PhD ya Musukuma yazua gumzo, Chuo kilichomtunuku hakitambuliki

PhD ya Musukuma yazua gumzo, Chuo kilichomtunuku hakitambuliki

Nilipokuwa sekondari Kuna mwandishi mmoja wa vitabu mwenye jina la kihaya nimemsahau alileta TAFRANI kwa baadhi ya VIONGOZI kwa kuwataja kuwa si madaktari wa kweli.......

Kuhusu hizi "HONORIS CAUSA" aliyopatiwa mh.Musukuma anaweza kupewa yeyote mwenye MCHANGO katika jamii ...hoja tu ni kutoka CHUO KIKUU GANI CHENYE ITHIBATI ZILIZOSIMAMA .....

Hata Nassib Abdul "alias" Diamond Platinumz naye ana SHAHADA ya heshima kutoka UDSM ........
Hapo udsm waliniangusha sana
 
Wachunguzi wanadai kwamba eti Chuo hicho kiko India na kwamba kina matawi yake Uingereza na Marekani bali uchunguzi unaonyesha kwamba hakijawahi kusajiliwa Uingereza wala Marekani na wala hakipo huko.

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.

Baba Askofu Bagonza amenukuliwa kwamba aliombwa dola 500 na chuo hicho ili aingizwe kwenye mchakato wa watakaopewa PhD hiyo na hicho chuo cha Musukuma ila yeye akagoma na akawaambia wahusika kwamba anazo ofa kadhaa kutoka kwenye vyuo vikubwa duniani vinavyomuomba akubali kupewa PhD za heshima, tena kwa vyuo vyenyewe kumlipa hadi USD Elfu 10, siyo kwa yeye kuvilipa vyuo kama chuo cha Musukuma kinavyodai.

Swali ni hili, ni nani anafaidika na vyuo vya uongo kama hiki cha Musukuma na ili iweje?

Eti askofu bagonza anajidai yeye ndio alikua alipwe $ 10000 ili kukubali apewe Phd ya heshima😂😂. Kuna watu wanajua kuji over asses. Hivi huyo askofu na msukuma nani katumikia wananchi kwa uhodari kuliko mwingine? Watu wamejaa ulaghai na kujidai kama askofu bagonza hakika ni wengi duniani.
Sisi tutaanza kumwita Msukuma Dr. Msukuma. Hakika ana akili nyingi kuliko askofu bagonza.
 
... Bungeni hana mchango wowote. Kwenye jamii hana mchango wowote zaidi ya kuvimba tu...
Kwenye jamii gani hana mchango au na wewe ni kama mimi hatujui lolote kuhusu mtu fulani ila tunamjua nje ndani?.
 
Kwenye jamii gani hana mchango au na wewe ni kama mimi hatujui lolote kuhusu mtu fulani ila tunamjua nje ndani?.
Mimi nipo Nzela huku Geita namfahamu vizuri huyu jamaa ni mzee wa kuvimba hana lolote ubunge unamsaidia tu kwenye biashara zake.
 
Huu ndio utani na matusi kwenye elimu. Zuzu hawezi kupewa PhD. Haya ni matusi, na tukiendelea hivi, mazuzu wanapewa vyeti tu kwa kununua, mwisho wake ni hatari sana. This PhD is shithole. 😡😡😡
 
Hii nchi ina mambo. Na ujanja wote anakubali PhD za kuungaunga ili aonekane ni msomi.[emoji134]
 
Huu ndio utani na matusi kwenye elimu. Zuzu hawezi kupewa PhD. Haya ni matusi, na tukiendelea hivi, mazuzu wanapewa vyeti tu kwa kununua, mwisho wake ni hatari sana. This PhD is shithole. [emoji35][emoji35][emoji35]

An honorary degree is an academic degree for which a university has waived all of the usual requirements. It is also known by the Latin phrases honoris causa or ad honorem.

Umeelewa?

Hongera King Dr. J.K Msukuma (Mb)
 
Mimi nipo Nzela huku Geita namfahamu vizuri huyu jamaa ni mzee wa kuvimba hana lolote ubunge unamsaidia tu kwenye biashara zake.

Humjui kabisa kama unadhani ubunge ndio unasaidia biashara zake!!

Msukuma anavimba?! [emoji1787]dude pls!!

Hongera sana King Dr. J.K Msukuma (Mb)
 
Back
Top Bottom