kwa moja katika meza kuu .Celline akawafuata waandishi wale na kuwauliza kama kila kitu kiko tayari na kama wanaweza kuanza.Kila kitu kilikuwa tayari hiyo moja kwa moja mkutano kati ya Rosemary Mkozumi na waandishi wa habari ukaanza

“ Ndugu zangu waandishi wa habari kwanza kabisa ninapenda kuwashukuru sana kwa kuitika wito na kufika kwa wingi japokuwa taarifa zimewafikia kwa kuchelewa sana.Ahsanteni sana kwa kufika kwenu.” Akaanzisha kikao Rose

“ Nimewaiteni hapa kuzungumza nanyi na kupitia ninyi taifa zima la Tanzania liweze kupata habari hii.Nina mambo moja kama si mawili ambayo ninataka kupitia kwenu watanzania waweze kuyafahamu.” Akanyamaza kidogo halafu akasema

“ Jambo la kwanza ambalo ninataka kuwafahamisha watanzania ni kwamba siku ya jana mida ya saa tano asubuhi nilivamiwa hapa nyumbani kwangu na watu wasiojulikana wakamuua mpenzi wangu kwa risasi na mimi wakaniteka.Ninaposema mpenzi wangu najua wengi wenu mtashangaa kwani mnamfahamu Deus Mkozumi kama mume wangu lakini mimi na yeye tulikwisha tengana muda mrefu na kila mmoja kwa sasa yuko huru na maisha yake kwa hiyo mimi nilikuwa na mpenzi wangu ambaye aliuawa na wavamizi hao.” Akanyamaza kwa sekunde kama tano hivi kisha akaendelea
“ Baada ya kuniteka wavamizi hao walinipeleka mahala nisipokujua wakanifunga na kunitesa sana.Walinitoboa sehemu mbalimbali za mwili wangu kwa kutumia mashine ya kutobolea na kama haitoshi walinikata vidole viwili vya miguu.Walinitesa sana .”
“ Ndugu waandishi wa habari mimi nimekuwa katika siasa kwa muda mrefu na nilimsaidia sana rais mstaafu Deus Mkozumi wakati huo nikiwa mke wake na kama mnavyofahamu kazi ya siasa ina maadui wengi na hasa pale unapokuwa unafanya vizuri .Hata mimi pia kuna watu ambao wananichukia hasa kutokana na kufanikiwa katika shughuli zangu za kisiasa na hasa zile zinazogusa maisha ya watu wa hali ya chini.Nimekuwa mstari wa mbele sana katika kuamsha ari na mwamko wa kisiasa kwa akina mama na vijana hapa nchi.Mimi na taasisi yangu ya mama Rosemary tumekuwa tunazunguka nchi nzima kuhamasisha wanawake na vijana kujiunga katia vikundi na kuwawezesha kiuchumi vile vile tumewahamasisha washiriki atika shughuli za kisiasa na kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali katika chaguzi zijazo.Jambo hili kuna watu ambao halikuwafurahisha na ndiyo maana wakatumia vijana wale waniteke na kunitesa namna hii.Lakini kubwa zaidi nililoligundua ni kwamba watu walionifanyia hivi kuna jambo moja kubwa wanaliogopa.” Akasema Rose na kunyamaza na baada ya muda akaendelea

“ Ndugu waandishi wa habari na watanzania najua baadhi yenu mmekwisha sikia tetesi tetesi kuhusu mimi kuhusishwa na kuwania urais baada ya muhula wa pili wa Dr Joshua kumalizika lakini sikuwahi kusimama hadharani na kuliongelea jambo hili .Leo kupitia kwenu waandishi wa habari nataka niliongelee suala hili na kuliweka wazi.” Akanyamaza akawatazama waandishi wa habari na kusema

“ Ndugu zangu waandishi wa habari,nimezunguka nchi nzima ,nimezifahamu shida za watanzania ,nimeuona umasikini wa watanzania na nina nia ya dhati ya kuwasaidia watanzania na kuwatatulia shida zao na ndiyo maana kupitia kwenu leo hii ninataka kutangaza rasmi kwamba nitagombea urais katika uchaguzi mkuu ujao.Nitaitisha tena mkutano mwingine mkubwa wa waandishi wa habari na wadau mbali mbali kutangaza vipaumble vyangu na nini nitawafanyia watanzania kama nikipata ridhaa ya kuwaongoza lakini katika mkutano huu wa leo ninataka kutuma ujumbe kwa wale watu wenye nia ya kunikatisha tamaa kwamba hawataweza.Nina dhamira ya dhati ya kuwatumikia watanzania na kwa hiyo juhudi zao hazitafanikiwa.Naomba niwaeleze watanzania kwamba tukio zima la mimi kutekwa nyara na kuteswa limeratibiwa na watu ambao hawataki mimi nigombee urais kwani wanajua wazi kwamba watanzania wananijua na lazima watanichagua .Walinitolea vitisho vingi vya kuniua endapo nitaendele ana harakati zangu za kutaka kuwania urais na mimi kupitia kwenu ninawaambia kwamba sintarudi nyuma nimejitolea kuwatumikia watanzania hata kama ikinibidi kupoteza uhai wangu.Ninaomba watanzania wote bila kujali itikadi zenu mniunge mkono katika dhamira yangu hii kubwa ya kuwatumikia na ninawaahidi kwamba licha ya juhudi nyingi za watu wanaotaka kunirudidisha nyuma sintokata tamaa. Ndugu zangu waandishi wa habari ninawashukuru sana kwa kufika kwenu na watanzania wamesikia kupitia kwenu na kama nilivyowaambia awali kwamba nitakuwa na mkutano nanyi hivi karibuni nitazungumza nanyi mambo mengi ila kwa leo nililokuwa ninataka watanzania walifahamu kupitia kwenu ni hilo.Mtanisamehe kutokana na hali yangu sintahitaji maswali kwa siku ya leo .Nitakapokutana nanyi siku nyingine mtapata nafasi kubwa y a kuuliza maswali “ akasema Rose na kuondoka pale bustanini
“ Mateso waliyonitesa wale washenzi yatanisaidia sana kunijenga kisiasa.Hawakujua kwa kunitesa vile wananitengenezea jina kubwa.Natumai taarifa hii ya leo itaitikisa nchi na hasa kutokana na namna itakavyopewa umuhimu mkubwa na vyombo vyote vya habari.” Akawaza Rosemary wakati anarudishwa ndani.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 35

MTUNZI😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Ninaomba watanzania wote bila kujali itikadi zenu mniunge mkono katika dhamira yangu hii kubwa ya kuwatumikia na ninawaahidi kwamba licha ya juhudi nyingi za watu wanaotaka kunirudidisha nyuma sintokata tamaa. Ndugu zangu waandishi wa habari ninawashukuru sana kwa kufika kwenu na watanzania wamesikia kupitia kwenu na kama nilivyowaambia awali kwamba nitakuwa na mkutano nanyi hivi karibuni nitazungumza nanyi mambo mengi ila kwa leo nililokuwa ninataka watanzania walifahamu kupitia kwenu ni hilo.Mtanisamehe kutokana na hali yangu sintahitaji maswali kwa siku ya leo .Nitakapokutana nanyi siku nyingine mtapata nafasi kubwa y a kuuliza maswali “ akasema Rose na kuondoka pale bustanini
“ Mateso waliyonitesa wale washenzi yatanisaidia sana kunijenga kisiasa.Hawakujua kwa kunitesa vile wananitengenezea jina kubwa.Natumai taarifa hii ya leo itaitikisa nchi na hasa kutokana na namna itakavyopewa umuhimu mkubwa na vyombo vyote vya habari.” Akawaza Rosemary wakati anarudishwa ndani.



ENDELEA…………………



Taarifa ya Rosemary Mkozumi kutaka kuwania nafasi ya urais ilianza kusambaa kwa kasi ya ajabu mara tu baada ya kumaliza mkutano wake na waandishiwa habari.Ukuaji wa teknolojia ulifanya taarifa ile iwafikie watu wengi ndani ya kipindi kifupi sananakuzua gumzo hasa katika mitandao ya kijamii.Wengi walionekana kumuunga mkono mama huyu hususan vijana ambaoamekuwa akiwawezesha sana kiuchumi.
Rosemary alianza kupokea simu za pongezi kutoka kwa watu mbali mbali wakimpa pole na kumpongeza kwa hatua yake ile ya ujasiri na wakiahidi kumuunga mkono katika mbio zake za kusaka urais.Ilikuwa ni siku njema sana kwa Rose na uso wake haukukaukiwa tabasamu licha ya maumivu ambayo badoaliendelea kuyasikia
Rais mstaafu Deus Mkozumi akiwa amejipumzisha nyumbani kwake alitumiwa video na rafiki yake ya alichokizungumza Rose katika mkutano wakena waandishi wa habarina kumstua sana.
“ Rosemary awe Rais?? Akasema Deus na kucheka kwa dharau kidogo.
“ Hapana haiwezekanai.Hili ni jambo lisilokubalika hata kidogo .Hatuwezi kuichezea nafasi hii nyeti sana kwa kuwaacha watu wachafu kama hawa watie nia ya kutuongoza.Nimeishi na Rose kwa miaka ishirini na nane,ninamfahamu vizuri kuliko mtu yeyote Yule..She’s a devil.Watu wanachanganyikiwa na misaadaya fedha anazowapatia bila hata ya kuhoji anazipata wapi.Ninaapa kamabado niko hai Rose hafanikiwi katika jambo hili” akawaza Deus na kuitazama video ile kwa mara nyingine i.
“ Ni akina nani waliokuwa wamemteka nyara Rosemary? Nakumbuka Peniela aliniambia kwamba anawafahamu watu waliomteka Rose na nikamsihi awaambie watu hao wasithubutu kumuachia Rose kwani ni mtu htari mno ninashangaa amewezaje kuwa huru? Kwa nini wamemuachia? Akajiuliza Deus.
“ nahitaji kuitisha kikao cha dharura haraka sana na timu yangu tulijadili suala hili na tuone namna tunavyoweza kulizuia lisifanyie.Hili si jambo la kufanyia mzaha hata kidogo lazima kwa gharama zozote zile nihakishe lengo la Rosemary halitimii.”akawaza Deus
“ Nimeanza kuwa na hisia kwamba yawezekana Rose akahusika hata katika kifo cha Amos.Nitafanya uchunguzi ili nibaini kama ni kweli alihusika na kama ni yeye ndiye aliyehusika nitamfanyia kitu kibaya sana” akawaza Deus na kuhukua simu akawapigia washirika wake akawataka wakutane kwa dharura jioni ya siku ile kulijadili suala lile la Rose.




*******


Kiza kimeanza kutanda angani .Nyumbani kwa Rosemary Mkozumi ulinzi uliimarishwa kwani rais Dr Joshua alitarajia kwenda kuonana na Rosemary jioni hiyo.
Saa moja na dakika ishirini na mbili Dr Joshua akawasili nyumbani kwa Rose na kupokewa na Rose ambaye alikuwa anatembea kwa kuchechemea wakaelekea bustanini mahala kulikokuwa kumeandaliwa maalum kwa ajili yao

“ Pole sana Rose.nani amekufanya hivi? Akauliza Dr Joshua
“ Ni hadithi ndefu Mr Presdent lakini napenda nichukue nafasi hii nikupe pole sana wewe pia kwa matatizo yaliyokupata”
“ Ahsante sana Rose.Mimi na familia yangu tunapitia kipindi kigumu sana cha majaribu lakini naamini kwa dua zenu tutasimama imara na tutashinda.Habari za siku nyingi Rose? Ni muda mrefu sana hatujaonana na ndiyo maana uliponiambia kwamba unataka kuonana nami nilistuka kidogo.By the way nataka binafsi nikupongeze kwa tamko ulilolitoa leo hii kuhusiana na kusudio lako la kutaka kuwania urais.Hongera sana kwa maamuzi hayo makubwa na ninahisi yawezekana jambo hili likawa miongoni mwa mambo yaliyotukutunanisha jioni hii” akasema Dr Joshua na kumfanya Rose atabasamu

“ Ahsante sana kwa pongezi Dr Joshua ingawa nilitegemea ungewahi kunipigia simu na kunipongeza mara tu baada ya kuzipata taarifa hizo lakini nashukuru hata hivyo kwa kunipa moyo.Suala hili litakuwa ni kama nyongeza tu katika yale masuala makubwa ambayo nimekuitia hapa .Kuna mambo mawli makubwa ninayotaka kuzungumza nawe.” Akasema Rose.Muhudumu wa Rose akafika na chupa ya mvinyo akawamiminia katika glasi

“ Kabla hatujaendelea mbele Rose,vipi maisha yanakwendaje? Akauliza Dr Joshua
“ Maisha yanakwenda vizuri sana .”
“ Vipi mnawasiliana na Deus?
“ hatuwasiliani kabisa.Mimi na Deus ni kama paka na panya hivi sasa na nina hakika ni yeye ambaye alikuwa nyuma ya vijana wale walionifanya hivi” akasema Rose

“ Are you sure Rose? Akauliza Dr Joshua
“ yes I’m sure.Ni yeye ambaye amekuwa akinipiga vita sana katika mambo yangu.Tulipoachana alitegemea labda ningeadhirika na kumpigia magoti lakini badala yake nimekuwa na mafanikio tofauti na alivyotegemea na ndiyo maana anafanya kila juhudi kutaka kunirudisha nyuma”
“ Deus is a monster.Anatakiwa akamatwe haraka sana na kufikishwa katika vyombo vya dola.kwa nini hukunitaarifu mapema ili tuweze kumchukulia hatua? Mimi sijali kama ni ras mstaafu lakini kama anahusika katika uporaji na utesaji wa watu lazima achukuliwe hatua kali” akasema kwa ukali Dr Joshua
“ Dr Joshua you know how Deus works,right? He’s a very smart person.Kwa sasa sina ushahidi wa moja kwa moja kwa moja wa kuweza kumtia hatiani Deus kwa tukio lile lakini ninakuhakikishia ndani ya siku mbili hizi nitakuwa nimepata ushahidi kamili na wa kutosha kabisa kwamba Deus ndiye aliyewatuma vijana wale waniteke nyara.” Akasema Rose

“ It must be him!!. Akasema Dr Joshua kwa ukali.Rose akamuangalia kisha akachukua glasi ya mvinyo akanywa kidogo na kusema
“ Why do you hate him so much? Akauliza Rose.Dr Joshua akachukua glasi akanywa mvinyo kidogo kisha akasema

“ Nitashindwaje kumchukia kwa mambo kama haya aliyokufanyia? Huu si ubinadamu hata kidogo”akasema Dr Joshua.Rose akaguna kidogo kisha akassema

“ You hate him because of what he did to me of because what he knows about you? Akauliza Rose huku akitabasamu
“ Deus knows me ? akauliza Dr Joshua
“ By the way pole sana kwa kifo cha Amos.” Akasema Rose

“ Ahsante sana.Umejuaje kama Amos amefariki dunia? Akauliza Dr Joshua.Rose akacheka kidogo na kusema

“ Dr Joshua tunaishi katika kijiji na kila kinachofanyika lazima nikijue.Kikubwa zaidi ambacho yawezekana hukuwa unakifahamu ni kwamba Amos alikuwa ni mtu wangu na mimi pia.Alikuwa ni mtu mwenye msaada mkubwa kwangu na alikuwa ananieleza kila kinachofanyika ndani ya ikulu.”
Dr Joshua akastuka akamtazama Rose kwa macho makali
“ Amos alikuwa anaripoti kwako pia? That bastard !! amekueleza mambo gani? akahamaki Dr Joshua
“ Usihamaki Dr Joshua.Amos hakuwa akiripoti kwangu tu vile vile alikuwa ni mtu wa Deus ndani ya ikulu na ndiye aliyekuwa anampatia Deus habari zako zote.”

“ Ouh my Gd !! akashangaa Dr Joshua
“ Ndiyo maana nikawa najiuliza huyu Deus amepataje habari zangu? Kumbe alikuwa anaambiwa na Amos.Dah ! nilikosea sana kumuamini .Kumbe ni yeye ambaye amekuwa ananiuza kwa muda wote huu.Kila kitu tukifanya kilikuwa kinajulikana kabla hata ya utekelezaji wake kumbe chanzo cha yote ni Amos.Tumekumbana na vikwazo lukuki kumbe chanzo ni Amos..Dah nashukuru amekwenda lakini amenistua sana.Kumbe katika hii dunia hupaswi kumuamini mtu yeyote.Nilimuamini sana mke wangu Flora naye akataka kunisaliti na kuvujisha siri nikalazimika kumuondoa.Ni nani basi nitakayemuamini kama watu wangu wa karibu wote wanageuka wasaliti?

“ unawaza nini Dr Joshua? Akauliza Rose na kumstua Dr Joshua toka mawazoni

“ Rose taarifa uliyonipa imenistua sana.Amos ni mmoja wa watu niliowamini kupita kiasi na sikutegemea kabisa kama angeweza kunifanyia kitu cha namna hii.Sikutegemea kabisa mtu kama Amos angeweza kunizunguka na kushirikiana na mtu kama Deus.”akasema Dr Joshua
“ Ulifanya makosa makubwa sana Dr Joshua kumuamini mtu kupita kiasi.Katika siasa hakuna mtu wa kumuamini.Kila aliye mbele yako ni adui yako mtarajiwa kwahiyo hili liwe ni fundisho kwako.Kuanzia leo hii usimuamini mtu yeyote Yule”akasema Rose
“Kinachonichanganya zaidi mambo yangu mengi sana anayafahamu kwa hiyo sijui amemweleza nani kitu gani”akasema Dr Joshua na kunywa mvinyo kidogo

“ he told me everything about your wife.Yeye ndiye aliyemuua Dr Flora kwa kumchoma sindano ya sumu,alinieleza pia kuhusiana na kifo cha Flaviana kilisababishwa na watu uliowatuma wakamuue jaji Elibariki,alinieleza pia kuhusiana na jambo unalotaka kulifanya la kuiuza package yenye kirusi Aby.Kwa ujumla alinieleza mambo mengi.Kila unachokifanya alikuwa ananieleza kwa hiyo ninakufahamu nje ndani” akasema Rosemary.DrJoshua akainama na kushika kichwa kwa mikono yake.
“ Najua umestuka sana Dr Joshua kuona kwamba ninafahamu mambo yako yote unayoyafanya huku ukidhani kwamba watu hatujui kumbe tunajua kila kitu.Lakini usiogope mimi siwezi katu kuufungua mdomo wangu kwa mtu yeyote Yule kwani hata mimi nilikuwa ninamtumia Amos ili niweze kuipata hiyo package.Wote tulikuwa na lengo moja la kujipatia kiasi kikubwa cha pesa kupitia package hiyo lakini kwa sasa baada ya Amos kufariki mimi na wewe tunapaswa kuwa washirika”
“ What !!..Dr Joshua akashangaa

“ Mbona unasangaa Dr Joshua? Sote lengo letu lilikuwa moja tu kupata pesa kwa hiyo ninataka tushirikiane katika suala hili kwani hata mimi nina hitaji pesa.Baada ya mauzo nitahitaji unigawie kiasi fulani cha pesa ili kinisaidie katika kuendesha kampeni yangu ya kuwania urais.” Akasema Rose

“ Hilo haliwezekani Rose.Siwezi kuwa na ushirika na wewe”akasema Dr Joshua
“ Kama haliwezekani then you wont sell the package” akasema Rose huku akitabasamu
“ Now you are threatening me Rose” akasema Dr Joshua
“ This is not a threat Dr Joshua this is a warning.Kama hutataka kushirikiana nami basi hutaweza kuuza huo mzigo.Dr Joshua umezungukwa katika kila kona na kamwe mpango wako huo hautafanikiwa na pindi ukijaribu kutaka kuitoa package ile ikulu ndio utakuwa mwisho wako.You will die in prison.Kuna watu ambao hawalali usiku na mchana wanakuwinda na wanaihitaji hiyo package zaidi ya roho yako.Ninafahamu mipango yao yote ninafahamu kila wanachokipanga na kama ukitaka tushirikiane basi utavuka vikwazo vyote na utafanikiwa lakini endapo utapuuza onyo hili hautasalimika kamwe.” Akasema Rosemary

“ Ouh Rosemary don’t ever try me my former first lady !! akasema Dr Joshua
“ Hilo ni jambo la kwanza Dr Joshua kuna jambo lingine la pili.Nitaendelea kuufumba mdomo wangu kuhusiana na mambo unayoyafanya na hususan kuhusika kwako katika kifo cha mkeo Dr Flora kama ukilikubali na kulitimiza”
“ No body will believe you.Hakuna ushahidi wowote wa kunihusisha na suala hilo”akasema Dr Joshua

“ Usijidanganye dr Joshua.Do you know this guy called Mathew? Huyu ni kijana hatari sana na huyu ameapa hatalala usingizi mpaka ahakikishe amekuangusha.Anafahamu kila kitu kuhusu wewe ana kila ushahidi wa kila unachokifanya.Nakuambia Dr Joshua kijana huyu ni hatari kuzidi hatari yenyewe lakini kama ukinitumia mimi niko tayari kukusaidia kumpata na kama ukimpata huyu then you are a free man..” akasema Rose.Dr Joshua akamtazama na kusema
“ Kitugani hasa unachokitaka toka kwangu Rose?

“ Kuna mambo mawili makubwa nayataka toka kwako.Moja nataka kushirikishwa katika mpango unaoendelea wa uuzwaji wa package yenye kirusi Aby.Nitaka na mimi nipate mgawo wangu sawa kwa sawa.Pili muda wako wa uongozi unaelekea ukingoni .Najua kwa sasa kuna mchakato wa kumpata mrithi wako ndani ya chama ,na mtu kama mimi sina nguvu kubwa ndani ya chama nataka utumie nafasi yako kama rais unipitishe niwe mgombea urais .”
“ What ?!!! akasema Dr Joshua na kusimama
“ Unataka nikufanyie nini? Akauliza kwa ukali
“ You are going to make me the next president of the united republic of Tanzania.”akasema Rose

“ No I cant!! Akasema Dr Joshua huku akigonga meza
“ Yes you can and you are going to do it !!! akasema Rose kw a kujiamini
“ Dr Joshua naomba usihamaki tafadhali.Najua una mipango mingi mizuri ya kuishi maisha mazuri siku za mbele baada ya kustaafu.Mimi ndiye mwenye kuamua hatima ya maisha yako baada ya kustaafu.Ukitaka kuishi maisha mazuri tafadhali kubaliana nami katika yale yote niliyokueleza .Si mambo magumu kwako hata kidogo”
“ You devil !! akasema Dr Joshua kwa ukali

“ I’m not a devil Dr Joshua.I’m your angel.Mimi ndiye msaada mkubwa kwako.I’m going to protect you”
“ Protect me ?

“ yes !! I can protect you.Kukuonyesha kwamba mimi ni msaada mkubwa kwako ninakwenda kukuonyesha kitu ambacho you’ve been dying to see. You will thank me “ akasema Rose na kumchukua Dr Joshua wakaelekea ndani.walipoingia sebuleni Rose akawageukia walinzi wa rais
“ Guys you can wait here.We’ll be fine..”akasema Rose.walinzi wale wakaonyesha kutokukubaliana naye
“ Its ok guys.we’llbe fine”akasema Dr Joshua kisha wakaelekea hadi katika chumba alichofungwa Elibariki.Mlango ukafunguliwa na taa ikawashwa.Dr Joshua akapatw ana mshangao mkubwa baada ya kuonana na jaji Elibariki mtu ambaye amekuwa anamuwinda kwa nguvu kubwa usiku na mchana.





TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 36


MTUNZI 😛ATRICK C.K

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ You devil !! akasema Dr Joshua kwa ukali
“ I’m not a devil Dr Joshua.I’m your angel.Mimi ndiye msaada mkubwa kwako.I’m going to protect you”

“ Protect me ?
“ yes !! I can protect you.Kukuonyesha kwamba mimi ni msaada mkubwa kwako ninakwenda kukuonyesha kitu ambacho you’ve been dying to see. You will thank me “ akasema Rose na kumchukua Dr Joshua wakaelekea ndani.walipoingia sebuleni Rose akawageukia walinzi wa rais

“ Guys you can wait here.We’ll be fine..”akasema Rose.walinzi wale wakaonyesha kutokukubaliana naye
“ Its ok guys.we’llbe fine”akasema Dr Joshua kisha wakaelekea hadi katika chumba alichofungwa Elibariki.Mlango ukafunguliwa na taa ikawashwa.Dr Joshua akapatw ana mshangao mkubwa baada ya kuonana na jaji Elibariki mtu ambaye amekuwa anamuwinda kwa nguvu kubwa usiku na mchana.




ENDELEA………………………




“ Elibariki?!! Dr Joshua akashangaa sana kumkuta Elibariki mle chumbani.Hakuwa ametegemea kabisa kuonana naye ana kwa ana
“ Mr President!! Akasema jaji Elibariki.Hu uso wake ukiwa umejikunja kwa hasira Dr Joshua akamgeukia Rosemary Mkozumi
“ What is the meaning of this Rose? Akauliza kwa ukali
“ Dr JoshuJaji Elibariki ni mtu ambaye ulikuwa unaota kumpata usiku na mchana.Umetumia nguvu kubwa ya vyombo vya dola kumtafuta lakini mpaka sasa hawajafanikiwa kumpata na wasingeweza kumpata kamwe.He wants to talk to you! akasema Rose
“ This man is ..!! akasema kwa ukali Dr Joshua lakini Rose akamzuia

“ Usihamaki Dr Joshua.You have to talk to him.Nakuhakikishia kwamba hutajuta kuzungumza naye” akasema Rose.Uso wa Dr Joshua ulionyesha hasira za wazi
“ hatimaye nimekupata mwanaharamu wewe.Nina hasira nawe sana .Wewe ni chanzo cha matatizo yangu mengi.Ni wewe uliyesababisha hadi mwanangu Flaviana akafariki.Ninakuchukia Elibariki na ninatamani hata nikuvamie na kukuua kwa mikono yangu mwenyewe.” Akawaza Dr Joshua huku akiuma meno kwa hasira halafu akachukua kiti akaketi .
“ Rose sijapendezwa kabisa na hiki ulichokifanya.Huyu mtu ni mhalifu na mida hii anatakiwa awe gerezani.Huyu ni chanzo mwanangu Flaviana kufariki dunia.I hate this man !!.Kwa nini umemuhifadhi hapa kwako?.akasema Dr Joshua kwa hasira
“Dr Joshua kwa nini tusiokoe muda na kuongea mambo ya msingi? Sisi sote hapa tunafahamu kila kinachoendelea na kwamba hayo yote unayoyasema hayana ukweli hata kidogo,Elibarikihahusiki hata kidogo katika kifo cha mkeo wala mwanao.You killed them yourself.” Akasema Rose na Dr Joshua hakujibu kitu akabaki anamtazama kwa hasira
“ Kwa taarifa yako Dr Joshua ni kwamba jaji Elibariki ndiye aliyeniokoa mimi mahala nilikokuwa nimefungwa nikiteswa na aliniokoa kwa dhumuni la kutafuta msaada wangu na msaada aliokuwa anauhitaji ni kuongea nawe.Kuna jambo la muhimu anataka kuzungumza nawe.Tafadhali msikilize” akasema Rose
“ Unataka kunieleza nini? Akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ Dr Joshua ahsante kwa nafasi hii na sitaki kuchukua muda wako mwingi nataka nijielekeze moja kwa moja katika kile ambacho kimenifanya nitake kuonana nawe.” Akasema Jaji Elibariki

“ Kwanza ninataka kuchukua nafasi hii kukupa pole kwa msiba wa mwanao na mke wangu Flaviana.Nimeumia sana kwa msiba ule japokuwa ninatuhumiwa kusababisha kifo kile.Mr President sote tunafahamu kwamba sikuhusika kabisa na kilichotokea usiku ule na wala sikuwa nimelipanga shambulio lile na hata siku moja nisingeweza kumdhuru mke wangu na wewe unafahamu kabisa nani waliomuua Flaviana lakini kwa kuwa una hasira mimi ukaamua kuniangushia kesi ile mbaya ya kusababisha mauaji” akasema Elibariki na Dr Joshua akaendelea kumuangalia kwa hasira.Elibariki akaendelea.

“ Yote haya yalianza baada ya kifo cha Dr Flora.Mazingira ya kifo cha Dr Flora yalimfanya Flaviana aingiwe na shaka na hivyo akaniomba nimsaidie kufanya uchunguzi kubaini nini kilichomuua mama yake.Kwa kushirikiana na wenzangu tulifanikiwa kugundua sababu ya kifo cha Dr Flora kwamba aliuawa kwa kuchomwa sindano ya sumu na hapo ndipo nilipoanza kuwindwa.Nilinusurika kuuawa na nikaokolewa na mwanamke mmoja ambaye simfahamu nikaenda kujificha kwa Pen………”

“ Hebu ngoja kwanza Elibariki,Unasema kwamba uliokolewa na mwanamke.Unamfahamu mwanamke aliyekuokoa? Akauliza Dr Joshua
“ Hapana simfahamu .Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonana naye na sifahamu ni kwanini aliniokoa.”
“ Unaweza ukanielezea muonekano wa mwanamke huyo ? Akauliza Dr Joshua
“ Ni mrefu kidogo,alikuwa na uso mpana na wenye macho madogo.Kingine ninachokikumbuka ambacho kinaweza kunipa urahisi kumtambua hata kama nikikutana naye kesho alikuwa na kovu katika jicho lake la kushoto.Mdom....
“ Wait ….!! Akasema Dr Joshua
“ Mkono wake wa kushoto una kovu la kuungua?

“ Sikuliona kovu hilo lakini alikuwa amevaa glovu mkono mmoja wa kushoto ila shingoni upande wa nyuma alionekana kama vile ana kovu la kuungua “ akasema jaji Elibariki

“ That’s Jesica!!.Ouh my God .I cant believe this.Jessica !!!..akasema kwa mshangao Dr Joshua
“ Unamfahamu? Akauliza Rosemary
“ Ninamfahamu.Anafanya kazi idara ya usalama wa taifa.Aliwahi kuwa mlinzi wangu wakati Fulani nikamuondoa baada ya kutoridhishwa na tabia zake.Ama kweli nimejifunza katika hii dunia usimuamini mtu yeyote Yule.Who sent her to help him??” akasema Dr Joshua.

“ I’ll find her and she will answer to me everything !! akasema Dr Joshua kwa hasira.
“ Endelea na simulizi yako “ Dr Joshua akamwambia Elibariki.
“ Nilipookolewa nilienda kujificha kwa Peniela na baadae nikachukuliwa na Mathew .”
“ Kwa hiyo taarifa za wewe kujificha kwa Peniela zilikuwa za kweli!! Akasema Dr Joshua
“ ni kweli nilijificha kwa Peniela kwa muda halafu nikaenda kujificha kwa Mathew.”

“ Who is Mathew?!!
“ He’s a monster who did this to me !!..akasema Rosemary

“ Mathew ni rafiki yangu ambaye ni mpelelezi wa kujitegemea ambaye ndiye aliyenisaidia katika kufahamu ukweli kuhusiana na kifo cha Dr Flora.Kwa kushirikiana naye tumegundua mambo mengi sana kuhusu wewe na hasa hili kubwa linaloendelea hivi sasa linalohusiana na kirusi Aby.Dr Joshua mambo ya kukuambia ni mengi lakini kwa kuokoa muda ninataka tuongelee mambo yanayotuhusu mimi na wewe.” Akasema jaji Elibariki .Dr Joshua akachomoa kitambaa mfukoni akajifuta jasho.Maneno aliyoambiwa na Elibariki yalimstua sana

“ Mr President ninajua ninatafutwa kila kona kwa agizo lako na endapo nikikamatwa maisha yangu yataharibika kwani nitaozea gerezani.Sitaki hilo linitokee.Nilijifanya jasiri kutaka kushinda nawe lakini hakuna nilichokipata zaidi ya kuwa mkimbizi nikijificha kama Sungura.Nimeinua mikono vita hii imenishinda.Siwezi kupambana nawe mheshmiwa rais kwa hiyo nimekuja kwako kukuomba msamaha sana kwa yale yote niliyokukosea .Nataka unisamehe na unirudishie maisha yangu ya kawaida tena.Nataka unifutie kesi inayonikabili na niendelee na kazi zangu kama kawaida .” akasema jaji Elibariki.Dr Joshua akamtazama akajifuta tena jasho halafu akasema

“ Natamani sana nikuamini tena jaji lakini kwa mambo uliyonifanyia siwezi kukuamini tena.Naomba nikuweke wazi kwamba ninakuchukia sana, sana, tena sana.Wewe ni adui yangu namba moja na lengo langu ni kukukuondoa kabisa katika uso wa hii dunia.Nilikuamini sana Elibariki nikakupa cheo kikubwa cha jaji wa mahakama kuu lakini badala yake ukaanza kunipuuza na hukunisikiliza tena.Sioni namna ya kukuamini tena Elibariki na kwa vile nimekwisha kuona hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutumia nguvu zangu zote nilizonazo kuhakikisha kwamba unapotea katika uso wa dunia.Ni heri ungebaki katika maficho yako kuliko kujitokeza.Umejileta mwenyewe katika mdomo wa mamba na ninakuhakikishia kwamba huu ndio mwisho wako.!! Akasema Dr Joshua kwa ukali.
“ He can be trusted ! akasema Rose
“ What ? Dr Joshua akashangaa

“ Do you trust this guy? Do you know who he is?akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ Yes I do trust him and you have too” akasema Rose.Dr Joshua akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Unanishangaza sana Rose.Huyu mtu hafai kabisa kuaminiwa.Amenifanyia mambo mengi sana ambayo siwezi kumsamhehe hata aseme nini !!
“ Dr Joshua naomba unisikilize.Nimekuleta hapa makusudi kabisa ili uweze kuonana na Elibariki mtu ambaye umekuwa ukiota kumpata usiku na mchana.Huyu ndiye aliyekuwa kikwazo kikubwa katika mpango wako wa kuuza kirusi Aby.Unapaswa ufurahi badala ya kukasirika .Kwa sasa huyu ndiye mkombozi wako.Huyu ndiye anayeweza akasababisha ukaimaliza biashara yako kwa amani na salama”

“ Huyu awe mkombozi wangu??? Rose nashindwa kukuelewa kwa nini unamuamini sana huyu mtu.Hafai huyu kuaminiwa hata kidogo.!!!! Akasema kwa ukali Dr Joshua
“ Ninamuamini kwa sababu ndiye aliyeniachia mimi huru kutoka mahala nilikokuwa nimefungwa.Aliwasaliti wenzake na kuniachia huru kwa lengo la kutaka nikukutanishe naye tu.Hata ukimuangalia machoni anamaanisha kile anachokiongea.Amechoka kukimbia kimbia huku na kule kila siku kujificha.He needs his normal life back na mtu pekee ambaye anaweza akalifanya hilo ni wewe. Elibariki alikuwa anashirikiana na watu ambao walikuwa wanakufuatilia usiku na mchana na ambao wana nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba mpango wako wa kuiuza package ile haufanikiwi.They are dangerous people and I swear kama ukipuuza basi huu utakuwa ni mwisho wako.Wana kila ushahidi wa kuweza kukutia hatiani.Elibariki anafahamu kila mpango wao namna walivyojipanga kukuangusha na anaweza akawa ni msaada mkubwa sana kwako” akasema Rose.Dr Joshua akamtazama tena kwa makini kisha akasema
“ Ni ya kweli hayo anayosema Rose? Watu hao uliokuwa unashirikiana nao ni akina nani? Wamepanga mipango gani kuhusu mimi? Akauliza Dr Joshua
“ Mr President anachokisema Rosemary ni kitu cha kweli kabisa.Nimeshirikiana na wenzangu ambao lengu letu lilikuwa ni kuhakikisha kwanza mpango wako haufanikiwi na pili ni kuhakikisha kwamba unapatikana ushahidi wa kutosha wa kuweza kukutia hatiani kwa kifo cha mkeo Dr Flora.Nimetafakari sana na nikaona kwamba hata kama tukifanikiwa kuizuia mipango yako na kufanikiwa kukufikisha mbele ya sheria ,hakuna faida yoyote ambayo ninaweza nikaipata kwani mimi bado nina kesi ya kujibu ya kusababisha kifo cha Flaviana.Ni wewe pekee ambaye unaweza ukanirejeshea maisha yangu ya kawaida hivyo nikaona njia pekee ni kuwasaliti wenzangu na kuonana nawe,nikuombe msamaha na tuweze kuyamaliza haya mambo.Dr Joshua tafadhali naomba uniamini kwamba haikuwa kazi rahisi kuwasaliti wenzangu na kumuachia huru Rosemary lakini nimefanya hivyo kwa lengo moja tu la kutaka kuishi maisha yangu ya kawaida” akasema jaji Elibariki

“ Jaji una maneno mazuri ambayo yananifanya nitake kukuamini tena lakini bado hujanishawishi nitawezaje kukuamini mtu ambaye nilikupenda kama mwanangu na nikakuamini lakini ukanigeuka na kunifanyia mambo ya ajabu kama uliyoyafanya? Kama nikikuamini leo hii nitakuwa na uhakika gani kwamba hutakuja kunigeuka tena na kunisaliti? Akauliza Dr Joshua
“ Mr President naomba uniamini.Najua bado haitakuwa rahisi kuniamini moja kwa moja lakini naomba nikuhakikishie kwamba I know things that you want to know so badly .I can tell you all the plans they have on you,nitakusaidia hata kuweza kuwapata hao wenzangu wote lakini nitayafanya hayo tu endapo utakuwa tayari kunisamehe na kunirejeshea uhuru wangu,kunirejeshea maisha yangu ya kawaida,kunirejeshea kazi yangu na kulisafisha jina langu.” Akasema jaji Elibariki.Dr Joshua akamtazama kwa zaidi ya dakika moja halafu akamgeukia Rose na kusema
“ Rose naomba tutoke tuongee nje kidogo”
Dr Joshua na Rose wakatoka nje ya kile chumba

“ Rose unaniweka katika wakati mgumu sana na kunitaka nimuamini huyu jamaa tena.Huyu ni mtu mbaya mno !! akasema Dr Joshua
“ Right now this is the only guy you need to trust with your life” akasema Rose
“ Elibariki anafahamu mambo yako yote na vile vile anifahamu mipango yote waliyoipanga akina Mathew juu yako.Tafadhali usiache kumuamini tena jaji.Hautapoteza kitu kama ukimuamini tena.Utafanikiwa katika malengo yako na wabaya wako wote watashindwa. This is your last call Mr President” akasema Rose..Dr Joshua akainama akafikiri kwa kama dakika mbili hivi halafu akasema

“ Ok nitafuata ushauri wako na nitamrejeshea Elibariki uhuru wake lakini anatakiwa aonyeshe kwanza juhudi za kunishawishi nimuamini kwa kuniwezesha kuikwepa mipango yote iliyopangwa na hao jamaa zake na kuwafutilia mbali na kama nikifanikiwa basi nitamuamini lakini kama ananidanganya I’ll kill him...”
“ That’s good.! Akasema Rose

“ What about me .Bado hujanipa jibu lolote lile kuhusu yale tuliyoongea.Kumbuka Elibariki works under my command !! akasema Rose.
“ Kuhusu suala la kwanza, nitakuweka katika mgawo endapo biashara ikifanikiwa kwenda vizuri.Suala la pili ninaomba niondoke nalo nikalitafakari kwanza na kuona namna ninavyoweza kulifanyia kazi na kisha baada ya msiba wa mwanangu kumalizika mimi na wewe tutakuwa na kikao kulijadili suala hili kwa upana wake lakini nakuhakikishia kamba nitakusaidia kwa sababu hata wewe umenisaidia sana kumpata huyu mtu ambaye vyombo vya dola vimeshindwa” akasema Dr Joshua kisha wakarejea ndani
“ Jaji ,nimeongea na Rose na amenishawishi nikubali kukuamini tena.Nimekubali kulifanya hilo na nitakurejesha uhuru wako.Nitaliondoa agizo la kukusaka,na utaendelea na maisha yako ya kawaida lakini kama tu ukiniwezesha kuwapata hao jamaa zako pamoja na kunieleza mipango yote waliyoipanga juu yangu.Endapo ukishirikiana nami vizuri basi unaweza ukafaidika sana badala ya kutaka mapambano na mtu kama mimi na unaishia kutanga tanga kama ndege.Nakuhakikishia kwamba endapo utanisaidia katika hili basi utafurahi mwenyewe.Utakuwa na maisha mazuri sana na utajilaumu kwa nini hukushirikiana nami toka mapema.Pamoja na hayo nataka nikuonye kwamba tayari unafahamu mambo yangu mengi kwa hiyo ninachokitaka kingine ni kuufunga mdomo wako.Sitaki uropoke chochote kama watu wengine ambao niliwaamini lakini kumbe ni wasaliti wakubwa kama akina Amos.Kitu cha mwisho ninachotaka kuwa muwazi kwako ni kwamba kwa sasa kwa kuwa bado sijarejesha imani kubwa kwako sintakupa nafasi ya kupumua. Nitakufuatilia usiku na mchana na kila mahala uendako utaongozana na mlinzi nitakaye mteua mimi na utachunguzwa katika kila unachokifanya,kila simu unayopiga na kila unayeongea naye.Nikiridhika kwamba unafaa kuaminiwa basi nitakuacha uwe huru kufanya unavyotaka lakini kwa sasa hadi hapo baadae you’ll be under my control!! Akasema Dr Joshua
“ Tumeelewana Elibarki?
“ Ndiyo Mr President,tumeelewana.!! Akasema Elibariki.

“ Mfungueni hizo pingu nitaondoka naye ili akahudhurie msiba wa mke wake” akasema Dr Joshua.Rose akampigia simu Fernando mlinzi wake na kumtaka afike mara moja naye hakupoteza muda akafika akamfungua jaji Elibariki pingu alizokuwa amefungwa
“ Take him somewhere to clean up.Hatakiwi kuonekana kama ametoka kifungoni” akasema Dr Joshua halafu wakatoka mle chumbani wakaongozana hadi sebuleni ambako Dr Joshua akakaribishwa kinywaji wakati akimsubiri jaji Elibariki aweze kuoga na kujiweka safi. Rosemary akamchukua Elibariki hadi katika chumba kilichokuwa cha Henry akamuacha mle ili aweze kuoga .Baada ya kuoga akagongewa mlango na kuletewa suti nzuri ya gharama iliyokuwa ya Henry.Elibariki akavaa na kupendeza kisha akashuka ngazi hadi sebuleni alikokuwako Dr Joshua.

“ Now you look like a gentleman.” Akasema Dr Joshua
“ Kwa sasa usijibu chochote endapo ukiulizwa mahala ulikokuwa na kuhusiana na shambulio lile ulilonusurika na lile lililosababisha kifo cha mkeo” akasema Dr Joshua kisha akaongozana na jaji Elibariki hadi katika gari wakapanda na kuagana na Rose wakaondoka.
“ Later tonight,me and you we’ll have a long and serious talk” akasema Dr Joshua na jaji Elibariki akatikisa kichwa kukubaliana naye

“ Elibariki anaonekana kufahamu mambo mnegi sana kuhusiana na kila ninachokifanya.Ameamua kurudi mwenyewe na kuomba msamaha .Kama angelifanya hivi mapema wala tusingefika hapa tulipofika.Tungeweza kupiga hatua kubwa sana na wala asinge hitaji tena hata kufanya kazi.Tatizo la hawa vijana wanatafuta ushujaa lakini matokeo yake ndiyo haya amekosa muelekeo na maisha yake yameharbika.Na kama asingestuka mapema na kuja kuniomba msamaha ningemfutilia mbali toka katika uso wa dunia.” Akawaza Dr Joshua

“ Hawa watu anaoshrikiana nao ni akina nani? Wanaonekana ni watu makini sana na wenye ujuzi wa hali ya juu kiasi cha kuweza kufahamu kila ninachokifanya.Watu hawa hawatakiwi kuachwa hai hata kidogo.NI watu ambao natakiwa kuwaondoa haraka sana “ akawaza Dr Joshua


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 37

MTUNZI: PATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Later tonight,me and you we’ll have a long and serious talk” akasema Dr Joshua na jaji Elibariki akatikisa kichwa kukubaliana naye

“ Elibariki anaonekana kufahamu mambo mnegi sana kuhusiana na kila ninachokifanya.Ameamua kurudi mwenyewe na kuomba msamaha .Kama angelifanya hivi mapema wala tusingefika hapa tulipofika.Tungeweza kupiga hatua kubwa sana na wala asinge hitaji tena hata kufanya kazi.Tatizo la hawa vijana wanatafuta ushujaa lakini matokeo yake ndiyo haya amekosa muelekeo na maisha yake yameharbika.Na kama asingestuka mapema na kuja kuniomba msamaha ningemfutilia mbali toka katika uso wa dunia.” Akawaza Dr Joshua

“ Hawa watu anaoshrikiana nao ni akina nani? Wanaonekana ni watu makini sana na wenye ujuzi wa hali ya juu kiasi cha kuweza kufahamu kila ninachokifanya.Watu hawa hawatakiwi kuachwa hai hata kidogo.NI watu ambao natakiwa kuwaondoa haraka sana “ akawaza Dr Joshua



ENDELEA…………………….




Mining’ono ilianza msibani mara tu baada ya Dr Joshua kurejea akiwa ameongozana na jaji Elibariki mtu ambaye alitajwa kuhusika katika kifo cha Flaviana.
“ Kuonekana kwako hapa kutazua maswali mengi na maneno mengi yatasemwa lakini unatakiwa uwe mvumilivu sana na usionyeshe aina yoyote ya wasi wasi” Dr Joshua akamnong’oneza jaji Elibariki.
Japokuwa ilikuwa ni usiku tayari lakini taarifa za kuonekana kwa jaji Elibariki pale msibani zilisambaa kwa kasi na watu mbali mbali wakaanza kuja kumpa pole na wengi wakitaka kushuhudia kama taarifa zile ni za kweli ama si kweli.
Nusura Dr Kigomba aanguke kwa mstuko pale alipowaona Dr Joshua akiwa ameongozana na mtu aliyemuita kama adui yake mkubwa ambaye ni jaji Elibariki.
“ What the hell is this ?!!! akajiuliza Dr Kigomba kwa mshangao mkubwa .Hakuamini macho yake kama ni kweli Dr Joshua alikuwa amengozana na adui yao mkubwa.

“ Dr Joshua ?!! anadiriki vipi kuongozana na Elibariki mtu ambaye ni hatari sana kwetu? Mtu huyu tayari anafahamu siri ya kilichomuua Dr Flora kwa hiyo ni mtu hatari sana na Dr Joshaua ametumia nguvu kubwa kumtafuta lakini nashangaa leo hii ameongozana naye bila wasiwasi wowote.Whats going on?? Kuna mambo Dr Joshua ananificha hanielezi ukweli? Aliniambia kwamba anakwenda kuonana na Rosemary Mkozumi lakini badala yake anarejea akiwa ameongozana na adui yetu mkubwa jaji Elibariki mbona kama vile kuna kitu kinaendelea hapa nisichokielewa? Akajiuliza Dr Kigomba.

“ Hapana lazima nimuulize Dr Joshua niufahamu ukweli kama kuna jambo linaloendelea na haniweki wazi.Nimeyaweka rehani maisha yangu ili kuhakikisha kwamba mambo yetu yanafanikiwa lakini kwa kitendo hiki cha kuongozana na jaji Elibariki kimenipa mashaka kidogo.I have to know the truth” akawaza Dr Kigomba na kumfuata Dr Joshua akamuomba waongee pembeni kidogo.Dr Joshua akainuka wakasogea pembeni akawaambia walinzi wake wasogee pembeni ili wapate ya kuongea na Kigomba ambaye uso wake ulionyesha ni wazi alikuwa na jambo linalomsumbua

“ Kigomba ninafahamu ulichoniitia.Najua unachotaka kukifahamu.Nitakueleza kila kitu lakini si sasa hivi.”akasema Dr Joshua

“ Dr Joshua mimi na wewe ni watu tunaoaminiana sana na hata siku moja sijawahi kwenda kinyume na maagizo yako na nimekuwa muaminifu sana kwako.Tumetumia nguvu kubwa kumuondoa Elibariki katika ramani lakini ghafla umeonekana ukiwa naye.Kitendo hiki kimezua maswali mengi sana si kwangu tu bali kwa watu wote kwani tayari kila mtu anafahamu kwamba Elibariki ndiye aliyesababisha kifo cha Flaviana.Utatumia sentensi gani kumsafisha Elibariki.Wale wote waliojitokeza hadharani na kutangaza kwamba jaji Elibariki ndiye mtuhumiwa namba moja wa kusababisha kifo cha mkewe wataonekanaje? Huoni kama wataonekana ni waongo na wanaobahatisha kazi zao? Ouh Dr Joshua please explain to me everything,.!! Akasema Dr Kigomba.

“ Dr Kigomba naomba unipe muda nitakueleza kila kitu kuhusiana na jaji Elibariki .Kuna mambo mengi ambayo mimi na wewe tunatakiwa kuyafahamu kuhusiana na jaji Elibariki” akasema Dr Joshua

“ Dr Joshua sikufichi ndugu yangu umeniweka katika wakati mgumu sana wa kuendelea kuifanya kazi hii.Anyway nitasubiri maelezo yako kama ulivyoniahidi.By the way Hussein amekwisha wasili,nimekwenda kumpokea na kumpeleka katika hoteli .Amekuja na msafara wa watu kumi na ulinzi nimeuimarisha sana katika eneo alilofikia ” akasema Dr Kigomba

“ Ahsante sana kwa taarifa hizo Dr Kigomba ila naomba usihofu kitu kuhusu Elibariki.Kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa na zaidi ya yote huyu jama atakuwa ni msaada mkubwa sana kwetu .Believe me” akasema Dr Joshua na kuachana na Kigomba akarejea mahala alikokuwa amekaa jaji Elibariki
“ Najua kutahitajika maelezo ya kutosha kuhusiana na jaji Elibariki lakini hakuna kitakachoharibika.Kila kitu kitakwenda vizuri tu.Potelea mbali watakavyoongea na waongee tu lakini jaji Elibariki ni mtu ambaye ninamuhitaji sana kwa sasa” akawaza Dr Joshua.
Taarifa za kuonekana kwa jaji Elibariki pale msibani zilimfikia pia Anna mtoto wa rais na kumstua sana ,haraka haraka akatoka na kumtafuta Elibariki mahala aliko.Akamkuta amekaa na baba yake akamsalimu kisha akarejea ndani .Hakupata nafasi ya kuongea naye jambo lolote zaidi ya salamu.

“ bado siamini naona ni kama maajabu.Elibariki ametokea msibani?!! Alikuwa amejificha wapi? Kwa nini ameongozana na baba wakati ni yeye ndiye aliyenihakikishia kwamba baba anahusika katika vifo vya mama na Flaviana? Kuna kitu gani hapa kinaendelea? Akajiuliza Anna wakati akirejea ndani.

“ Lazima nipate nafasi ya kumuhoji na kuufahamu ukweli kuhusu yale yote aliyonieleza na kwa nini anashirikiana tena na baba wakati anajua kabisa kwamba ndiye aliyesababisha kifo cha mkewe na mama. “ akawaza



******



Takribani masaa mawili yamekatika sasa Anitha akiwa katika chumba ambacho kimepewa jina la Room 5.Hiki ni chumba ambacho kipo ndani ya jumba la Rosemary Mkozumi ambacho hutumiwa kwa ajili ya kutesea watu. Anitha alikuwa amefungwa miguu na mikono katika kitanda akiwa hoi na hakuwa akitazamika kwa namna alivyochafuka kwa damu.Ndani ya chumba kile alikuwamo Rosemary Mkozumi ,mlinzi wake mkuu Fernando pamoja na mtu mwingine ajulikanaye kwa jina la Gabon.Huyu kazi yake kubwa ni kutesa watu.Ndani ya chumbakile kulikuw ana mitambo mbali mbali maalum kabisa kwa ajili ya kutesea watu.

“ Madam nadhani kwa leo inabidi tuishie hapa kwani tukiendelea zaidi ya hapa anaweza akapoteza masha.Tumuache apumzike na tuendelee tena na zoezi kesho” akasema Gabon .Rosemary Mkozumi akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Ni mara ya kwanza leo kukusikia ukimuonea huruma mtu na kupendekeza tusiendelee kumtesa.You’ve let me down Gabon..I’m totally disappointed!! Akasema Rose
“ Madam tumemtesa sana huyu msichana na wewe mwenyewe umeshuhudia .Ninaomba nikiri kwamba katika muda wote wa kuifanya kazi hii hata siku moja sijawahi kumtesa mju jasiri kama huyu.Nimetumia kila aina ya mateso lakini bado hajafungua mdomo wake na kutupatia kile ambacho tunakitaka.Naomba mnisikilize na tumuache kwa leo apumzike hadi kesho.Tukiendelea kulazimisha kumtesa zaidi tunaweza kumuua na kukosa kila kitu”akasema Gabon

“ Gabon hujamminya vya kutosha huyu.Endelea na kazi hadi nitakaposema mwenyewe basi”akasema Rosemary Mkozumi
“ madam nadhani Gabon yuko sahihi.Tumpumzishe huyu msichana hadi kesho.Tunaweza kumpoteza na kukosa kila kitu” akasema Fernando.Rose akamtazama tena Antha halafu akasema
“ ok sawa .Tumpumzishe hadi kesho ila kesho lazima tuhakikishe anafumbua mdomo wake na kutupata kile tunachokitaka” akasema Rosemary Mkozumi na kuinuka akaelekea chumbani kwake.
“ Huyu Mathew na kundi lake wanaonekana ni watu waliokubuhu sana katika hizi kazi.Huyu msichana pamoja na mateso yote lakini bado hajathubutu luufungua mdomowa wake na kutamka hata neno moja.Ujasiri wa namna hii hupatikana kwa wanajeshi ama majasusi pekee. Watu hawa wamekula yamini Ya kutokusema jambo lolote lile na nina hakika hata tukimtesa vipi yuko tayari kufa kuliko kutueleza mahala Mathew aliko.Kama huyu msichana mdogo yuko hivi je huyo Mathew atakuaje? Lakini pamoja na yote lazima nihakikishe kwamba nimemtia mikononi Mathew kwa gharama zozote zile ndani ya kipindi kifupi sana na kama nisipofanya hivyo he will haunt me like a ghost.”akawaza Rose huku akielekea chumbani kwake.
Gabon akisaidiana na Fernando wakamfungua Anitha na kumtoa mle chumbani wakamrejesha katika chumba alichokuwa amefungwa.Hakuwa akitazamika,uso wake wote ulikuwa umetakapaa damu.Hakuwa na hata nguvu za kusimama.Baada ya kumlaza kitandani Gabon na Fernando wakatoka mle chumbani na kukifunga chumba.
“ Fernando simfahamu msichana huyu ni nani na amefanya nini lakini nakuhakikishia kwamba ni mmoja kati ya wanawake majasiri mno.Kwa mateso niliyompa sina hakika kama hata mimi ningeweza kuvumilia ,lazima ningesema tu ninachotakiwa kukisema .Nina hakika hata kama tukiendelea kumtesa tena kesho hatasema chochote.Ana ujasiri wa kipekee sana na yuko radhi kufa kuliko kuonyesha mahala aliko huyo mwenzake.Huyu si mtu wa kawaida lazima atakuwa amepata mafunzo ya hali ya juu sana kuhusiana na kutokutoa siri ..Pamoja na hayo kwa usiku wa leo tunatakiwa tumchome sindano ambayo itampunguzia maumivu na atalala vizuri bila matatizo.madam Rose anatulipa pesa nyingi sana lakini nyakati nyingine lazima tuwe na mioyo ya kibinadamu.Tumsaidie huyu msichana” akasema Gabon .Fernando akafikiri kidogo na kusema

“ lakini endapo Madam akifafahamu kuhusu jambo hili sote tutakuwa matatizoni.”
“ Usjili kuhusu hilo hawezi kujua.Its just you and me” akasema Gabon na kuingia tena chumbani akafungua sanduku lake na kutoa kichupa Fulani cha dawa akamchoma Anitha kisha wakatoka.

“ Nimekuwa mtesaji kwa muda mrefu lakini sijui ni kwa nini kwa huyu dada moyo unaniuma sana kumtesa.Laiti ningekuwa na uwezo wa kumsaidia ili aweze hata kutoroka basi ningefanya hivyo lakini sina uwezo wa kumsaida.”akawaza Gabon wakati akitoka mle chumbani



********


Ni watu wachache walioonekana kuwa macho pale msibani.Wengi tayari walikuwa wamekwisha lala.Wakati wengine wakiwa usingizini ndani ya chumba cha maongezi ya farahgha ndani ya jumba hili ,Dr Joshua na jaji Elibariki walikuwa na maongezi ya muhimu sana.
“ Mr Judge it’s me and you now.We have all the time in the world so tell me everything .”akasema Dr Joshua
“Mr president kwanza kabisa napenda nikushukuru tena kwa kunipa uhuru huu na nimeweza kuhudhuria msiba wa mke wangu kitu ambacho sikuwa natarajia ningekipata.Kama nilivyokueleza awali ni kwamba hii sintofahamu yote ilianza baada ya kesi ya Peniela.Kama utakumbuka mimi ndiye niliyeamua kesi ile na kumuachia huru.Kesi ile ilikuwa na sintofahamu nyingi na baada ya maamuzi yale niliyoyatoa ya kumuachia huru Peniela mambo mengi sana yali zungumzwa na zaidi sana nilipokea lawama nyingi na hata wewe mwenyewe ulinilaumu sana kwa kupuuza kile ulichokuwa umeniamuru kukifanya.Baadaya kesi ile nilijiuliza sana kwa nini nguvu kubwa ilitumika kutaka peniela akutwe na hatia na kufungwa? Nilikosa jibu na nikaamua kuutafuta ukweli ni nani aliyemuua Edson na kumtupia kesi Peniela?.Sikuwa na taaluma ya kufanya uchunguzi hivyo ikanilazimu kumtafuta mtu ambaye ana weza akafanya kazi hii na nikampata Mathew.Mathew aliwahi kufanya kazi katika idara ya ujasusi na baadae aliamua kuiacha kazi hiyo baada ya familia yake yote kuteketezwa kwa moto.” Elibariki akanyamaza kidogo kisha akaendelea
“ wakati uchunguzi ukiendelea kuhusiana na nani alimuua Edson,kukatokea kifo cha Dr Flora.Flaviana akaomba nimsaidie kufanya uchunguzi wa kubaini sababu ya kifo chake.Kwa kumtumia Mathew tuliweza kufanikiwa kugundua nini kilimuua Dr Flora na taarifa ile tutakuletea na kwa bahati mbaya ukaikataa na badala yake ukaileta ripoti ile ambayo ulidai ilitoka kwa madaktari wa hospitali kuu ya taifa.Usiku wa siku ile Flaviana akanipigia simu na kuniomba tuonane na akaniomba tuachane na mambo yale ya ripoti zile za uchunguzi kwani hazitatusaidia chochote.Mimi kama jaji na ambaye siku zote ninaitaka haki sikukubaliana naye nikaondoka.Kabla sijaingia katika gari nikapigiwa simu na mwanamke mmoja ambaye simfahamu akaniomba nisiingie katika gari kwani kuna mpango w a kuniua.Nilimpuuza na nikaendelea na safari yangu.Garini nilikuwepo mimi na mwenzangu anaitwa Noah.Baade tulishambuliwa na Noah akapoteza maisha na mimi nikachukuliwa na Yule mwanamke nisiyemjua nikaenda kujificha kwa peniela.Baadae Mathew akaja kunichukua akaenda kunificha kwake” akanyamaza akameza mate na kuendelea
“ Kitendo kile cha mimi kunusurika kuuawa kiliongeza udadisi na kutufanya tutake kuchunguza zaidi na ndipo tukagundua mambo mengine yaliyojificha zaidi.Kwanza tuligundua uwepo wa kikundi kiitwacho Team Sc41.Kikun………….”
“ Wait !! Dr Joshua akamkatisha

“ Umesema Team Sc41? Ni kitu gani hicho? Akauliza
“ Hiki ni kikundi kidogo kinachofanya shughuli zake kwa siri kubwa hapa nchini lengo lao kuu likiwa ni kulinda maslahi ya Marekani hapa nchini.”

“ What ?!! Yaani hapa nchini kuna kitu kama hicho? Kwa nini mimi nisifahamu? Kimeanza lini hicho kikundi?
“ Si rahisi kufahamu kuhusu kikundi hiki kwani ni cha siri sana na kilianza wakati wa awamu ya Deus Mkozumi.Kikundi hiki ni cha watu wachache ambao hujishughulisha na kazi moja tu ya kuhakikisha kwamba maslahi ya Marekani yanalindwa kwa hiyo wamepenyeza mizizi yao katika serikali na wanaweza kupata habari za kila kinachoendelea na hivyo wanaweza kujua kama kuna hatari yoyote katika uwekezaji mkubwa wa Marekani hapa nchini” akasema Elibariki
“ Team Sc41 waliweza kufahamu kuhusiana na biashara uliyokuwa unataka kuifanya ya package yenye kirusi Aby na wana mikakati ya kuipata package hiyo”
“ Hebu subiri kidogo jaji,umesema Team SC41 waligundua kuhusiana na package,nataka kujua waligunduaje wakati suala hili lilikuwa ni siri kubwa na tuliokuwa tunalifahamu ni watu watatu tu,mimi Dr Kigomba na Captain Amos? Hao wenzako uliokuwa unashirikiana nao ,pia ni Team SC41? Akauliza Dr Joshua
“ Watu niliokuwa ninashirikiana nao si washirika wa Team Sc 41 .Kuhusu Team Sc 41 waligunduaje kuhusu mpango wa kuiuza package ile yenye kirusi Aby ni kwamba tayari walikuwa na watu wao waliokuwa wanawatumia kupata habari zote na kila kilichokuwa kinafanyika.”

“ Walikuwa na watu wao?? Akauliza Dr Joshua kwa mshangao

“ Ndiyo.Hukuwa unalifahanmu hili mr President lakini watu waliokuwa wanawatumia ni Captain Amos na Peniela”
“ Peniela !!! Dr Joshua akastuka na Ghafla akasimama akamshika Jaji Elibariki kwa nguvu na kumkaba shingoni




TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
PENIELA SEASON 3

SEHEMU YA 38

MTUNZI 😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Hebu subiri kidogo jaji,umesema Team SC41 waligundua kuhusiana na package,nataka kujua waligunduaje wakati suala hili lilikuwa ni siri kubwa na tuliokuwa tunalifahamu ni watu watatu tu,mimi Dr Kigomba na Captain Amos? Hao wenzako uliokuwa unashirikiana nao ,pia ni Team SC41? Akauliza Dr Joshua
“ Watu niliokuwa ninashirikiana nao si washirika wa Team Sc 41 .Kuhusu Team Sc 41 waligunduaje kuhusu mpango wa kuiuza package ile yenye kirusi Aby ni kwamba tayari walikuwa na watu wao waliokuwa wanawatumia kupata habari zote na kila kilichokuwa kinafanyika.”
“ Walikuwa na watu wao?? Akauliza Dr Joshua kwa mshangao
“ Ndiyo.Hukuwa unalifahanmu hili mr President lakini watu waliokuwa wanawatumia ni Captain Amos na Peniela”

“ Peniela !!! Dr Joshua akastuka na Ghafla akasimama akamshika Jaji Elibariki kwa nguvu na kumkaba shingoni


ENDELEA……………………..


“ Sikiliza jaji,najua wewe na wenzako mmekwisha nichunguza sana na mmefahamu mambo mengi kuhusu mimi kwa hiyo nina hakika tayari umekwisha fahamu Peniela ni nani kwangu so be very carefull when you mention that name in front of me !! asema Dr Joshua halafu akamuachia jaji Elibariki aliyekuwa akikohoa kutokana na kukabwa shingoni .
“ I don’t want the name Peniela to appear in our conversations. Do you understand ? Dr Joshua akamuuliza jaji
“ Mr Preseident ulitaka nikueleze ukwelI na ndicho kitu ninachokifanya hapa.I’m telling you the truth. Ukweli ninaokueleza hapa utakuwa na msaada mkubwa kwako Mr President na ili mambo yako yafanikiwe unatakiwa utulie na unisikilize kila kile nitakachokuambia na ninaomba uniamini hata kama utaumia” akasema jaji Elibariki

“ Vyovyote vile itakavyokuwa lakini nimesema sitaki kusikia jina la Peniela likitajwa humu ndani !! akaendelea kusisitiza Dr Joshua kwa ukali
“ Dr Joshua nimewasaliti wenzangu waliojitolea maisha yao kwa ajiliyangu kwa hiyo sina haja ya kuficha tena jambo lolote lile.Niruhusu nikueleze ukweli wote bila kukuficha hata kitu kimoja” akasema jaji Elibariki.Dr Joshua hakujibu kitu akabaki kimya alionekana kuchanganywa sana na jaji Elibariki kumtaja Peniela

“ Dr Joshua ukimya huo ni ishara kwmba ninaruhusiwa kuendelea .” akasema jaji Elibariki halafu akaendelea.

“ Peniela ni mtu ambaye team Sc41 wanamtumia sana katika mipango yao mingi na walim..”
“ jaji Elibairki tafadhali naomba nisirudie tena kulisema hili,sitaki jina Peniela liingie katika maongezi yetu !! Kwa nini hutaki kunisikia?!! Peniela ni malaika wangu na hawezi katu kunifanyia hayo unayoyasema !! Akasema Dr Joshua kwa ukali
“ What do you want me to say Mr President? You don’t want to know the truth?!! Akauliza jaji Elibariki Dr Joshua hakujbu kitu
“ Kama hutaki kuusikia ukweli ninaokueleza basi hakuna haja ya kuendelea na maongezi haya.Watu ambao hutaki niwaseme ndio hao hao ambao wamekusaliti na kutoa habari zako.Peniela ambaye umekuwa ukimuona kama malika wako hakupendi hata chembe na ndiye anayeongoza mipango yote ya kukuangamiza.Anatumiwa na team SC41 ambao ndio waliompa mafunzo na wakamuunganisha kwako makusudi kabisa wakimtumia captain Amos .Walikuwa na lengo moja tu la kuipata package hiyo.Nakuhakikishia tena Mr President kwamba Peniela ni mwanamke hatari sana ambaye hana mapenzi yoyote kwako bali anayetumiwa ili kukumaliza.Na kama huniamini hili nikwambialo basi usichukue hatua zozopte na baada ya muda utaamini kile nikwambiacho.Peniela amekuwa akiutumia uzuri wake ili kupata taarifa mbali mbali toka kwa watu tofauti tofauti.Unafahamu kwamba mpaka sasa tayari Peniela na Dr Kigomba wana mahusiano ya kimapenzi?
” What ?!! Dr Joshua akastuka sana

“ Lazima ustuke kwa sababu ni kitu ambacho hujakitegemea kabisa lakini huo ndio ukweli.Dr Kigomba na Peniela ni wapenzi.”
“ No I cant believe this !!!..akasema Dr Joshua

“ Ulimpa Dr Kigomba jukumu la kumchunguza Peniela kamaana mahusiano yoyote na mimi si ndiyo?

“ Ndiyo nilimpa kazi hiyo baada ya kupata taarifa kwamba ulikuwa umejificha kwa Peniela “ akasema Dr Joshua

“Basi ulipompa jukumu hilo alijikuta akiingia katika mahusiano na peniela na akasahau hata jukumu ulilomkabidhi.Kukuhakikishia hilo kuna saa ambayo Peniela alimpatia Dr Kigomba ambayo akiivaa humuonyesha kila sehemu alipo kwa hiyo inakuwa rahisi kwao kumfuatilia.Wanamfuatilia Dr Kigomba kwa sababu wanafahamu ndiye unayemtumia sana katika mipango yako mingi na hasa huu wa package.kwa kumtumia Peniela waliweza kuiunganisha simu ya Dr Kigomba katika kompyuta yao kwa hiyo walikuwa na uwezo wa kusikia kila kile ambacho Dr Kigomba alikuwa anakiongea katika simu yake.Kila ambacho ulikuwa unaongea naye katika simu tulikuwa tunakisikia.Tayari wanafahamu kuhusu kila mpango mnaoupanga .Wanafahamu kuhusu ujio wa Hussein ambaye ndiye anayekuja kuichukua package hiyo ,kwa ujumla niseme wanafahamu siri zako nyingi sana na hii yote imewezekana kwa sababu ya Peniela.” akasema jaji Elibairki

“ Ouhmy God !! akasema Dr Joshua na kuinama
“ Peniela ..Peniela …!! Akasema kwa uchungu na kusimama kisha kwa hasira akaibinua meza
“ Aaaaghhhh !!! akapiga ukelele mkubwa halafu akakaa chini na kuanza kudondosha machozi
“ Mr President tafadhali naomba unyamaze na tuendelee na maongezi yetu.Wewe ni mtu mkubwa ndiye kiongozi wa nchi hii kwa hiyo hutakiwi kudondosha chozi hata ukiumia vipi. Crying is the sign of defeat and you are the powerful man in this country so don’t let them defeat you.I can help you Mr President” akasema jaji Elibariki na kumshika mkono Dr Joshua akamketisha sofani.
“ Jaji nimeshindwa kuvumilia imenibidi nitoe machozi kutokana na namna nilivyoumizwa na taarifa hizi.Ninampenda Peniela kwa moyo wangu wote na kila ninachokifanya ninakifanya kwa ajili yake.Ouh jamani kwa nini Peniela anifanyie hivi? Nilimpenda Yule msichana na nilikuwa tayari kufanya kila nililoweza ili kumfurahisha lakin kumbe nilikuwa ninamfurahisha nyoka.Nimeumia sana .” akasema Dr Joshua
“ Pole sana dr Johsua .Hivyo ndivyo watu walivyo.Wale unaowapenda na kuwaamini ndio hao hao ambao kesho watakuangamiza.,Unatakiwa uwe makini sana kabla ya kuamini mtu yeyote Yule” akasema jaji Elibariki

“ Ahsante sana jaji kwa kunifumbua macho.Nilikuwa nimepofushwa na Peniela naniliamini yeye ni malaika kumbeni ibilisi aliyekuwa anaitafuta roho yangu.Umeniokoa sana jaji.Sikutegeema kama siku moja ungegeukana kuwa mkombozi wangu.Ninakuahidi nitasakaPeniela kokote aliko na nitampata tu.!!
“Dr Joshua kwanza kabisa kabla ya kuwatafuta Peniela na Mathew kuna mambo ambayo lazima tuyafanye.”

“ Hebu nishauri kijana wangu “ akasema Dr Joshua
“ Kwani peniela umekwisha wasiliana naye toka jana? Akauliza Elibariki.
“ Nilikuwa na miadi ya kuonana naye jana mchana lakini nilimpigia simu na haikuwa ikipatikana.”

“ Basi lengo la kutaka kuonana nawe lilikuwa ni uipata simu yako ili aweze kuzipata namba za simu za Hussein kwani badompaka sasa hawamfahamu na kupitia namba hizo za simu wangeweza kumfahamu kirahisi sana.Lakini endapo akikupigia simu na kutaka muonane usimweleze chochote kuhusu haya niliyokuambia na upange kukutana naye na hiiitakuwa ni njia rahisisana ya kuweza kumkamata kwani mpakassa bado hajafahamu kama niko nawe.Pili n kuhsu Dr Kigomba.Simu yake inatakiwa kuchukuliwa na kuzimwa kabisa na ile saa anayoivaa aliyopewa na peniela inatakiwa kuvuliwa kwani akina Mathew wanamfuatailia na kufahamu kila mahala alipo kwa kutumia vitu hivi viwili. Wanatumia teknolojia ya haliya juu sana na haya yote yanafanyw ana Anitha ambaye ni mshirika wa Mathew.Huyu mwanadada ana utaalamu wa hali ya juu sana wa mamboya elekroniki na ndiye anayebuni programu hizi zote.Kwasasa Anitha anashikiliwa nyumbani kwa Rose na ninakushauri umwambie Rose amchunge sana na asije akamuachia mwanadada huyu kwani ndiye roho ya Mathew.Huyu ndiye anayemuwezesha Mathew kufanya kazi zake kirahisi.Tukimshikilia huyu Mathew atapata wakati mgumu sana wa kutekeleza mipango yake “ akasema Elibariki

“Huyu Mathew anaishi wapi?
“ kwa sasa hana makazi kwa sababu nyumba aliyokuwa anaishi Rosemary aliiteketeza kwa moto na kila kilichokuwamo ndani yake kiliteketea .Kwa hivi sasa sifahamu ni wapi alipo Mathew lakini kwa kumtumia Anitha tunaweza kufahamu yuko wapi.”

“ Elibariki nakushukuru sana kwa kunitoa usingizini.Sikujua kama nina maadui wakubwa namna hii tena walio karibu kabisa na mimi na ambao wangeweza hata kunimaliza sekund e yoyote .Kuanzia sasa wewe ndiye utakayekuwa mshirika wangu mkuu.I’ll give back to you all that I took from you.Nisaidie tuimalize biashara hii na ninakuahidi kwamba uakuwa ni mtu mkubwa sana. kuna jambo ambalo sikuwa nimelifikiria lakini kwa sasa limekuja akilini.I’ll make you the next president of Tanzania”
Jaji Elibariki alibaki mdomo wazi akimkodolea macho Dr Joshua asiamini kile alichoambiwa.

“ Umesema nini mzee? akauliza

“ kwa mambo uliyonifanyia jaji umenifanya nikuthamini ghafla kuliko watu wote kwani bila wewe ningeendelea na mipango yangu yote bila kufahamau chochote na mwisho wangu ungekuwa ni wa aibu kubwa.Ni wewe ambaye nilikuwa nimekuweka katika kundi la adui zangu wakubwa lakini ndiye umekuja na kunifumbua macho.kwa hili ulilolifanya nimesema kwamba nitakufanyia kitu ambacho sikuwa nimekusudia kukifanya.Nitakufanya uwe rais wa jamhuri ya muunganowa Tanzania.” Akasema Dr Joshua.jaji Elibarki machozi ya furaha yakamdondoka.
“ is this true Dr Joshua?
“ Ndiyo Elibarik.Uwezo huo ninao na nitafanya hivyo na hakuna anayeweza kunizuia kufanya hivyo.I’ll make you a very powerfull man in this country na nina hakikani wewe ambaye utaweza kuendelea kuyalinda maslahi yangu.Nilikuwa nafikiria sana ni nani ambaye ninaweza nikampa nchi na akaendelea kuyalinda maslahi yangu lakini nashukuru nimekupata wewe.Nina hakika wewe ni mtu sahihi kabisa na unafaa.”Akasema Dr Joshua.Jaji Elibariki akainuka na kwenda kumpa mkono akamshukuru
“ Dr Joshua sikuwahi kufikiri kuhusu jambo kama hili ! akasema kwa furaha jaji Elbariki
“kwa hiyo kama halikuwa katika ndoto zako anza sasa kuota kwamba umekuwa rais wa Tanzania kwani jambo hili linakwenda kutimia.Nitakuelekeza nini cha kufanya muda utakapofika lakini lazima ukae ukijua kwamba wewe ndiye utakayekuwa rais wa Tanzania baada ya mimi kuondoka madarakani.Lakini pamoja na hayo kuna jambo nataka nikuombe”
“Jambo gani Dr Joshua?
“ Samahani lakini kwa kulisemahilikabla hata hatujamzika Flaviana mkeo lakini ni ukweli ulio wazi kwamba Kwa sasa baada ya Falivana kututoka utabaki mwenyewe na kwa kuwa bado kijana lazima utaoa tena lakini mimi lengo langu kubwa ni kutaka familia yangu iendelee kukaa katika neema ya uongozi kwahiyo basi ninakutaka ujenge mazoea ya karibu na Anna mbaye naye kwa sasa yuko mwenyewe baada ya mpenziwake kufariki.Ninajua umenielewa ninaposema hivyo kwani ninataka utakapokuwa rais yeye awe ni mke wa rais na familia yetu iendelee kutawala.Unalionaje wazo hili? Akauliza Dr Joshua
“ Hilo ni wazo zuri Dr Joshua lakini naomba uniachie kwanza jambo hilo nilitafakari na kulifanyia kazi na nitakupa majibu”akasema Elibarik,.Dr Joshua akafungua mlango na kumuita msaidizi wake akamuomba amuite Dr Kigomba ambaye alifika mara moja .Dr Joshaua akamuangalia kwa macho makali kwa sekunde kadhaa kisha akasema
‘ Kigomba give me your phone” .Huku akishangaa Dr Kigomba akachukua simu yake na kumpatia Dr Joshua.

” Kuanzia sasa hautaitumia simu hii utatafuta simu nyingine.Vua na hiyo saa mkononi”akaamuru Dr Joshua
“ Dr Joshua whats going on? Akauliza Dr Kigomba kwa wasiwasi.
“ Kigomba nadhani umekwisha fahamu nini kinaendelea.Nilikupa kazi ya kumchunguza peniela na badala yake ukaanzisha mahusiano naye.Ulifanya kosa kubwa sana Kigomba”
“ Nani kakueleza habarihizo dr Joshua?
“ Kigomba tayari ninafahamu kila kitu kwa hiyo hakuna haja ya mabishano. Siku zote nimekuwa nkikuonya kuhusiana na udhaifu wako kwa wanawake lakini hukutaka kunisikia.”
“ Dr Joshua sikuelewi una maanisha nini” akasema Dr Kigomba.Dr Joshua akamtazama kwa macho makali na kusema

“ Kigomba unafahamu Peniela ni nani? Unafahamu ni kitu gani alichotufanyia kupitia kwako?
“ hapana Mr President.”akajibu Dr Kigomba

“ Peniela ni nyoka mkubwa na tayari ameunganisha simu yako katika program yao na wanasikia kila kitu unachokiongea kupitia simu yako.Kama hiyo haitoshi alikupa saa hii kama zawadi uivae lakini kwa taarifa yako saa hii imefungwa kifaa maalum ambacho kina uwezo wa kuwaonyesha kila mahala ulipo.Tumshukuru sana Elibariki ambaye ametufumbua macho na kama si yeye tusingeweza kujua chochote kinachoendelea” akasema Dr Joshua.Kigomba alibaki kimya akiwatazama.

“ I’m sorry Mr President,sikuwa ninafahamu lolote kuhusiana na alichokifanya Peniela.” Akasema Dr Kigomba

“ Kigomba mimi na wewe tutakuwa na maongezi yetu baadae lakini kwa sasa naomba nikufahamishe kwamba mipango yetu yote imekwisha gundulika na kama tusipochukua hatua za tahadhari angali bado mapema basi hatutaweza kufanikiwa.Cha kwanza tunachotakiw a kukifanya ni kumuhamisha kwa siri Hussein na ujumbe wake mapema kesho asubuhi na kesho hiyo hiyo jioni kila kitu kikamilike na Hussein aondoke nchini haraka na baada ya hapo tutaendelea na zoezi la kumsaka mtu aitwaye Mathew ambaye huyu ndiye adui yetu mkubwa sana kwa sasa.”akasema Dr Joshua
“Mr President ninaomba niuliz……………”Dr Kigomba akataka kuuliza swali lakini Dr Joshua akamzuia
“ Kigomba hakuna muda wa maswali sasa hivi.Anza sasa hivi kushughulikia hoteli ya kuwahamisha Hussein na ujumbe wake.Tutaongea baada ya mambo yote kukamilika” Akasema Dr Joshua na Dr Kigomba akatoka mle chumbani
Jaji Elibarikina Dr Joshua waliendelea na maongezi na ilipotimu saa tisa za usiku wakaagana.

“ Nenda kalale jaji kesho tuna siku ndefu sana.Kesho tutamzika Flaviana na kisha tutaendelea na mchakato mwingine.Tutaongea zaidi kesho lakini nakushukuru sana jaji.” Akasema Dr Joshua na kumuongoza jaji Elibariki kuelekea katika chumba maalum cha wageni


.

MATHEW NA PENIELA WAKO WAPI NA WANAFANYA NINI? DR JOSHUA ATAFANIKIWA KATIKA MIPANGO YAKE YA KUKIUZA KIRUSI ABY? MWISHO WA PENIELA SEASON 3 .USIKOSE KUISOMA PENIEAL SEASON 4 HIVI KARIBUNI……….
 
Mkuu LE
WAKUU TUFANYE HIVI 2 KAMILI HAIFIKI NITAKUWA NIMEWEKA MZIGO NA KUIMALIZA KABISA SEASON YA 3.

natamani sana nibwage mzigo uishe lkn mambo yananisonga kidogo lkn sio mbaya maana kwa siku lazima zifike sehem 5 nazaidi. ningesema niweke kila siku sehem 1 tungekesha
LEGE tunashukuru unapenda ushauri hK
Kilichobaki ili kazi iwe rahisi... Penny atoe papuchi kwa fernando au vicent, lakini tayari kashammanulia deus ambae ni partner wa vicent.... Labda kwa fernando... Si ndio silaha take ya maangamizi.... Papuchi ake..
Na huko walikokwenda kujificha penny na mathy.. Kuna jipya lenye kuleta matumaini..... Ila tusiwasahau team sc41... Nao wanahaha... Kujua penny alipo....
Ila mpaka hapa team sc41 ... Yote ya east africa sawa na mathy mmoja....
Kama kwenye hii story Peniela ana ngoma basi ataua wengi dah hiyo papuchi
 
Huyu jaji mdomo mwepesi kama kiberenge kayamwaga yote hiyo ndio fitna kijiji bwana kigomba lake hilo jumba bovu.
 
Back
Top Bottom