Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Athmani Kondo ni mmoja wa Wazee Mashuhuri na Maarufu wa Tabora walionialika kuzungumza katika Kongamano la CCM kuhusu mchango wa Tabora katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Nilizungumza Ukumbi wa Chuo Cha Uhazili Tabora.
Athmani Kondo ameniletea picha hizo hapo chini zikionyesha mambo kama yalivyokuwa katika Mkutano wa TANU wa mwaka wa 1958 kujadili Kura Tatu.
Hizi ni picha adimu kupita kiasi ambazo zingestahili kuning'inizwa katika kuta za Makao Makuu ya CCM Dodoma na hali kadhalika kuhifadhiwa Makumbusho ya Taifa.
Mapokezi ya Rais wa TANU na wajumbe wa mkutano Ofisi ya TANU Barabara ya Usagara, Gongoni Ofisi ya TANU ilikuwa katika nyumba ya kupangisha ya Issa Kibira.
Julius Nyerere na Bibi Titi wakiwa na wenyeji wao majina yao hayakuweza kupatikana.
Ndani ya ukumbi wa mkutano wa Kura Tatu Parish Hall, Tabora.
Wananchi wakielekea Uwanja wa Polisi kuhudhuria mkutano wa TANU baada ya TANU kupitisha Azimio la Busara kuamua kushiriki Kura Tatu.
Mkutano wa hadhara wa TANU Uwanja wa Polisi Mwalimu Nyerere alizungumza na katika ya hotuba alinyamaza na kulia akisema kuwa ikiwa Waingereza hawatakubali kutoa uhuru TANU itamshtakia Mungu. Uwanja mzima uliangua kilio.
Nilizungumza Ukumbi wa Chuo Cha Uhazili Tabora.
Athmani Kondo ameniletea picha hizo hapo chini zikionyesha mambo kama yalivyokuwa katika Mkutano wa TANU wa mwaka wa 1958 kujadili Kura Tatu.
Hizi ni picha adimu kupita kiasi ambazo zingestahili kuning'inizwa katika kuta za Makao Makuu ya CCM Dodoma na hali kadhalika kuhifadhiwa Makumbusho ya Taifa.
Mapokezi ya Rais wa TANU na wajumbe wa mkutano Ofisi ya TANU Barabara ya Usagara, Gongoni Ofisi ya TANU ilikuwa katika nyumba ya kupangisha ya Issa Kibira.
Julius Nyerere na Bibi Titi wakiwa na wenyeji wao majina yao hayakuweza kupatikana.
Ndani ya ukumbi wa mkutano wa Kura Tatu Parish Hall, Tabora.
Wananchi wakielekea Uwanja wa Polisi kuhudhuria mkutano wa TANU baada ya TANU kupitisha Azimio la Busara kuamua kushiriki Kura Tatu.
Mkutano wa hadhara wa TANU Uwanja wa Polisi Mwalimu Nyerere alizungumza na katika ya hotuba alinyamaza na kulia akisema kuwa ikiwa Waingereza hawatakubali kutoa uhuru TANU itamshtakia Mungu. Uwanja mzima uliangua kilio.