Picha: Hospitali ya Rufaa ya Chato iliyowekwa jiwe la msingi na Rais Filipe Nyusi. Kuhudumia takriban watu milioni 18 mikoa ya Kanda ya Ziwa

Picha: Hospitali ya Rufaa ya Chato iliyowekwa jiwe la msingi na Rais Filipe Nyusi. Kuhudumia takriban watu milioni 18 mikoa ya Kanda ya Ziwa

Na iwe tu.....

Lowassa alisifiwa na kujisifu kwa MAAMUZI MAGUMU....
Watanzania waliyataka hayo maamuzi MAGUMU....

JPM anakikata KIU CHAO KIKALI.....
Maamuzi magumu ni kuelekeza miradi mikubwa ya maendeleo nyumbani kwako? Hakuna Wilaya iliyopata miradi mingi kama Chato nchi hii! Sasa huo kama sio upendeleo ni nini?
 
Hakika ni msaada mkubwa kwa watu wa kanda ya ziwa ambao wapo mbali na Bugando. Nimeona ipo karibu na ziwa nashauri pawekwe kiutalii zaidi ili kusudi wagonjwa wawe wanarelax
Hospital ipo karibu na ziwa ni fursa kiutalii sehem iwe vizuri ili wagonjwa na watu wanaokuja wawe wanapata utulivu na kurelax na eneo liwe wazi lisiwe block mbele kusudi kupata view
 
Halafu mwisho wa siku utakuta wengi wa manesi, madaktari, madaktari bingwa, wafamasia, wakuu wa vitengo nk. watakaohudumia hiyo hospitali ni kizazi kile kile kutoka kule kule Kaskazini mwa Tanzania (Kilimanjaro na Arusha). Alileta TRA Chato wale jamaa wa Kaskazini wakajaa ofisini, Akapeleka CRDB bado wale wale, akajenga Airport bado wale wale.

Wazee wa fursa wameshatinga chato, wanakwenda na upepo unapovuma, wanavuna pesa za wajinga wajinga Chato na kupeleka Moshi kuzitumbua kila Disemba!
Lugha za kibaguzi, ccm mtaifanya nchi hii kimwagika damu, maana ipo siku watu watachoka.
Mioyo yao itageuka na kutaka kulipa kisasi, ikishasema liwalo na liwe kutakuwa na mito ya damu.

Kuamini kuwa mna nguvu kuliko wananchi ni UPUMBAVU

Kuamini mna Mungu huku mnawabagua wengine
ni UPUMBAVU

Kuamini Mungu yupo Tanzania tu, na yupo kwaajili ya ccm tu, NI UPUMBAVU USIOTIBIKA
 
Tunawalisha samaki nchi nzima, tunawalisha dagaa nchi nzima, tunawapa madini Sasa tusipowawekea mazingira mazuri Ili mje kuchukua mizigo na biashara kwa uzuri mnataka mkija mteseke? Na mkiumwa mkose hospital, Mimi nimependa style hii ya maendeleo Sasa waliokimbia mikoa yao kwenda kukaa dar bila shughuli ya muhimu Sasa tunawatanya mrudi mikoani mkajinufaishe mapema.
Sio warudi mikoani bali waende Chato! Yanayofanyika Chato hayajashuhudiwa wilaya yoyote nchini!
 
Hakika ni hatua kubwa mno ITAKAYOPIGWA.

Kuhudumia wananchi milioni 18 wa nchi hii si jambo DOGO haswaaa.

Tunategemea mengi yatafanywa na kuachwa kama LEGACY kwa ajili yetu wananchi kipindi hiki cha awamu ya 5.
Ina maana kwa idadi ya watanzania hospitali tatu kama hizo zinatosha!!!
 
Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ni kwamba hospitali ya Rufaa ya Chato itahudumia takribani watu milioni 18.

Kwamba wagonjwa 700 watahudumiwa kila siku.

Kwamba mikoa 6 ya kanda ya ziwa itahudumiwa na hospitali hii

Kwamba hospitali ya Rufaa Chato itahudumia takribani 1/3 ya Watanzania wote

Hivyo ni muhimu ujenzi wa hospitali hii ukakamilika mapema.

Maendeleo hayana vyama!
Hivi nilikuwa sijui kumbe pale Chato ni katikati ya mikoa 6 ya kanda ya ziwa.

Maana yake ni kwamba itakuwa rahisi watu kufika pale kutoka kila upande.

Ninachojua, hii hospitali itakuwa ya mfano ndani ya miaka hii mitano. Itapata support yote ya serikali na high class vifaa tiba ila bada ya mitano hii sijui kitakachofuata
 
Halafu mwisho wa siku utakuta wengi wa manesi, madaktari, madaktari bingwa, wafamasia, wakuu wa vitengo nk. watakaohudumia hiyo hospitali ni kizazi kile kile kutoka kule kule Kaskazini mwa Tanzania (Kilimanjaro na Arusha). Alileta TRA Chato wale jamaa wa Kaskazini wakajaa ofisini, Akapeleka CRDB bado wale wale, akajenga Airport bado wale wale.

Wazee wa fursa wameshatinga chato, wanakwenda na upepo unapovuma, wanavuna pesa za wajinga wajinga Chato na kupeleka Moshi kuzitumbua kila Disemba!
Duh.. Utakuta huyu nae ni msomi ana digrii alafu kaandika huu utopolo
 
Halafu mwisho wa siku utakuta wengi wa manesi, madaktari, madaktari bingwa, wafamasia, wakuu wa vitengo nk. watakaohudumia hiyo hospitali ni kizazi kile kile kutoka kule kule Kaskazini mwa Tanzania (Kilimanjaro na Arusha). Alileta TRA Chato wale jamaa wa Kaskazini wakajaa ofisini, Akapeleka CRDB bado wale wale, akajenga Airport bado wale wale.

Wazee wa fursa wameshatinga chato, wanakwenda na upepo unapovuma, wanavuna pesa za wajinga wajinga Chato na kupeleka Moshi kuzitumbua kila Disemba!
Tanzania ni ya wote. Sasa kama wasukuma hamtaki kusoma tuwafanyeje? Wachaga tutakuja kuwahudumia
 
Hivi kusini wana Hospitali kubwa ama ya Rufaa yoyote yaani Ruvuma, Lindi, Mtwara pamoja na maeneo ya nyanda za kusini. Maana sijawahi kusikia na kama haipo si ingekuwa vyema nao wakapatiwa
Mashangazi wanajitibia na maua ya Korosho
 
Bado Chato University College Of Healthy And Allied Science (CUCHAS)
Kasema hatua planned zote zikamilike kwa pamoja, si jambo dogo, ukisikia vision waziri wa afya itakutakuwa mbali ya huduma bigwa, chuo cha tiba na utalii wa tiba...Burigi Chato....Huenda ikawa ya kipekee Africa, ushauri wangu tukawekeze Chato.
 
Hivi nilikuwa sijui kumbe pale Chato ni katikati ya mikoa 6 ya kanda ya ziwa.

Maana yake ni kwamba itakuwa rahisi watu kufika pale kutoka kila upande.

Ninachojua,hii hospitali itakuwa ya mfano ndani ya miaka hii mitano.Itapata support yote ya serikali.na high class vifaa tiba.ila bada ya mitano hii sijui kitakachofuata
Ulishawahi ona Kijiji Cha Mabutu, baada ya kupinduliwa!
 
Back
Top Bottom