Peter Kibatala alibeba kisheria suala la mwananchi aliyeamuliwa kuwekwa ndani na Waziri Jerry Silaa huko Morogoro

Na wanahabari walitakiwa kufuatilia kujua wanaenda naye na kwa kosa gani?
 
Jerry Slaa nilikuwa nimeanza kumkubali wakati anashughulukia ardhi iliyoporwa kutoka kwa wanyonge lakini sasa naona ameanza kulewa madaraka. Ulevi wa madaraka utamtapisha asipokuwa makini
 
Nchi ina viongozi wapumbavu kama hawa
 
Vijana wa taifa wangepaza sauti ili waziri atolewe kwenye kiti kwa kutumia madaraka yake vibaya!

Lakini tunabakia kutoa macho na kusema kwao morogoro, yule sawa na mzee wake wa kumzaa nk

CCM bado sana, itaendelea kuwepo
Mfumo umeoza kuanzia juu mpk chini
 
Utawala wa Sheria ufuatwe,na wanasiasa au watendaji wa Serikali.Cheo ni dhamana
Haya mambo ni rahisi sana kuongea mitandaoni. Lkn jaribu kuwaza kitu kimoja - wewe kama mwananchi ni kitu gani unaisaidia Serikali ili utawala wa sheria ufuatwe?

Ndio maana tunasisitiza sana tujenge utamaduni wa kujitolea kwa ajili ya Taifa letu na tutajikuta tuna ushawishi mkubwa sana kwenye mamlaka za ki Serikali badala ya kuwa social media heros
 
Vijana wa taifa wangepaza sauti ili waziri atolewe kwenye kiti kwa kutumia madaraka yake vibaya!

Lakini tunabakia kutoa macho na kusema kwao morogoro, yule sawa na mzee wake wa kumzaa nk

CCM bado sana, itaendelea kuwepo
Tunaendelea kusisitiza tujenge utamaduni wa kujitolea free kwa ajili ya Taifa letu wenyewe.

Tukifanya hivyo wananchi watakuwa na mamlaka makubwa sana kwa watumishi wa umma.

Lkn wengi wa watu zaidi ya kulalamika mitandaoni hawana nguvu nyingine yoyote ile.

Matatizo mengi ya nchi hii yamesababishwa na wananchi wenyewe na wananchi wenyewe wakiamua wanaweza kuyatatua hata bila waziri kuwepo.
 
Madaraka hulevya, wachache sana wanajua mipaka ya madaraka yao.
 
Na kale kengine kanaropokwa eti "usimjibu waziri hivyo" utadhani yule mzee alitukana au aliongea kwa maudhi au dharau kuna siku watakutana na watu akili zimeenda likizo watakosa pa kutokea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…