Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa

Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa

Wengi hili suala la gesi hamjalijua vizuri. Tanzania tunazlisha CNG, hatuzalishi LPG(hii mitungi ya kupikia).
CNG kuigeuza kuwa LPG ni ngumu na gharama na ni hatuwezi kabisa.
Option iliyopo ni kutumia mabomba kupitisha hii CNG ili iweze kutumika direct. Mradi wa kujenga mabomba kwa nchi nzima hadi vijijini ni gharama na ni ngumu sana, nadhani unakumbuka mradi wa bomba la gesi mtwara tulitumia tril 2.4 na zilikua za mkopo ambao hadi leo haujaisha.

Hapo ni kutoka mtwara kuja dar, vipi kutoka mtwara kwenda Bukoba, kigoma, mwanza, katavi, Tabora, geita n.k tena mabomba yafike kila Kijiji. Ni trillions ngapi hizo zitakua??

Ndio maana tunanunua hii LPG(mitungi) kutoka nje, na hasara yake ni Kama unavyoona kwenye mafuta, ni ngumu kucontrol bei na upatikanaji. Ambapo watu wataendelea bado kutumia mbadala kwa kuwa ni rahisi na unapatikana(mkaa na kuni).

Unasema miti inaisha? Ni kweli inaisha, Ila kwenye hili kwanza ningeishauri serikali kusitisha tena biashara ya magogo maana imeanza tena na yanasafirishwa nje ya nchi.

Lakini kwa watu wa vijijini kwa umaskini huu uliopo, na hayo niliyokueleza unafikiri watakuwa na laki 1 kila mwezi ili kutumia gesi? Ikiwa tu chakula ni shida kukipata? Wafanyakazi hawa tu wa serikali wenye mishahara huo ubavu hawana
Hebu agiza kinywaji huko ulipo
Nakuja kukulipia
Asiyekuelewa hapa basi tena

Ova
 
Mkuu labda mtungi ukiwaishia
Watajaziwa bure....

Ova
Labda iwe hivyo, hapo mm pia nitakubali inawezekana.

Jambo ambalo haliwezekani tuwe tunakubali tu haliwezekani. Ni sawa na kupeleka yard ya magari katavi, unaenda kumuuzia nani?
 
Kwamba mtungi mdogo wa gas unaweza kuwa mbadala wa umeme na kukidhi mahitaji yaliyokuwa yanatatuliwa na umeme??
 
Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa.

Inawezekanaje? PESA za REA zielekezwe kwenye ruzuku ya gesi.

Takwimu zinasema umeme umeenda nchi nzima vijiji kibao vijiji vichache tu vimesalia kupata umeme

Pesa za REA sasa zipelekwe kwenye gesi ya kupikia.
Umeenda umewafikia watumiaji?

Ebu tuwailize watu wa Kongwa jirani Spika wa zamani. Sagara A na Sagara b, nenda hadi Pemba moto kote huko Rea ikifika nakuwasha nyuma zisizo zidi Tano Tano. Kila Kijiji.

Katavi wilaya ya Tanganyika, vijiji kaza Nako ilikua hivyo. Kuna Kijiji wilaya ya Muleba , umeme uliwashw mskitini ukatoka wakawasha vibanda 3vya biashara umetoka hapo wakawasha numba zisizo zidi kumi mradi imefika mwisho.
Kijiji Bwa Rushanje Zamani Bushumba.wanchi hawana umeme na wanauona umepita kwenye mashamba Yao. Mbunge Mwijage Charles, anajua.
 
Umeenda umewafikia watumiaji?

Ebu tuwailize watu wa Kongwa jirani Spika wa zamani. Sagara A na Sagara b, nenda hadi Pemba moto kote huko Rea ikifika nakuwasha nyuma zisizo zidi Tano Tano. Kila Kijiji.

Katavi wilaya ya Tanganyika, vijiji kaza Nako ilikua hivyo. Kuna Kijiji wilaya ya Muleba , umeme uliwashw mskitini ukatoka wakawasha vibanda 3vya biashara umetoka hapo wakawasha numba zisizo zidi kumi mradi imefika mwisho.
Kijiji Bwa Rushanje Zamani Bushumba.wanchi hawana umeme na wanauona umepita kwenye mashamba Yao. Mbunge Mwijage Charles, anajua.
Umeelewa nilichoandika?

Kuna bado vijiji vichache sana ambavyo havijafikiwa na umeme wa REA

REA inakusanya mabilioni sasa yote sasa yaende wapi EWURA inakusanya yaende posho za wafanyakazi wa REA au?
 
Unaposema vijijini unaapajua lakini? unajua vipato vyao? mtu anunute mtungi mdogo wa 35,000 wakati chakula cha kukipika kwenye hiyo gesi ni mtihani? Hizo pesa wanataka kuzipiga tu na si vinginevyo
Sehemu kubwa hiyo mitungi ni kodi za Serikali

Serikali iondoe kodi kwenye mitungi.kwa kutumia pesa za REA
 
Umeelewa nilichoandika?

Kuna bado vijiji vichache sana ambavyo havijafikiwa na umeme wa REA

REA inakusanya mabilioni sasa yote sasa yaende wapi EWURA inakusanya yaende posho za wafanyakazi wa REA au?
Wote wanakusanya ukinunua mafuta na umeme
 
Wote wanakusanya ukinunua mafuta na umeme
Sawa walikuwa wakikusanya kwa ajili ya kupeleka umeme vijijin

Umeme uko chini ya wizara ya nishati na Madini sasa kama umeme umesikia high percentage hizo hela ziende wapi zaidi.ya kwenda kwenye cooking gas kuwezesha wengi watumie gas vijijini
 
Sawa walikuwa wakikusanya kwa ajili ya kupeleka umeme vijijin

Umeme uko chini ya wizara ya nishati na Madini sasa kama umeme umesikia high percentage hizo hela ziende wapi zaidi.ya kwenda kwenye cooking gas kuwezesha wengi watumie gas vijijini
Bado sana wangekuwa wafikia mbali wasingeongeza bei ya ume?e wa REA kutoka 27k hadi 300k+ labda uniambie zinaingia kwenye matumbo yao, ushasikia nafasi hata ya kuhamia REA?

Kama huijui REA tuulize tuliopitapita kufunua majalada ofisi kadhaa za umma
 
Sawa walikuwa wakikusanya kwa ajili ya kupeleka umeme vijijin

Umeme uko chini ya wizara ya nishati na Madini sasa kama umeme umesikia high percentage hizo hela ziende wapi zaidi.ya kwenda kwenye cooking gas kuwezesha wengi watumie gas vijijini
Ila wewe akili huna. Msiwe mnajiingiza kwenye mijadala ambayo hamuelewi chochote. Pia Hakuna wizara ya nishati na madini
 
Bado sana wangekuwa wafikia mbali wasingeongeza bei ya ume?e wa REA kutoka 27k hadi 300k+ labda uniambie zinaingia kwenye matumbo yao, ushasikia nafasi hata ya kuhamia REA?

Kama huijui REA tuulize tuliopitapita kufunua majalada ofisi kadhaa za umma
Huyo jamaa ni mweupe kabisa kichwani. pesa inayotokana na REA ni around bil 40 tu kwa mwaka. Bil 40 kwa mwaka unaweza kusaidia vijiji gani watumie gas? Anafikiri gas ni masihara
 
Sawa walikuwa wakikusanya kwa ajili ya kupeleka umeme vijijin

Umeme uko chini ya wizara ya nishati na Madini sasa kama umeme umesikia high percentage hizo hela ziende wapi zaidi.ya kwenda kwenye cooking gas kuwezesha wengi watumie gas vijijini
Unajua pesa kiasi gani inapatikana kutokana na REA?? Alafu usikifiri hiyo nishati ni raisi hivyo, kwenye umeme tu kuunga kwa 27k tumeshindwa kumaintain.
 
Kila kijiji kina umeme; JE KWA NINI HAO WANANCHI HAWAPIKII UMEME? Yehodsya ukitoa jibu sahihi, naomba mjadala ufungwe.
Note: Kuna baadhi ya vijiji hata Kimi/umeme vinanunuliwa kwa mbinde, wake ngangari wanazfuata km kadhaa
 
Ni kweli na inasaidia ,na inahitaji mkono wa serikali na sekta binafsi
 
Unajua REA tunakusanya sh ngapi? Au utasaidiaje?
REA ni muhimu sana ,ndio maana nmesema ni bora zote kufanya kazi ,maana REA inasaidia sana hasa kwenye umeme ,na gesi zitasaidia kwenye kupunguza hewa ya ukaa.
 
Back
Top Bottom