KWELI Picha inayoonesha watu wakinywa maji machafu pembeni ya dimbwi imepigwa nchini Tanzania

KWELI Picha inayoonesha watu wakinywa maji machafu pembeni ya dimbwi imepigwa nchini Tanzania

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Oicha hii inasambaa sana kwenye mitandao ya kijamii. Baadhi ya watu wanadai imepigwa nchini Tanzania, lakini kutokana na uwekezaji mkubwa ambao Serikali yetu imefanya mimi siamini kama ni kweli imepigwa nchini kwetu.

Je, hii picha ni Tanzania?

1669363812704.png
 
Tunachokijua
JamiiForums imefanya ufuatiliaji na kubaini kuwa picha hii ni mazingira ya Tanzania, ilipigwa kijiji cha Wami Sokoine wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.

Picha hii ilipigwa na kutumiwa katika ukurasa wa X (Zamani Twitter) wa East Africa Radio na ITV mnamo Novemba 4, 2015. Picha hii ilitumika kuelezea adha ya maji iliyokuwapo katika kijiji cha Wami.

Pia, Capital Radio walichapisha picha hii siku hiyo ya Novemba 4, 2015.

Wananchi wa kijiji hicho walikuwa wakilalamika kutumia maji machafu yanayotumiwa na mifugo kwa muda mrefu hali iliyotishia afya za wananchi hao kwa kuhofia kupata magonjwa, na hununua dumu moja lenye maji safi lita 20 kwa Tsh. 1500/-

Aidha, JamiiForums imefanya mawasiliano na baadhi ya wakazi wa eneo hilo ili kujua hali ya sasa ya eneo hilo ambapo wamekiri bado eneo hilo lina ukame.

Mkazi huyo ambaye hakutaka jina lake liwekwe wazi alisema

"Hii sehemu ni Dakawa Wilayani Mvomero ndiyo kuna hivi vijiji. Inaishi jamii ya Wamasai ambao wanategemea maji kwenye mabwawa. Jua likiwakwa Mabwawa huwa yanakauka. Kulikuwepo na uhaba wa maji ila Wiki hii Mvua imenyesha sana"
Ooh kama toka 2015 had sasa wapo hvo, serikali Iko wap hapo,
Au serikali ipo DAR pekeake,
 
Je, hii picha ni Tanzania?

View attachment 2427093

Viongozi wetu hawaipendi nchi wala watu wake.

Haya ni maji (water table is superficial). Kinachopaswa ni kujenga miundombinu thabiti ili kugema maji mengi zaidi kutoka kwenye hii superficial water table. Kisha kuyasambaza kwenye vijiji vya jirani kulingana na hifadhi ya maji iliyopo kwenye hiyo water table reservoir.

Badala ya kutekeleza miradi hii, viongozi wetu wao ni mwendo wa perepete kali kali bila vitendo maridhawa.
 
Tukingoja kila tatizo watatue tutateseka sn. Wananchi wenye tatzo hilo nao ni tatizo, wameshindwa kuweka mkakati wa uchimbaji visima vya kawaida, kwakuishirikisha serikali ya kijiji. Nguvu kazi(vijana) ipo, nimaamuz tu ndo yanakosekana.

Fikra za kila tatizo hutatuliwa na fedha kwasasa inabid tuondokane nalo. System ya utawala imekuwa corrupted, utu umefunikwa kwa vipande vya sarafu, ubinafsi na tamaa za kujilimbikizia mali zinawatafuna, mbaya zaidi hakuna dira ya maendeleo. Kupanga ni kuchagua, waendelee kuteseka kwa tatzo hilo mpaka pale serikali itakapoguswa au wachukue maamuzi wao.
 
Back
Top Bottom