Peter Kibatala alibeba kisheria suala la mwananchi aliyeamuliwa kuwekwa ndani na Waziri Jerry Silaa huko Morogoro

Viongozi wapuuzi sana Hawa machawa hawaelewi kitu chochote kabisa!
 

Jerry Silaa ni mwanasheria? Alisomea wapi? Na alifaulu kabisa? Sijawahi kuona msomi wa sheria anamihemko kama ya mpiga debe anaponyimwa mia mbili na kondakta.

Msomi wa sheria anakosa uwezo wa kusikiliza? Labda kama alisoma hizo sheria akiwa tayari na mamlaka ndio nitaelewa tatizo lilipo.

Wasomi wa sheria waliosoma na kufaulu vizuri ninaowajua ni watu wenye uwezo mzuri wa kusikiliza kwa utulivu na kisha kufanya maamuzi.
 
Hapo kwenye bold kasoma sheria open university
 
CCM wao walituzoeza hivi, Ukiulizwa na mkubwa usijibu, na usipojibu unakiburi au umeshindwa unaadhibiwa.

Ukiulizwa na ukajibu wewe unakiburi, unajeuri na ni mpinzani wa ccm na unajipima nguvu na mamlaka.

Wamezoe kutuambia 'Mama anaenda nje kutuletea pesa, kutujengea barabara,hospitali shule, na huduma zote za kijamii" na ukiuliza pesa zinazokusanywa na TRA na mamlaka zingine zinakwenda wapi, tayari wewe ni jeuri, ni mpinga CCM na hufai kwenye jamii.

Enzi zile tunadumisha fikra tukufu za mwenyekiti zimepitwa na wakati, CCM badirikeni.
 
jerry is not a lawyer, ni law graduate. wekeni records sawa. lawyer hawezi kubehave kama yeye.
 
Duniani bhana watu wataaluma moja wanawindana iyo inaitwa one mistake one goal kama lamine yamal alivyotamba leo na nico williams plus cole palmer ambapo gareth southgate waingereza watamshambulia sana
 
Kitambo nilisema juu ya Mh. wetu huyu. Wizara ya ardhi ni moja ya wizara chache ambazo waziri/naibu waziri kamwe hawezi akatatua au kusikiliza matatizo yake na akawa sahihi kimamlaka. Hii ni kwasababu migogoro yote au matatizo yote ya ardhi yanajadiliwa na kusuluhishika kwenye mabaraza ya ardhi na mahakamani tu.

Hapo utakuja kushtuka, alichokuwa anakifanya plus alichokiamuru vyote ni batili kwenye jicho la sheria.

Ukiwa waziri hiyo kada unatakiwa kufanya siasa ya kupooza wananchi tu wala usilete masuluhishi wala majadiliano ya kero zao sababu huna hayo mamlaka kisheria.
 
Matatizo ya Ardhi na hivyo vyombo vya kutatua navyo ni matatizo, Kwanza wafanyakazi wa Ardhi, pili mabaraza ya Ardhi kubariki, ubovu wa wafanyakazi, Mwisho ni mahakama.
 
Matatizo ya Ardhi na hivyo vyombo vya kutatua navyo ni matatizo, Kwanza wafanyakazi wa Ardhi, pili mabaraza ya Ardhi kubariki, ubovu wa wafanyakazi, Mwisho ni mahakama.
Watumishi ndio tatizo ila mfumo ni mzuri sana kwenye makaratasi. Tatizo kupata watu sahihi.

Na kukosa watu sahihi kunatokana na jamii yetu kuwa corrupt kuanzia ngazi za familia inaenda hadi taifa
 
Sasa OCD amemchukua kwenda naye wapi na kwa kosa lipi hapo?CCM bwana,muhusika wa jambo anaongea...unataka aongee unavyofikiri wewe kisa ni waziri....?Yale yale ya Mfalme Zumaridi ya Polisi CCM kumfungulia mashita ya kusafirisha eti watu kiharamu,ilihali watu wanakwenda Kanisani kwake kwahiari..na wanaonekana kwq macho.Akawashinda kesi kwa aibu ya kushindwa hata mwendesha mashitaka wa Polisi kujibu maswali kizimbani.
 
Waziri atapiga simu nyingi sana kuomba yaishe mana ameyatimba, kujinwambafai kwa nini vijana? Wewe nikiongozi lakini hujiamini ukitazama mzee wa watu wala hakujibu vibaya alikua anaelezea chamgamoto kwa undani ambayo waziri hakutaka kusikiliza sasa kiongozi usietaka kusikiiiza wewe sio kiongozi
 
mimi natamani viongozi kama hawa wawajibishwe na kutoa fidia binafsi kwa raia kama hawa, watu wawashitaki mahakamani, walipe fidia. mbona yule polisi na DC wa Manyara waliamriwa na mahakama kulipa mil.10 kwa kumweka mtu mahabusu kijingajinga? na wanalipa wao toka mifukoni mwao, hazilipo ofisi zao.
 
Tone ya jamaa haijaonesha respect kwa waziri..
 

Hakuna kesi hapo.
 
Hakuna kesi hapo.
bibi kizee kumbe mimi na wewe sote tupo nje ya nchi, kule bongo sasaivi wamelala. tujuane basi wapi ulipo huwezi jua kama huna bwana nikutafutie bwana huku mamtoni. atu tukutane tunywe kahawa, ila usivae mabom.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…