Peter Msechu adai kupungua kilo 7 baada kuwekewa puto Tumboni

Peter Msechu adai kupungua kilo 7 baada kuwekewa puto Tumboni

Mbona ghafla sana? Rate ya upunguaji ni kubwa sana ,kwa siku kilo moja siyo mchezo,atakuja kuleta matatizo mengine.
ntashangaa sana kama Muhimbili watasema hii ni sawa.
Kwamba hii rate ya ushukaji wa hizi kilo ndo lengo pekee haijalishi mwili unapitia mchakato mwingine upi unaohusisha na kuathiri viungo vipi?
Kazi ipo!
 
Msanii Peter Msechu amefanikiwa kupunguza uzito wa kilo saba ndani ya siku saba tangu alipowekewa puto na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila ili kumsaidia kupunguza uzito.

Msechu aliwekewa puto hilo Januari 25, 2023 akiwa na uzito wa kilo 143.4 lakini kufikia leo Februari Mosi 2023, ana uzito wa kilo 136.5, wastani wa punguzo la uzito la kilo moja kila siku.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa leo kwenye ukurasa wa Instagram wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila, imethibitisha kwamba msanii huyo wa Bongo Flava amepunguza uzito huo ndani ya muda mfupi.

“Msanii Peter Msechu amepungua kilo saba, toka afanyiwe huduma tiba ya kuwekewa puto (intragastric balloon) kwenye tumbo la chakula ili kumsaidia kupungua. Huduma hiyo alifanyiwa Januari 25, 2023, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila,” inaeleza taarifa hiyo.

Msechu pia ameandika katika ukurasa wake wa Instagram kuonyesha kwamba amepunguza uzito huo huku wakiwashukuru madaktari wa Hospitali ya Muhimbili Mloganzila kwa kufanikisha azma yake ndani ya muda mfupi.

“Eeeh Mwenyezi Mungu sijui nikushukuru vipi, niliwekewa puto Januari 25, 2023, picha hiyo nilipiga asubuhi wakati naenda hospitali asubuhi. Leo ni siku ya saba baada ya kumeza puto Februari Mosi, 2023 nimepiga picha hiyo muda ule ule wa asubuhi kama wakati naenda hospitali. Nimepunguza kilo saba kwa siku saba, ina maana kila siku kilo moja inazikwa. Muhimbili hii mmetishaa.

MWANANCHI

“Kipekee kabisa asanteni sana wataalamu wote na madakatari kutoka Hospital ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila, haki ya nani mmebadilisha maisha yangu tayari ndani ya wiki moja tu. Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili Profesa Janabi kongole sana,” ameandika Msechu.
Nilishawahi kumwambia mtu humu ndani,kuwa unene wa watu wengine huwa unatokana na kula sana akabisha,sasa ilivyo ni kuwa tumbo likishatanuka na kuwa kubwa huwezi kukaa tena muda mrefu bila ya kutia kitu tumboni,na mwishowe kupunguza unene inakuwa ni mtihani kwake,kwahiyo kwa kuwekewa puto,food intake yake inakuwa imepunguzwa sana.Naona sasa hivi atakuwa ananielewa...
 
Msanii Peter Msechu amefanikiwa kupunguza uzito wa kilo saba ndani ya siku saba tangu alipowekewa puto na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila ili kumsaidia kupunguza uzito.

Msechu aliwekewa puto hilo Januari 25, 2023 akiwa na uzito wa kilo 143.4 lakini kufikia leo Februari Mosi 2023, ana uzito wa kilo 136.5, wastani wa punguzo la uzito la kilo moja kila siku.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa leo kwenye ukurasa wa Instagram wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila, imethibitisha kwamba msanii huyo wa Bongo Flava amepunguza uzito huo ndani ya muda mfupi.

“Msanii Peter Msechu amepungua kilo saba, toka afanyiwe huduma tiba ya kuwekewa puto (intragastric balloon) kwenye tumbo la chakula ili kumsaidia kupungua. Huduma hiyo alifanyiwa Januari 25, 2023, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila,” inaeleza taarifa hiyo.

Msechu pia ameandika katika ukurasa wake wa Instagram kuonyesha kwamba amepunguza uzito huo huku wakiwashukuru madaktari wa Hospitali ya Muhimbili Mloganzila kwa kufanikisha azma yake ndani ya muda mfupi.

“Eeeh Mwenyezi Mungu sijui nikushukuru vipi, niliwekewa puto Januari 25, 2023, picha hiyo nilipiga asubuhi wakati naenda hospitali asubuhi. Leo ni siku ya saba baada ya kumeza puto Februari Mosi, 2023 nimepiga picha hiyo muda ule ule wa asubuhi kama wakati naenda hospitali. Nimepunguza kilo saba kwa siku saba, ina maana kila siku kilo moja inazikwa. Muhimbili hii mmetishaa.

MWANANCHI

“Kipekee kabisa asanteni sana wataalamu wote na madakatari kutoka Hospital ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila, haki ya nani mmebadilisha maisha yangu tayari ndani ya wiki moja tu. Mkurugenzi Mkuu wa Muhimbili Profesa Janabi kongole sana,” ameandika Msechu.
Shida gani tena kwa Msechu mpaka anafikia kilo 143?! Mzee ulimeza mtu au nini?Mmhh?! Eeeh, watu wakishafanikiwa huku Africa wanaishia kula kama simba na kupelekea kuharibu maisha yao. Au ni nini kilimpata huyu bwana? Mtu unashindwa kujizuia kula mpaka uwekewe puto tumboni?!
 
Msechu Mwenye Enzi Mungu akubariki sana na akupe haja ya moyo wako walahi!
 
Bado ana kilo 136.5, kwani haiwezekani kumeza maputo matatu apunguze kilo tatu kwa siku?
 
Nimeondika mpaka nimekosa cha kuandika.
Dah! Watu waelejezwe kubugia vyakula hai kutuna kama mdudu ni ishara ya maadili duni.
Sawa Lakini upande siyo hivyo, kuna watu wameumbwa na mili minenetu hata ale mawe yeye atakuwa mnenetu.
 
Kupungua kilo moja ndani ya siku moja, hilo siyo jambo la kufurahia.

Kitu umekiweka kwa miaka kadhaa ukiondoe kwa siku moja. Ni hatari.
Mabondia hupunguza hadi 3kg kwa siku
 
Pita(Petero) kama unapitia JF kuwa makini na hilo puto aiseee kusoma nyuzi za Tanzia sio poa kabisa
 
Back
Top Bottom