Si bure we utakuwa unaishi kwa shemej yko.......si kwa wivuu huu.....dunia nzima huwez kukuta cheap house ya type hyo......na thaman ya ardhi ya south iko juu kuliko hapa....cz kule maisha ya watu yako juu na watu wenye pesa toka sehemu zote dunian wapo kule afu leo uje ufananishe price ya ardhi ya j'burg na mikochen sijui mbezi beach....kawadanganye watoto wadada bana......ingekuwa hivyo south kusingekuwa na slums kama zile cz serikali ingeweza kuwapa tu watu nyumba za kuishi bure tuu.....bt kule kila ardhi inamwenyewe
You have to attack my points not my person. It is always important to remember that in discussion/debate. You don't know me, what I know, and what I have got just as I don't know you.
Back to the point. Mimi sijasema hiyo nyumba ni cheap.
Lakini ninachokuambia ni kuwa Tanzania tuna tatizo kubwa sana la kutokupima ardhi hasa mijini. Sehemu kubwa ya mji wa Dar es Salaam imekuwa ni ghetto tu. Hakuna barabara, sewage system, ukusanyaji takataka, n.k. Hata huko mnakosema kumepimwa ni vumbi tu. Tazama Mbezi Beach, Sinza, n.k. Sehemu ambayo ni afadhali ni Oysterbay. Hata Masaki kuna barabara nyingi tu za vumbi na maji kwa ndoo/simtank.
Miji ya South Africa ipo vizuri kama ulaya. Lakini kwa vile miji yote imepimwa, basi viwanja na nyumba huwa ni vingi sana na bei hupungua sana. Vilevile wenzetu wanajenga kwa mikopo kuliko Tanzania ambako ni lazima udundulize au uibe. Ndiyo maana wewe unapoona hiyo nyumba unafikiria itakuwa Masaki ya South Africa.
Unapozungumzia slums South Africa kumbuka kuwa kwa vile South Africa kila kipande cha ardhi kina mwenyewe ambao wengi ni wazungu siyo rahisi kwa mtu wa kawaida sana, asiye na kazi ya maana kumiliki nyumba ya maana.
Ukitaka kujua bei za nyumba South Africa tembelea tovuti za Property Agents kama Seeff Properties na linganisha bei za hizo nyumba na bei ambayo ungeambiwa Tanzania. Kumbuka Rand 1 ni sawa na USD 14.
Nakupa tovuti ya Seeff Properties kwa maeneo ya Centurion. Kama unajua mitaa mingine badilisha unavyotaka:
Properties for sale in Centurion | Seeff Properties