Pentekoste iliyochangamka

Una shida kwenye mfumo wako wa kufikiri, uko utumwani wewe ni MATEKA uko kwenye njia inayokupotosha na bado unajiona uko sahihi
 


Nchi ya kiseng3 sana hii .... sijui watu wanatafuta nini makanisani hadi yanazitupa lulu zao kwa nguruwe na nguruwe wana geuka kuzikanyaga kanyaga na kuwararua kama ilivyo andikwa ....hao wamama wote wenye makanisa no ndiyo nguruwe ...kina mwamposa ..gamanywa ...kakobe ...kiboko ya wachawi....wote hawa ndiyo NGURUWE WALIO ANDIKWA KWENYE BIBLIA
 
biblia inaeleza wazi bahari ni watu wengii ambao huyo mnyama anakaa juu yao
Nafsi inakaa ndani ya mwili hivyo mwili upo juu ya nafsi...mnyama ni miili yetu wenyewe mtu mwenye akili awezi kutokujua hili.
 
Matendo ya Mitume 2:1-2
[1]Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.

[2]Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Siku ya pentecoste walikuwa pamoja ndipo roho mtakatifu akawashukia, so pentekoste sio kushuka kwa roho mtakatifu ilikuwa ni siku ambayo wayahudi walikusanyika pamoja, na katika siku hiyo roho mtakatifu akawashukia
 
Saa hizi nimejifunza kujiombea na kujitakia mema binafsi kuliko kusubr dini ama kiongozi wa kiroho,

Ikiwa hata kujiombea siwezi au imani ya kupata sina mpaka aniombee yeye huoni pa zito hapo ?
 
soma io kjv ilipotimiaa siku ya pentekoste. inamana ilishaanzaaaa,
kwa kale ilikuwa ni kama siku ya jubelee ya kuachiliwa watumwa. pentekoste ilikuwa hamsini kamili. na ndipo roho mtkt alishuka. pentekoste ni tukio la kushuka kwa roho mtakatifu, kabla ya hapo kulikuwa na kukusanyika kwingi. ila hazikuwa pentekoste. pentekote ilikuwa ni moja na ilitukia siku hio
 
Nafsi inakaa ndani ya mwili hivyo mwili upo juu ya nafsi...mnyama ni miili yetu wenyewe mtu mwenye akili awezi kutokujua hili.
sijakuambia nyama nimekuambia mnyama.

ufunuo 17;15
Kisha yule malaika akaniambia, ‘‘Yale maji
uliyoyaona, yule kahaba akiwa ameketi juu yake
ni jamaa za watu, makutano, mataifa na lugha.
 
injili haitegemei pesa kabisaaa ili isonge mbele. kama hukujua biblia imekuwa ikihubiriwa na maskini. yesu hakuwahi kuwa mtu wa injili ya pesa, hata biblia inasema mmepewa bure toeni bure.
Ibrahimu alikuwa tajiri. Biblia inasema ktk wanna wa Israel watatoka wafalme. Daud, Suleiman na kadhalika, lengo Ni kuonesha kwamba Mungu sio wa kimaskini na umaskini kwa Mungu haiwezekani Mungu anaweza fanya kitu kidogo tu na kikawa sababu ya utajiri kumbuka yakobo kwa Laban, yusuph kwa pharao na hata yesu yuda alikuwa mshika mfuko wa fedha. Je hizo fedha zilitoka wapi?
 
Mtumishi ambaye utasema muongo nikakuelewa Ni kiboko ya wachawi, huyu yupo laivu siwezi kupinga sababu hata maneno yake yanaonyesha wazi. Lkn wakina mwamposa na wengine unaowajua wewe lete hapa vioja vyao tuone kama inaingia akilini
 
si kwamba alimradi mtu anafanya miujiza ni mtumishi wa mungu kaka. fumbuka macho uweze kuonaa. maandiko yapo wazi
Hakuna Cha maandiko yapo wazi. Wewe kinachokusumbua Ni wivu kuona kina mwamposa wanapata pesa. Ungeongelea zumaridi ningekuelewa vizuri sababu zumaridi hamuhubiri yesu yeye anamungu wake.
 
sijakuambia nyama nimekuambia mnyama.

ufunuo 17;15
Kisha yule malaika akaniambia, ‘‘Yale maji
uliyoyaona, yule kahaba akiwa ameketi juu yake
ni jamaa za watu, makutano, mataifa na lugha.
Sasa miili ya binadamu si ndiyo mnyama na ndiyo maana ya kahaba na miili sindiyo imebeba hayo yote kabila lugha rangi ....kahaba ni mwili wa binadamu kinacho kufanya wewe usielewe ni kushindwa kujua misingi ya dini....dini ina misingi mikuu ambayo mambo yote na fumbo zote zinategemea hiyo misingi nayo ni
1)MUNGU
2)SHETANI
3)MWANADAMU
4)THAWABU
5)DHAMBI
6)UTAKATIFU
7)LAANA
8)PEPONI
9)JEHANAM
10)MBINGUNI
11) MALAIKA
12)MAJINI
Hakuna fumbo lolote lililo nje ya hivi vitu 12 hivyo hayo mafumbo yasikutishe wala siyo mambo mapya
 
Mtumishi ambaye utasema muongo nikakuelewa Ni kiboko ya wachawi, huyu yupo laivu siwezi kupinga sababu hata maneno yake yanaonyesha wazi. Lkn wakina mwamposa na wengine unaowajua wewe lete hapa vioja vyao tuone kama inaingia akilini
Wote hao ni waongo
 
bwana yesu mbona alisha waambia njia ya kupimaa.
unamana unaishi na huifaham umbali huu.
pima kwa neno tuu.
Kwamba wewe unakioimo cha kupima ukatoliki.. aisee mental case are real
 
Shida sio kanisa shida ni msingi wa kuanzisha kanisa husika.Umeanzisha kanisa kwa madhumuni ya watu wamfuate Kristo au kwa manufaa yako binafsi?Unawahubiria waumini wako ukweli ?hususan ni kuachana na dhambi (kuzini,kuiba,kutembea na waume za watu)au unawahuburia wanachotaka kusikia masikioni mwao.
Wengi wao huduma zao ni kwa manufaa yao wenyewe,wanahubiri habari za mafanikio ya kidunia wanasahau kuhusu mafanikio ya kiroho,wanapotosha waumini na kuwafundisha ubinafsi.Hawahubiri katika roho bali wanahubiri katika mwili(motivational speaker)

Mchungaji mahubiri yake yote hujawahi kusikia akiongelea kuhusu dhambi na namna ya kukua kiroho,yeye mahubiri ni miujiza ,namna ya kufanikiwa kibiashara,kuangalia fursa na mengineyo ambayo siyo kwa ustawi wa roho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…