BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kampuni ya Vodacom Tanzania imetangaza kumteua Ndg. Philip Besimire kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya kuanzia Oktoba 25, 2022.
Philip anajiunga kutokea kampuni ya MTN ya Afrika Kusini, alipokuwa na wadhifa wa Afisa Mkuu wa Mauzo, Usambazaji na Uendeshaji.
Besiimire anachukua nafasi ya Hilda Bujiku ambaye alikuwa akitumikia nafasi hiyo kama Kaimu Mkurugenzi kufuatia kuondoka kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu Sitholizwe Mdlalose.
Philip anakuja na uzoefu wa kimataifa wa uongozi na ufahamu mkubwa unaoendana na nafasi hii muhimu. Uteuzi wake unaakisi jitihada za Bodi ya Vodacom Tanzania kuimarisha nafasi ya kampuni hiyo katika sekta hii muhimu na kuendeleza kauli mbiu ya Vodacom - kuiongoza Tanzania katika ulimwengu wa kidigitali na kubadili maisha ya Watanzania kupitia Teknolojia.
Katika uzoefu wake wa miaka 15 katika MTN, pia aliwahi kuwa mkuu wa masoko na kaimu Mkurugenzi Mtendaji nchini Eswatini (Swaziland).
Vodacom imesema kuwa katika uteuzi wa Besimiire ni ishara ya wapi wanatamani kwenda kwa pamoja huku wakipanua nafasi zao na kuendelea kutekeleza mkataba na madhumuni yao ya kijamii ambayo wanasema ni kuifikisha Tanzania katika zama za kidijitali na mabadiliko ya maisha. kupitia teknolojia.
Besimiire ana Shahada ya Uzamili katika Utawala wa Biashara kutoka Uholanzi na Shahada ya Kwanza ya Sanaa katika sayansi ya jamii kutoka Chuo Kikuu cha Makerere Kampala, Uganda.
Philip anajiunga kutokea kampuni ya MTN ya Afrika Kusini, alipokuwa na wadhifa wa Afisa Mkuu wa Mauzo, Usambazaji na Uendeshaji.
Besiimire anachukua nafasi ya Hilda Bujiku ambaye alikuwa akitumikia nafasi hiyo kama Kaimu Mkurugenzi kufuatia kuondoka kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu Sitholizwe Mdlalose.
Philip anakuja na uzoefu wa kimataifa wa uongozi na ufahamu mkubwa unaoendana na nafasi hii muhimu. Uteuzi wake unaakisi jitihada za Bodi ya Vodacom Tanzania kuimarisha nafasi ya kampuni hiyo katika sekta hii muhimu na kuendeleza kauli mbiu ya Vodacom - kuiongoza Tanzania katika ulimwengu wa kidigitali na kubadili maisha ya Watanzania kupitia Teknolojia.
Katika uzoefu wake wa miaka 15 katika MTN, pia aliwahi kuwa mkuu wa masoko na kaimu Mkurugenzi Mtendaji nchini Eswatini (Swaziland).
Vodacom imesema kuwa katika uteuzi wa Besimiire ni ishara ya wapi wanatamani kwenda kwa pamoja huku wakipanua nafasi zao na kuendelea kutekeleza mkataba na madhumuni yao ya kijamii ambayo wanasema ni kuifikisha Tanzania katika zama za kidijitali na mabadiliko ya maisha. kupitia teknolojia.
Besimiire ana Shahada ya Uzamili katika Utawala wa Biashara kutoka Uholanzi na Shahada ya Kwanza ya Sanaa katika sayansi ya jamii kutoka Chuo Kikuu cha Makerere Kampala, Uganda.