Picha: Lulu atoa sadaka ya shukrani kanisani

Picha: Lulu atoa sadaka ya shukrani kanisani

Ulitaka wamtenge?! Una mawazo ya "KI-FARISAYO!"

Yesu hakufa msalabani kwa ajili ya watu "WAKAMILIFU" kama wewe, bali kwa ajili yetu "WATENDA MAOVU."

Unaikumbuka habari ya mwana mpotevu?

Yesu alikaa na watoza ushuru, wezi, makahaba, majambazi nk, ili awafundishe na kuwasaidia.

Kama mtawatenga wanaohitaji kuokolewa, neema ya wokovu wataipata wapi? Watasikia wapi Neno la Kristo ili waokolowe? Kwa sababu Imani huja kwa kusikia Neno la Mungu.

Hebu TAFAKARI maandiko haya;

"Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. Mafarisayo na waandishi wakanung'unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao. Akawaambia mfano huu, akisema, Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi. Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu." - Luka 15:1-7

Ubarikiwe!
kanisa lako liko wap mchungaji?
 
dah, ila kweli kadri tunavozidi kwenda mbele mnazidi kukua na kumfikia Mungu urefu, nadhani bdo kidogo watu mtaanza kumwita mjomba enu sasa.

Mungu ana njia zake. Hafanyi mambo kwa mtazamo na hisia za watu. Msiingilie kazi ya Mungu ambaye ndiye pekee mwenye mamlaka ya kuhukumu. Wanadamu wote wana dhambi hakuna mwenye uhalali wa kumhukumu mwingine.
 
Ukishatubu toba ya kweli kwamba wewe ni mwenye dhambi Mungu anasamehe sasa huyu changudoa toka ameokoka lini? Na je ajatembea na waume za watu tena,ajazini,avai nguo nusu uchi? Sasa hapa kaokoka kipi na alitubu dhambi zipi? Hizi dini zingine tuseme ukweli tu zimekaa ki biashara tu.
 
Ukishatubu toba ya kweli kwamba wewe ni mwenye dhambi Mungu anasamehe sasa huyu changudoa toka ameokoka lini? Na je ajatembea na waume za watu tena,ajazini,avai nguo nusu uchi? Sasa hapa kaokoka kipi na alitubu dhambi zipi? Hizi dini zingine tuseme ukweli tu zimekaa ki biashara tu.

Dahhh hata kama hufanyi anayoyafanya ila nawe unacho kibanzi chako kinachokuangusha dhambini Mara kwa Mara.....haujakamilika hadi umhukum mtoto huyu...

Lulu ni mvumilivu sana maana anashushwa kwa mambo mengi ila bado anaendelea na maisha yake.lulu ni strong girl kwa kweli
 
Kwa Mungu kila dhambi inasameheka.

Mchungaji Illovo hebu njoo uhubiri huku.



No kweli kwa kila dhambi anasamehe isipokua ile ya kumkufuru Roho Mt tu. Kwa iyo MTU anaweza.kuwa mbaya leo, lkn kesho akaokoka na akawa safi MBELE za Mungu. Wapo watu kiukweli mioyo yao inampenda Mungu ila wamefungwa tu.

Kwa anaehtj maombez, au kuokoka, au unahtj ushauri wasiliana nami kwa 0786100772 au 0757856336 .
MUNGU AWABARIKI
 
Baada ya kushinda tuzo ya ‘Best Movie East Africa’ @elizabethmichaelofficial siku ya jana aliweza kuhudhuria ibada katika kanisani la Living Water Centre (Kawe Makuti) likiwa chini ya Mtume ‘Enesmo Ndegi’ kutoa sadaka ya shukrani kwa Mungu aliyemuwezesha kupata ushindi wa tuzo.
“Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu pamoja Baba na Mama hakika sijutii kuokoka kwangu na ata wakisema vyovyote I don’t care mimi ni mradi namuomba Mungu na mambo yangu yanaenda.” Lulu

View attachment 331957
Kuna ulazima gani mtu akitoa sadaka uje utangaze??? Unaelewa maana ya sadaka???
Je kila mtu akitoa sadaka akija kutangaza hapa patakalika????
 
Kuna ulazima gani mtu akitoa sadaka uje utangaze??? Unaelewa maana ya sadaka???
Je kila mtu akitoa sadaka akija kutangaza hapa patakalika????

Mkuu unafikiri hiyo picha kaipiga warumi?

Wao wenyewe wamefanya coverage kwa lengo la kuwafikia mashabiki, wametangaza wenyewe.
 
umaarufu bongo ni ghali saaana.kwa wadada bila papuchi kuwekwa dyu dyu mambo hayaendi.ona sasa vicky kamata kaolewa na katibu wizara ya fedha,komba kamjengea nyumba lulu,faraja kota kaolewa na nyarandu,mengi kamuoa ntuyabaliwe?nk nk nk.huwa najiuliza hawa mademu wale majanki waliogonga lebo kabla ya hawa waheshimiwa kula makombo wanakuwaga wapi??jitahidini ukikuta demu mkali na ana shobo za ustaa chapa mimba tuu.subirini msikie lulu kachumbiwa na lee mutuuzi.we haya wee
 
Ndege wafananao huruka pamoja, hivyo msistaajabu ya lulu na huyo mtume kanisani kwake.
 
Umejuaje kuwa we we waabudu kwa roho na kweli duniani hakuna mkamilifu wote tuna mapungufu. Na kwa Mungu hakuna dhambi kubwa wala ndogo. Sasa wabongo huwa MNA hukumu kiukubwa eti wa dhambi
Dada soma vzur uelewe sijasema mimi ila nimewazungumzia wale SIKU NYINGINE USOME NA KUELEWA sio unasoma harakaharaka kama umezma cm ya mtu
 
Kanisa la Kisanii Lazima wasanii wakafanyie usanii wao huko.
 
Makubwa halafu pia sadaqa haitangazwi km unatoa toa na mungu wako ndo shahidi hamna haja ya matangazo.
 
Baada ya kushinda tuzo ya ‘Best Movie East Africa’ @elizabethmichaelofficial siku ya jana aliweza kuhudhuria ibada katika kanisani la Living Water Centre (Kawe Makuti) likiwa chini ya Mtume ‘Enesmo Ndegi’ kutoa sadaka ya shukrani kwa Mungu aliyemuwezesha kupata ushindi wa tuzo.
“Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu pamoja Baba na Mama hakika sijutii kuokoka kwangu na ata wakisema vyovyote I don’t care mimi ni mradi namuomba Mungu na mambo yangu yanaenda.” Lulu

View attachment 331957


Hii inatuhusu nini

Movie zenyewe za hovyo craap tupu tupa kulee
 
Back
Top Bottom