PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka

Kundunduliza ni misemo ya kimaskini.
Ukitoa Rostam ndio Mabilionea/Milionea wa Tanzania wanavyopata hela.

Bakhresa Anauza Ice cream soda, Unga na biashara ndogo ndogo, MO anauza soda, sabuni na biashara nyengine ndogo etc.

Hizo 500 anazidunduliza nyingi mpaka zinafika Trilioni.

Serikali ina majengo mengi sana Kariakoo, wakiweza kupata hata Jengo moja kwa mwaka 1B tunaongelea Mamia ya Mabilioni hadi Trilioni pato la mwaka, je hio fedha haiendeshi Wizara?
 
Kwa mahesabu ya mezani hiyo 2.5Bn inakuja kirahisi sana. Ila tukienda kwenye dunia ya uhalisia, bado hatujajua Occupancy rate ya hilo jengo itakuwa ni asilimia ngapi? Kuna uzoefu wa majengo mengi kujengwa na kukosa wateja.
 
Kariakoo ni mji mkongwe hakunaga kitu kinaweza kufanyika tena pale
 
Hayo matatizo mbona madogo sana kutatua, watu wamejenga treni za chini ya ardhi, wamebomoa majumba, itakuwa kuondoa machinga mtaani tu?

Tatizo watu hawana imagination na nia.

Ukiwa na imagination na nia hayo mengine yote yanafanyika.
Ukiwaondoa hao wafanyabiashara wadogo na Soko nalo linakufa vile vile.

Swali moja kwako, kwanini uwapokonye wafanyabiashara wadogo kariakoo wakati kuna maeneo yaliyotengwa ya biashara ya kimataifa yenye ukubwa zaidi ya mara 10 ya kariakoo? Eneo kote kuanzia Mjini na barabara ya salender kwenda hadi mwenge kuna Eneo kuubwa lenye maelfu ya Biashara za kimataifa.
 
Hayo matatizo mbona madogo sana kutatua, watu wamejenga treni za chini ya ardhi, wamebomoa majumba, itakuwa kuondoa machinga mtaani tu?

Tatizo watu hawana imagination na nia.

Ukiwa na imagination na nia hayo mengine yote yanafanyika.
Ukiwaondoa hao wafanyabiashara wadogo na Soko nalo linakufa vile vile.

Swali moja kwako, kwanini uwapokonye wafanyabiashara wadogo kariakoo wakati kuna maeneo yaliyotengwa ya biashara ya kimataifa yenye ukubwa zaidi ya mara 10 ya kariakoo? Eneo kote kuanzia Mjini na barabara ya salender kwenda hadi mwenge kuna Eneo kuubwa lenye maelfu ya Biashara za kimataifa.
 
Kama jengo litajengwa mtindo wa magorofa hakuna mpangaji atakayeingia humo kupanga. Chukueni somo kutoka Machinga complex imebaki mahame.
Usiishi kwa kukariri, wenzetu nchi zilizoendelea majengo yao yanajengwa hivyo na hakuna mashaka kama uliyonayo. Case ya machinga complex ni tofauti sana na hii ya DDC.
 
Wapi imeandikwa litagharimu 50B?

Hamuelewi mnachokisoma au ni ukondoo tu?
Wewe unaejua tuelezee imeandikwa Bilion ngapi...

Unaelewa kwanza tofauti ya Construction costs, other costs na total investment costs?
 
Huyu yupo kwenye exclusive world mkuu, achana nae...

Soko la Kariakoo ni la wachuuzi, wahindi, waarabu, wachaga , wakinga, waha, wanyakyusa etc...

Hizo blabla ndio walizileta soko la Karume wakajenga Machinga complex kwa hiz hizi hallucinations... Muulize limengiza bei gani
 
Usiishi kwa kukariri, wenzetu nchi zilizoendelea majengo yao yanajengwa hivyo na hakuna mashaka kama uliyonayo. Case ya machinga complex ni tofauti sana na hii ya DDC.
Kariakoo maghorofa yote yamebanana tofauti na enzi za Msajili wa Majumba

Dar ipanuke Kariakoo ndio imefika mwisho ile

Makosa yalifanyika Wa Swahili walipoanza kuuza Nyumba zao kwa Wakinga 😂😂🔥
 
Naona watu wamekurupuka kuchangia uzi kwa mihemko bila kuelewa kilichoandikwa. Mmeambiwa mradi ni wa serikali na mbia. Wakati ujenzi ukiendelea serikali itakuwa ikijipatia 2b kwa mwaka na baada ya mradi kukamilika serikali itajipatia 2.5b kama kodi ya jengo (kumbuka m'bia naye ana mgao wake nje ya hizo 2.5b) na bado hapo serikali itakusanya kodi na shuru nyingine kutoka kwenye uwekezaji huo. Kwa namna wakurupukaji wanavyochangia ni kama walitaka serikali ikusanye kilakitu na mbia asipate chochote kitu ambacho hakiwezekani. Nilidhani tungempongeza kwanza Kafulila kabla ya kucomment kwa chuki na mihemko.
 
Hao unaowaita wafanyabiashara wadogo kwanza ni wapoteza nguvukazi ya taifa tu. Hiyo ni disguised unemployment tu hakuna biashara hapo.

That is part of the problem, watu hawa add value yoyote wanachafua mji tu.

Hao watu wanatakiwa kupewa biashara za kweli na sehemu za kufanya biashara, si kuchafua mji.

Again, hatuwezi kuelewana kwa sababu uko stuck ulipo na mimi nafikiria kinachoweza kufanyika far beyond ulipo.
 
Wewe uliielewa embu tueleweshe step by step...
1.Serikal inalipwa kwa minajili gani kama jengo jalijakamilika?

2.Serikali ni mbia no 1 kwa biashara zote nchini by 30% of the total profit, kulikuwa kuna haja gani ya kushirikiana na wananchi kwenye kujenga frame

3.Serikal ingepangisha ardhi ya ya lile eneo hudhan kwamba ingeokoa fedha zaid?

4.Huo usuhuru na kodi nyingine hudhani kwamba ni speculations tu na zinaweza zisiwe realistic? Una speculate kodi na ushuru kwa biashara ambazo bado hazipo?

Embu fafanua mkuu tuache kukurupuka
 
Na wewe unapenda ku copy sababu nchi X imefanya Y kutotoboa na sisi unataka tupitie humo humo, kila nchi ina changamoto zake na namna ya kuzitatua.

Mfano mzuri angalia tu Mobile money kama Mpesa na Tigo Pesa ni kitu chetu tunajivunia Africa, tumeanzisha kitu na kimefit utamaduni zetu, so far Dunia nzima ina copy mfumo wa mobile money na Africa ikiwa pioneer.

Kwa logic zako hizi miaka 20 iliopita ungetaka na sisi tuegemee kwenye mifumo kama ya Ulaya ya Benki.

Hao unaoita wachuuzi wengi wanaingiza hela nyingi kwa mwezi kuliko Waalimu na wafanyakazi wengine wa Serikali, kawaida kkoo machinga kuingiza hadi laki kwa siku, kuna ma ofisa kibao serikalini wanatembea na Gari na kuendeshwa hawapati hio hela. So hao unaowadharau ni hope ya Taifa hili.

Siku zote mheshimu mtu ambaye Unampa 1000 anaweza akaizalisha na kesho akawa na 2000.
 
Mobile money (tigopesa, Airtel money nk) ni ya mwingereza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…